Rais Samia sijakuelewa hapa unapotaka Kushauri na Kuamrisha kuwa Jina la Wafungwa libadilishwe na sasa wawe wanaitwa Wanafunzi

Rais Samia sijakuelewa hapa unapotaka Kushauri na Kuamrisha kuwa Jina la Wafungwa libadilishwe na sasa wawe wanaitwa Wanafunzi

Wafungwa wakiitwa wanafunzi, na wanafunzi wataitwaje?

Zanzibar hakuna neno gereza, Kuna chuo Cha mafunzo. Na Kuna neno skuli badala ya shule.
 
Kwahiyo Muuaji au Mbakaji au Jambazi ambaye alifanya Vitendo hivyo akiwa anajua na ana Akili timamu kabisa huko Gerezani ndiyo anaenda Kuhitimu zaidi Kiuhalifu na kuwa Mwanafunzi bora au?

Kwa Ubongo huu ndiyo Tanzania ipae?
Lengo la kupelekwa gerezani ni kubadilika tabia, kama huku nje ulikua mwizi na ukaiba. Unapelekwa kule ili ujue kama wizi sio mzuri na ubadilike. Na ili ubadilike ni lazima upatiwe mafunzo yatakayokubadilisha. Kuna wemgine wanabadilika na wengine wanakua hawabadiliki. Ni sawa na wanafunzi wa skuli kuna wanaofeli na wanaopasi
 
Nadhani mama anataka kubadili tamaduni na lugha ya Tanzania bara iwe sawa na kwao Zanzibar. Utofauti wetu wa lugha na tamaduni zetu ndio uimara wetu. Asituharibie lugha yetu Bara. Hatutaki kuita shule- skuli, Kufundisha--Kusomesha, Gereza- Chuo cha mafunzo.
Anachofanya ni kutumia maneno ya kiswahili fasaha na inavohitaji. Hata Prof. Ndalichako amekosolewa na haikua shida
 
Huku Zanzibar ndo tunavowaita. Na ukifungwa unaambia utaenda chuo cha mafunzo kwa muda wa miezi 6, yaani utakua gerezani kwa miezi 6. Lengo la kuita wanafunzi ni kua kule mnakua mnafundishwa. Kwa huku Zanzibar wafungwa wanafundishwa kulima, kujenga, kazi zaseremala na inategemea na wewe interest yako.
Atuongoze Bara kwa Sheria na taratibu zake. Vinginevyo na Sisi Bara tuwe na haki ya kugombea urais Zanzibar ili nasi tulete huko ya Kibara. Nchi hizi mbili ni tofauti kabisa na ninashangaa ni kwa nini turuhusu upande mmoja uwe unaweza pia kuongoza upande wa Nchi nyingine. Tunahitaji katiba mpya na Muungano ufumuliwe ili tuuweke Sawa tuje na Muungano ambao unayo mambo machache ya kushirikiana kama yapo.
Unaona sasa mnataka kudhalilisha uanafunzi Bara. Yaani haiwezekani kabisa Mwanafunzi wa shule awe na jina la Mfungwa wa aliyembaka. Samahani Sana kama ninakuudhi Ila pia huoni Hilo jina mnaita Wafungwa Zanzibar ndiyo maana hata Kielimu matokeo yakitoka hamuwezi kabisa kuuifikia Bara? Kwa kuwa tayari Wanafunzi wenu Zanzibar ni Wafungwa kisaikolojia inaathiri mno. Badilisheni Hilo jina waitwe tu jina lingine lakini siyo Wanafunzi. Chondechonde isije Bara hii kitu ibaki Zanzibar.
 
Yaani Mtu Kaiba na Kaua au amesababisha Hatari Kubwa ama katika Jamii au Nchi halafu akihukumiwa na Mahakama kwenda Jela Kisheria asiitwe tena Mfungwa na sasa aitwe Mwanafunzi?

Kwahiyo Mbakaji awe anaitwa Mwanafunzi Mbakaji, Muuaji nae awe anaitwa Mwanafunzi Muuaji huku Jambazi nae awe anaitwa Mwanafunzi Jambazi?

