Rais Samia, suala la Machinga kuwa nalo makini. Usije ukajichanganya

Rais Samia, suala la Machinga kuwa nalo makini. Usije ukajichanganya

Hii mistake nilikuwa naifikiria mwisho wake utakuwaje na mbaya zaidi umefikia sehemu inakuwa ngumu kui control,hakika busara zaidi inahitajika kuli solve hili.
Ni rahisi tu,Lila kitongoji au Baathist ya mitaa, kama pale kariakoo mtaa wa Congo na mitaa mingine kama mitatu , kule temeke au Tandika chagua mitaa miwili mitatu funga weka wamachinga na hata mjini kati chagua mitaa miwili au mitatu hivi funga shughuli za magari ruhusu mtu yeyote mwenye chake akauze,

mbezi vilevile, kimara vile vile vile
Na mikoani iwe hivyo hivyo, baada ya hapo, piga marufuku maeneo mengine yote ambayo hayajaruhusiwa, hapo utakuwa umekomesha

nawasilisha, ni suala tu la wanaohusika kuumiza vichwa, hata ulaya kuna maeneo kama hayo, au kama inawezekana kuna watu wananchi maeneo makubwa ambapo wanaweza kuruhusiwa kuanzisha masoko binafsi na serikali ikala kodi yake.
 
Sheria na taratibu za mipango miji zilitingwa zanini kama suala la wamachinga linaleta kigigumizi,Hapo kabla hakukuwapo halaiki ya namna hii katika barabara.Magufuli aliiharibu nchi kila mahali huku akijinadi kutetea wanyonge.
 
Ahsante kwa kutambua kuwa mimi Nina nidhamu ,kuliko wewe ambae huna nidhamu,unaonyesha huna nidhamu hata kwa wazazi wako,tunajadili juu ya machinga,wewe unaleta hoja za mtu alietangulia mbele ya haki,kama nchi,tunaowajibu wa kulinda ustawi wa miji yetu,na ustawi wa machinga,hii nchi si ya matajiri tu,kila mtu ni lazima afurahie matunda ya uhuru wa nchi yake,
Huna nidhamu yoyote, bali ww ni mnafiki aliyepoteza ramani. Na kama unalazimisha kuwa nayo basi ni ya woga. Utajadili nini kama una element za unafiki zaidi ya kuwa bendera fuata upepo?
 
Niliwahi kuhoji kwenye uzi mmoja wapo humu kuhusu hawa Wamachinga.

Hivi ufumbuzi ni kupangiwa tu eneo lingine au pia ni kuona ni kwa jinsi gani watakutana na Wateja?...mbona tunakuwa na Vichwa vinavyopenda kutafuta ufumbuzi rahisi?.

Kama Serikali imeajiri Watu kwa taaluma zao na inawalipa kila mwezi nadhani wana jukumu la kutafuta ufumbuzi sahihi na si shortcut ya kuwaambia tu nendeni kule.

Serikali za miji ziumize vichwa namna ya kutengeneza maeneo mapya yenye kuwakutanisha Wauzaji na Wapita njia/Wanunuzi.
Hilo ndio jibu, wahamishwe baada ya mazingira ya kibiashara wanayopata sasa kuwekwa maeneo watakayopelekwa.
 
Hatuwezi kuacha kufuata utaratibu eti kwa kuogopa kundi kubwa hv umepita Kariakoo kuona jinsi kulivyo? Mtu anaweka meza kwenye barabara kabisa nenda mtaa wa Narung'ombe au Uhuru kajionee kulivyo.Lazima tuishi kwa kufuata utaratibu na sheria zipo sema Hayati alikuwa hafuati.Nenda Posta ndio balaa mibanda ya chuma kwenye mtaa hadi kero.Nenda Kigali kama utakuta uupuuzi uliopo Dar es salaam. Kwa walioko posta wametakiwa kuwa na miamvuli tuu na meza kama ilivyokuwa zamani.
 
Ndugu Rais,

Hili suala la wamachinga ni very sensitive nakushauri uende nalo kwa busara kubwa sana.

Nadhani uliona maelfu ya waliotoka mabarabarani kumlilia Magufuli, naweza kusema probably kuwa zaidi ya 70% ni Wamachinga.

Hili ni jeshi kubwa sana ambalo ukilizingua litakuzingua kweli.

