Rais Samia, tengua uteuzi wa Waziri Makamba na Bodi nzima ya TANESCO. Au na wewe una maslahi na kinachoendelea?

Rais Samia, tengua uteuzi wa Waziri Makamba na Bodi nzima ya TANESCO. Au na wewe una maslahi na kinachoendelea?

Makamba JR na bodi ndio wameleta ukame? Hivi ni chuki zinawasumbua au ni ni hasa?

In fact wapuuzi wa awamu ya 5 ndio wametufikisha hapa,haiwezekani unaweka pesa nyingi Kwenye mradi ambao haujui utaisha lini maana pesa za kuukamilisha huna na hujawekeza kujiandaa na hali ya dharura kama ukame huku ukitegegemea kudra za Mungu.Huu ni utaahira kabisa.
Na maji ya kujaza hilo libwawa lao sijui yatatoka wapi na haya mabadiliko ya tabia nchi yasiyotabirika
 
Ewaaaa...

Sasa hii timu mwendazake inadhani kutunbua ndio suluhisho la matatizo. Wametumbuliwa wangapi na bado tuko palepale

Tatizo ni watu walioamua kujipa madaraka uongozi wa nchi kwa.kutumia nguvu za dola.

Akili zilizoleta mharibiko ndio akili hizohizo eti zinataka kuondoa mharibiko na kuleta maendeleo

CCM yajenga nchi

Huwezi kupata majibu tofauti ya tatizo iwapo unatumia njia zile zile kulitatua!!!
 
Na maji ya kujaza hilo libwawa lao sijui yatatoka wapi na haya mabadiliko ya tabia nchi yasiyotabirika
Ndio mpaka Mungu apende.Lazima serikali iwe na umeme wa vyanzo ambavyo havitegemei Hali ya hewa hata pindi Bwawa likikamilika maana itafika mahali nalo litaathirika tuu regardless of how big is the dam..

Hilo Bwawa litakuwa na maana tuu kama kuna mvua kinyume chake ni useless.
 
Mkiambiwa jengeni uchumi na miundombinu imara mnaleta siasa zenu za wizi wa chaguzi na kuteuana, haya miaka zaidi ya sitini ya uhuru bado mnasumbuliwa na matatizo ya maji, umeme, madarasa, zahanati na vituo vya afya hadi mnakopea pesa.....hovyo kabisa.
 
Kwani washamba wako bado wapo madarakani?

Si chama kimerudi kwenye mikono salama?
Baraza la mawaziri la Magufuli bado lipo kwa zaidi 90%.Kwahiyo huwezi kuwaondoa kwenye lawama hizi.
 
Teuzi ya January Makamba imebuma mapema mno, unasubiri mambo yaharibike kwa kiwango gani ndio uchukue hatua?
Hivi jibu la utatuzi wa matatizo haya ni kutengua? Kwani ni lini mlimshauri Makamba J. abadili jambo fulani ili matatizo yaishe akakataa ushauri wenu huo? Kama una ushahidi mliwashuri wateuliwa hawa wabadili mambo ili maboresho yatekelezeke ulete hapa jamvini; kama hauna ushahidi huo, basi wakutenguliwa kwanza kabla ya wateuliwa ni wewe mleta mada!
 
Kauli yako, ya waziri mkuu na ya waziri January Makamba inaonyesha kuna udanganyifu mkubwa sana kwa mamlaka unaoendelea nchini.

Kauli zenu ndio zinafanya Watanzania watilie shaka weledi wenu kama viongozi wakuu wa nchi.

Teuzi ya January Makamba imebuma mapema mno, unasubiri mambo yaharibike kwa kiwango gani ndio uchukue hatua?

Sababu zote mlizozitoa zinatushangaza Watanzania, tena ni za gafla na kinzani.

Haiwezekani kuondoa wabobezi wa fani ya masuala ya umeme wote kwa mkupuo ukafanikiwa, never!

Hii teuzi ukiing'ang'ania itakuharibia kila jema uwazalo kwa Watanzania, hafai, lawama zote zitakuangukia wewe kiranja mkuu.

Ulisema, unasoma mitandaoni sana, kilio na mtazamo wa wananchi umeusikia, hivyo kwa sasa ni ngumu kwadanganya Watanzania.

Amua haraka kwa faida ya nchi, si dhambi kurekebisha kosa.
Huu ni mtihani mkubwa kwa Rais Samia S H. Ana uamuzi wakunyoa au kusuka. Atahuzunika sana baada ya uchaguzi wa 2025. Hata kama atapita, lakini ukweli katika masanduku ya kura ataambiwa na wapambe wake. Nia ni kumuonyesha jinsi walivyofanya kazi kubwa kumuokoa japo alikuwa anaanguka. Fadhila zitahitajika.

Huzuni kubwa zitampata Mama Samia.
 
Makamba ndiye kazuia mvua zisinyeshe? Ndiye amesababisha muwe wajinga na kutegemea chanzo cha umeme kimoja cha maji badala ya kugeukia njia mbadala (Gas)? Na kwa mabadiliko haya ya hali ya hewa hilo libwawa lenu mnalojenga bila akili litajaza matope na vyura tu...
kwa sasa kisingizio kimekua mvua akati tangu mwezi wa 9 alipoteuliwa kila siku umeme ulikatika na alipoulizwa sababu alidai repair, kama tatizo lilikua ukame why hakusema?
 
Makamba ndiye kazuia mvua zisinyeshe? Ndiye amesababisha muwe wajinga na kutegemea chanzo cha umeme kimoja cha maji badala ya kugeukia njia mbadala (Gas)? Na kwa mabadiliko haya ya hali ya hewa hilo libwawa lenu mnalojenga bila akili litajaza matope na vyura tu...
Hivi kwa plant ya uzalishaji umeme pale Kidatu, unasemaje maji yamepungua wakati mto Ruaha unaingia kila siku?
Watu wasiwe wanafiki. Wawe wawazi kama alivyokuwa JPM. Waseme kwamba wanatengeneza frasturation ya supply ili kutengeneza uhalali wa kuja na maamuzi yao.
 
Huu ni mtihani mkubwa kwa Rais Samia S H. Ana uamuzi wakunyoa au kusuka. Atahuzunika sana baada ya uchaguzi wa 2025. Hata kama atapita, lakini ukweli katika masanduku ya kura ataambiwa na wapambe wake. Nia ni kumuonyesha jinsi walivyofanya kazi kubwa kumuokoa japo alikuwa anaanguka. Fadhila zitahitajika.

Huzuni kubwa zitampata Mama Samia.
CCM haijawahi kushindwa
 
Kubebwa tu jina baba yake.
Tuambie hizo wizara alifanya kipi Cha maana?
"Kipi cha maana" unamaanisha nini? Una Mfano wowote kwenye wizara yeyote ambapo kimefanyika "kipi cha maana"? Kabebwe na wewe kama ni rahisi kubebwa
 
kwa sasa kisingizio kimekua mvua akati tangu mwezi wa 9 alipoteuliwa kila siku umeme ulikatika na alipoulizwa sababu alidai repair, kama tatizo lilikua ukame why hakusema?
Repair zimeanza kufanyika alipoingia, hata kwenye taarifa ya TANESCO ya jana wameelezea vituo ambavyo wanarepair ili kuongeza umeme kwenye grid ya taifa, then Ukame umeingilia hapa kati na kulifanya tatizo liwe worse! Inashangaza kidogo kumchukia mtu ambaye hata hamumfahamu zaidi ya kumuona kwenye TV na magazetini
 
Back
Top Bottom