Rais Samia, unapotulalamikia sisi kuwa kinachokusanywa kama kodi kinaibiwa, je unataka sisi tufanyaje ? Wewe si ndio Rais

Nina mashaka kama wewe sio Lucas Mwashambwa a form four failure with division 4 unayetumia different ID
Ha hahahaha!!! Mbona kama unaada mbinu za kunitimua kwenye uzi wako Aisee na umeishanitoa kwenye usomi!!!

Yaani Mimi naweza kumpiku Lucas...kweli??!!
====
Mkuu ninachokifanya ni kujaribu kuwezesha wanataka masuala ya fikra tunduizi washiriki (critical thinking) kwenye uzi huu. Bila hivyo, kwa mawazo yangu, uzi wako hautanoga.

Kwa hiyo, Mkuu naomba uniache nivinjari kwenye uzi wako huu.

Natanguliza Shukrani za dhati kwa kuridhia niendelee kukaa hapa .Ha haaa!
 
Wahusika kina nani hawahawa TAKO-KURU!?? TISSCCM !! POLICCM au nani !??... Rais analalamika, makamu analalamika, Waziri Mkuu analalamika !?? Hio ni nchi au bwawa la kambale kila mtu ana ndevu si mtoto mama Wala baba.....
 
Baada ya taarifa ya mdhibuti mkuu wa hesabu zaserikali ,(CAG), tume huundwa nyuma ya mikamera majibu ya hizo tume nyuma ya pazia, hata hivyo mfumo wa kodi hauko wazi hata sheria zake nizakificho
 
Sababu anaogopa kulisamakama directly tabaka lisilolipa kodi
 
Wabunge na Rais walipe kodi. Kwa nini hawalipi kodi halafu wanalalamika walipa kodi wachache?
 
...si mtoto mama Wala baba.....
Duh! Ngoja nijipange.
===
Ili mambo haya yajadiliwe bila kuonea upande wowote, nadhani tulete na tukio halisi la ulalamishi wa wale uliowataja tuone kama "ulalamishi wao" ulifanyiwa kazi ama la.

Karibu Mkuu.
 
Unatuchonganisha na mamlaka. Unataka tutolewe humu jf sio bure wewe 🤔🤔🤔🤔
 
Wabunge na Rais walipe kodi. Kwa nini hawalipi kodi halafu wanalalamika walipa kodi wachache?
Hii ni hoja inahitaji kujadiliwa, Hata hivyo, tupate uhakika kama kweli hawalipi Kodi. Na kama hawalipi ninkwa mujibu wa sheria ama la! Kama sheria ndiyo inakataza wasilipe Kodi basi sheria ndiyo ishughulikiwe kama Kuna ulazima wa kufanya hivyo lakini kama Sheria inasema walipe Kodi na hawalipi hilo ni jambo la uvunjifu wa sheria na hatua stahiki zifuatwe.

Asante na Karibu
 
Duh! Ngoja nijipange.
===
Ili mambo haya yajadiliwe bila kuonea upande wowote, nadhani tulete na tukio halisi la ulalamishi wa wale uliowataja tuone kama "ulalamishi wao" ulifanyiwa kazi ama la.

Karibu Mkuu.
Umri huu wako nikuletee nini sasa!?? Ripoti ngapi za CAG umezisikia katika Umri wako!?? Nani aliyekamatwa ama kushitakiwa mpaka nikuletee ushahidi!? .... Mahalmashauri mangapi wakurugenzi na wahasibu wamekutwa na makosa ya matumizi ya fedha na wanahamishwa tu vituo!?? ... Nikuletee ushahidi Mimi!?? ....
 
Ikiwa kama amekiri kuwa zinaingia kwenye mifuko ya wachache, na hao wachache yeye na mamlaka zimewashindwa; je itakuwaje kama hao wachache 'wakizaliana' na kuwa kundi kubwa?
 
Chawa mwingine
 
Vijana wa siku hizi mnaliangusha snaa taifa, sijui ni uoga wa kukosa ajira. Msomî kama wewe una behave kichawa, tutatoboa kweli . Samia must be told , she is unfit for the throne and that has been proven beyond doubts . Tukianza kutoa evidence hapa as to why she is unfit , tutajaza page nyingi sana . I believe wewe kama ni typical Tanzanian , you must hzve known as to how she is unfit . Kwa sasa nchi ni kama gari lililokosa dereva
Yoyote anakuwa chochote, ukitaka kuteka watu na kuua watu , just do , ukitaka kubaka watu , just do , ukiweza kuiba, just do
Ukiweza kuiba kodi just do , ukiweza kupitisha mizigo bandarini bila kodi , just do

Kila kitu kinajiendesha chenyewe bila control

It is the worst moment in our country’s history since independence. JPM had his issues with democracy, but he stabilized the country, and we could see he was delivering

# je hii serikali au Serikali ya Samaki?
 
Achana
Wahusika kina nani hawahawa TAKO-KURU!?? TISSCCM !! POLICCM au nani !??... Rais analalamika, makamu analalamika, Waziri Mkuu analalamika !?? Hio ni nchi au bwawa la kambale kila mtu ana ndevu si mtoto mama Wala baba.....
hiyo ni Serikali ya Samaki.
 
