Rais Samia tangaza kuruhusu Mikutano ya vyama vya siasa katika 'open ground', itakusaidia sana

Rais Samia tangaza kuruhusu Mikutano ya vyama vya siasa katika 'open ground', itakusaidia sana

Shocker

JF-Expert Member
Joined
Sep 15, 2012
Posts
1,958
Reaction score
3,890
Hakuna asiyejua kuwa mikutano hii ilipigwa ban kimagumashi na mapolisi kushikilia bango na bado haki hii kikatiba imebamizwa kwa visingizio hivi na vile.

Tunahitaji Rais Samia autangazie umma kuwa haki hii ipo wazi na vyama vifanye mikutano yake kwa raha mustarehe bila ya kubugudhiwa, tupo kwenye nchi huru, muhimu mipaka ya uhuru huo uzingatiwe kwa mujibu wa sheria.

Wananchi wanahitaji mihemko ya wakati ule wa mikutano nchi ilichangamka na wananchi kujiona wapo huru. Wananchi wengi ni wakulima inapokuwepo mikutano ya vyama vya siasa kunakuwepo na kama kasehemu cha kujiliwaza.

Tusikae kwenye nchi huru kama wafiwa mikutano huru ya kisiasa ni tochi kwa serikali iliyopo madarakani. Na bora pia nikiongezea katika kila Mkoa uwepo au iwepo sehemu ya kajiuwanja kadogo hapo paruhusiwe free speech za kisiasa kwa mtu yeyote yule aweze kusema yaliyo rohoni mwake bila ya kuguswa na sheria ya aina yeyote ile, mtu amalize joto lake hapo, ila inakuwa ni sehemu hio tu kama kwa kila mkoa au wilaya, aina hio huwa na kufanyika kwenye sehemu chaguliwa tu na ni tofauti na ile mikutano ya kichama. Nafikiri huko Ulaya zipo sehemu hizo.
 
Mikutano ya siasa sawa ila isiwe ya kutukana na kudhalilisha wengine kinyume cha sheria kutafuta political mileage. Kila uhuru una mipaka yake huo ndiyo ukweli. Mikutano yenye kuchochea mifarakano na isiyo na tija kiusalama wa nchi haifai iendelee kuzuiwa.
 
Mikutano ya siasa sawa ila isiwe ya kutukana na kudhalilisha wengine kinyume cha sheria kutafuta political mileage. Kila uhuru una mipaka yake huo ndiyo ukweli. Mikutano yenye kuchochea mifarakano na isiyo na tija kiusalama wa nchi haifai iendelee kuzuiwa.
Lini na wapi alitukanwa nani kwenye mikutano zaidi watu kwenye mikutano ya kisiasa watu huzungumza siyasa na mambo yahuyo siasa mwana siasa akisema mfano Magufuli kashindwa kuongoza kwenu linakua tusi?
 
Pia mama afahamu safu iliyomzunguka haimtakii mema.

Tunaona kwenye groups za WhatsApp viongozi wakubwa wa vyombo nyeti wakimteta vibaya wazi wazi, hawamwelewi kabisa na wanadiriki kuonesha hivyo publicly wakati enzi za mwendakuzimu hakuna aliyethubutu kufanya hivyo.

Mama ajue watu pekee watakaokuwa nae kipindi 'Wanyambilisi' wakimtingisha ni watanzania tu, nao ni kama tu akiwapatia katiba mpya!
 
Mikutano ya siasa sawa ila isiwe ya kutukana na kudhalilisha wengine kinyume cha sheria kutafuta political mileage. Kila uhuru una mipaka yake huo ndiyo ukweli. Mikutano yenye kuchochea mifarakano na isiyo na tija kiusalama wa nchi haifai iendelee kuzuiwa.
Hiyo ni mipaka feki maana matusi, kudhalilishana na kutishana kukifanywa na mwenye nguvu mnafumbia macho. Wengine wakirudia yale yale mnataka wachukuliwe hatua.

Amandla.....
 
Mnasifia Mama kushughulikia suala la Corona kisayansi ila hapo hapo mnataka mruhusiwe kukusanyana pasina ulazima, sasa hiyo social distance inapatikana vp? Mbona mnazidi kumuwekea ugumu Mama?
Chama chake hawakusanyani?

Amandla...
 
Wewe ni ngumbaru.Suala la mikutano ya kisiasa ni haki yetu kikatiba wala siyo hisani,takwa, au mapenzi ya Rais.Rais hana haki wala wajibu wala mamlaka ya kuruhusu au kuzuia mikutano ya kisiasa.

Pia Rais hana haki wala mamlaka ya kupanga mikutano ya kisiasa ifanyike lini na wapi.Vilaza kama ninyi mnaofikiri kuwa Rais yupo juu ya katiba ndiyo mnafanya Tanzania inazidi kubaki kuwa masikini japo tumepata uhuru miaka 60 iliyopita.
 
