Rais wa JMT akemea makundi yanayodai ufisadi umerudi. Je, ni makundi gani?

 
Hao ni kundi la mwendazake na genge lao na ndio Hilo halilali Ili kumfitinisha Rais na wananchi Ili aonekane hawezi..

Mfano yule Jamaa wa mtara alisema maji ya kuzalisha umeme yapo sasa iweje kuna Mgao? Inamaana watendaji maslahi walikuwa wanafanya kusudi na kupotosha Waziri matokeo yake ndio hizo kauli.

Ni vyema mama awapukutishe wote serikali na aweka pure safi yake,wakiwa nje ni rahisi kuwashughulikia na watakosa mwanya wa kumharibia.
 
Mara ya mwisho nimemsikia Mh. akisema hataongea tena bali kalamu itafanya kazi, leo vipi tena, kalamu imeisha wino?
Kinachotakiwa ni kuliondoa hili kupe,linaloitwa CCM,wanatuona sie mazuzu,analalamika nini wakati hili kupe ndo lipo nasi toka uhuru wetu?NAKERWA SANA NA HAWA VIONGOZI

Sent from my SM-A105F using JamiiForums mobile app
 
Ameanza kwa kuwachamba.Anaichamba mihuni iliyopo kwenye chama chake.Mihuni itakuwa imenuna sana huko ilipo!
Huo ni udhaifu mkubwa sana yaani rais mwenye mamlaka yote unawachamba wahuni?badala ya kuwatia adabu, inaonekana hiyo mihuni ina nguvu sana!!yaani Afrika vituko haviishi, yaani rais wa nchi naye analalamika , kama raia wake wanavyolalamika!!!mi CCM yote ni ile ile tu, na adui mkubwa wa utawala huu ni mihuni ya awamu ya tano!
 
Hao ni kama joka lenye vichwa vingi.Kuliangamiza unapaswa kwenda kwa tahadhari na mbinu za hali ya juu.Unapotaka kuyadhalilisha,yenyewe yanawaza upotee!Kazi ni kwako!
 
Mama anaamini akiwafokea basi wataacha😀😀😀😀😀😀😀
 
Ninachoshangaa yy hakuwa sehemu ya serikali hiyo?Kama alikuwepo kwa nn hakuresign kuonyesha haiungi mkono serikali hiyo.kama hakujiuzuru basi wote walikuwa sehemu ya mambo haya.nimbaya kumtwiga mzigo mtu ambaye hatunaye Wala hawezi jitetea.wakati yupo wote walikaa kimywa na hata walikuwa machampioni wa kutoa kauli tata leo hii kageuka yy ndo alikuwa mbaya pekee yake
 
Very weak president, yeye ndo Rais , hayo makundi Kwa nini asiyafute? Huo wizi Kwa nini asiukomeshee, kazi yake nini kulalamika au kuchukua maamuzi? Hana huo uwezo no dhaifu.
 
Leo kaamua mbwai mbwai, hatakubali kuangukiwa jumba bovu, aisee leo kachefukwa,ila hakuna namna so far ni Rais lazima akubali tu , na ikizingatiwa ni Chama hicho hicho

Alafu na Katiba ambayo haipo kuwasimamia viongozi hasa Rais ,kila aneingia anafanya anavyofikili
 
Hili lipo na linawezekana,ila subiri 2024 tukikaribia uchaguzi JPM ataimbwa sana na tutaenda sana ziara chato

Si inajua uchaguzi bila machinga hauendi.
Hii comment ni ya kuprint kabisa na kuifanyia lamination
 
Ng'ombe wa bwana Heri kala shambani kwa bwana heri! Walimane tuu.!
La msingi tarehe 9 aamue kuachana na kesi ya ubambikiaji kwani nayo ni jumba bovu awaache wale Sikukuu na familia zao.
 
Ukiona Rais aliyepewa jeshi,polisi,TRA,Wabunge 10,Takukuru,na wizara zote zipo chini yake halafu anakuja kulalamika eti bla bla na uwezo wa kuwajibisha anao jua ni "DHAIFU"
 
Ai
Ng'ombe wa bwana Heri kala shambani kwa bwana heri! Walimane tuu.!
La msingi tarehe 9 aamue kuachana na kesi ya ubambikiaji kwani nayo ni jumba bovu awaache wale Sikukuu na familia zao.
Aisee Mkuu nilitaka kusema ivyo ,KWAMBA Kama ndo anashutuka kuangukiwa na jumba bovu leo Basi amechelewa walishaanza kitambo muangushia jumba bovu ikiwemoa Kesi ya Mbowe ambayo alianza kusukwa kipindi Cha mwendazake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…