Rais Samia: Wanaosema tunakopa sana, waseme pia tunalipa sana

Rais Samia: Wanaosema tunakopa sana, waseme pia tunalipa sana

Hii ya sasa tu haitumiki, watu wanaikwepa. Ukiwa na hotel nyota 3 alafu bado hupati wateja, solution sio kujenga ya nyota 5 hapo.bali unapaswa kujua kwa nn hiyo ya nyota 3 watu hawalali.

Reli ya tazara kuna shida kubwa ambayo ipo miaka na miaka, inapaswa kutatuliwa hiyo kabla ya kuijenga tena
Shida gani hiyo? Na reli ya Kati mbona haitumiki pia Ila inajengwa?
 
Nimefarijika kuona hiyo reli inaenda Kigoma, kwa lengo kuu la kusafirisha malighafi kutoka DRC.

Serikali ianze mikakati mapema ya kunufaika na malighafi kutoka Congo. Ikewezekana wajenhe mapema masoko ya madini ya kutosha tu huko Kigoma. Lakini pia wajenge mitambo ya kuchenjua hayo madini, ili yakitoka hapo; ni sokoni moja kwa moja.

NB: Relo iishie mpakani tafadhali. Utakuwa ni ujinga wa hali ya juu iwapo serikali itakubali kushirikiana na hizo nchi kwenye ujenzi wa reli ndani ya nchi zao. Maana sisi tunajenga kwa jasho letu.

Kamwe tusikubali madudu kama yale ya TAZARA! Yaani yale majamaa ni mavivu, na muda wote yanawaza starehe tu! Na mtazamo wangu, nahisi yanachangia karibia 60% kwenye kuizorotesha hiyo reli.

Na chakushangaza, sijui Wachina waliingia mkataba wa aina gani na hizi nchi mbili! Maana sioni sababu ya nchi zote mbili kuendelea kushirikiana kuiendesha hiyo reli ya TAZARA. I wish kila nchi ingejitegemea kuendesha reli yake.

bado natafakari namna gani Copper ya katanga inafika Kigoma then kwenye reli Dar es salaam..
 
..Raisi anazungumzia deni la taifa kimasihara sana.

..inaelekea hajui hatari ya deni hilo kwa uchumi wa taifa.

..pia haijui historia ya nchi hii na matatizo yaliyowahi kutukuta kutokana na kufumuka kwa deni hilo.

..kauli zake kuhusu masuala ya uchumi, fedha, na deni la taifa, zinathibitisha kwamba hakujiandaa, wala hakuandaliwa, kuwa Raisi.
 
Kikwete hakwepeki katika utendaji wa SSH anategemewa tatizo anao ushawishi wenye kundi kubwa la watu nyuma yake na baadhi yao ni wachafu sana.

..tatizo Dr.Ssh hana uwezo.

..angekuwa strong na muelewa wa kazi yake wasingejitokeza watu wa kutaka kumsaidia.

..Dr.Ssh anazungumzia nchi kukopa halafu anasema, "...kuna wakati tutaomba msamaha wa deni...," unadhani anatosha ktk nafasi yake?
 
Bora mama msema kweli. Kanyaga twende tumecheleweshwa mnooo kama taifa zaidi ya miaka 7.




Tunachokijua:
 
..tatizo Dr.Ssh hana uwezo.

..angekuwa strong na muelewa wa kazi yake wasingejitokeza watu wa kutaka kumsaidia.

..Dr.Ssh anazungumzia nchi kukopa halafu anasema, "...kuna wakati tutaomba msamaha wa deni...," unadhani anatosha ktk nafasi yake?
Kauli na vitendo vyake ni vitu tofauti. Ukubwa wa kazi anayoifanya bila ya kutumia nguvu kubwa kuyatangaza matokeo ya kazi ni umahiri alionao ambao marais wengi wanaume huwa hawana.

Tukio la kusaini mkataba wa SGR leo ikulu angekuwa rais wa kiume angehakikisha ardhi yote ya Tanzania mpaka ingetetemeka, lakini kwake ni tukio la kawaida tu lisilo na mbwembwe za ziada.

Namuona anatosha sana kwa mtindo wa kufanya kazi wa serikali alioamua kuja nao awamu ya sita.
 
Kauli na vitendo vyake ni vitu tofauti. Ukubwa wa kazi anayoifanya bila ya kutumia nguvu kubwa kuyatangaza matokeo ya kazi ni umahiri alionao ambao marais wengi wanaume huwa hawana.

Tukio la kusaini mkataba wa SGR leo ikulu angekuwa rais wa kiume angehakikisha ardhi yote ya Tanzania mpaka ingetetemeka, lakini kwake ni tukio la kawaida tu lisilo na mbwembwe za ziada.

Namuona anatosha sana kwa mtindo wa kufanya kazi wa serikali alioamua kuja nao awamu ya sita.

..kwa hiyo unasema tupuuze kauli au hotuba zake?
 
Makalla huwa hana hadhi ya kuwa mwanasiasa. Ana sura na muonekano wa mbeba mizigo wa bandarini. Huwa anaongea ujinga .
Linapokuja swala la kutia shombo basi wewe bi kinara humu, daah😂😂😂.
 
