DOKEZO Rais tuokoe Wananchi wako wa Dodoma Jiji juu ya dhuluma hii ya Mkurugenzi Jiji. Mkuu wa wilaya kashindwa

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
Mpaka leo suala hili halijatatuliwa..wananchi wamebolewa serikali haijui wanaishi wapi mwaka wa pili..kila wakienda kwa mkurugenzi wanarushwa na kupigwa kalenda mara MCHUMI hayupo mara mkurugenzi kaja mpya...viwanja walivyopewa fidia medeli block 157 kumbe walishawapa MSD yaani nchi inaenda kihuni sana
 
Wahuni Sana Nkuhungu broad acre Magige na Luisi wamengangania maeneo ya watu yenye upimaji kwakusingizia Wavamizi kama ni Wavamizi kwanini wasiwalipe wenye hati
Wezi Sana hawa uonezi mtupu na utawala Wilaya Mkoa wapo lkimya Rushwa tupu
Mtaka Rc alipo fuata haki itendeke wakamuhamisha
 
Mtaka alikuwa mtu yule...na kweli alikuwa tishio kwa inshu zao za udhulumati
 
Kwamba kuna mtu keshakula pesa yao?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mambo ya DP hayo
 
Nyie wagogo pamoja na kuletewa uwekezaji mkubwa kabisa wa majengo ya serikali, maofisi, watumishi wengi wa umma wamehamia hapo, inakuwaje Mkoa wenu bado masikini?
Mkuu nyie mkoa wenu upi ambao sio masikini
 
Kwa kifupi nyie watu 10 mmepigwa na kitu kizito kichwani. Ushauri wangu kama mna uhakika ni serikali iliwapanga nendeni mahakamani ila kwa ninavojua na maelezo yako kwa 100% mmekutana na matapeli waliotumia jina la serikali.
 
Hichi ndicho kilichobaki
 
Amkeni na mapanga, mkimsubiri mama mtakesha.

Sent from my Infinix X688B using JamiiForums mobile app
 
Jamani kuweni na huruma kidogo, mama mwenyewe hamumuoni anaomba kusaidiwa li nchi limegeuka zigo la misumari? Na hili likitizamwa mtaambiwa mnapiga kelele tu ama mnademka demka
 
Mpaka leo kimya hii nchi ngumu sana...watu zaidi ya miaka miwili baada ya kubomolewa hakuna fidia ..au kwa vile viwanja vya Morena hotel block C 157 medeli wakubwa Mmegawana na ndio mnashindwa kuwasaidia wananchi hawa kupata haki yao?
 
Rais Rais tunakuomba hii dhuluma inawatesa wananchi... mkurugenzi aliyepita Mafuru ni zaidi ya mnyama...yeye na na iliyokuwa timu yake mipango miji... Wameumuza sana wananchi wa Dodoma jiji
 
Kuna mtu aliwahi kuniambia nisifanye haraka kununua ardhi Dodoma. Dodoma kuna migogoro mingi sana ya ardhi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…