Rais Samia waonee huruma maskini wa Tanzania, watu wanakufa kwa kukosa dawa huku wengine wakichota mabilioni

Rais Samia waonee huruma maskini wa Tanzania, watu wanakufa kwa kukosa dawa huku wengine wakichota mabilioni

fazili

JF-Expert Member
Joined
Jun 10, 2011
Posts
16,427
Reaction score
22,418
Naomba kuchukua nafasi hii kuandika kwa kifupi kabisa ombi moja kwa niaba ya watanzania.

Nakuomba Mheshimiwa Rais wetu Mama Samia tafadhali wachukulie hatua za kisheria wote wanaohusika na ufisadi wa kutisha unaoendelea katika nchi yetu.

Tunakopa matrilioni, lakini tunapoteza matrilioni kizembe sana kila mwaka. Ukienda kwenye vituo vya afya utaumia sana kuona watu wakiachwa wafe kisa wamekosa shilingi laki 6 za kufanyiwa upasuaji mdogo. Akina mama wanajifungulia nyumbani kwa kukosa fedha za kulipia hospitali. Ni mengi mno ya hovyo yanaendelea.

Maofisini watu wanatamka waziwazi wanasema; wakati wa “kupiga” hela ni huu, mtu ashindwe mwenyewe tu.

Niombe tena kurudia ombi langu kwamba mheshimiwa Rais chukua hatua kali kwa wasaidizi wako la sivyo nchi hii itatafunwa kama kitumbua na kumalizwa na wachache wanaojipendekeza kwako! Kataa kusifiwa kinafiki!

Hali ya ubadhirifu sio nzuri hata kidogo chukua hatua kali! Walioiba fedha za umma sio tu waachishwe kazi ili wakatulie na kula walichoiba, bali pia warudishe fedha hizo kwa namna yoyote na kwenda jela!

Ahsante.
 
Naomba kuchukua nafasi hii kuandika kwa kifupi kabisa ombi moja kwa niaba ya watanzania.

Nakuomba mheshimiwa rais wetu Mama Samia tafadhali wachukulie hatua za kisheria wote wanaohusika na ufisadi wa kutisha unaoendelea katika nchi yetu.

Tunakopa matrilioni, lakini tunapoteza matrilioni kizembe sana kila mwaka. Ukienda kwenye vituo vya afya utaumia sana kuona watu wakiachwa wafe kisa wamekosa shilingi laki 6 za kufanyiwa upasuaji mdogo. Akina mama wanajifungulia nyumbani kwa kukosa fedha za kulipia hospitali. Ni mengi mno ya hovyo yanaendelea…

Maofisini watu wanatamka waziwazi wanasema; wakati wa “kupiga” hela ni huu, mtu ashindwe mwenyewe tu.

Niombe tena kurudia ombi langu kwamba mheshimiwa rais chukua hatua kali kwa wasaidizi wako la sivyo nchi hii itatafunwa kama kitumbua na kumalizwa na wachache wanaojipendekeza kwako! Kataa kusifiwa kinafiki!

Hali ya ubadhirifu sio nzuri hata kidogo chukua hatua kali! Walioiba fedha za umma sio tu waachishwe kazi bali pia warudishe fedha hizo kwa namna yoyote!

Ahsante.
Haa lini mtakuja kufaham pale kinachoita rahisi ni myth something which does not existing .tumepigwa
 
Naomba kuchukua nafasi hii kuandika kwa kifupi kabisa ombi moja kwa niaba ya watanzania.

Nakuomba mheshimiwa rais wetu Mama Samia tafadhali wachukulie hatua za kisheria wote wanaohusika na ufisadi wa kutisha unaoendelea katika nchi yetu.

Tunakopa matrilioni, lakini tunapoteza matrilioni kizembe sana kila mwaka. Ukienda kwenye vituo vya afya utaumia sana kuona watu wakiachwa wafe kisa wamekosa shilingi laki 6 za kufanyiwa upasuaji mdogo. Akina mama wanajifungulia nyumbani kwa kukosa fedha za kulipia hospitali. Ni mengi mno ya hovyo yanaendelea…

Maofisini watu wanatamka waziwazi wanasema; wakati wa “kupiga” hela ni huu, mtu ashindwe mwenyewe tu…

Niombe tena kurudia ombi langu kwamba mheshimiwa rais chukua hatua kali kwa wasaidizi wako la sivyo nchi hii itatafunwa kama kitumbua na kumalizwa na wachache wanaojipendekeza kwako! Kataa kusifiwa kinafiki!

Hali ya ubadhirifu sio nzuri hata kidogo chukua hatua kali! Walioiba fedha za umma sio tu waachishwe kazi ili wakatulie na kula walichoiba, bali pia warudishe fedha hizo kwa namna yoyote na kwenda jela!

Ahsante.
Hawawezi kutusikia. Wanachosikia nikutuongezea Tozo hawana huruma nasisi
 
Halafu akitoka hapo anapanda ndege kwenda kutafuta mikopo ya masharti nafuu.
 
Tatizo ni chama chetu cha CCM, na pengine na katiba yetu.
1. CCM wezi ni wengi kuliko waadilifu
2.Katiba yetu ni mbovu kuliko maelezo. Rais analazimika apate wasaidizi kutoka upande mmoja tu wa CCM (wezi). Katiba ina matobo mengi mno.
 
Mie nasubiri yale magari ya mitambo kuchimba visima virefu, hela ya Covid-19, sasa mnanichanganya nasiki hela imepigwa!
 
Naomba kuchukua nafasi hii kuandika kwa kifupi kabisa ombi moja kwa niaba ya watanzania.

Nakuomba Mheshimiwa Rais wetu Mama Samia tafadhali wachukulie hatua za kisheria wote wanaohusika na ufisadi wa kutisha unaoendelea katika nchi yetu.

Tunakopa matrilioni, lakini tunapoteza matrilioni kizembe sana kila mwaka. Ukienda kwenye vituo vya afya utaumia sana kuona watu wakiachwa wafe kisa wamekosa shilingi laki 6 za kufanyiwa upasuaji mdogo. Akina mama wanajifungulia nyumbani kwa kukosa fedha za kulipia hospitali. Ni mengi mno ya hovyo yanaendelea.

Maofisini watu wanatamka waziwazi wanasema; wakati wa “kupiga” hela ni huu, mtu ashindwe mwenyewe tu.

Niombe tena kurudia ombi langu kwamba mheshimiwa Rais chukua hatua kali kwa wasaidizi wako la sivyo nchi hii itatafunwa kama kitumbua na kumalizwa na wachache wanaojipendekeza kwako! Kataa kusifiwa kinafiki!

Hali ya ubadhirifu sio nzuri hata kidogo chukua hatua kali! Walioiba fedha za umma sio tu waachishwe kazi ili wakatulie na kula walichoiba, bali pia warudishe fedha hizo kwa namna yoyote na kwenda jela!

Ahsante.
Tanzania hakuna Rais kwasasa mpaka 2030..
 
Back
Top Bottom