Wewe ni ngumbaru.Suala la mikutano ya kisiasa ni haki yetu kikatiba wala siyo hisani,takwa, au mapenzi ya Rais.Rais hana haki wala wajibu wala mamlaka ya kuruhusu au kuzuia mikutano ya kisiasa.

Pia Rais hana haki wala mamlaka ya kupanga mikutano ya kisiasa ifanyike lini na wapi.Vilaza kama ninyi mnaofikiri kuwa Rais yupo juu ya katiba ndiyo mnafanya Tanzania inazidi kubaki kuwa masikini japo tumepata uhuru miaka 60 iliyopita.
Pangupakavu punguza munkari,kikubwa atangaze tu ,katiba mtafuata nyinyi msioweza kuandamana,tunahitaji tamko la mkuu wa Nchi sio katiba,aafu mwalimu Nyerere alisema katiba sio msahafu kwa maana hio inabadilishika na magu aliibadili kwa kuzuia,ni wewe mwenyewe tu,utakavyoamua.

Siasa na matusi haviendani mbali,kuna ndani ya siasa kitu kinaitwa propaganda ni siasa lazima mengine wahusika wamezee,kisa cha Dr.Omar Ali Juma na Malimu Seif Sharifu Hamad ,Allah awasamehe madhambi yao,wote wameshatangulia kimati,hawa waliweza siasa kama utakumbuka ilifika Maalim kumwambia Dr.Omari anaenda kwa waganga na kukalia fenesi kisa Dr.alisema balahau huna chama.

Mwanasiasa ni lazima kuna mambo uyakubali ndio itakuwa umekamilika kisiasa yakiwemo hayo matusi,na ukitukanwa vyombo vya sheria vipo,ukiandikwa visivyo vyombo vipo tena unadai donge nono tu,tatizo lipo wapi.
 
Mikutano ya siasa sawa ila isiwe ya kutukana na kudhalilisha wengine kinyume cha sheria kutafuta political mileage. Kila uhuru una mipaka yake huo ndiyo ukweli. Mikutano yenye kuchochea mifarakano na isiyo na tija kiusalama wa nchi haifai iendelee kuzuiwa.
Ulidangaywa sana na mwendazake kwa sababu yeye alikua anaogopa challenge. Kwake zikizungumzwa hoja ambazo hawezi kuzijibu, alikimbilia kusema ni matusi. Amewaaminisha wenye uwezo mdogo wa kujenga hoja kwamba vyama vingine vilikua vinatukana na kusababisha vurugu ili ku justify uzuiaji mikutano huru ya kisiasa ambayo iko kikatiba, watu mkaamini. Mkuu ondoka huko kwenye mawazo mfu.
 
Ndio maana nikasema mnazidi kumuwekea ugumu, pengine sasa anafikiria kuzuia hiyo mikusanyiko ya chama chake ila nyie ndio kwanza mnakuja na ugumu zaidi.
Na kwa nini chama chake kilikua kikifanya siasa wakati vingine vikiwa vinaminywa?
 
Waruhusu tu ili uwajue mapema rangi yao halisi,maana sasa full kujipendekeza.
 
Mnasifia Mama kushughulikia suala la Corona kisayansi ila hapo hapo mnataka mruhusiwe kukusanyana pasina ulazima, sasa hiyo social distance inapatikana vp? Mbona mnazidi kumuwekea ugumu Mama?
Hawajielewi hao
 
Mdanganyeni afanye hvyo na mwaka 2025 kuwepo na uchaguzi huru nadhani ndo atakuwa Rais wa kwanza Tanzania kuhudumu miaka 4

Huyu mama hajulikani sana kwa wananchi wa kawaida(mitaani) kwani yupo kiofisi zaidi ndo maana inatumika nguvu kubwa kumpamba hana mvuto kwa wananchi wa kawaida kwani hawamjui support aliyonayo ni mitandaoni,wapinzani wa JPM,wanaharakati wenzake(NGOs) na baadhi ya na watu wachache ambao wanafaidika na mfumo wake lakini ukisema mitaani ni tofauti kabisa huyu mama hana tabia ya kuwa karibu na wananchi ambao wengi ndo wapiga kura , ndo maana mpk leo hakuna mkutano wowote aliofanya na wananchi zaidi ya vile vizee vya ccm na ambao haukuwa mkutano ilikuwa ni hotuba yake wazee wanamsikiliza

Mdanganyeni tu yeye akae ofisini watu waongee na wapiga kura uchaguzi huru then muone itakavyotokea .

Watanzania wengi wanachaguaga mtu wanaemjua si sera umaarufu wa Samia ni mitandaoni tu si mitaani au kwa wananchi wa kawaida kabisa
 
Back
Top Bottom