Mwanamageuko
JF-Expert Member
- Oct 31, 2010
- 8,604
- 5,583
Ukiwauliza wale walioambiwa wafunge mikanda miezi kumi na nane ya shida watakupa majibu.. ukiwauliza wale waliokuwa wakitembea kwa miguu ubungo mpaka temeke watakujibu... ukiwauliza ambao waliaminishwa luninga ni anasa hawatokaa kimya... ukiwauliza waliokimbizana na gari za ugawaji kisa nusu kilo ya dona la yanga na kibaba cha maharagwe hakika hawatonyamaa... usiishie waliovaa viraka na katambuga za kuwa mtoko... watakueleza kama kulipatikana maendeleo ama laa!!Baada ya kulivunja maendeleo yalipatikana?
Sawa. Sio kwamba yeye ndio alikuja kumaliza zote kwa mkupuo. Kwingine wapi zilikuwepo? Na hazipo tena,badala kuna nyumba za bati?. Hayo ndio maendeleoSingida, Dom, Tabora, Shinyanga n.k mbona bado kuna nyumba za tembe/nyasi?
Walioahidi kuziondoa tembe na nyumba za nyasi bado ni walewale na ndio haohao wanaoahidi kushuka kwa bei za umeme na saruji....Singida, Dom, Tabora, Shinyanga n.k mbona bado kuna nyumba za tembe/nyasi?
Hahahahaha...Yeye anawaza ndege....
Hakika bwashee!Sawa. Sio kwamba yeye ndio alikuja kumaliza zote kwa mkupuo. Kwingine wapi zilikuwepo? Na hazipo tena,badala kuna nyumba za bati?. Hayo ndio maendeleo
Mkuu ukiangalia kwa makini, utagundua kwamba mabaya mengi ya kuuwa uchumi aliyoyafanya mtangulizi wake msalaba wote alibebeshwa Mwinyi, na yale mazuri yote aliyoyafanya Mwinyi kuwaletea wananchi wake maendeleo alipewa Mkapa. Ndio maana leo ni kawaida kusikia mtu au kijana aliezaliwa miaka ya 90 anakwambia kwamba Mwinyi ktk utawala wake hajafanya kituBwashee una kumbukumbu nzuri sana.
cc: Pascal Mayalla na mrangi
Kama kazi ilikuwa ndogo kwa nini mtangulizi wake alishindwa mpaka tukawa tunatembea matako nje,vifo vingi vya watoto kwa ajili ya utapiamlo,kukimbizana na magari ya maiti(trekta)tukifikiri ni magari ya ugawaji nk?Kazi yake ilikuwa NDOGO SANA YAANI "KILA KITU RUKSA"....
Sisi walalahoi picha tulikuwa tunaenda kuangalia Drive in Cinema tulikuwa tunaangalia kibubububu huku tukipigwa na baridi na tulikuwa tukiludi home usiku kwa mchakamchaka sisi ndio tuliokuwa tunaishi mjini sijui hao wa vijijini ilikuwaje?Umesahau moja; Television( Tuliita video) nazo zikaruhusiwa kuingia nchini maana kabla, wengi walikuwa wanazisikia tu kwenye stori za vijiweni.
Anadhani ni madaraja sgr na ma wawa sijui madimbwi road na majengo haaaa hizi shule haijatusaidia kwa kiwango kikubwa mm ni mmoja waoHivi neno "Maendeleo" unalitafsiri vipi?
Akajiita "Mtukufu Rais".Baada ya kulivunja maendeleo yalipatikana kwa kufufua uchumi uliokufa enzi za mtangulizi wake. Bidhaa dukani zilijaa kama vile unga, sukari, mchele, ngano, mafuta ya taa na ya kupikia, sabuni za kuogea na kufulia. Maduka makubwa nayo hayakuwa nyuma watu wakaanza kuingiza TV, Redio na vitu mbali mbali vinavyotumia umeme. Pia magari ya kila aina yakaanza kuingia kwa wingi yakiwemo mabasi ya abiria, barabara zikapanuliwa kutokana na mahitaji ya kipindi kile, moja ya barabara na alama aliyoacha Mwinyi ni hii ya morogoro road ambapo lile daraja la manzese lilijengwa wakati wa utawala wake, shule za serikali ziliongezeka, na za binafsi pia zikajengwa kwa wingi, nguo za mitumba na dukani zikaanza kuingia kwa wingi hata ww leo unavaa kiatu kizuri, jinsi zuri na unaenda kunyoa salon kwa mashine, hizo ni juhudi za Mwinyi ktk kuwaletea maendeleo raia wake. hapo sijataja hospital nyingi za serikali na private zilizojengwa kwa wingi chini ya utawala wake including madawa nk. Hakika Mwinyi ameifanyia mengi ya kiutu nchi hii, na alikuwa na uwezo wa kuthubutu bila kujali nani anasema nini.