Pamoja na mapungufu mengi tu ya mtangulizi wako katika masuala ya uongozi lakini katika vitu alivyotumia akili ni namna ya kudeal na wamachinga. Baada ya mtangulizi wako kugundua kuwa hakubaliki katika cadre ya wasomi na wafanyabiashara wakubwa, aliamua kurudi chini kwenye grassroots na kufanya urafiki na wamachinga. Hawa ndo waliomzika!

Pia tambua kuwa nchi hii ina tatizo kubwa la ajira, shukuru Mungu kuwa kuna namna japo haipendezi ambayo mamilioni ya wananchi wanajipatia riziki yao. Tafadhali usianze kuwadisturb hawa wamachinga, utapata tabu sana kutawala kama kundi hili la mamilioni litakukataa. Na utapata wakati mgumu zaidi wakitokea watu wa kuwasongesha mtaani.

Pia fahamu kuwa kitendo cha kundi hili kuweza kujipatia riziki kulipunguza sana wimbi la ujambazi mitaani. Chondechonde nakuomba Ndugu Samia, usidisturb kabisa kundi hili bali litafutie utaratibu mzuri wa biashara zao bila kuwaswaga ghafla.

Ndugu, Rais ukivunja vibanda vya wamachinga leo, sisi wenye kipato tutakushangilia, lakini kabla hujafanya hilo jiulize hawa wanaopata rizki kutokana na hivyo vibanda wakale wapi?

Ndugu Rais, naongea haya nikiwa mtu ninayependa miji iwe safi kweli, lakini sasa Wenzetu hawa wanahitaji nao mkono kwenda kinywani tufanyeje?

Angalia dissatisfaction isije ikawa kubwa sana mtaani utapata tabu sana kutawala nchi hii.

Ni lazima uendelee kujali watu masikini bila kuumiza Matajiri, Ukiigeuza serikali yako kuwa ya Matajiri na wenye kipato tu bila kuwaangalia walalahoi utafeli

Kuwa Makini sana!
Machinga walimzika wapi ?

Mimi niliona maaskofu na wanajeshi wakimzika
 
Well said mkuu.

Hapa New Bagamoyo RD Tangi Bovu hadi Shule kuna kipindi wanapanga matoroli yao kwenye packing ya daladala.

Nahisi kilichokosewa ni kuruhusiwa kufanya biashara bila kubugudhiwa na bila kupangiwa utaratibu. YES wafanye biashara bila kubugudhiwa ila viongozi wahusika wa Kata na Mtaa wawape namna nzuri ya kufanya biashara.

Ukiwa ni kujengewa vizimba au namna yoyote itakayoleta mazingira ya kupendeza badala ya kero. Mathalani Wizara ya viwanda na biashara waki team up na VETA wakatengeneza aina flani ya "street furniture" ambazo zitakua za chuma nadhani ingekua bomba sana
wameambiwa wawe na miamvuli na watoke kwenye njia za kwa waenda kwa miguu,nimesikia Posta gari la jiji likiwatangazia wamepewa mpaka tarehe 18/5
 
Wakikurupuka hili zoezi litasababisha vifo vingi kulikamilisha. Kumekuwa na uporaji toka upande wa serikali inaposimamia operesheni kama hizi. Sioni machinga wa kuvinjiwa banda lake na kuporwa mali zake akisema hewara.

Kunaweza kuwa na mapambano ya kutisha yatakayosababisha vifo vingi.
Wamepewa muda wa kuondoa hivyo vitu vyao kwa mjini maeneo ya Posta mpaka tarehe 18/5 wameondoa na wameambiwa kabisa wataboboa baada ya hapo.Sasa kama hujatoa kosa la nani?
 
Wanaotaka wamachinga waondolewe mabarabarani, leteni suluhisho,wapelekwe wapi?

Hizo sehemu mnazotaka wapelekwe zipo za kutosha?.

Suala la wamachinga halina short term solution, Ufumbuzi wake ni mipango ya muda mrefu ambayo lazima itengewe bajeti.

Sanasana tumwambie mama aliweke hil suala katika ajenda yake, lakini tusimshauri akurupuke aende akawapige virungu awaondoe wamachinga bila kuwa na sehemu za kutosha za kuwaweka!
Nenda machinga complex pale uone jengo linaishi panya tu na popo,,, hawa wamachinga hawataki kupelekwa maeneo special wao wanataka wapange bidhaa zao popote wanapojiskia ni majipu hao jamaa
 
Wanaotaka wamachinga waondolewe mabarabarani, leteni suluhisho,wapelekwe wapi?

Hizo sehemu mnazotaka wapelekwe zipo za kutosha?.

