Rais Samia, suala la Machinga kuwa nalo makini. Usije ukajichanganya

Rais Samia, suala la Machinga kuwa nalo makini. Usije ukajichanganya

CCM ya mwendaze isilete chokochoko awamu yao ishakwenda na maji tupo awamu ya sita ya Mama yetu!! Hateki wala hauwi mtu for yor info....msimdanganye maza mapemaa hivi aanze vita na wamachinga..mshindwee!! Mbona wakati baba yenu yupo hamkuviondoa??
Kuna watu wanataka mama aingie kwwnye mgogoro na wamachinga.

Akifanya hivyo atapelekea social unrest ya kutisha.

Nimkumbushe Rais Samia kuwa Magufuli alikuwa very popular mwaka 2016 mpaka pale alipoanza kuvuruga maisha ya watu kama vile kuvunja nyumba za wananchi wa Kimara-Mbezi kiuonevu, hapo ndipo alipoanza kupoteza sapoti kubwa aliyokuwa nayo hadi kufikia kutumia njia za kimafia kurudisha sapoti.

Sasa Samia moment yake ya U turn ya kupoteza Uungwaji mkono nchini inaweza kuwa ni namna atakavyodeal na wamachinga. Akitumia miguvu bila akili serikali yake ikachukiwa atajikuta kwenye hali ngumu sana ya kiuongozi nchini!
 
Siwasemi vibaya wamachinga, sijui tatizo ni wapi? Kuna mji mmoja hapa nchini, sasa hivi wamachinga wanajenga mabanda mpaka kwenye kona za barabara. Sasa ukiwa unaingia mainroad kwa baiskeli, pikipik, au gari hauoni kushoto na kulia. Ni hatari sana.
 
Unatakiwa ufikiri kwa usahihi,na pia uwe na uwezo wa kuchakata na kupambanua ipi kweli na ipi sio,wewe unaakili tofauti na mnyama km mbwa,ni kweli mbwa anaweza kufundishwa na KUELEWA,lkn uwezo wake unakomea kwenye kukalili tu,hana uwezo wa kutafakari,kuchambua wala kufikiri,na wewe inaonekana umekalilishwa,jifunze kutafakari,
Nijifunze kutafakari kwa utashi wako ama?
 
Sidhani kama wanavunjiwa tu bila kupatiwa eneo la kwenda. Kikubwa wapangiwe maeneo maalumu ya biashara zao, na serikali ichukue jukumu la kuweka mazingira hayo sawa kibiashara kwa Wamachinga.
Niliwahi kuhoji kwenye uzi mmoja wapo humu kuhusu hawa Wamachinga.

Hivi ufumbuzi ni kupangiwa tu eneo lingine au pia ni kuona ni kwa jinsi gani watakutana na Wateja?...mbona tunakuwa na Vichwa vinavyopenda kutafuta ufumbuzi rahisi?.

Kama Serikali imeajiri Watu kwa taaluma zao na inawalipa kila mwezi nadhani wana jukumu la kutafuta ufumbuzi sahihi na si shortcut ya kuwaambia tu nendeni kule.

Serikali za miji ziumize vichwa namna ya kutengeneza maeneo mapya yenye kuwakutanisha Wauzaji na Wapita njia/Wanunuzi.
 
Niliwahi kuhoji kwenye uzi mmoja wapo humu kuhusu hawa Wamachinga.

Hivi ufumbuzi ni kupangiwa tu eneo lingine au pia ni kuona ni kwa jinsi gani watakutana na Wateja?...mbona tunakuwa na Vichwa vinavyopenda kutafuta ufumbuzi rahisi?.

Kama Serikali imeajiri Watu kwa taaluma zao na inawalipa kila mwezi nadhani wana jukumu la kutafuta ufumbuzi sahihi na si shortcut ya kuwaambia tu nendeni kule.

