Rais Samia: Waliosema nimeuza Bandari na Bahari faida yake ndio hii

Rais Samia: Waliosema nimeuza Bandari na Bahari faida yake ndio hii

Kwa hiyo huyu mzanzibari kaja huku kuuza bandari zetu, stupid kabisa kauze bandari za huko kwenu zanzibar
 
My Take
Mlisema Samia ameuza Bandari Kuna bango lenu hili hapa, ni spana tuu Kwa kwenda mbele.

Tafuteni hoja nyingine 👇👇


======


“TPA (Mamlaka ya Bandari Tanzania) mwaka jana (2023) nina hakika kiwango chenu hakikuwa hiki, lakini kwa mageuzi yaliyotokea bandarini mmeweza kufikia kiwango hiki na mwakani tunatarajia kiwango kikubwa zaidi pengine mara mbili yake ya hiki mlicholeta leo, hakuna sababu kama mtaendesha bandari na sekta iliyopo pale na pale kuna watu wawili ambao tumeshawaruhusu.

Mmeomba maombi zaidi lakini hata wale wawili mwakani mnaweza kuleta mara mbili ya hiki kiwango na huko ndiko tulikuwa tunaelekea ndugu zangu . Wale waliopiga kelele mama kauza bahari sijui mama kauza bandari mama kauza nini mama kauza..mauzo yale faida yake ni hii hapa leo, na huu ni mwanzo tutatarajia kutapata faida kubwa zaidi kwa bandari zetu zote kubwa ambazo zipo ndani ya nchi”- Dkt. Samia.

View: https://www.instagram.com/reel/C8E2TrhNxHA/?igsh=MWNhMXI1cWM2dGVvMQ==

Mnafikiri mtawadanganya watz kwa hoja nyepesi kama hizi?

Kama gawio ni halisi mbona mmeenda kopa Korea ili mlipe madeni

Si mgetumia hela ya gawio kulipa madeni?

Acheni siasa za kitoto
 
We ja
Hawafanyi vizuri kama unavyosema wewe, wana underperform kulingana na uwezo wa Bandari Yao.

Pili sio sawa kulinganisha Kenya na Tanzania, wale ni business minded siku nyingi huku Tanzania ni wezi na wabinafsi.

Tatu hata nao wanatafuta wawekezaji vile vile
We jamaa mpumbavu sana

Kama bandari no sector sensitive unadhani kumpa dp word bandari kwa mikataba ya kifisadi ndo kutaongeza mapato ?
 
Kuna jinsi sijaelewa ukisikiliza dakika ya 50-51 anasema Mauzo yale ndio yameleta faida hizi. So kweli bandari zimeuzwa?
SI ulishaconclude bandari zimeuzwa kabla ya hapo, alafu unauliza Tena so ni Kweli bandari zimeuzwa!!??😂😂😂😂

Wabongo nuksi 😂😂
 
.." makabidhiano rasmi " si ndio kuanza kazi kwenyewe?

..kama hujakabidhiwa rasmi, maana yake si bado uko nje ya taratibu?
Wamejichanganya, tu wakati mwingine Mungu humsahaulisha mwizi ili amuumbue

Ingekuwa kweli bandari haina faida isingetoa gawio Leo

Kitendo Cha kutoa gawio kabla dp wahajatake over ni ushahidi tosha kuwa tunaweza endesha bandari wenyewe na kupata faida
 
Hatari sana, sidhani kama Rais yuko serious kweli na maendeleo ya Taifa hili au anawaza tu uchaguzi 2025.

Tuache kufanya mambo kwa kuwaza kushinda uchaguzi tu,tujaribu kupima sana performance zetu kwa kuangalia maslahi ya Taifa na vizazi vyake.
 
..kwa hiyo hilo gawio tumepewa na DP world?

..bila DP world tulikuwa hatuna uwezo wa kupata gawio hilo?
Adani naye kapewa juzi tayari tuna gawio! kwa mwendo huu mwakani hakuna kufanya kazi, tunasubiri magawio tu
 
153 bilioni kwa mwaka haiwezi kujustify walichofanya, kama tuna uwezo wa kukusanya 2000 billion kwa mwezi mapato ya ndani
153 Billion? Umepata wapi hizo figures. TPA tu ilikusanya zaidi ya 6 Trillion kwa mwaka so sidhani figures zako ziko sawa
 
Wamejichanganya, tu wakati mwingine Mungu humsahaulisha mwizi ili amuumbue

Ingekuwa kweli bandari haina faida isingetoa gawio Leo

Kitendo Cha kutoa gawio kabla dp wahajatake over ni ushahidi tosha kuwa tunaweza endesha bandari wenyewe na kupata faida
Tokea October 2023 Dp world ilianza kazi je miezi 9 haitoshi kutoa gawio?

Tuseme tu ukweli, hao TPA ni wala rushwa wakubwa hata JPM licha ya ukali wake walimshinda. So hata Dp World wakifeli ni kheri wapewe hata JWTZ ila sio kuwarudishia TPA maana ni majizi tu.
 
Una uhaakika gani mwaka huu hawajakopa kutoa gawio?
Kwa sababu balance sheet zinaonesha ikiwemo Mbeya Cement ambao wametoa Gawio Kwa mara ya kwanza baada ya hasara ya miaka 10 mfululizo.

Pili hakuna anaewalazimisha kutoa Gawio kama mambo Yao yameenda mrama kama awamu ya Jiwe ya maonesho.

Au wewe umeona TRC na ATCL wametoa Gawio? Maana hao wanakula hasara
 
Kwa sababu balance sheet zinaonesha ikiwemo Mbeya Cement ambao wametoa Gawio Kwa mara ya kwanza baada ya hasara ya miaka 10 mfululizo.

Pili hakuna anaewalazimisha kutoa Gawio kama mambo Yao yameenda mrama kama awamu ya Jiwe ya maonesho.

Au wewe umeona TRC na ATCL wametoa Gawio? Maana hao wanakula hasara
Wewe ndezi sana, sorry for disrespecting you mkuu.
 
Nikikumbuka gawio la TTCL na ATCL naishia kwa kusema let's wait and see.
Samia hafanyi maigizo,ambao hawapati faida Gawio la nini? Wanatoa wapi?

Na mama ndio alitumegea Siri kwamba hataki ule ujinga wa kampuni kukopa Benki na kutoa Gawio kama ilivyokuwa awamu ya 5.
 
Kwa kasi hii kumbe DPW watatufaa sana.Kama wamekabidhiwa rasmi bandari hata mwezi mmoja haujaisha wametoa gawio hilo,je baada ya mwaka mmoja itakuwaje.
 
Back
Top Bottom