ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 66,537
- 75,687
Ujumbe umewafikia Chadema na Mabwana zao Mabeberu.👇👇
Ndugu zangu wananchi ili tuendelee kupata tunayoyapata haya miradi ya kila aina, vituo vya umeme na mambo mengine msiende kufanya makosa (kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, Novemba 2024), kwanza dumisheni uhuru na utulivu katika wilaya yenu hii. Amani na utulivu ndiyo itakayowawezesha kufanya shughuli zenu za maendeleo, ndiyo itakayowawezesha muweze kwenda shambani kulima vizuri, kuvuna vizuri na kuja kuuza hapa (Kituo cha manunuzi ya mahindi cha Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA)) kwa raha kabisa. Amani na utulivu ndiyo inayotufanya hata majumbani tucheke, tukae vizuri tuangalie michezo ya kwenye runinga, kukiharibika hayo yote hayapo.
Niombe sana, wale wanaokuja kuwashawishi kwa neno lolote lile kwa sababu yoyote ile kuharibu amani na utulivu wa eneo lenu msikubaliane nao, ninataka kuwaambia kuwa wameishiwa, hawana pa kupenya, wameshaona mbele mambo magumu kwao, sasa wanalolifanya ni kuharibu amani na utulivu wa nchi yetu ili wananchi waishi kwa mashaka, muone nchi yenu siyo njema, ndiyo lengo lao, niwaombe sana msikubaliane nao"- Rais Samia.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema hayo mbele ya wakazi wa Mbinga alipotembelea kituo cha manunuzi ya mahindi cha Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA), Matika Mbinga Mjini Mkoani Ruvuma, Jumatano tarehe 25 Septemba, 2024.
View: https://www.instagram.com/reel/DAVpMalondE/?igsh=MXcxdGRrcDB1cWhraQ==
My Take: Hakuna Kibaraka ataruhudiwa kuvuruga amani ya Nchi hii,wafikishieni ujumbe waliowatuma.
Ndugu zangu wananchi ili tuendelee kupata tunayoyapata haya miradi ya kila aina, vituo vya umeme na mambo mengine msiende kufanya makosa (kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa, Novemba 2024), kwanza dumisheni uhuru na utulivu katika wilaya yenu hii. Amani na utulivu ndiyo itakayowawezesha kufanya shughuli zenu za maendeleo, ndiyo itakayowawezesha muweze kwenda shambani kulima vizuri, kuvuna vizuri na kuja kuuza hapa (Kituo cha manunuzi ya mahindi cha Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA)) kwa raha kabisa. Amani na utulivu ndiyo inayotufanya hata majumbani tucheke, tukae vizuri tuangalie michezo ya kwenye runinga, kukiharibika hayo yote hayapo.
Niombe sana, wale wanaokuja kuwashawishi kwa neno lolote lile kwa sababu yoyote ile kuharibu amani na utulivu wa eneo lenu msikubaliane nao, ninataka kuwaambia kuwa wameishiwa, hawana pa kupenya, wameshaona mbele mambo magumu kwao, sasa wanalolifanya ni kuharibu amani na utulivu wa nchi yetu ili wananchi waishi kwa mashaka, muone nchi yenu siyo njema, ndiyo lengo lao, niwaombe sana msikubaliane nao"- Rais Samia.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema hayo mbele ya wakazi wa Mbinga alipotembelea kituo cha manunuzi ya mahindi cha Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA), Matika Mbinga Mjini Mkoani Ruvuma, Jumatano tarehe 25 Septemba, 2024.
View: https://www.instagram.com/reel/DAVpMalondE/?igsh=MXcxdGRrcDB1cWhraQ==
My Take: Hakuna Kibaraka ataruhudiwa kuvuruga amani ya Nchi hii,wafikishieni ujumbe waliowatuma.