Pre GE2025 Rais Samia: Waacheni wajifunze, muda wao wa kuendesha dola bado

Pre GE2025 Rais Samia: Waacheni wajifunze, muda wao wa kuendesha dola bado

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Nyendo

JF-Expert Member
Joined
Jun 4, 2017
Posts
1,336
Reaction score
4,731
Rais Samia akizungumza na wananchi wa kata ya Laela ,Wilaya ya Sumbawanga Vijijini Rukwa mesema leo tarehe 17 Julai 2024 ikiwa siku ya mwisho ya kukamlisha kwa ziara yake ya siku tatu "Wengine waacheni waendelee kujifunza bado wachanga, muda wao wakuendesha Dola bado Kabisa"


"Lazima tuwe na Serikali makini inayowekwa na chama makini, niwaombe sana, mwaka huu mwisho wa mwaka mwezi wa 10 wa 11 kule tunakwenda kuwa na uchaguzi wa Serikali za Mitaa, tunakwenda kuchagua viongozi wa mitaa na viongozi wa vitongoji.

Niwaombe sana ndugu zangu, nendeni mkachague chama cha Mapinduzi, nendeni mkatuchague Chama cha Mapinduzi kwa sababu ndicho chama kilichoweka Serikali makini inayomimina maendeleo kwa watanzania, inayomimina maendeleo kwa watu, wa majimbo ya Tanzania.

Unapozungumza maji, elimu, afya umeme, kilimo na mambo mengine ni chama cha Mapinduzi, naomba sana chagueni chama cha Mapinduzi, tupite vizuri ili maendeleo yaje na mengine na mengine na mengine zaidi.

Wengine waacheni bado waendelee kujifunza, bado ni wachanga ni watoto wetu wa chama cha Mapinduzi, kwa hiyo waachieni waendelee kujifunza muda wao wa kuendesha dola ni bado kabisa kabisa kabisa, kwa hiyo niwaombe sana niwaombe sana ndugu zangu kachagueni chama cha cha Mapinduzi."


Pia soma:
 
Msafara wa MaGari 150? Shule ndio hizi👇😝
watoto.jpg

Hii ni zamu yetu CHADEMA kuiongoza Tanzania msituibie kura tu.
 
Rais Samia akizungumza na wananchi wa kata ya Laela ,Wilaya ya Sumbawanga Vijijini Rukwa mesema leo tarehe 17 Julai 2024 ikiwa siku ya mwisho ya kukamlisha kwa ziara yake ya siku tatu...
Mama anahangaika na watoto wachanga wa nn si anatakiwa kitokuwaongelea? Au wanamsumbua? Na bado acheze tu Rukwa, Ruvuma, Morogoro na Mikoa mingine. Hao huenda wakamuelewa.
 
Bullshit!

Lugha za kikoloni hizo.

Nyerere alikuwa na ukomavu gani alipo chukua nchi toka kwa wakoloni?

Samia ni mweupe sana aisee.

Imagine Samia ana debate na Lissu…..

It would be a massacre!
Kuna mila hipo huko visiwani kwao wanaorudi nyumbani wanachapwa viboko na huyu mama nahisi angepatabakora zaidi ya kitimoto
 
Na yeye kwenye kapevuka kwenye siasa za kitapeli, siasa za kuuza bandari kwa waarabu, mbuga za wanyama kwa waarabu, hifadhi za misitu kwa waarabu, viwanja vya ndege na sasa mwendokasi kwa waarabu. Kwa uuzaji wa rasilimali za nchi, hana mpinzani. Hajawahi kupatikana Rais wa hivyo!!
 
Back
Top Bottom