Rais Samia: Wenye akili za kawaida ndiyo wananikosoa kusafiri nje

Rais Samia: Wenye akili za kawaida ndiyo wananikosoa kusafiri nje

Mkuu unajua GDP ya Botswana ni ngapi? Ni 15 Bilion USD, Tanzania ni 62 Bilioni USD,
Sijui hicho kipimo cha kuwa madini yanachangia 7% ya gdp umetoa wapi ila mimi takwimu ninazijua madini yanachangia 10% ya gdp, na inaonyesha 35% ya 15 ni ndogo kuliko na 10% ya 62
[emoji23][emoji23][emoji23] Unazidi kumdharirisha huyu akili za kawaida mkuu.[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Dar es Salaam. Rais Samia Suluhu Hassan amesema ziara zake za kikazi nje ya nchi zimekuwa na mchango mkubwa katika utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo nchini.

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo Jumatatu Julai 4, 2022 Ikulu jijini Dar es Salaam wakati wa utiaji saini mkataba wa ujenzi wa kipande cha nne cha Mradi wa Reli ya Kisasa (SGR) Isaka-Tabora chenye thamani zaidi ya Sh2 trilioni.

Katika hotuba yake, Mkuu huyo wanchi ametumia nafasi hiyo kujibu hoja za baadhi ya watu wanaobeza ziara zake za kikazi nje ya nchi.

“Kwa leo tumesaini mradi wa gharama Sh2.94 trilioni na Dar es Salaam-Mwanza ni Sh16.92 trilioni, siku ninasema tutajenga vipande vyote hivi sikujua pesa nitaitoa wapi lakini kwa sababu ya kufunguka, kufuata watu, kuita watu tuzungumze hii pesa imepatikana,”amesema.

“Tunakwenda kuanza awamu ya pili, tukaungane na wenzetu wa Kigoma. Kwa hiyo awamu ya pili pia tuko kwenye mazungumzo namna ya kuzipata hizo pesa, kwa hiyo mambo yote ni mazungumzo, tunapowaita watu, tunapowafuata kuzungumza matokeo yake ndio haya,

“Wenye akili za kawaida ni rahisi kulaumu ‘Rais anasafiri tu, Rais hakai, badala ya kutembelea mikoa anatembelea tu nje, lakini matokeo yake ndio haya.” amesisitiza
Kwa mkataba upi
 
Ilifika kipindi katika nchi hii alisafiri mpk kufikia hatua analipa mishahara ya wafanyakazi kwa pesa za mkopo!

Sema kujenga kazi
Na ndiye Rais pekee aliyetoa fursa kwa raia kukuza uchumi kwa kuruhusu raia kufanya biashara na shughuli za uchumi bila ya kulipa kodi yoyote,hali ambayo ilipelekea raia kukua kiuchumi na kufikia viwango vya kulipa kodi yenye tija kwa taifa.
Bila maono yake hayo mazuri na bora kabisa,TRA ingelikusanya nini?.
 
Nimeshuhudia matusi, dhihaka na ghadhabu za Watanzania leo baada ya mh Rais baada ya kutetea kusafiri nje kuwa wananikosoa wana akili za kawaida

''Wale wenye akili za kawaida ni rahisi kulaumu, wanasema ‘Rais anasafiri tu, hakai, hatembelei mikoa’, nikienda mkoani tajenga siasa ya ndani hakuna maendeleo, nikienda nje nakwenda kutafuta fedha za maendeleo.''

Swali akili za kawaida ndio zipi?

USSR
Kwa muendelezo huohuo Mama, ebu malizia kabisa kuwa hao wenye akili ya kawaida wala sijisumbue kukupigia kura 2025. Mentor wako aliwahi kutamka kama hivyo 2010 kwa wafanyakazi na bado kura alipata. Na wewe usiogope Mama. Wachane tu!
 