Hata lile Daraja la Manzese(Msufini)kipindi linajengwa na upanuzi wa ile barabara ya Morogoro yalikuwa ni maendeleo makubwa na yamfano kwa kipindi hichoNdiyo. Tulianza kununua na TV kuona kinachoendelea duniani ikiwemo Ligi ya Uingereza. Nayo hayop ni maendeleo. Tatizo mmekaririshwa na mwendazake kwamba maendeleo ni Flyovers za Ubungo kumbe hata uhuru wa mawazo na uhuru wa kujieleza ni maendeleo. Mwendazake ameliharibu Taifa na kupandkiza roho mbaya kwa wengi sana!
Kasesela alikuwa hakosekani hapo Drive in na alikuwa na tofali lake ambalo hakalii mtu mwingine!Sisi walalahoi picha tulikuwa tunaenda kuangalia Drive in Cinema tulikuwa tunaangalia kibubububu huku tukipigwa na baridi na tulikuwa tukiludi home usiku kwa mchakamchaka sisi ndio tuliokuwa tunaishi mjini sijui hao wa vijijini ilikuwaje?
Hizo cheche zilenge kuleta mzunguko mzuri wa pesa kitaa, vinginevyo cheche zake akawashie Moto tu.Mhuu mfano mzuri, Rias ngoja akalie kiti vizuri mtaona cheche zake.
Dudumizi, ulikuwa na umri gani wakati huo??Baada ya kulivunja maendeleo yalipatikana kwa kufufua uchumi uliokufa enzi za mtangulizi wake. Bidhaa dukani zilijaa kama vile unga, sukari, mchele, ngano, mafuta ya taa na ya kupikia, sabuni za kuogea na kufulia. Maduka makubwa nayo hayakuwa nyuma watu wakaanza kuingiza TV, Redio na vitu mbali mbali vinavyotumia umeme. Pia magari ya kila aina yakaanza kuingia kwa wingi yakiwemo mabasi ya abiria, barabara zikapanuliwa kutokana na mahitaji ya kipindi kile, moja ya barabara na alama aliyoacha Mwinyi ni hii ya morogoro road ambapo lile daraja la manzese lilijengwa wakati wa utawala wake, shule za serikali ziliongezeka, na za binafsi pia zikajengwa kwa wingi, nguo za mitumba na dukani zikaanza kuingia kwa wingi hata ww leo unavaa kiatu kizuri, jinsi zuri na unaenda kunyoa salon kwa mashine, hizo ni juhudi za Mwinyi ktk kuwaletea maendeleo raia wake. hapo sijataja hospital nyingi za serikali na private zilizojengwa kwa wingi chini ya utawala wake including madawa nk. Hakika Mwinyi ameifanyia mengi ya kiutu nchi hii, na alikuwa na uwezo wa kuthubutu bila kujali nani anasema nini.
Kile kichwa kibovu sana bora kiondolewe.Mama kuwa mwenyekiti wa chama sio dalili njema kwa boss wa bunge. Suruali inaweza kuanza kutoboka kwa nyuma kabla hajaona kwa mbele.
Heeeeee!!!,Boss wa chama anaweza kumkataa bosi wa Bunge jina lake likatupiliwa mbali kabla ya kupelekwa Bungeni.Inawezekanaje boss wa bunge awe na hofu wakati anapigiwa kura na bunge? Nilidhani ambaye anaweza kuwa na hofu ni boss wa Mawaziri kwa kuwa jina lazima litoke kwa boss wa Nchi
By the way kila la kheri Mama kwenye kupewa mikoba ya Chama
Kipindi hicho tulikuwa tunaongopeana tu huyu anaitwa Wan yu miluzi,Bruce mawani,Bruce kijeba, aisee kwa kweli tukikumbuka shida tulizokuwa tunapata kipindi kile halafu anakuja mtoto wa miaka ya90 anamtukana(mdhalau) Mzee Mwinyi unatamani kumchapa kibaoKasesela alikuwa hakosekani hapo Drive in na alikuwa na tofali lake ambalo hakalii mtu mwingine!
Nilikuwa sijui boss, but shukrani kwa clarifications zako.Heeeeee!!!,Boss wa chama anaweza kumkataa bosi wa Bunge jina lake likatupiliwa mbali kabla ya kupelekwa Bungeni.
Sent from my Infinix X688C using JamiiForums mobile app
Hapana yeye ndio alikataa utaratibu wa kuwaita/kumwita raisi mtukufu, akisema kwamb kwa imani yake (uislam ) utukufu ni wa Mungu tu pekee