#COVID19 Rais Samia, Serikali yako imekiri Corona ipo na bado inashiriki kuisambaza kwa kuruhusu matamasha

Tusidanganyane mkuu hadi kiama ntaamini corona ni mchezo wa wakubwa kataa ukubali umeiona fainali ya EURO jana?? Waingereza walivyojazana uwanjani na mitaani hiyo ilikuwa vita ya kiuchumi na watu au viongozi wachache kupiga hela naungana na polepole pale tulipoishia tuendelee hivyohivyo kupambana na corona
 
Mnachekeshaga! Si uache wewe mwenyewe kwenda kwenye mikusanyiko? Kama vipi piga marufuku hata mke wako na watoto wako kukusanyikana na wengine ili mjilinde. Ukiona na mke wako nae anakuzingua lala vyumba tofauti kabisa. Hii nchi siyo yenu peke yenu na msituzingue na corona yenu. Tumekataa kuipa promo sisi na tutaendelea na life kama kawaida.

Nimesikia serikali italeta chanjo, ikifika kuwa wa kwanza kuchanja.
 
Nasikitika Serikali hii ambayo inatangaza Corona ipo Mtaani huku ikiruhusu matamasha makubwa ya muziki.

Maeneo ambayo Tamasha hili limepita maambukizi ni makubwa mno hadi kufikia baadhi ya hospital kutangaza kuishiwa mitungi ya gas #Mwanza #Kigoma #Dodoma na tutegemee Arusha ndani ya wiki hii kutokea mlipuko mwingine serikali ijiandae kuongeza mitungi ya gas huko.

Nashindwa kuelewa ni kwanini serikali inashindindwa kuchukua hatua madhubuti ya kupambana na ugonjwa huu ingawa kupitia vyombo vya habari wamekuwa wakitangaza wananchi kuchukua tahadhari.
 
Mwanza kumechafuka. Baada ya hilo festival ukapita mwenge na kumba kumba.
 
Pitia taarifa za mwezi uliopita, UK wamekuwa na lockdown muda mrefu sana, wamepigabsana kampeni ya kuchanja watu wake.

Watu unaowaona pale wamechanjwa wote, ukichanjwa unaingia kwenye record na taarifa zako zinakuwa shared kwenye mtandao ambapo zinapohotajika wanaweza kuretrieve.

Sasa endeleeni kujifananisha na Ulaya, wenzetu wakati wanakufa na ugonjwa sisi tulikuwa tunamshabikia bwana yule aliyekufa na huohuo ugonjwa na sasa mnataka kujifananisha na wazungu.

Wao wameshatoka huko, we unadhani kwa nini hiyo ni EURO 2020? wakati wamejifungia sisi tuliendelea kujigamba. Sasa wakimaliza watu wao kuchanjwa ngoma inahamia afrika kama walivyosema 2023 afrika itakuwa kwenye peak ya ugonjwa. Tulibisha sana Ila wanahakikisha baada ya wao kuchanjwa wote, hakuna mdudu kutoka afrika ataingia kwako .

Tusiwe wajima sana.
 

 
Hakika ni mambo ya ajabu sana kuona serikali inayowatangazia wananchi wake achukue taadhali ya maambukizi ya ugonjwa hatari wa corona ambao sharti moja wapo ni kuepuka misongamano..
Mh Rais huwa anapita humu, Nandi inaweza kula kwake, ikasimamishwa hio festival!

Still wasaidizi hawamshauri vizuri Mh Rais
 
Hafu namshauri mama aachane na ziara kipindi hichi Cha third wave yasije mpata COVID-19 ka ya jiwe bure maana ziara zake zinakusanya watu wengi kwa wakati mmoja
 
na UK ina cases ngap za covid toka UERO ianze?
Nyingi tu, juzi walitangaza kwamba zaidi ya raia 2,400 waliokuwa wamekwisha pata chanjo kamili ya KOVID baadae walikumbwa na maambukizi - yaani chanjo hizi type ya mRNA haziaminiki.

Kuna Profesa mmoja wa Ufaransa amesema kwamba chanjo za mRNA ndio zinachangia kuzalisha variant chungu nzima za COVID,in other words ndio tanuru linalo tumika ku-mutate virusi kwa kuwafanya baadhi ya walio pata chanjo kuwa carriers wa maabukizi ya viriant mapya hatari.

Marehemu Dk.Magufuli alilitambua sana hili ndio maana siku moja alisikika akisema kuna baadhi ya Watanzania walio kimbilia kupata chanjo nje ya Nchi ndio hao wametuletea tena magonjwa ya ajabu ajabu Nchini - Magufuli alicho kisema ni sahihi kabisa, lakini WHO inakalia kubatiza variant za kovid na elufi za kiyunani Mara: Alpha,Delta,Gamma,Omega, Beta nk - WHO wanashindwa ku-address kiini kinacho leteleza matatizo yote haya kwamba ni chanjo zinazo zalishwa kwa teknolojia ya kijinetiki (mRNA) ambayo short/long term effect ni highly unpredictable kutokana kwamba ndio mara ya kwanza Duniani kuzalisha chanjo kwa teknolojia ya kijinetiki.

Mbona hatuoji kwa nini Western Big Pharma Companies hawataki kutumia a proved conventional technique ya miaka mingi kuzalisha chanjo!! Mbona Wenzao wa Uchina, Urusi na Cuba wanatumia mbinu za traditional kuzalisha chanjo za Covid na hatujasikia chanjo hizo zikileta madhara kwa watumiaji vikiwemo vifo vya ghafla.

Profesa huyo wa Ufaransa kuongezea kusema kwamba, sio kwamba wana sayansi hawajui matatizo yanayo letelezwa na chanjo za mRNA, hilo wanalijua sana, kasema madhara makubwa yataonekana ndani ya miaka miwili/mitatu ijayo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…