Rais Samia Suluhu akiendelea kumkumbatia Majaliwa na Baraza lake Serikali yake haitofanikiwa, Hawana jipya

Rais Samia Suluhu akiendelea kumkumbatia Majaliwa na Baraza lake Serikali yake haitofanikiwa, Hawana jipya

Quinine

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2010
Posts
22,227
Reaction score
49,628
Kila Rais huwa na Vision yake na ambitions zake, vision ya hayati Magufuli ilikuwa Tanzania ya viwanda ambayo ilishindwa chini ya uongozi wa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, sijajua vision ya rais mpya Mama Samia kuwa ni ile ile ya Tanzania ya viwanda au atakuja na nyingine au hana vision kabisa.

Mwelekeo wa uongozi wa Serikali ya mama Samia haujawa na sauti moja means mwelekeo mmoja, nafikiri hili linatokana na labda na mama Samia kutoonyesha msimamo wake.

Jana Waziri mkuu kaja na vipaumbele 6, kimojawapo ni ‘Hakuna kurudi nyuma’ means wanaendeleza ya mtangulizi kana kwamba Rais aliyepo hana vipaumbele vyake, huku Spika akisema hayati Magufuli alikuwa akishauriwa vibaya means tubadilike.

Mimi naona kama kuna mkakati wa makusudi wa kumkwamisha Rais Samia au kumlazimisha afate vision ya mtangulizi wake. Pamoja na kwamba alisema atayaenzi ya mtangulizi wake haina maana yeye hajui anataka Tanzania ya aina gani.

Mkapa alipoingia madarakani alisema atayaenzi ya muasisi wa Taifa Mwalimu Nyerere ‘yale mazuri’ lkn alikuja kubinafsisha mashirika ya umma kinyume na mwasisi wake tena Mwalimu angali akiwa hai.

Bila ya Rais Samia kuja na serikali yake iliyobeba maono yake itamuwia ngumu kuipeleka Tanzania aipendayo, kwa sababu baraza zima bado ni lilelile, linataka kuendeleza yaleyale maana yake ‘halina jipya’, Waziri mkuu bado ni yule yule aliye na vision ya Tanzania ya viwanda iliyoshindwa. Tutegemee miujiza.
 
'
20210414_085417.jpg
 
Kumbuka kilichopo mbele yao ni ilani ya uchaguzi 2020 - 2025.

Hope kutakuwa na review ya hapa na pale kuondoa ile ujeshi wa mtu mmoja.

Hotuba ya Magufuli ufunguzi bunge la pili ilitoa natumaini mazuri Sana. Ni vema yakakamilika ili na sir tuenjoy.

Kama hujaisoma nenda ukaisome.

Kama uliisoma juu juu kaisome Tena mara ya pili uielewe vema.
 
Kwani samia ametokana na serikali gani? Alikuwa anayahubiri ya nani? Amekabidhiwa ilani ipi? Amenadi sera zipi? MAJIBU YA HAYA MASWALI YATAKUFANYA UFIKIRI UPYA.
Sawa, kila Rais huwa na maono yake, utawala wa Kikwete na Magufuli ulikuwa tofauti kabisa pamoja na kutumia ilani ileile ya CCM.
 
Kila Rais huwa na Vision yake na ambitions zake, vision ya hayati Magufuli ilikuwa Tanzania ya viwanda ambayo ilishindwa chini ya uongozi wa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, sijajua vision ya rais mpya Mama Samia kuwa ni ile ile ya Tanzania ya viwanda au atakuja na nyingine au hana vision kabisa..
Isikupe wasiwasi. Huwezi tathmini dira na misimamo ya kiongozi ndani ya siku 25. Viongozi hupimwa kwa siku 100, 90 na hatimaye mwaka.

Hiyo hotuba ya Waziri Mkuu ilitayarishwa kuanzia Desemba 2020 na by Machi ilikuwa imekamilika. Asingeweza kubadili chochote kilichomo mule so soon.

