Nimefarijika kuona hiyo reli inaenda Kigoma, kwa lengo kuu la kusafirisha malighafi kutoka DRC.
Serikali ianze mikakati mapema ya kunufaika na malighafi kutoka Congo. Ikewezekana wajenhe mapema masoko ya madini ya kutosha tu huko Kigoma. Lakini pia wajenge mitambo ya kuchenjua hayo madini, ili yakitoka hapo; ni sokoni moja kwa moja.
NB: Relo iishie mpakani tafadhali. Utakuwa ni ujinga wa hali ya juu iwapo serikali itakubali kushirikiana na hizo nchi kwenye ujenzi wa reli ndani ya nchi zao. Maana sisi tunajenga kwa jasho letu.
Kamwe tusikubali madudu kama yale ya TAZARA! Yaani yale majamaa ni mavivu, na muda wote yanawaza starehe tu! Na mtazamo wangu, nahisi yanachangia karibia 60% kwenye kuizorotesha hiyo reli.
Na chakushangaza, sijui Wachina waliingia mkataba wa aina gani na hizi nchi mbili! Maana sioni sababu ya nchi zote mbili kuendelea kushirikiana kuiendesha hiyo reli ya TAZARA. I wish kila nchi ingejitegemea kuendesha reli yake.