Serikali za miji ziumize vichwa namna ya kutengeneza maeneo mapya yenye kuwakutanisha Wauzaji na Wapita njia/Wanunuzi.
Yaap,sihitaji kujua elimu yako,hili andiko fupi limedhibitisha uwezo wako kiakili,big up
 
Sio kwa utashi wangu,bali kwa uharisia wake,kile unachopost kinaonyesha umbirikimo wa fikra,unatafakuri yenye matege,ustawi wa mtu kiakili,hupimwa na kile anaongea,

Kwa vyovyote vile ww lazima utakuwa ni mzee, japo umejiunga hapa jukwaani mwaka jana mwishoni. Sioni kama una hoja zozote za msingi zaidi ya kuleta mitazamo mfu, kisha kutaka kila mtu aone una jipya. Katafute wazee wenzio mzungumze mitazamo ya ujamaa uchwara, na nidhamu za kinafiki+ uoga.
 
Mama asiangalie Nyani usoni linapokuja swala la Sheria, au swala la Machinga lipelekwe Bungeni watungiwe sheria ya kujenga mabanda yao pembezoni mwa Barabara, ili sisi madereva tukiwapitia lisiwe kosa letu.
 
Uchumi wa nchi haukuzwi kwa umachinga bali kupitia uzalishaji. Machinga ni wachuuzi yaani ni madalali wa viwanda vya china kwa nia ya kukuza uchumi wa china.97% za wauzavyo machinga ni made in China.

Ukiboresha kilimo wote wakiingia kwenye uzalishaji badala ya uchuuzi uchumi utakua.

Niliwahi kuandika uzi humu wa Jamhuri ya wachuuzi watu wakanipinga.
 
Kwa vyovyote vile ww lazima utakuwa ni mzee, japo umejiunga hapa jukwaani mwaka jana mwishoni. Sioni kama una hoja zozote za msingi zaidi ya kuleta mitazamo mfu, kisha kutaka kila mtu aone una jipya. Katafute wazee wenzio mzungumze mitazamo ya ujamaa uchwara, na nidhamu za kinafiki+ uoga.
Unaona jinsi ulivyompiga ramli?!, unazidi kudhihirisha ulivyo na fikra fyongo na akili zenye matege,hoja ya uzee imetoka wapi lofa wewe,jadili kwa fikra pana,jamii foramu ni jiko au tanuru la kupika na kuchochea fikra na mitizamo yenye masirahi ya nchi,sio wewe unaeongozwa na chuki za kijinga na kimaskini,,
 
Unaona jinsi ulivyompiga ramli?!, unazidi kudhihirisha ulivyo na fikra fyongo na akili zenye matege,hoja ya uzee imetoka wapi lofa wewe,jadili kwa fikra pana,jamii foramu ni jiko au tanuru la kupika na kuchochea fikra na mitizamo yenye masirahi ya nchi,sio wewe unaeongozwa na chuki za kijinga na kimaskini,,

Nasema hivi, ww ni mzee na huna lolote jipya zaidi ya nidhamu za kinafiki. Ungekuwa na hoja ungeziweka hapa tuzione, na sio kupangia wanaume cha kujadili. Kama umekuja na marking scheme humu ndani basi umepotea njia, rudi kwenye vijiwe vya mapeasant wenzio mkapigiame zile story outdated.
 
Endeleeni kuvuruga tu shauri lenu, mtu kafa lakini kutwa mnateseka naye. Kwanini mnapambana na kivuli cha marehemu angali mlikuwa naye na mkafyata mikia? Sahivi mko huru sana mie nawashauri tu fanyeni kila mnachotaka make mda mnao na uwezo pia. Na mkiona vipi tumieni hata risasi
 
Nasema hivi, ww ni mzee na huna lolote jipya zaidi ya nidhamu za kinafiki. Ungekuwa na hoja ungeziweka hapa tuzione, na sio kupangia wanaume cha kujadili. Kama umekuja na marking scheme humu ndani basi umepotea njia, rudi kwenye vijiwe vya mapeasant wenzio mkapigiame zile story outdated.
Ahsante kwa kutambua kuwa mimi Nina nidhamu ,kuliko wewe ambae huna nidhamu,unaonyesha huna nidhamu hata kwa wazazi wako,tunajadili juu ya machinga,wewe unaleta hoja za mtu alietangulia mbele ya haki,kama nchi,tunaowajibu wa kulinda ustawi wa miji yetu,na ustawi wa machinga,hii nchi si ya matajiri tu,kila mtu ni lazima afurahie matunda ya uhuru wa nchi yake,
 
Ndugu Rais,

Hili suala la wamachinga ni very sensitive nakushauri uende nalo kwa busara kubwa sana.

