Rais Samia usipangue Wakurugenzi wa Halmashauri, ile ni nafasi ya utumishi wa umma

Rais Samia usipangue Wakurugenzi wa Halmashauri, ile ni nafasi ya utumishi wa umma

Huihui2

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2012
Posts
7,021
Reaction score
11,475
Mwaka 2015 Magufuli alipoingia madarakani alipanua wigo wa uteuzi na kuapisha. Tulishuhudia akiteua waliokuwa makada wa CCM zaidi ya 200 na kuwapa nafasi za Ukurugenzi wa Halmashauri (DED) na wengine wakiwa na DAS ( maafisa tawala wa wilaya). Na kisha akawaapisha. Hii ilipelekea ma DED wengi waliokuwapo kabla kubakia "Bench" bila kazi

Kabla ya Mwendazake nafasi hizi zilikuwa ni za watumishi waliopo Halmashauri na wilayani walikuwa wanazipata kwa kupanda ngazi kutegemeana na upatikanaji wa nafasi ya wazi (vacant position) baada ya aliyekuwapo kustaafu, kufariki au kuchukuliwa hatua za nidhamu. Ndipo Wizara inafanya mchakato wa ndani na kupeleka majina kwa Rais kwa uteuzi.

Alichofanya Mwendazake ilikuwa ni uvunjifu wa katiba ya JMT kuwaleta kwenye utumishi wa umma watu ambao ni wanachama wa Chama cha Siasa.

Nashauri kwa Rais SSH chonde chonde katika vitu vibaya vya Mwendazake ulivyoamua kuviacha basi na hiki cha kuteua makada kuwa ma DED na ma DAS usithubutu. Acha mchakato wa utumishi wa umma uchukue nafasi.
 
Hapana ni vizuri kupangua ili kupanga timu yake ila hao ambao waliingia kama wanasiasa anaweza kuwaondoa lakini kulingana na utendaji wao. Vinginevyo wakurugenzi wa halmashauri ni wateule wa Rais na ni mamlaka yao ya nidhamu ni muhimu kuwapangua ili kujenga ufanisi wa kazi kwa mujibu wa sheria ya utumishi wa umma 2002. Sheria hiyo inampa madaraka ya kupangua na kuhamisha watumishi wa umma.
 
Mwendazake aacha makada na madiwani waliobebwa naye wakivurugana mfano tukio hili, kila mmoja anaona ni 'mteule' wa JPM, si mwanasiasa wala mtumishi wa halmashauri wote wanaona wameteuliwa na mamlaka moja yaani Rais

19 May 2021
Dar es Salaam, Tanzania


VURUGU ZAIBUKA KINONDONI,MEYA NA MKURUGENZI WASHIKANA​


VURUGU ZAIBUKA BARAZA LA MADIWANI KINONDONI,MEYA NA MKURUGENZI WAVIMBIANA
Source : DarMpya TV
 
Mwendazake aacha makada na madiwani waliobebwa naye wakivurugana mfano tukio hili, kila mmoja anaona ni 'mteule' wa JPM, si mwanasiasa wala mtumishi wa halmashauri wote wanaona wameteuliwa na mamlaka moja yaani Rais

19 May 2021
Dar es Salaam, Tanzania


VURUGU ZAIBUKA KINONDONI,MEYA NA MKURUGENZI WASHIKANA​


VURUGU ZAIBUKA BARAZA LA MADIWANI KINONDONI,MEYA NA MKURUGENZI WAVIMBIANA
Source : DarMpya TV

Hii ndivyo inatakiwa Ligi hadharani
 
Walishawahi kutangaza nafasi za kazi na watu waapply? Kama waliteuliwa kutenguliwa pia inawezekana.
 