Hivi ni kwanini Viongozi huwa mnapenda Kukurupuka hasa katika Fikra na Matamko? Sasa Mhalifu leo hii akiitwa Mwanafunzi nini Hadhi tena ya Mwanafunzi hapo? Yaani leo hii Rais Samia hujui kuwa neno Mwanafunzi lina Hadhi Kubwa mno Kitaaluma na kwamba leo kutaka Kwako Kushauri kuwa hata hawa Wahalifu wa Kisheria ( Wafungwa ) nao waanze Kuitwa Wanafunzi ni Kuwadhalilisha Wanafunzi na hata Wanataaluma Wote?

Na kwa jinsi Mamlaka husika za Tanzania na Watu wanavyopenda Kujipendekeza Kwako nina uhakika huu Ushauri wako wataupokea bila ya hata Kuutathmini na Kuuchambua Kimantiki ( Logically ) kisha wataweka Pamba katika Masikio yao na Kuukubali ( Kukukubalia ) ili mradi tu uone Unanyenyekewa huku Mioyoni mwao wakiwa Wanakusanifu na pengine hata Kukudharau.

Rais Samia leo ( tena mapema tu hivi ) Mimi GENTAMYCINE naukataa wazi wazi hapa huu Ushauri wako ( Pendekezo lako ) kuwa kuanzia sasa Wafungwa wawe Wanaitwa jina la Wanafunzi bali kwa dhana ya Kujenga, Kudhibiti na hata kutoa Fundisho kwa Wengine waendelee tu kuitwa Wafungwa hivyo hivyo na kama hilo Jina wakiona linawakera basi waachane na Vitendo vyao vya Uhalifu katika Jamii.

Yaani Raia ( tena Amiri Jeshi Mkuu ) kabisa badala ya kuwa Mkali na Kuchukia Vitendo vya Kiuhalifu, Kuvikemea na kuonyesha kuwa huvitaki na huvipendi Wewe bila hata haya ( aibu ) kama Rais unakuja na Hoja Nyepesi ya kutaka wasiitwe tena Wafungwa bali waitwe Wanafunzi?

Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu na hata Taasisi Nyeti hebu jitahidini sana Kumjenga Mama hasa katika yale ambayo anataka Kuyasema kwani ni kama naanza kuona Rais Samia huwa anatoa Kauli zake kwa Kukurupuka na Kimihemko zaidi hali ambayo inaweza sasa Kumfanya aanze Kudharaulika na hata Kuonekana Kituko na wale Waliobarikiwa Ubongo mzuri ( Akili Kubwa ) na Mwenyezi Mungu.

Nitawadharau mno Wanasheria ( ambao nawaheshimu sana ), nitawadharau mno BAKITA na nitamdharau zaidi Jaji Mkuu wa Tanzania ( ambaye namheshimu kutokana na kuwa na Akili sana na pia Poti wangu kutoka Mkoani Mara ) na nitamdharau kuliko Maelezo Waziri na Wizara husika kama Wote hawa kwa pamoja wataukubali huu Ushauri mwepesi na hafifu wa Rais Samia kuwa kuanzia sasa Wafungwa wawe Wanaitwa Wanafunzi.

Kwa wale mnaotaka kujua zaidi juu ya Ushauri huu mwepesi na hafifu alioutoa ( alioupendekeza ) Rais Samia nendeni ITV Tanzania mtaukuta huko na Mimi huku sasa nikiendelea tu Kuwakumbuka Marais wangu makini na Werevu ( Intelligent ) kuwahi kutokea nchini Tanzania Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Hayati Benjamin William Mkapa na Hayati Rais Dkt. John Pombe Magufuli na sishangai ndiyo maana kila mara GENTAMYCINE huwa si tu nawakumbuka bali hata huwa nawalilia huku nikiionea Huruma Tanzania yangu inakoelekea.
Mambo ya nchi hii!! Tutafika mbinguni tumechoka sana!![emoji1732][emoji1732]
 
Huku Zanzibar ndo tunavowaita. Na ukifungwa unaambia utaenda chuo cha mafunzo kwa muda wa miezi 6, yaani utakua gerezani kwa miezi 6. Lengo la kuita wanafunzi ni kua kule mnakua mnafundishwa. Kwa huku Zanzibar wafungwa wanafundishwa kulima, kujenga, kazi zaseremala na inategemea na wewe interest yako.
Vipi kwa wale wanaofungwa kifungo Cha maisha jela au kunyongwa,nao wanajifunza nini Cha kuwasaidia maishani mwao??.

