Rais Samia umeanza kutuangusha kabla ya siku 100 za uongozi wako

Rais Samia umeanza kutuangusha kabla ya siku 100 za uongozi wako

Acheni chuki zenu .sasa hii nchi kila mtu nimjuaji.....Mlisema Magu sasa Mama nae hamuoni jema....Kwani lazima waje wakenya..yeye katoa fursa na wakenya wenye vigezo waje...hapo kuna shida gani??
 
Ohooo,Nini hii sasa? Kumbe ndo Alivyo,mraibu wa mapenzi kaja na hoja.
 
Nimesikiliza Hotuba ya mama huko Kenya naweza kusema.

Mama sio mzuri wa hoja nzito, ni mwepesi wa Ku Give In.

Anasema Wakenya waje Tanazania kuwekeza kwenye madini, Mkenya Gani anamtaji wa kuja kuwekeza kwenye Madini, Kama Mwekezaji mkubwa wa madini?

Mama anadanganywa na watu wake wa Karibu kwa udhaifu wake wa ndiyo ndiyo, Hivi ina maana mama hasomagi Takwimu za Dunia kuwa Tanzania kuna Mabilionea(USD Millionaires) wengi kuliko Kenya?

Mama anasema Tanzania ina ardhi Kubwa ana wakaribisha Wakenya, Je anajua uhaba wa Ardhi Kenya ni kwa sababu ya familia chache zenye nguvu kisiasa kuhodhi ardhi?
Mama anajua kuwa Wakenya zaidi ya asilimia 80 hawana ndoto wala hawataweza kabisa kujenga wala kumiliki Nyumba zao kipindi chote cha maisha yao?,

Mama anasahau hoja kuwa Tanzania ina watu wengi (Soko Kubwa), Huduma za Kijamii na mahitaji yote ya msingi kufanya biashara ni conducive Tanzania kuliko Kenya?

Mana anasahau au aliona aibu kusema mazingira mazuri yaliyopo kenya kwa wafanya biashara ni urahisi wao kutoa Rushwa kuliko Tanzania?

Mzee Mangula tunaomba Mlisisitize Bunge limchunge huyu Mama, na 2025 mfanye uchaguzi upya.
Suala la Ardhi Mh. Lukuvi nilimsikiliza kwenye kipindi cha DK 45 ITV "ni vigumu kwa mgeni kupewa ardhi " kama ni ya uwekezaji ni sawa.
Hata hivyo sisi tutabaki kuwa Wafrika, hivyo Umoja Wetu ndiyo Ushindi.
 
Suala la Ardhi Mh. Lukuvi nilimsikiliza kwenye kipindi cha DK 45 ITV "ni vigumu kwa mgeni kupewa ardhi " kama ni ya uwekezaji ni sawa.
Hata hivyo sisi tutabaki kuwa Wafrika, hivyo Umoja Wetu ndiyo Ushindi.
ni kweli lakini iwaje yeye amerikishe ardhi mabeberu mbaka wengine wakose
 
Kwahiyo kama Tanzania ina watu wengi na soko kubwa la ndani tufunge mipaka tusiwe na uwekezaji kutoka nje, sio ? Kama kuna mtu 'msomi msomi' unamjua muulize kuhusu "Foreign Direct Investment (FDI)" na umuhimu wake katika uchumi wa nchi.
Tatizo mmepoteana hakuna tena mtu mmoja anayewapa maelekezo ya nini muandike, kipi mpinge, wapi mtukane na kikubwa zaidi muandike nini. Mishale imepoteana sio? Farasi wanarudi wenyewe.
 
Mkuu wewe ni mtu hatari sana! Hakuna Mkenya mwenye mtaji wa kuwekeza kwenye madini? Yaani unajua mitaji ya wakenya wooote?

Mbona Mzee mengi aliwekeza kwenye madini? Au hakuna tajiri wa mtaji kama wa Mengi Kenya?
Jomba Mengi aliwekeza kwenye madini yapi...wajameni au kwenye vitalu vya kudalalia..anyway tusimzungumze marehem kwa sasa
 
Mama ni mgeni katika taasisi tumpe muda isipokuwa angalizo asipelekeshwe.

Kila la kheri mama
 
Nimesikiliza Hotuba ya mama huko Kenya naweza kusema.