Mwaka 2015 Magufuli alipoingia madarakani alipanua wigo wa uteuzi na kuapisha. Tulishuhudia akiteua waliokuwa makada wa CCM zaidi ya 200 na kuwapa nafasi za Ukurugenzi wa Halmashauri (DED) na wengine wakiwa na DAS ( maafisa tawala wa wilaya). Na kisha akawaapisha. Hii ilipelekea ma DED wengi waliokuwapo kabla kubakia "Bench" bila kazi

Kabla ya Mwendazake nafasi hizi zilikuwa ni za watumishi waliopo Halmashauri na wilayani walikuwa wanazipata kwa kupanda ngazi kutegemeana na upatikanaji wa nafasi ya wazi (vacant position) baada ya aliyekuwapo kustaafu, kufariki au kuchukuliwa hatua za nidhamu. Ndipo Wizara inafanya mchakato wa ndani na kupeleka majina kwa Rais kwa uteuzi.

Alichofanya Mwendazake ilikuwa ni uvunjifu wa katiba ya JMT kuwaleta kwenye utumishi wa umma watu ambao ni wanachama wa Chama cha Siasa.

Nashauri kwa Rais SSH chonde chonde katika vitu vibaya vya Mwendazake ulivyoamua kuviacha basi na hiki cha kuteua makada kuwa ma DED na ma DAS usithubutu. Acha mchakato wa utumishi wa umma uchukue nafasi.
Naunga mkono hoja tatizo langu kubwa hizi nafasi kuteuliwa na Rais hizi nafasi walitakiwa wawajibike katika ngazi ya mkoa huwezi kuwa Rais anateuwa PM, sijui waziri wa Tamisemi, RC, Mkuu wa wilaya mpaka mkurugenzi nyote wateuliwa wa mtu mmoja tech nyote level moja ndio maana hakuna uwajibikaji. Hata kama Rais anapitia teuzi hizi akipitisha natolea mfano mkuu wa Wilaya basi waziri husika ndio amtangaze na aape mbele ya mkuu wa mkoa sio kwa Rais hii itafanya Mkurugenzi ku report kwa mkuu wa Wilaya, Mkuu wa wilaya report kwa RC, RC ku report kwa Waziri, Waziri areport kwa PM direct na indirect kwa Rais. Hatuwezi kuwa sote tuna report kwa mtu mmoja au tunawajibika kwa mtu mmoja. Raisi achikilie mpini kuteuwa na kutengua lazima upate baraka zake kwanza lakini maamuzi yatangazwe ngazi tofauti kuepusha chuki binafsi.
 
Naunga mkono hoja tatizo langu kubwa hizi nafasi kuteuliwa na Rais hizi nafasi walitakiwa wawajibike katika ngazi ya mkoa huwezi kuwa Rais anateuwa PM, sijui waziri wa Tamisemi, RC, Mkuu wa wilaya mpaka mkurugenzi nyote wateuliwa wa mtu mmoja tech nyote level moja ndio maana hakuna uwajibikaji. Hata kama Rais anapitia teuzi hizi akipitisha natolea mfano mkuu wa Wilaya basi waziri husika ndio amtangaze na aape mbele ya mkuu wa mkoa sio kwa Rais hii itafanya Mkurugenzi ku report kwa mkuu wa Wilaya, Mkuu wa wilaya report kwa RC, RC ku report kwa Waziri, Waziri areport kwa PM direct na indirect kwa Rais. Hatuwezi kuwa sote tuna report kwa mtu mmoja au tunawajibika kwa mtu mmoja. Raisi achikilie mpini kuteuwa na kutengua lazima upate baraka zake kwanza lakini maamuzi yatangazwe ngazi tofauti kuepusha chuki binafsi.
Kama tunataka mabadiliko ya kweli, nafasi ya Mkuu wa Wilaya ni ya kufuta kabisa.
 
Mwaka 2015 Magufuli alipoingia madarakani alipanua wigo wa uteuzi na kuapisha. Tulishuhudia akiteua waliokuwa makada wa CCM zaidi ya 200 na kuwapa nafasi za Ukurugenzi wa Halmashauri (DED) na wengine wakiwa na DAS ( maafisa tawala wa wilaya). Na kisha akawaapisha. Hii ilipelekea ma DED wengi waliokuwapo kabla kubakia "Bench" bila kazi

Kabla ya Mwendazake nafasi hizi zilikuwa ni za watumishi waliopo Halmashauri na wilayani walikuwa wanazipata kwa kupanda ngazi kutegemeana na upatikanaji wa nafasi ya wazi (vacant position) baada ya aliyekuwapo kustaafu, kufariki au kuchukuliwa hatua za nidhamu. Ndipo Wizara inafanya mchakato wa ndani na kupeleka majina kwa Rais kwa uteuzi.