Bado najiuliza sipati majibu, ...kama tumeamua kujenga reli ya kisasa, SGR_TZ .... Pembeni ya reli ya zamani MGR_TZ:
1.Reli inakamikima, Kwa nini tuliamua kununua mabehewa ya mitumba badala ya mapya? Kulikuwa na haraka gani ya kuagiza mitumba badala ya kutoa order yanunuliwe mapya?
Mabehewa mapya ni kwamba unatoa order na linaanza kutengenezwa toka chasis. Haya makampuni ni kama ndege. Hawatengenezi kitu hadi kwa order, sio kwamba utaenda ukute mabehewa yamepangwa sokoni kama nyanya

Sasa order ya mabehewa mapya inaweza kuchukua miaka mitatu, wakati ya mitumba yanachukua labda kuanzia miezi sita, ndio maana wakaamua tuanze na ya mitumba wakati tunasubiri mapya, na ukizingatia mabehewa yaliyopo ni chakavu sana, yana kunguni na viroboto na breki zake nadhani ulishaona picha mitandaoni. Ukumbuk pia order ya mabehewa ni kwa ajili ya SGR na reli ya zamani.

Na pia kama ambavyo gari used la Mjapan ni sawa na jipya kwa Mtanzania, behewa used la Mjerumani ni sawa na jipya kwa Mtanzania. Wazungu hawana upuuzi wa kukojoa ndani ya behewa au kuchana viti makusudi

Swali ulilopaswa kuuliza ni kwamba - kwa nini hawakufanya timing ya order ya mabehewa na ujenzi wa SGR, ili ujenzi unapokamilika na mabehewa yanakuwa tayari - na jibu ni hapo ni watu wenye akili ndogo kupewa mamlaka makubwa.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Makalla huwa hana hadhi ya kuwa mwanasiasa. Ana sura na muonekano wa mbeba mizigo wa bandarini. Huwa anaongea ujinga .
 
Madeni makubwa hayajawahi kuwa kitu kizuri kabisa kwa mataifa maskini.
 
..Raisi anazungumzia deni la taifa kimasihara sana.

..inaelekea hajui hatari ya deni hilo kwa uchumi wa taifa.

..pia haijui historia ya nchi hii na matatizo yaliyowahi kutukuta kutokana na kufumuka kwa deni hilo.

..kauli zake kuhusu masuala ya uchumi, fedha, na deni la taifa, zinathibitisha kwamba hakujiandaa, wala hakuandaliwa, kuwa Raisi.
We unategemea mshauri mwenyewe Madelu, atakushauri nini, uchumi kausomea kwenye makaratasi
 
Madeni makubwa hayajawahi kuwa kitu kizuri kabisa kwa mataifa maskini.

Sijui Dr.Ssh alikuwa wapi au akijishughulisha na nini wakati wa awamu ya Rais Mkapa.

Kwasababu kipindi hicho tulikuwa na hali ngumu sana ya uchumi iliyosababishwa na deni kubwa la taifa.

Mwalimu Nyerere na Mzee Mkapa walihangaika kufanya kampeni kuziomba nchi wafadhili zitusamehe madeni hayo.

Leo hii Rais Ssh kutoa kauli zinazoashiria kwamba deni la taifa ni jambo jepesi, nadhani ni kutokujua historia ya nchi yetu na masuala ya kiuchumi, au ni jaribio la kulaghai wananchi.
 
Bado najiuliza sipati majibu, ...kama tumeamua kujenga reli ya kisasa, SGR_TZ .... Pembeni ya reli ya zamani MGR_TZ:

1.Reli inakamikima, Kwa nini tuliamua kununua mabehewa ya mitumba badala ya mapya? Kulikuwa na haraka gani ya kuagiza mitumba badala ya kutoa order yanunuliwe mapya?

2. Kama zimeagizwa Rolling Stock 5 mpya za kutumika kwenye reli mpya, kwa nini chaguo letu lilijikita kwenye treni zenye speed ya hadi kilometra 160 kwa saa? Kwa nini hatukuchagua kilometa 250-300 au hata zaidi, kwa maana ya kisasa zaidi, ukizingatia ukubwa wa nchi yetu yenye zaidi ya kilometa 900 elfu za mraba?

3. Wametumwa vijana wa kitanzania kwenda Korea ya kusini kujifunza namna ya kuendesha na kuhudumia wasafiri wa reli na treni yetu ya kisasa, Je,ni teknolojia ipi wanaenda kujifunza? ni hii ya MGR au SGR ?

Baada ya miaka kumi tutawatuma kujifunza tena baada ya hii teknolojia ya sasa tuliyochagua kuwekeza kupitwa na wakati?.

Maswali niliyonayo ni mengi mno kwenye uwekezaji huu....natamani kusoma maoni ya wengine kwenye uzi huu kwanza! [emoji848]
Ingekuwa kuna nafasi ya kuwauliza maswali haya papo kwa papo,hawa viongozi wetu wengi wangeshakufa kwa pressure ya kuulizwa maswali yenye akili wakati huo hawana uwezo wa kujibu kwa ufasaha
 
Back
Top Bottom