Suala la wamachinga halina short term solution, Ufumbuzi wake ni mipango ya muda mrefu ambayo lazima itengewe bajeti.

Sanasana tumwambie mama aliweke hil suala katika ajenda yake, lakini tusimshauri akurupuke aende akawapige virungu awaondoe wamachinga bila kuwa na sehemu za kutosha za kuwaweka!
Nenda machinga complex pale uone jengo linaishi panya tu na popo,,, hawa wamachinga hawataki kupelekwa maeneo special wao wanataka wapange bidhaa zao popote wanapojiskia ni majipu hao jamaa
 
Sidhani kama wanavunjiwa tu bila kupatiwa eneo la kwenda. Kikubwa wapangiwe maeneo maalumu ya biashara zao, na serikali ichukue jukumu la kuweka mazingira hayo sawa kibiashara kwa Wamachinga.
Wapangie sehemu pia wapelekewe na wateja maana wakipelekwa kisha wateja hakuna watarudi walipokuwa sasa hapo ndo kuna mbichi na mbivu,

Uwatoe kwa nguvu au uwaache waendwlee huku kule ulupoandaa napo ni hasara
 
Ndugu Rais,

Hili suala la wamachinga ni very sensitive nakushauri uende nalo kwa busara kubwa sana.

Nadhani uliona maelfu ya waliotoka mabarabarani kumlilia Magufuli, naweza kusema probably kuwa zaidi ya 70% ni Wamachinga.

Hili ni jeshi kubwa sana ambalo ukilizingua litakuzingua kweli.

Pamoja na mapungufu mengi tu ya mtangulizi wako katika masuala ya uongozi lakini katika vitu alivyotumia akili ni namna ya kudeal na wamachinga. Baada ya mtangulizi wako kugundua kuwa hakubaliki katika cadre ya wasomi na wafanyabiashara wakubwa, aliamua kurudi chini kwenye grassroots na kufanya urafiki na wamachinga. Hawa ndo waliomzika!

Pia tambua kuwa nchi hii ina tatizo kubwa la ajira, shukuru Mungu kuwa kuna namna japo haipendezi ambayo mamilioni ya wananchi wanajipatia riziki yao. Tafadhali usianze kuwadisturb hawa wamachinga, utapata tabu sana kutawala kama kundi hili la mamilioni litakukataa. Na utapata wakati mgumu zaidi wakitokea watu wa kuwasongesha mtaani.

Pia fahamu kuwa kitendo cha kundi hili kuweza kujipatia riziki kulipunguza sana wimbi la ujambazi mitaani. Chondechonde nakuomba Ndugu Samia, usidisturb kabisa kundi hili bali litafutie utaratibu mzuri wa biashara zao bila kuwaswaga ghafla.

Ndugu, Rais ukivunja vibanda vya wamachinga leo, sisi wenye kipato tutakushangilia, lakini kabla hujafanya hilo jiulize hawa wanaopata rizki kutokana na hivyo vibanda wakale wapi?

Ndugu Rais, naongea haya nikiwa mtu ninayependa miji iwe safi kweli, lakini sasa Wenzetu hawa wanahitaji nao mkono kwenda kinywani tufanyeje?

Angalia dissatisfaction isije ikawa kubwa sana mtaani utapata tabu sana kutawala nchi hii.

Ni lazima uendelee kujali watu masikini bila kuumiza Matajiri, Ukiigeuza serikali yako kuwa ya Matajiri na wenye kipato tu bila kuwaangalia walalahoi utafeli

Kuwa Makini sana!
Rais Obama wa Marekani alitawala vizuri sana baada ya kuwajali maskini kupitia "Obamacare". Ikiwezekana na Mama aanzishe "Suluhucare".
 
Tatizo kubwa n kwamba ss binadamu tukiambiwa kufuata utaratibu tunaona kama tunaonewa. Maeneo yametengwa lakin watu hawataki wako radhi waende maeneo ambayo yanaleta kero kwa wengine na wkuondolewa wanalilia kuonewa kitu ambacho sio kabsaa.
Siukahemee mlimani City shida nini wewe kenge
 
Rais Obama wa Marekani alitawala vizuri sana baada ya kuwajali maskini kupitia "Obamacare". Ikiwezekana na Mama aanzishe "Suluhucare".
Kabisa, katika watz 50m only 2m ndio wako kwenye formal employment, ukikubali wakuendeshe your finished, hawa machinga tunaweza wageuza furs na usiamini.

