Rais Samia: Serikali itashirikiana na Machifu, Viongozi wa Kimila

beth

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
3,880
Reaction score
6,368
Akishiriki Tamasha la Utamaduni lililofanyika leo Januari 22, 2022 Mkoani Kilimanjaro Rais Salia Suluhu Hassan ameeleza, "Kumekuwa na maneno mengi ndani ya Tanzania kuhusu Serikali na Uchifu. Tumeamua kuwa na jukwaa la pamoja baina ya Serikali, Machifu na Wazee wa Kimila ili kuhifadhi Mila na Desturi zetu"

Aidha, amesema Wizara ya Mambo na Nje na Wizara ya Utalii zinaendelea na majadiliano ya urejeshwaji wa Mafuvu ya Machifu yaliyochukuliwa wakati wa ukoloni ili yatumike kwa Utalii na kuelimisha Jamii

Chifu Mkuu wa Kabila la Kichaga Chifu Mareale akimkabidhi Ngao na Mshale Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan, kama ishara ya kumkaribisha rasmi kwenye kabila hilo wakati wa Uzinduzi wa Tamasha la kwanza la Utamaduni wa Mkoa wa Kilimanjaro lililozinduliwa leo tarehe 22 Januari, 2022.
 
Mama anaupiga mwingi sana…halaf anajua sana kukera wale wanaomchukia…
 
Aidha, amesema Wizara ya Mambo na Nje na Wizara ya Utalii zinaendelea na majadiliano ya urejeshwaji wa Mafuvu ya Machifu yaliyochukuliwa wakati wa ukoloni ili yatumike kwa Utalii na kuelimisha Jamii
 
Tunarudi nyuma. Ni mwendo wa kujenga na kubomoa. Hii kitu ni kinyume na katiba ya nchi. Mama kuna wakati anateleza, bado kuanguka tu.
 

Kumbe machifu wapo - kwa sheria ipi jamani?
 
Kiongozi anapokuwa mshirikina ni hatari sana
 
Labda kinachotafutwa kurudishwa ni usultan who knows? Unaanzia kupiga chenga mbali ili uje u justify usultan na umwinyi.
 
0neni hapa priorities za wenzetu - just five months since UPNDP took office.



 
mpaka 2025,atakuwa kabandikwa majina yote ya machifu,huko nako sijui wamemsilimishwa kwa jina gani!? mwanza walimpa chifu hangaya, Kilimanjaro sijui wamemwitaje,bado Dodoma ,iringa ,nakadharika
 
Kweli ukiwa mwanasiasa na Dini kwaheri
Wala hatushangai kwani Siasa imebadilisha imani za wengi sana
 
Kwani mama kateleza wapi? Tuacheni chuki za kizembe kwa mama. Tumuache mama achape KAZI.
Kazi gani? Ya kutwa zima kuwanga na machifu?

Tunataka maendeleo yatokanayo na sayansi na sio huu ushirika! Who does that today!?
 
Kosa kubwa tunalolifanya ni kuona mila na desturi zetu ni kwa ajili ya wageni na sio sisi. Priority inatakiwa iwe jamii yetu na utalii uwe by the way. Tuki wa prioritise watalii kuna hatari ya kubalisha uasili wake ili iwe na mvuto kwa wazungu.

Amandla...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…