Nadhani uliona maelfu ya waliotoka mabarabarani kumlilia Magufuli, naweza kusema probably kuwa zaidi ya 70% ni Wamachinga.

Hili ni jeshi kubwa sana ambalo ukilizingua litakuzingua kweli.

Pamoja na mapungufu mengi tu ya mtangulizi wako katika masuala ya uongozi lakini katika vitu alivyotumia akili ni namna ya kudeal na wamachinga. Baada ya mtangulizi wako kugundua kuwa hakubaliki katika cadre ya wasomi na wafanyabiashara wakubwa, aliamua kurudi chini kwenye grassroots na kufanya urafiki na wamachinga. Hawa ndo waliomzika!

Pia tambua kuwa nchi hii ina tatizo kubwa la ajira, shukuru Mungu kuwa kuna namna japo haipendezi ambayo mamilioni ya wananchi wanajipatia riziki yao. Tafadhali usianze kuwadisturb hawa wamachinga, utapata tabu sana kutawala kama kundi hili la mamilioni litakukataa. Na utapata wakati mgumu zaidi wakitokea watu wa kuwasongesha mtaani.

Pia fahamu kuwa kitendo cha kundi hili kuweza kujipatia riziki kulipunguza sana wimbi la ujambazi mitaani. Chondechonde nakuomba Ndugu Samia, usidisturb kabisa kundi hili bali litafutie utaratibu mzuri wa biashara zao bila kuwaswaga ghafla.

Ndugu, Rais ukivunja vibanda vya wamachinga leo, sisi wenye kipato tutakushangilia, lakini kabla hujafanya hilo jiulize hawa wanaopata rizki kutokana na hivyo vibanda wakale wapi?

Ndugu Rais, naongea haya nikiwa mtu ninayependa miji iwe safi kweli, lakini sasa Wenzetu hawa wanahitaji nao mkono kwenda kinywani tufanyeje?

Angalia dissatisfaction isije ikawa kubwa sana mtaani utapata tabu sana kutawala nchi hii.

Ni lazima uendelee kujali watu masikini bila kuumiza Matajiri, Ukiigeuza serikali yako kuwa ya Matajiri na wenye kipato tu bila kuwaangalia walalahoi utafeli

Kuwa Makini sana!
Ni kweli wako wengi na ni time bomb, ila lazima sheria ziheshimiwe. Waliziweka wenyewe na mji kwa kweli ni mchafu sana sana. Hawa watu hawana leseni na hawalipi kodi. Iweje serikali idai kodi kwa wafanya biashara wakubwa na inawalea machinga ambao wamewabana wafanyabiashara wakubwa hata hawafanyi biashara vizuri? Mkuu kama vile wewe na mimi tunatii sheria hilo kundi nalo lazima litii sheria za nchi. Mwenda zake alikuwa na yake tu alivyokuwa anawaacha. Na kama unakumbuka vizuri hili suala la kuwaacha machinga lilianzia mwanza. Aliwatetea wale wasukuma wasivunjiwe na ndipo ikabidi afumbe macho nchi nzima maana alitengeneza precedent!!!
 
Wanaotaka wamachinga waondolewe mabarabarani, leteni suluhisho,wapelekwe wapi?

Hizo sehemu mnazotaka wapelekwe zipo za kutosha?.

Suala la wamachinga halina short term solution, Ufumbuzi wake ni mipango ya muda mrefu ambayo lazima itengewe bajeti.

