Rais Samia Suluhu ataruhusu maandamo yoyote ya wanaharakati, vyama vya upinzani na hata chama chake?

Rais Samia Suluhu ataruhusu maandamo yoyote ya wanaharakati, vyama vya upinzani na hata chama chake?

jitombashisho

JF-Expert Member
Joined
Jun 11, 2020
Posts
667
Reaction score
2,245
Hayati Magufuli alikomesha pasi na ajizi maandamo ya aina yoyote tofauti na mtangulizi wake Mzee JK.

Hoja yake kubwa Hayati Magufuli kuhusu kuzuia maandamo ilikuwa ni muda wa kufanya kazi na haukuwa muda wa kuandamana. Aliweza.

Ndipo kipindi ambacho kwa takribanI miaka mitano si wanavyuo, vyama vya upinzani na pia wanaharakati si tu hawakuthubutu kuandamana bali pia waliufyata kwa sababu JPM alitisha na alisimamia vyema kila alichokiamini.

Sasa basi, kipimo sahihi cha uungwana wa huyo mama hasa kwenu mnaomsifia upo hapo mtakeni awaruhusu japo muandae maandamo ya kumpongeza kwa kuruhusu wafanyabiashara wabembelezwe, kwa kuruhusu madini yachimbwe kwenye mbuga za hifadhi ya Taifa na zaidi amekubali kodi kwa maana ya makusanyo hata ya kipungua hakuna tatizo.
 
Hata asiporuhusu, sie tunachojua na kukifurahia ni Mungu kusikia dua zetu na kutufanyia wepesi kwa kutuletea mama atuongoze.
 
Suala la maandamano siyo mapenzi,hisani,kudra wala takwa la Rais.

Suala la maandamano ni haki yetu kikatiba.

Haki huwa haiombwi wala huwa haitolewi bure kama unavyodhania bwana mleta uzi bali haki huchukuliwa kwa nguvu.

Rais hana wajibu wala haki wala nguvu wala amri ya kuzuia au kuruhusu maandamano na pia hatuna haja wala wajibu wa kumuomba Rais aruhusu maandamano bali ni haki yetu na mtu yoyote yule ikiwa ni pamoja na Rais akituzuia tuna wajibu kikatiba wa kuchukua haki hiyo kwa nguvu.

Rais atake asitake suala la maandamano ni haki yetu kikatiba wala siyo mapenzi yake na asipotaka tuna wajibu kikatiba wa kumlazimisha.

Umeelewa mleta mada?
 
Suala la maandamano siyo mapenzi,hisani,kudra wala takwa la Rais.

Suala la maandamano ni haki yetu kikatiba.

Haki huwa haiombwi wala huwa haitolewi bure kama unavyodhania bwana mleta uzi bali haki huchukuliwa kwa nguvu.

Rais hana wajibu wala haki wala nguvu wala amri ya kuzuia au kuruhusu maandamano na pia hatuna haja wala wajibu wa kumuomba Rais aruhusu maandamano bali ni haki yetu na mtu yoyote yule ikiwa ni pamoja na Rais akituzuia tuna wajibu kikatiba wa kuchukua haki hiyo kwa nguvu.

Rais atake asitake suala maandamano ni haki yetu wala siyo mapenzi yake.

Umeelewa mleta mada?
...ulithubutu kuandamana miaka 5 iliyopita?
 
...ulithubutu kuandamana miaka 5 iliyopita?
Haki pamoja na juhudi za kudai haki zaweza kuchelewa kutokana na sababu kama vile kiwango cha elimu,level ya vitisho kutoka kwa watawala na kadhalika lakini kamwe haki hizo pamoja na juhudi za kudai haki hizo haziwezi kushindwa milele.Huwa ni suala la muda tu.Na hili linathibitishwa na ukweli kwamba tokea dunia iumbwe hakuna dikteta wala mminya haki ambae aliwahi kufanikiwa,wote huishia mwisho wenye aibu.
 
Hata asiporuhusu, sie tunachojua na kukifurahia ni Mungu kusikia dua zetu na kutufanyia wepesi kwa kutuletea mama atuongoze...
Kwa maelezo yako

Chanjo hujachanjwa
Nyungu hujapiga
Hujajifungia unaenda kazini kila siku


Mbona hujafa na corona sasa??
 
Tuliwapinga Makaburu wa Afrika kusini sio Kwasabubu ya Rangi zao bali ni Matendo yao ya kimyama na ukatili dhidi ya binadamu.

Hatawew ukiwa Mweusi kama sisi ukifanya Matendo yale yale kama Makaburu tutakupinga na kukuona ni kaburu tuu tofauti yenu ni Rangi tuu..
J.K.Nyerere (1926-2000)
 
Kwa maelezo yako

Chanjo hujachanjwa
Nyungu hujapiga
Hujajifungia unaenda kazini kila siku


Mbona hujafa na corona sasa??
Mbona kama unateseka?
Hapa mjadala ni maandamano...

Mambo ya sijui chanjo, nyungu, kujifungia na kufa yametoka wapi?

Endeleeni kuwa na subira, hii nchi ni yetu sote. Mwendazake kashaumaliza mwendo, wengine wamepokea kijiti..
 
Back
Top Bottom