Na kinachosomwa kwenye budget more or less ni ahadi tu siyo lazima kitekelezwe
 
Kila Rais huwa na Vision yake na ambitions zake, vision ya hayati Magufuli ilikuwa Tanzania ya viwanda ambayo ilishindwa chini ya uongozi wa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, sijajua vision ya rais mpya Mama Samia kuwa ni ile ile ya Tanzania ya viwanda au atakuja na nyingine au hana vision kabisa...
Muachage ujinga, Rais hana vipaumbele, kuna vipaumbele vya chama ambavyo ni ilani ilishinda baada ya kupigiwa kura na wananchi, mbona mnakuwa mapopoma, Samia ni Rais wa kurithi, hana ubavu wa atakavyo
 
Kimsingi kama ni kukwama tayari Magufuli alishakwamisha nchi, hao walioko sasa hawajui wafanyeje ili kuinasua nchi. Hapo ndio kila mtu anaongea lake ili ajaribu kunasua tulipokwama. Lakini nina uhakika kama mama hatambadili PM na waziri wa fedha, ataangoza kwa mitazamo ya kimagufuli ambapo atakwama zaidi.
 
Kila Rais huwa na Vision yake na ambitions zake, vision ya hayati Magufuli ilikuwa Tanzania ya viwanda ambayo ilishindwa chini ya uongozi wa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, sijajua vision ya rais mpya Mama Samia kuwa ni ile ile ya Tanzania ya viwanda au atakuja na nyingine au hana vision kabisa..
Upo sahihi kabisa lakini sidhani mama atakuwa halijui hilo
 
Wanamkwamisha kwenye nini?

Yeye kuna sehemu amekulalamikia kuwa anakwamishwa? Mazungumzo yake na Majaliwa unayajua? Unajuaje kama majaliwa anamkwamisha?

Tuache kuwa wapiga ramli na wasoma nyota, tumuache mama afanye anavyotaka. Tusimpangie watu wa kufana nao kazi. Yeye ni mtu mzima ana utashi wake.

Waganga njaa sasa mnataka kumpangia mama watu wa kufanya nae kazi.
 
Kila Rais huwa na Vision yake na ambitions zake, vision ya hayati Magufuli ilikuwa Tanzania ya viwanda ambayo ilishindwa chini ya uongozi wa Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, sijajua vision ya rais mpya Mama Samia kuwa ni ile ile ya Tanzania ya viwanda au atakuja na nyingine au hana vision kabisa...
Akili yako fupi mno mno pole sana.

Kasome ilani ya uchaguzi ya CCM.

Kazi zinazofanyika ni zile walizoahidi wakati wa kampeni ambazo Magu alishaanza.

Ama unataka maza aje na project zake ie Tanzania kwenda sayari ya Pluto?
 
Muachage ujinga, rais hana vipaumbele, kuna vipaumbele vya chama ambavyo ni ilani ilishinda baada ya kupigiwa kura na wananchi, mbona mnakuwa mapopoma, samia ni rais wa kurithi, hana ubavu wa atakavyo
Vision ni tofauti na vipaumbele ‘priorities’
 
Muachage ujinga, rais hana vipaumbele, kuna vipaumbele vya chama ambavyo ni ilani ilishinda baada ya kupigiwa kura na wananchi, mbona mnakuwa mapopoma, samia ni rais wa kurithi, hana ubavu wa atakavyo
Uko sahihi kabisa.

Hata Magufuli vipaumbele vyake aliviweka kwenye ilani ya chama.

Rais hana vipaumbele vyake bali ni vya chama.

Sasa watu wanajiropokea tu wakishakula wali maharage wakashiba.
 
Mpaka sasa, kitendo cha yeye Samia kutounda serikali yake hasa huko top..asitegemee mafanikio.

Hawa ni watubwaliokuwa poluted na mfumo wa magufuli ambao wengi wameupinga kwa nguvu.

Kujitofautisha hata kama naye alikuwepo,tunaelewa hakuwa na sauti wala mamlaka kwa bosi wake achilia mbali nafasi yenyewe kikatiba...ni hamna kitu..

Kama alivyofanya kwa katibu mkuu kiongozi alipaswa aende na mbio hizo kwa PM, mawaziri.
 
Back
Top Bottom