Mama sio mzuri wa hoja nzito, ni mwepesi wa Ku Give In.

Anasema Wakenya waje Tanazania kuwekeza kwenye madini, Mkenya Gani anamtaji wa kuja kuwekeza kwenye Madini, Kama Mwekezaji mkubwa wa madini?

Mama anadanganywa na watu wake wa Karibu kwa udhaifu wake wa ndiyo ndiyo, Hivi ina maana mama hasomagi Takwimu za Dunia kuwa Tanzania kuna Mabilionea(USD Millionaires) wengi kuliko Kenya?

Mama anasema Tanzania ina ardhi Kubwa ana wakaribisha Wakenya, Je anajua uhaba wa Ardhi Kenya ni kwa sababu ya familia chache zenye nguvu kisiasa kuhodhi ardhi?
Mama anajua kuwa Wakenya zaidi ya asilimia 80 hawana ndoto wala hawataweza kabisa kujenga wala kumiliki Nyumba zao kipindi chote cha maisha yao?,

Mama anasahau hoja kuwa Tanzania ina watu wengi (Soko Kubwa), Huduma za Kijamii na mahitaji yote ya msingi kufanya biashara ni conducive Tanzania kuliko Kenya?

Mana anasahau au aliona aibu kusema mazingira mazuri yaliyopo kenya kwa wafanya biashara ni urahisi wao kutoa Rushwa kuliko Tanzania?

Mzee Mangula tunaomba Mlisisitize Bunge limchunge huyu Mama, na 2025 mfanye uchaguzi upya.
Nonsense.

Mataga bado unaweweseka ee..

Zama zimebadilika,sasa tunaye raisi mpya,mama shupavu mwerevu,Samia Suluhu Hassan. Mama ni akili kubwa,nyinyi wenye akili za kushikiwa na jiwe hamuwezi kumwelewa! Sisi tunamuelewa ..wacha mama atengeneze nchi ambayo ilikuwa imeharibiwa vibaya na mwendazake.
 
Liwalo na liwe mama amerudisha furaha kwenye mioyo yetu ..Kama alivyosema Nyalandu!
Mengine baadaye!
Potelea pote mama karudisha furahaa zaidi ameturuhusu tumkosoe pale tutakapo ona ameboronga...zaidi hata kule Kenya karudia kauli hii kwa kusema.kuwa ..."tukikosea mtukosoe" huu ni ushindi mkubwa kwa Watanzania dhidi ya mawimbi yale tulipitia enzi zilizopita
 
Nimesema Tanzania ina Mabilionea wengi kuliko Kenya (Dollar Millionaires wengi), Kwa nini hawa tusiwasisitize.

Unatakiwa uwe na mtaji wa zaidi ya TSH Billioni 500 ndio uhesabiwe wewe ni Mwekezaji mkubwa wa Madini
Hakuna unachojua kuhusu mabiliomea wala uchumi.

Wewe ni mbumbumbu kabisa. Siku hizi unaweza kupata taarifa hata google! Ongeza kwanza ufahamu wako ndipo uje huku.
 
Kwahiyo kama Tanzania ina watu wengi na soko kubwa la ndani tufunge mipaka tusiwe na uwekezaji kutoka nje, sio ? Kama kuna mtu 'msomi msomi' unamjua muulize kuhusu "Foreign Direct Investment (FDI)" na umuhimu wake katika uchumi wa nchi.
Tatizo mmepoteana hakuna tena mtu mmoja anayewapa maelekezo ya nini muandike, kipi mpinge, wapi mtukane na kikubwa zaidi muandike nini. Mishale imepoteana sio? Farasi wanarudi wenyewe.
Hivi bila aibu unasema unataka Foreign Investment kutoka Kenya Kweli?

Kampuni ya Helium One iliyogundua Helieum Rukwa inafanya mpango wa Kuraise kama 25M USD ndio ije ichimbe madini.

Watu mnahitaji exposure kwa kweli, Kenya wanatengeneza nini ambacho sisi hatutengenezi?

Tanzania ukanda wetu ndio tunavutia Real FDI hapa.