Mfano JK alikimbizana na wachimbaji wadogo, leo jpm kawageuza fursa kwa kurasimisha kazi zao, leo mapato ya wachimbaji wadogo yame supercede mapato ya utalii, hivi wasingekuwa wauza dhahabu na hii mikorona tungekuwa wapi?
 
Ndugu Rais,

Hili suala la wamachinga ni very sensitive nakushauri uende nalo kwa busara kubwa sana.

Nadhani uliona maelfu ya waliotoka mabarabarani kumlilia Magufuli, naweza kusema probably kuwa zaidi ya 70% ni Wamachinga.

Hili ni jeshi kubwa sana ambalo ukilizingua litakuzingua kweli.

Pamoja na mapungufu mengi tu ya mtangulizi wako katika masuala ya uongozi lakini katika vitu alivyotumia akili ni namna ya kudeal na wamachinga. Baada ya mtangulizi wako kugundua kuwa hakubaliki katika cadre ya wasomi na wafanyabiashara wakubwa, aliamua kurudi chini kwenye grassroots na kufanya urafiki na wamachinga. Hawa ndo waliomzika!

Pia tambua kuwa nchi hii ina tatizo kubwa la ajira, shukuru Mungu kuwa kuna namna japo haipendezi ambayo mamilioni ya wananchi wanajipatia riziki yao. Tafadhali usianze kuwadisturb hawa wamachinga, utapata tabu sana kutawala kama kundi hili la mamilioni litakukataa. Na utapata wakati mgumu zaidi wakitokea watu wa kuwasongesha mtaani.

Pia fahamu kuwa kitendo cha kundi hili kuweza kujipatia riziki kulipunguza sana wimbi la ujambazi mitaani. Chondechonde nakuomba Ndugu Samia, usidisturb kabisa kundi hili bali litafutie utaratibu mzuri wa biashara zao bila kuwaswaga ghafla.

Ndugu, Rais ukivunja vibanda vya wamachinga leo, sisi wenye kipato tutakushangilia, lakini kabla hujafanya hilo jiulize hawa wanaopata rizki kutokana na hivyo vibanda wakale wapi?

Ndugu Rais, naongea haya nikiwa mtu ninayependa miji iwe safi kweli, lakini sasa Wenzetu hawa wanahitaji nao mkono kwenda kinywani tufanyeje?

Angalia dissatisfaction isije ikawa kubwa sana mtaani utapata tabu sana kutawala nchi hii.

Ni lazima uendelee kujali watu masikini bila kuumiza Matajiri, Ukiigeuza serikali yako kuwa ya Matajiri na wenye kipato tu bila kuwaangalia walalahoi utafeli

Kuwa Makini sana!
Hili suala la wamachinga wako wanaomshauri vibaya Rais wetu...ni very sensitive...sisi wengine tuko nao na tunasikia wanachoongea...Sasa hivi wanaongea vibaya Sana...hatua zikichukuliwa za kuwafurusha mitaani Nina wasiwasi Yale ya Afrika Kusini yatakuwa Cha mtoto...kwa Hali ilivyo uchaguzi ukifanyika leo CCM itapata zaidi kidogo ya asilimia 50 kwa waliopiga kura...lakini wengi hawatapiga kura kwa kupoteza imani na CCM...JPM alikuwa mjanja kura zake nyingi zilikuwa za watu wa kawaida wakiwemo wamachinga....JPM alijitam bulisha na watu wa kawaida au wanyonge...Awamu Hii naona inataka kujitambulisha kwa makundi yote...ni sawa lakini kisiasa siyo sawa...wakwepa Kodi ni lazima washughulikiwe siyo kuwabembeleza. Watumbuaji ni lazima wachukuliwe hatua..mamilioni ya vijana wako mitaani hawana kazi...Kila mwaka vyuo vinatapika maelfu ya vijana mitaani...Mimi nimewaona baadhi ya vijana waliomaliza chuo kikuu wakiuza vocha mitaani na wengine wakiendesha bodaboda na Bajaj...ni hatari kubwa...
 
Sidhani kama wanavunjiwa tu bila kupatiwa eneo la kwenda. Kikubwa wapangiwe maeneo maalumu ya biashara zao, na serikali ichukue jukumu la kuweka mazingira hayo sawa kibiashara kwa Wamachinga.
Kwani juzi walikwisha waonesha pa kwenda? Ingekuwa hivyo unadhani jamaa aliye amua kudhalilika mbele ya watoto na watu wengine angefanya vile????
 
Back
Top Bottom