Umri huu wako nikuletee nini sasa!?? Ripoti ngapi za CAG umezisikia katika Umri wako!?? Nani aliyekamatwa ama kushitakiwa mpaka nikuletee ushahidi!?
Asante Mkuu kwa kujibu bandiko langu.
Hata hivyo, Mkuu ni kama umehamisha Magoli. Kwenye orodha ya uliowataja CAG hakuwemo. Halijaharibika neno, nitaeleza juu ya report za CAG.

Ni kweli CAG amekuwa akitoa ripoti zinazoonyesha baadhi ya Taasisi za serikali na halmashauri kufanya ubadhilifu. Na hatua zimekuwa zikichukuliwa kudhibiti ubadhilifu huo.
Kwanza ilikuja kugundulika kuwa wakati mwingine CAG hawi objective kwenye kazi zake kiasi Hata cha kulalamikiwa na PASKALI Mayalla kuwa CAG anafanya kazi ya audit tu badala ya ku control pia.

Mfano (si halisi) uliotolewa ni wa kumuandikia audit query kind of hati chafu muhusika kwa kununua Mabasi matatu ya tata ambayo yatabeba abiria 180 badala ya kununua gari moja la Yutong la kubeba abiria 56 kwa gharama Ile Ile kisa awali iliandikwa inunuliwe Youtong!!

Hata hivyo, mbali na mapungufu haya niliyoeleza serikali imejitahidi kudhibiti ubadhilifu huu Kwa kuchukua hatua mbalimbali. Hatua kubwa kabisa kwa mwaka huu ni serikali kuandaa mswada wa kuboresha sheria za Kodi na fedha kwa ujumla ambazo zimepitishwa na Bunge hivi majuzi. Hatua nyingine ni serikali kuunda tume/Bodi ya kushauri masuala Kodi.

Kwa si kweli kuwa hakuna kinachofanyika!!!
 
Pole sana kwa kumsikia hiyo juzi wenzako tushamsikia kitambo na sio mara moja mpaka tushamzoea analalamika kama mwananchi mwingine wa kawaida.
 
Huyu unayemsimulia hizi hekaya zako anayajua yote hayo..... Unatunga SHERIA wakati umeshawaambia "KULENI KWA UREFU WA KAMBA" ..Halafu inakuja kulalamika haukusanyi Kodi ipasavyo zinapotelea mifukoni mwa watu .... Tatizo la afya ya akili ni kubwa sana Kwa minajili hii....
 
kulalamika haukusanyi Kodi ipasavyo zinapotelea
Kibinadamu na Hata ukiwa kiongozi Kuna makosa kufanyika, Hata Mwalimu Nyerere, Baba wa Taifa, alikiri hili.

Hata hivyo, nadhani kwa haraka baada kugundua kuwa kunaupotoshaji mkubwa wa tafsiri ya kauli yake ya" kula kwa urefu wa kwamba yake" amefanya jitihada za kurekebisha ikiwemo kutunga sheria nilizoeleza hapo Juu. Kauli ambayo Mheshimiwa Rais kwa tafsiri yangu isiyo Rasmi alimaanisha kuwa, kila mmoja anazo terms of references za ufanyaji kazi ambazo aliziona wakati anaomba kazi hiyo ama anapangiwa kazi hiyo na ujira wake kwa kazi hiyo, kwa hiyo Kila mmoja apate stahiki zake kwa kazi yake hiyo. Kama Kuna kazi ya ziada ambayo Haina mgongano wa maslahi na kazi yake ya utumishi wa serikali ama binafsi aendelee Nako kupata stahiki zake bila bughudha. Hii ndiyo tafsiri yangu juu ya kauli ya Mama Rais Dr Samia Suluhu Hassan ya kula kwa urefu wa kwamba yake.
 
Her responce amid attrocities against lives of Tanzanians is purely standards on how she is unfit to the position.

We (and yes am included), did our beat to console and share opinions and advises but she has her own plans.

Your suggestion is positive, but the reality is, she needs them not to be advised. During the 60yrs anniversaru of Jeshi la Polisi, she vows on such while repremanding diplomats amid their open letter concerning abductions and killings of innocents nchini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…