Alichofanya Mwendazake ilikuwa ni uvunjifu wa katiba ya JMT kuwaleta kwenye utumishi wa umma watu ambao ni wanachama wa Chama cha Siasa.

Nashauri kwa Rais SSH chonde chonde katika vitu vibaya vya Mwendazake ulivyoamua kuviacha basi na hiki cha kuteua makada kuwa ma DED na ma DAS usithubutu. Acha mchakato wa utumishi wa umma uchukue nafasi.
Ufafanuzi wsko ni nzuri sana lakini umeuharibu kwa kutoa ushauri mbovu. Kama Magufuli alivunja katiba katika kufanya uteuzi wa nafasi hizo maana yake ni ubatili.

Hivi huoni kwamba kurudisha utaratibu wa kikatiba wa uteuzi wa nafasi hizo Rais angekuwa anatekeleza kwa vitendo kiapo chake cha kuilinda na kuitetea katiba?
 
🤣🤣🤣🤣

Yaani unamshauri RAIS katika mambo aliyopewa mamlaka nayo na KATIBA(presidential decree) ?!!! Ha ha ha ha ha
 
Mwaka 2015 Magufuli alipoingia madarakani alipanua wigo wa uteuzi na kuapisha. Tulishuhudia akiteua waliokuwa makada wa CCM zaidi ya 200 na kuwapa nafasi za Ukurugenzi wa Halmashauri (DED) na wengine wakiwa na DAS ( maafisa tawala wa wilaya). Na kisha akawaapisha. Hii ilipelekea ma DED wengi waliokuwapo kabla kubakia "Bench" bila kazi

Kabla ya Mwendazake nafasi hizi zilikuwa ni za watumishi waliopo Halmashauri na wilayani walikuwa wanazipata kwa kupanda ngazi kutegemeana na upatikanaji wa nafasi ya wazi (vacant position) baada ya aliyekuwapo kustaafu, kufariki au kuchukuliwa hatua za nidhamu. Ndipo Wizara inafanya mchakato wa ndani na kupeleka majina kwa Rais kwa uteuzi.

Alichofanya Mwendazake ilikuwa ni uvunjifu wa katiba ya JMT kuwaleta kwenye utumishi wa umma watu ambao ni wanachama wa Chama cha Siasa.

Nashauri kwa Rais SSH chonde chonde katika vitu vibaya vya Mwendazake ulivyoamua kuviacha basi na hiki cha kuteua makada kuwa ma DED na ma DAS usithubutu. Acha mchakato wa utumishi wa umma uchukue nafasi.
Lazima watapewa makada hakuna namna, katiba ni mbovu haswa
 
Naunga mkono hoja tatizo langu kubwa hizi nafasi kuteuliwa na Rais hizi nafasi walitakiwa wawajibike katika ngazi ya mkoa huwezi kuwa Rais anateuwa PM, sijui waziri wa Tamisemi, RC, Mkuu wa wilaya mpaka mkurugenzi nyote wateuliwa wa mtu mmoja tech nyote level moja ndio maana hakuna uwajibikaji. Hata kama Rais anapitia teuzi hizi akipitisha natolea mfano mkuu wa Wilaya basi waziri husika ndio amtangaze na aape mbele ya mkuu wa mkoa sio kwa Rais hii itafanya Mkurugenzi ku report kwa mkuu wa Wilaya, Mkuu wa wilaya report kwa RC, RC ku report kwa Waziri, Waziri areport kwa PM direct na indirect kwa Rais. Hatuwezi kuwa sote tuna report kwa mtu mmoja au tunawajibika kwa mtu mmoja. Raisi achikilie mpini kuteuwa na kutengua lazima upate baraka zake kwanza lakini maamuzi yatangazwe ngazi tofauti kuepusha chuki binafsi.
Well said
 
Back
Top Bottom