LNG Plant ni Karibu 10B USD, Nickel Mine, Heliem, SGR, JNHPP, Bagamoyo Port, EACOP,

Biashara kati ya Kenya na Tanzania ni ya kuuziana Nyanya, Hatuwezi tukawa kwenye position ya kuuza raw materials

Tafuta miradi 2 Kenya inayifikia robo ya hizo thamani.
 
Suala la ardhi si la kuendana nalo kienyeji!!! Hivi tunavyozungumzia masuala ya ardhi kuruhusiwa wawekeze Wakenya ni kwa upande mmoja uliojivika koti ama pande zote za Muungano!? Kama ni pande zote tuanze upande mmoja kwanza ambao umekuwa ukikosa mwitikio wa wawekezaji kwa sababu ya kubanwa banwa na upande mwingine. Sijui nimeeleweka...! Au ndiyo nimejichanganya kabisa🥴🥴🥴🥴🥴 Yawezekana Yawezekana sijielewi aiseee!
 
Hivi bila aibu unasema unataka Foreign Investment kutoka Kenya Kweli?

Kampuni ya Helium One iliyogundua Helieum Rukwa inafanya mpango wa Kuraise kama 25M USD ndio ije ichimbe madini.

Watu mnahitaji exposure kwa kweli, Kenya wanatengeneza nini ambacho sisi hatutengenezi?

Tanzania ukanda wetu ndio tunavutia Real FDI hapa.

LNG Plant ni Karibu 10B USD, Nickel Mine, Heliem, SGR, JNHPP, Bagamoyo Port, EACOP,

Biashara kati ya Kenya na Tanzania ni ya kuuziana Nyanya, Hatuwezi tukawa kwenye position ya kuuza raw materials

Tafuta miradi 2 Kenya inayifikia robo ya hizo thamani.
Ni wazi huelewi uchumi unavyoendeshwa, kwahiyo kama kuna uwekezaji wa equinor ndiyo tusitake uwekezaji toka nje ? Unauliza kuhusu kitu tusichoweza kutengeneza ambacho hatuwezi, kwahiyo tangu sasa tunataka wawekezaji walete mitaji yao ktk nchi ambazo zinavitu tusivyoviweza tu ? Sijui ni akili za vipi hizi. Kwahiyo ni bora Unilever (EA) azalishe kenya halafu auze Tz kuliko kuzalisha huku kwetu sio ?? Kuhusu biashara ya mazao kati ya tz na kenya. Narudia tafuta mtu anayejua jua akueleze kuhusu FDI na faida zake.
 
Ni wazi huelewi uchumi unavyoendeshwa, kwahiyo kama kuna uwekezaji wa equinor ndiyo tusitake uwekezaji toka nje ? Unauliza kuhusu kitu tusichoweza kutengeneza ambacho hatuwezi, kwahiyo tangu sasa tunataka wawekezaji walete mitaji yao ktk nchi ambazo zinavitu tusivyoviweza tu ? Sijui ni akili za vipi hizi. Kwahiyo ni bora Unilever (EA) azalishe kenya halafu auze Tz kuliko kuzalisha huku kwetu sio ?? Kuhusu biashara ya mazao kati ya tz na kenya. Narudia tafuta mtu anayejua jua akueleze kuhusu FDI na faida zake.
Nyie ndio mnashangilia Kuuza mahindi alafu muuziwe unga
 