Sent from my Infinix X688C using JamiiForums mobile app
 
Vipi kwa wale wanaofungwa kifungo Cha maisha jela au kunyongwa,nao wanajifunza nini Cha kuwasaidia maishani mwao??.

Sent from my Infinix X688C using JamiiForums mobile app
Kuna kitu kinaitwa confession, ukishakiri ndani ya maisha yako basi utaenda kwa amani. Wanapewa mafunzo ili wakiri makosa yao na wakifa wafe kwa amani
 
Atuongoze Bara kwa Sheria na taratibu zake. Vinginevyo na Sisi Bara tuwe na haki ya kugombea urais Zanzibar ili nasi tulete huko ya Kibara. Nchi hizi mbili ni tofauti kabisa na ninashangaa ni kwa nini turuhusu upande mmoja uwe unaweza pia kuongoza upande wa Nchi nyingine. Tunahitaji katiba mpya na Muungano ufumuliwe ili tuuweke Sawa tuje na Muungano ambao unayo mambo machache ya kushirikiana kama yapo.
Unaona sasa mnataka kudhalilisha uanafunzi Bara. Yaani haiwezekani kabisa Mwanafunzi wa shule awe na jina la Mfungwa wa aliyembaka. Samahani Sana kama ninakuudhi Ila pia huoni Hilo jina mnaita Wafungwa Zanzibar ndiyo maana hata Kielimu matokeo yakitoka hamuwezi kabisa kuuifikia Bara? Kwa kuwa tayari Wanafunzi wenu Zanzibar ni Wafungwa kisaikolojia inaathiri mno. Badilisheni Hilo jina waitwe tu jina lingine lakini siyo Wanafunzi. Chondechonde isije Bara hii kitu ibaki Zanzibar.

Suala la kugombea ni jambo la kikatiba, sifikirii kama hapa ni mahala pake na wala sisi hatuongelei katiba, na hata hiyo katiba ikifumuliwa usitegemee kama kuna kipengele cha Mtanganyika kugombea Zanzibar kitakuwepo. Hata hiyo katiba ya Warioba hicho kitu hakikukuwepo. In general suala la kuita wanafunzi kua wafungwa halihusiani pia na matokeo ya darasani. Wanafunzi wanafeli kwa sababu nyengine na hiyo haimo wala haijawahi kuwemo. Punguza povu
 
Suala la kugombea ni jambo la kikatiba, sifikirii kama hapa ni mahala pake na wala sisi hatuongelei katiba, na hata hiyo katiba ikifumuliwa usitegemee kama kuna kipengele cha Mtanganyika kugombea Zanzibar kitakuwepo. Hata hiyo katiba ya Warioba hicho kitu hakikukuwepo. In general suala la kuita wanafunzi kua wafungwa halihusiani pia na matokeo ya darasani. Wanafunzi wanafeli kwa sababu nyengine na hiyo haimo wala haijawahi kuwemo. Punguza povu
We jamaa ni mzanzibari nini [emoji41][emoji41][emoji41]





Ova.
 
Kuna kitu kinaitwa confession, ukishakiri ndani ya maisha yako basi utaenda kwa amani. Wanapewa mafunzo ili wakiri makosa yao na wakifa wafe kwa amani
Km ni hivyo,kwani hiyo confession hawawezi kuifanya wakiwa mtaani??.Je,Una uhakika kuwa Kwa kuwapa adhabu hiyo ndio wanafanya hiyo confession?.

Sent from my Infinix X688C using JamiiForums mobile app
 
Km ni hivyo,kwani hiyo confession hawawezi kuifanya wakiwa mtaani??.Je,Una uhakika kuwa Kwa kuwapa adhabu hiyo ndio wanafanya hiyo confession?.

Sent from my Infinix X688C using JamiiForums mobile app
Mtaai ndiko kulikokufanya ukafanya uovu, kama ungekua na uwezo wa kufanya mtaani ungekua mwema. Wala hawapewi adhabu bali wanafundishwa ndiyo maana huwakuti wafungwa wa kisiasa wakafanyishwa kazi ngumu. Wao wanakua wanazuiliwa tu.
 
Unataka tupoteze nguvu kazi ya taifa kwa watu ambao tayar wameshakufa na kubakwa hao Ni wanafunzi waelimishwe namna ya kuishi baadae warudi uraiani wajenge taifa
 
Yaani Mtu Kaiba na Kaua au amesababisha Hatari Kubwa ama katika Jamii au Nchi halafu akihukumiwa na Mahakama kwenda Jela Kisheria asiitwe tena Mfungwa na sasa aitwe Mwanafunzi?