Kwahiyo siku hizi maendeleo hayaletwi na watazania wenyewe kama alivyokuwa akihubiri mwalimu ,bali wakubwa huko nje?
 
Kuna mtu aliwai kusema hii nchi inaendeshwa na mzee wa Msoga sasa naamini...mama samia ni kikwete alie changamka
 
Nimeshuhudia matusi, dhihaka na ghadhabu za Watanzania leo baada ya mh Rais baada ya kutetea kusafiri nje kuwa wananikosoa wana akili za kawaida

''Wale wenye akili za kawaida ni rahisi kulaumu, wanasema ‘Rais anasafiri tu, hakai, hatembelei mikoa’, nikienda mkoani tajenga siasa ya ndani hakuna maendeleo, nikienda nje nakwenda kutafuta fedha za maendeleo.''

Swali akili za kawaida ndio zipi?

USSR
Nakumbuka mada yangu sikuimalizia kuongea kwa dharau na kuongea kwa mamlaka. Well nisiongee sana wacha walio muweka wafurahie. Sisi tunamuomba Mungu. Atajibu sisi wa akili za kawaida asante.
 
Uzuri au ubaya hiyo miradi ilianza chini huyo alieshusha na tuliona ikitekelezwa kwa kasi kuliko sasa.

Africa atuna uchungu na nchi zetu, hatutaman maendeleo ya kweli ha nchi zetu kwa vizazi vya kesho, si tunajua leo nilipe vizuri ili kesho niende Dubai kwenye maendeleo ya vitu nikatanue kwenye vitu vyao, ila hamuwazi vile vitu walivioataje! Fungeni mikanda mjemge nchi zenu.
Hiyo miradi ingetekelezwa kwa Kasi kuliko Sasa ingekua imekamilika
 
Nimeshuhudia matusi, dhihaka na ghadhabu za Watanzania leo baada ya mh Rais baada ya kutetea kusafiri nje kuwa wananikosoa wana akili za kawaida

''Wale wenye akili za kawaida ni rahisi kulaumu, wanasema ‘Rais anasafiri tu, hakai, hatembelei mikoa’, nikienda mkoani tajenga siasa ya ndani hakuna maendeleo, nikienda nje nakwenda kutafuta fedha za maendeleo.''

Swali akili za kawaida ndio zipi?

USSR
MTIHANI HUU NAMKUMBUKA MAREHEMU
 
Waarabu wanachojua ni kuwinda tu kutalii wala hawajui shenzi kabisa na watumwa wao.
 
Tunaweza hata kujiendesha tukiamua. Shida yetu ni ufisadi na mifumo mibovu. Hata hizo anazokwenda kuhemea huko nje si zinaishia kupigwa tu na wajanja wachache?

Mpaka tutakapokuwa siriazi na ufisadi hakuna kitakachobadilika katika nchi hii.

Wachina mpaka walipoamua kuwa siriazi na ufisadi wao ndo kidogo wameweza kunyanyuka. Kule ukifisadika na ukagundulika ni kuuwawa tu hakuna cha msalie mtume. Wajapan kule utajiua mwenyewe kwa kuleta aibu kwenye ukoo wako na familia. Marekani utafungwa na kila senti uliyoiiba utairudisha.

Sisi jitu linatajwa kabisa laivu kuwa limekwapua bilioni 100 halafu halifanywi cho chote na lipo tu linazidi kudunda mtaani na jamii inalishangilia na kuliita eti lijanja toto la mjini. Ripoti ya CAG huwa inaibua pengine si zaidi ya robo ya ufisadi wote, imagine ufisadi wote ungewekwa hadharani. Ni zaidi ya nusu ya bajeti yetu ya taifa [emoji51][emoji51][emoji51][emoji706][emoji706]
Kama nchi imekosa hadi muafaka wa kuzalisha mafuta ya kula ya kutosheleza ilihali mashamba yapo, basi ni kipimo tosha cha kuwa omba omba.
 
Back
Top Bottom