Rais Samia: Waliosema nimeuza Bandari na Bahari faida yake ndio hii

Rais Samia: Waliosema nimeuza Bandari na Bahari faida yake ndio hii

DP World kaleta cranes tuu, tractors na software kitu ambacho tungefanya wenyewe, pesa kubwa na uwekezaji wote ulifanyika na JPM Kwa mkopo wa World Bank, hao ni madalali tuu wamekula kukufanya, na 150 billion ni ndogo sana Kwa Bandari kubwa kama yetu, pale tunahitaji at least trillion mbili Kila mwezi, kumbuka nchi sita zinategemea ile bandari, I hope atatokea kiongozi atakayeona utajiri wa hii bandari na kula nayo 100%
 
Propaganda tu,DP world wameanza kazi mwezi 2 hayo mapato ni kuanzia Julai,2023-May,2024.
Wastani wa mapato ya Bandari kwa mwaka hata kabla ya DP world ni 1 trillion,na miaka yote wamekuwa wakipeleka gawio la wastani wa 150 billion.
 
My Take
Mlisema Samia ameuza Bandari Kuna bango lenu hili hapa, ni spana tuu Kwa kwenda mbele.

View: https://www.instagram.com/p/C8Ht26kMeDf/?igsh=eWlxY2ljY3I3YnZ6

Tafuteni hoja nyingine 👇👇


“TPA (Mamlaka ya Bandari Tanzania) mwaka jana (2023) nina hakika kiwango chenu hakikuwa hiki, lakini kwa mageuzi yaliyotokea bandarini mmeweza kufikia kiwango hiki na mwakani tunatarajia kiwango kikubwa zaidi pengine mara mbili yake ya hiki mlicholeta leo, hakuna sababu kama mtaendesha bandari na sekta iliyopo pale na pale kuna watu wawili ambao tumeshawaruhusu.

Mmeomba maombi zaidi lakini hata wale wawili mwakani mnaweza kuleta mara mbili ya hiki kiwango na huko ndiko tulikuwa tunaelekea ndugu zangu . Wale waliopiga kelele mama kauza bahari sijui mama kauza bandari mama kauza nini mama kauza..mauzo yale faida yake ni hii hapa leo, na huu ni mwanzo tutatarajia kutapata faida kubwa zaidi kwa bandari zetu zote kubwa ambazo zipo ndani ya nchi”- Dkt. Samia.

View: https://www.instagram.com/reel/C8E2TrhNxHA/?igsh=MWNhMXI1cWM2dGVvMQ==

Watanganyika ndio wenye kelele, huwezi sikia upande wa pili wakilalamika, Fedha zimekuja na maendeleo tunayaona kama matund aya uuzwaji.
 
Back
Top Bottom