Rais Samia Suluhu awasili Kenya, aweka kidole Mkataba wa Bomba la gesi Dar-Mombasa

Rais Samia Suluhu awasili Kenya, aweka kidole Mkataba wa Bomba la gesi Dar-Mombasa

Nipo hapa naangalia KTN kwenye kipindi (LEO MASHINANI) naona wameweka Kipindi cha ZIARA YA RAIS SAMIA.
Wanamponda sana Mwendazake na kumsifia Mama Samia.
Kenya Mwendazake hapendwi na mfumo,lakini walalahoi wanamkubali sana.
 
Yaani wamshukuru sana Mungu ,watu wazima wangeliadhirika, Uhuru Kenyata alicheka na kufurahi kindanindani mpaka mabega yakaanza kurukaruka kisa Rais Samia kalitamka neno,najiuliza mbona alipolitamka yeye Rais wetu Samia hakucheka.

Samia nae alijikaza kisabuni lakini alikuwa tiyari ameshachukuliwa na mkondo wa lile neno,akameza mate.

Sikucheka ila nimefurahi kuona Maraisi wetu wapendwa wamo ndani ya furaha ya pamoja,kama walikuwa maskani vile na mastori ya hapa na pale na kiswahili kikataka kuwaponza mbele ya kadamnasi,kweli yajayo yanafurahisha.
 
Neno gani? Mbususu ama!
Viongozi wenu wanapozungumza kwenye hotuba, mnatakiwa muwe watulivu sana sana, unasikiliza mstari baada ya mstari na ndio utaelewa kwa kina, na hata maneno yanayochomekewapia uyagundue, maana mengine yananogesha, nimeirudia na uona hata walinzi wa kike nao waliingia kwenye mkumbo kusikia lile neno, Kiswahili kina ufundi kukizungumza. Samia kweli nae alipigilia msumari kivyake.
 
Naona sasa ni mwendo wa kupukuchulia angani rasilimali za nchi yetu; sasa zile harakati za kupishana angani zinanyemelea baada ya kuzinduliwa rasmi pale kwa M7. Bi Mkubwa hasomeki, kurasa za hotuba na ahadi zake tifutifu & futefute zimefutika.

#Mtanikumbuka kwa mema, na wala si kwa mabaya.
Ntamkumbuka kwa mabaya tu hta iweje
 
Sogea Chato ukapalilie kaburi, acha kulialia.. Rais lazima azunguke kulitafutia taifa maendeleo.. sio kujifungia ndani kishamba na kukwapua hela za mifuko ya jamii na hela za wafanyabiashara wakubwa.
Tanzania sio kisiwa mama lazima atoke
 
Back
Top Bottom