Kwahiyo Mbakaji awe anaitwa Mwanafunzi Mbakaji, Muuaji nae awe anaitwa Mwanafunzi Muuaji huku Jambazi nae awe anaitwa Mwanafunzi Jambazi?

Hivi ni kwanini Viongozi huwa mnapenda Kukurupuka hasa katika Fikra na Matamko? Sasa Mhalifu leo hii akiitwa Mwanafunzi nini Hadhi tena ya Mwanafunzi hapo? Yaani leo hii Rais Samia hujui kuwa neno Mwanafunzi lina Hadhi Kubwa mno Kitaaluma na kwamba leo kutaka Kwako Kushauri kuwa hata hawa Wahalifu wa Kisheria ( Wafungwa ) nao waanze Kuitwa Wanafunzi ni Kuwadhalilisha Wanafunzi na hata Wanataaluma Wote?

Na kwa jinsi Mamlaka husika za Tanzania na Watu wanavyopenda Kujipendekeza Kwako nina uhakika huu Ushauri wako wataupokea bila ya hata Kuutathmini na Kuuchambua Kimantiki ( Logically ) kisha wataweka Pamba katika Masikio yao na Kuukubali ( Kukukubalia ) ili mradi tu uone Unanyenyekewa huku Mioyoni mwao wakiwa Wanakusanifu na pengine hata Kukudharau.

Rais Samia leo ( tena mapema tu hivi ) Mimi GENTAMYCINE naukataa wazi wazi hapa huu Ushauri wako ( Pendekezo lako ) kuwa kuanzia sasa Wafungwa wawe Wanaitwa jina la Wanafunzi bali kwa dhana ya Kujenga, Kudhibiti na hata kutoa Fundisho kwa Wengine waendelee tu kuitwa Wafungwa hivyo hivyo na kama hilo Jina wakiona linawakera basi waachane na Vitendo vyao vya Uhalifu katika Jamii.

Yaani Raia ( tena Amiri Jeshi Mkuu ) kabisa badala ya kuwa Mkali na Kuchukia Vitendo vya Kiuhalifu, Kuvikemea na kuonyesha kuwa huvitaki na huvipendi Wewe bila hata haya ( aibu ) kama Rais unakuja na Hoja Nyepesi ya kutaka wasiitwe tena Wafungwa bali waitwe Wanafunzi?

Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu na hata Taasisi Nyeti hebu jitahidini sana Kumjenga Mama hasa katika yale ambayo anataka Kuyasema kwani ni kama naanza kuona Rais Samia huwa anatoa Kauli zake kwa Kukurupuka na Kimihemko zaidi hali ambayo inaweza sasa Kumfanya aanze Kudharaulika na hata Kuonekana Kituko na wale Waliobarikiwa Ubongo mzuri ( Akili Kubwa ) na Mwenyezi Mungu.

Nitawadharau mno Wanasheria ( ambao nawaheshimu sana ), nitawadharau mno BAKITA na nitamdharau zaidi Jaji Mkuu wa Tanzania ( ambaye namheshimu kutokana na kuwa na Akili sana na pia Poti wangu kutoka Mkoani Mara ) na nitamdharau kuliko Maelezo Waziri na Wizara husika kama Wote hawa kwa pamoja wataukubali huu Ushauri mwepesi na hafifu wa Rais Samia kuwa kuanzia sasa Wafungwa wawe Wanaitwa Wanafunzi.

Kwa wale mnaotaka kujua zaidi juu ya Ushauri huu mwepesi na hafifu alioutoa ( alioupendekeza ) Rais Samia nendeni ITV Tanzania mtaukuta huko na Mimi huku sasa nikiendelea tu Kuwakumbuka Marais wangu makini na Werevu ( Intelligent ) kuwahi kutokea nchini Tanzania Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, Hayati Benjamin William Mkapa na Hayati Rais Dkt. John Pombe Magufuli na sishangai ndiyo maana kila mara GENTAMYCINE huwa si tu nawakumbuka bali hata huwa nawalilia huku nikiionea Huruma Tanzania yangu inakoelekea.
Ameingiza tamaduni ya kizanzibar Bara,huku ni kujitafutia mgogoro wa bure.
 
Back
Top Bottom