Rais Samia: Tutaanza kutoa Tsh 10,000/= kwa siku kwenye pesa za kujikimu (Boom) kwa wanachuo

Rais Samia: Tutaanza kutoa Tsh 10,000/= kwa siku kwenye pesa za kujikimu (Boom) kwa wanachuo

Ndugu zangu watanzania,

Rais Samia Ambaye ndiye kiongozi mwenye ushawishi Zaid Barani Afirika kwa Sasa na ambaye hotuba zake zinatajwa kuwa Bora,zenye kugusa mioyo ya watu,zenye kuleta matumaini,zenye kuonyesha muelekeo na dira na ambazo zimekuwa zinafuatiliwa na watu wengi Sana Barani Afrika kutokana na maono yake makubwa ya Uzalendo na ambaye amekuwa akichukuliwa Kama mtetezi wa Afrika na sauti ya Afrika Ameendelea kuwa gumzo na Kuiteka mioyo ya makundi mbalimbali kutokana na utendaji kazi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.

Rais Samia ameitetemesha kwa furaha mioyo ya Wanavyuo nchini kwote ,Taarifa hizo zilizosambaa kwa Kasi ya ajabu hapa nchini juu ya Rais Samia kuridhia ongezeko la Fedha ya kujikimu kutoka 8500-10000 kwa siku limewafurahisha ,kuwagusa na Kuiteka mioyo ya wanafunzi na hata wazazi wenye watoto wanaosoma.

Wanavyuo na wadau mbalimbali kupitia mitandao ya kijamii wameendelea kumshukuru Rais Samia na kumpongeza Sana kwa usikivu wake, wengi wamesema hakika hakuna mfupa mgumu mbele ya Rais Samia,hakuna mlima mrefu kwa Rais Samia,hakuna Jambo lisilo wezekana kwa Rais Samia,hakuna changamoto na kero isiyo na majibu mbele ya Rais Samia.

Hakika Rais Samia Ni kiongozi wa aina yake, Sasa wanafunzi wanakwenda kusoma kwa amani na utulivu,Sasa wenye mipango wanakwenda kujipatia mitaji baada ya kuhitimu masomo yao kwa kuwekeza kidogo kidogo,Sasa akili zote za wanafunzi zitaelekwezwa katika masomo tu,Rais Samia ni mama mwenye huruma na upendo mkubwa Sana na watu wake.

Wanavyuo wamesikika wakisema watampigia kampeni Rais Samia nyumba kwa nyumba katika kumuombea Kura za Urais ,wengine wamesikika mitaani wakisema watamchangia fedha ya kuchukua fomu ya Urais na wengine wamesema Ni mama Samia mpaka 2030,Hakika uongozi Ni Akili na maarifa,Ni karama na unatoka kwa Mungu,hakika Mungu Ndiye aliye mpa uongozi Rais Samia na ndiye anayeendelea kumpa maarifa na njia ya kuongoza Taifa letu,

Ni mwanachuo yupi atamnyima Rais Samia Kura yake? Ni mzazi yupi atamnyima Rais Samia Kura ya Urais? Ni mtanzania yupi asiyeona juhudi za mh Rais wetu mpendwa kipenzi Cha watanzania mama Samia suluhu Hassani? Tunataka Nini watanzania? Tufanyiwe Nini Turidhike? Kwani hatuoni kuwa Yote tuliyoyahitaji miaka yote Rais Samia katekeleza na anaendelea na kazi? Kipi hajafanya Rais wetu? Kipi hajasikiliza Rais wetu? Nani amenyimwa nafasi ya kuongea kero yake? Kwanini tusimshukuru Rais Samia kwa hapa alipotufikisha? Kwanini Tusimuunge mkono?

Ndugu zangu watanzania Rais Samia Ni zawadi kwetu watanzania tunayopaswa kujivunia na kuiheshimu Sana,Ni zawadi inayopaswa kutunzwa Sana.

Kazi Iendeleee,mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627
Huu ujinga wakujisifiasifia kijinga uliasisiwa na shetani.
 
10 yrs ago nikiwa chuo wapo baadhi walipata ufadhiri wa wizara ya fedha wakati yetu ikitoka kapu la serikali walikuwa wanalamba 10,000 tulikuwa tunawaona kama bharhesa
 
Haa huyu raisi si wa kumwamin kabisa yeye yupo tiari kumridhisha na kumfurahisha kiLa mtu lakini kumbe hazina hamna kitu .waulize wale watumishi wa meimosi waakaambulia 10000
Utakufa kwa presha na wivu wako kwa kuona mh Rais anavyokubalika na kuungwa mkono na mamillion ya watanzania, watumishi wakamkubalia Sana mh Rais na kumuunga mkono,kwa kuwa ndani ya muda mfupi wengi wao walipandishwa madaraja na kulipwa stahiki zao,malimbikizo ya madeni Yao wengi wamelipwa ,mishahara wamepandisjiwa kwa 23% hasa wale wa kima Cha chini
 
Hiyo hela ni ndogo sana!

Hiyo ni sawa na ile aliongeza mshahara kwa sh elfu 20 alafu kupitia mitozo yake na kufungua nchi gharama za maisha zikapanda kwa 200%

Nchi nyingine wanafunzi wa vyuo ndio chachu ya kuleta mabadariko ila haya manafunzi ya kwetu yanadanganywa kwa vitu cheap kama hivyo na kuwaza ngono tu!

Mavi matupu!
Wanafunzi wa vyuo washazungushiwa fensi
 
Hiyo hela ni ndogo sana!

Hiyo ni sawa na ile aliongeza mshahara kwa sh elfu 20 alafu kupitia mitozo yake na kufungua nchi gharama za maisha zikapanda kwa 200%....
Kwahiyo mkuu 2025 utamchagua nani?
 
Ni sawa kabisa coz alicontrol inflation vilivyo.hakukua na kujipangia bei kiholela kwa wafanyabiashara kama ilivyo sasa.

Inflasheni ya ny0kh0? Alikuta sukari 1500 ameondoka 2800 ,mchele 1800 super ,ameondoka mchele 2800 ,mafuta ya kupikia lita 3500 kaondoka lita elfu 6 ,mafuta ya taa 900 kaondoka 2800 ,nauli ferry ilikuwa 100 kaipandisha hadi 200 akasema asiyeweza apige mbizi.
 
Kama alikuwa na sifa na alichagua kozi za kipaombele kwa mujibu wa miongozo unapokuwa umetolewa na akawa amekosa mkopo ilitakiwa skate rufaa muda ule ....
Ahahahahah! Kwahiyo unahisi unanifafanulia nisichojua? Ahahahahah! Kwa taarifa yako, mimi babaake mzazi ni mnufaika wa mkopo 2006 hadi 2009. Sasa hivi kuna utaratibu wa hovyo afadhali kipindi chetu. Anyway, kwakuwa mimi babaake nipo, mwanangu atasoma tu.
 
Back
Top Bottom