Sanasana tumwambie mama aliweke hil suala katika ajenda yake, lakini tusimshauri akurupuke aende akawapige virungu awaondoe wamachinga bila kuwa na sehemu za kutosha za kuwaweka!
Kweli magufuli alitutegea bomu!! Sasa hivi tunaogopa hata kulisogelea hilo bomu! Missile of the Nation anashauri hili bomu tuliache tu likae kwa kuwa limetegwa mahali pabaya mno!! Swali ni je tutaliacha hadi lini? Hadi litakapokuwa hatari zaidi? Hadi tutakapolazimika kujenga daraja juu ya bomu hili? Au tutumie ile dhana ya nerd immunity dhidi ya bomu? Bomu halina cha immunity wala chanjo wakuu! Bomu ni la kuteguliwa tu,kama kutakuwa na collaterral demage naamini zitakuwa well calculated,well controlled etc!! Mama ameamua kutegua bomu! Tumuunge mkono,asante
 
Mleta Mada amenena wazi kabisa, maana asilimia kubwa ya waishio mijini shughuli zao ni biashara ndogondogo, ambazo lazima zitengenezewe mazingira mazuri kwa ustawi wa Taifa letu.
Kabla ya kuchafua mji walikuwa wapi? Sheria za nchi lazima zifuatwe na mji wetu lazima upendenze na uwe safi siyo mpaka aje Obama ndiyo tuwafukuze kwa muda ili mji uwe safi. Kwanini waliwafukuza alipokuja Obama kama ni sawa wao kuwepo? Wageni wanashangaa sana jiji lilivyochafu. Hao watu kwanza haingizi chochote serikalini maana hata leseni hawana. Hiyo 20 wanayokata ni cha mtoto kwa biashara wanazofanya na huwa wanaazimana hizo kadi.
 
Ni kweli wako wengi na ni time bomb, ila lazima sheria ziheshimiwe. Waliziweka wenyewe na mji kwa kweli ni mchafu sana sana. Hawa watu hawana leseni na hawalipi kodi. Iweje serikali idai kodi kwa wafanya biashara wakubwa na inawalea machinga ambao wamewabana wafanyabiashara wakubwa hata hawafanyi biashara vizuri? Mkuu kama vile wewe na mimi tunatii sheria hilo kundi nalo lazima litii sheria za nchi. Mwenda zake alikuwa na yake tu alivyokuwa anawaacha. Na kama unakumbuka vizuri hili suala la kuwaacha machinga lilianzia mwanza. Aliwatetea wale wasukuma wasivunjiwe na ndipo ikabidi afumbe macho nchi nzima maana alitengeneza precedent!!!
Sijasema suala la wamachinga liachwe hivihivi bila kupatiwa ufumbuzi, bali ninasema lisiwe suala la vamia, piga, vunja bila kuwapa wamachinga alternative ya namna ya kuendesha shughuli zao.

Tukikurupuka kwenye hili, tutatengeneza bomu litakalotuvuruga vibaya sana!
 
Usijiangalie wewe tu
Angalia mamilioni ya watu nchini ambao kula, vaa, somesha watoto wao, matibabu ni kwa umachinga wao!

Sasa ni kweli,, wamejenga vibanda kila mahali hadi ikapelekea muonekano mbaya kabisa mijini, Lakini hawa wenzetu wamesaidiwa na serikali hiyohiyo kufanya hayo, tena walitozwa elfu ishirini ishirini ili waruhusiwe kufanya biashara katika mtindo huo.

Sasa busara, siyo kwenda kuwatoa kwenye maeneo waliyozoea kupata rizki zao kwa ghafla bin vuup, kwa kuwapiga n. k, Hapa inahitajika approach nzuri, tena siyo approach ya kukurupuka, ni iliyopangiliwa vizuri tena kwa phases. Nje ya hapo unataka watu wafe njaa au wageuke wapiga roba na majambazi
Hii mistake nilikuwa naifikiria mwisho wake utakuwaje na mbaya zaidi umefikia sehemu inakuwa ngumu kui control,hakika busara zaidi inahitajika kuli solve hili.
 
Back
Top Bottom