Rais Samia ukikubali tu Kukutana na Wazee wa Yanga SC akina Said Motisha Watanzania Werevu Watakudharau na Utajiaibisha mno

MINOCYCLINE

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2015
Posts
8,018
Reaction score
16,802
Tafadhali Rais wangu Mpendwa Samia Suluhu Hassan kamwe usikubali Kuingizwa katika huu Mtego wa Kukutana na Wazee Njaa na Wazee Majungu wa Yanga SC kwani watakuharibia, hutoamini na inaweza hata Kuathiri Ndoto zako za kuwa Rais mwaka 2025 hasa katika Sanduku la Kupiga Kura.

Na kibaya zaidi katika hao (hawa) Wazee wa Yanga SC wanaotaka kuja Kukuona hakuna aliye wa hovyo hovyo kama Mmoja wao aitwae Said Motisha ambaye kwa Watu wa Mpira (hasa wa hapo Uwanja wa Uhuru na Taifa) katika Baa Mbili Maarufu za Kwa Chichi na Mianzini tunamjua hana Chumba cha Kulala na analala ndani ya Malori au Mabasi yanayopaki hapo hapo au katika Viti vya hizo Baa Mbili hizo tajwa na Kutwa tu Kazi yake ni Kupiga Watu Mizinga na kugongea Bia za Bure huku akitishia Watu kwa kujifanya ni Mganga wa Kienyeji.

Kwa mengi zaidi ya Kumhusu huyu Mzee wa hovyo hovyo Said Motisha tafadhali Wasaidizi wake wakienda hapo wamuulizie Mtu aitwae Makongoro au Mapinduzi (Bingwa wa Kutoingia Uwanjani kutizama Mechi ila Mpira ukiisha anaweza Kuuelezea Kiuchambuzi kuliko walioingia) anbaye ndiyo huwa ni Mlinzi wa Gari za Watu zinazopaki usawa wa Msikitiki unaotizamana na Uwanja wa Uhuru wampe mengineyo zaidi.

Hawa Wazee ( hasa huyu Said Motisha ninayemjua ndani nje ) wanataka kuja Kwako Ikulu Magogoni au Chamwino Kukupiga Mizinga (Kukuomba tu Pesa) kisha wajifanye Wanakupenda sana na wana Uwezo wa Kukufanyia Tiba ya Kiushirikina (Uganga) kisha ukiwaamini na Kuwakubalia waanze Kukutengeneza Kimjini Mjini ili Ujae na Wakupige Hela.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…