Nyie ndio mnashangilia Kuuza mahindi alafu muuziwe unga
Nitakueleza maana huwenda hukielewi unacho zungumza, tuchukulie mfano uliotoa wa tz kuuza mahindi kisha ketewa unga. Kwakua tuna mahindi lakini hatuna viwanda serikali sasa imeona tuite wenye viwanda(au walau wenye uwezo wakuwa navyo) lakini hawana mahindi ,ambayo ni malighafi ya viwanda hivyo. Tutakapopata viwanda hivi maana yake
1. Hatutasafirisha mahindi nje badala yake tutakuwa na unga uliozalishwa hapa hapa nchini, kitu ambacho wewe ndio unakitaka sio ?
2. Wakileta viwanda hivi watakuwa wameleta mtaji wao kwetu sio ? Maana yake pale kwenye kiwanda hicho patapata chanzo kipya cha pesa kwa shughuli ha ujenzi tu wa kiwanda husika.
3. Watu wetu watapata ajira, zote rasmi na zisizo rasmi, za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja hivyo serikali kwa namna fulani itakuwa imepunguzs chamgamoto ya ajira. Ajira hizi zipo za namna nyingi tumezowea za moja kwa moja lakini zipo nyingine ambazo si za moja kwa moja, hizi zitatoka katika sekta zote ambazo kwa namna yeyote zinagusika na uwepo wa kiwanda hichi, kama mabenki, sheli, huduma za kijamii nk.
4. Serikali itapata kodi, kila mwisho wa mwaka wa hesabu serikali itapata 30% ya faida ya kiwanda hicho (bila kuweka mtaji!) Hii hiwa ni kodi, lakini pia serikali itapata kodi nyingine kama kodi ya ongezeko la thamani, kodi ya mapato ya wafanyakazi na masurufu mengine mengi.
5. Wazawa watapata uelewa na uzoefu wa uendeshaji na utawala wa viwanda vya aina hiyo, hivyo kurahisisha ongezeko la viwanda vya namna hiyo.
6. Kuongezeka kwa uzalishaji nchini, kukua kwa pato la taifa na kukuza sekta nyingine kama usafirishaji. Faida nyingine lukuki nimeacha kuzitaja,.
Umepata mwanga wa kuelewa japo kidogo kwanini tunataka waje tuu kiwekeza na kufiata taratibu zetu na sheria ??
 
Wawekezaji wote wakishapata mgodi wanaingia bank kukopa usipotoshe watu mkuu. Tena sometimes kama hujui wanakopa bank za humu humu Tz
Tuambie Barrick walikopa Benki gani ya humu nchini?
 
Nitakueleza maana huwenda hukielewi unacho zungumza, tuchukulie mfano uliotoa wa tz kuuza mahindi kisha ketewa unga. Kwakua tuna mahindi lakini hatuna viwanda serikali sasa imeona tuite wenye viwanda(au walau wenye uwezo wakuwa navyo) lakini hawana mahindi ,ambayo ni malighafi ya viwanda hivyo. Tutakapopata viwanda hivi maana yake
1. Hatutasafirisha mahindi nje badala yake tutakuwa na unga uliozalishwa hapa hapa nchini, kitu ambacho wewe ndio unakitaka sio ?
2. Wakileta viwanda hivi watakuwa wameleta mtaji wao kwetu sio ? Maana yake pale kwenye kiwanda hicho patapata chanzo kipya cha pesa kwa shughuli ha ujenzi tu wa kiwanda husika.
3. Watu wetu watapata ajira, zote rasmi na zisizo rasmi, za moja kwa moja na zisizo za moja kwa moja hivyo serikali kwa namna fulani itakuwa imepunguzs chamgamoto ya ajira. Ajira hizi zipo za namna nyingi tumezowea za moja kwa moja lakini zipo nyingine ambazo si za moja kwa moja, hizi zitatoka katika sekta zote ambazo kwa namna yeyote zinagusika na uwepo wa kiwanda hichi, kama mabenki, sheli, huduma za kijamii nk.
4. Serikali itapata kodi, kila mwisho wa mwaka wa hesabu serikali itapata 30% ya faida ya kiwanda hicho (bila kuweka mtaji!) Hii hiwa ni kodi, lakini pia serikali itapata kodi nyingine kama kodi ya ongezeko la thamani, kodi ya mapato ya wafanyakazi na masurufu mengine mengi.
5. Wazawa watapata uelewa na uzoefu wa uendeshaji na utawala wa viwanda vya aina hiyo, hivyo kurahisisha ongezeko la viwanda vya namna hiyo.
6. Kuongezeka kwa uzalishaji nchini, kukua kwa pato la taifa na kukuza sekta nyingine kama usafirishaji. Faida nyingine lukuki nimeacha kuzitaja,.
Umepata mwanga wa kuelewa japo kidogo kwanini tunataka waje tuu kiwekeza na kufiata taratibu zetu na sheria ??
Hayo ni mawazo ya kimaskini mkuu. Please think out of the box. Ingekuwa hivyo hata nchi zilizoendelea zingefikiria hivyo lakini zinawafikiria kwanza wananchi wake kwanza.
 
Back
Top Bottom