Rais wa Nchi anapofariki akiwa madarakani Nchi huwa katika nyakati za hatari zaidi kuliko wakati wowote ule

Huoni yeye kutangaza nia ili hali amekataza wengine wasiinue vichwa inaleta mkanganyiko kwamba kawekwa hapo kwa maslahi ya watu fulani?
CCM ina ada na kawaida zake....

Ni utamaduni wa kumuachia nafasi aliyepo madarakani.......

Mh.Rais SSH alikuwa VP na Sasa ni Rais kikatiba....atakuwaje hapo nje ya maslahi ya taifa?!!! 😳😳

Amefanya vyema KUKITULIZA CHAMA DHIDI YA MINYUKANO YA KUWANIA MADARAKA.....

#SiempreJMT
 
Kwa hiyo unamshauri samia suluhu hassan apunguze speed ya kuonesh nia ?
 
Uchunguzi Magumashi. Watuhumiwa namba moja kama kweli mnatafuta mchawi waanze na PSU ambao wako na Rais siku zote, masaa yote, dakika zote na sekunde zote.
 
Ulipofananisha MOSSAD na utopolo wa UVCCM waliojaa hapo St.Peter's nimekudharau sana.

Usirudie tena kufananisha MOSSAD na UVCCM.
Pole sana. Kwa africa ni #1. Mleta uzi anaonekana yupo well informed na this is just warning kwa wahusika. Ila ni hatari sana tena sana. Kumbe tuna vipindi vigumu sana mbele yetu kama taifa. Ina maana walioshangilia na wanaoendelea kushabikia kifo cha Dkt Magufuli wanaingia 18. Nimeogopa sana hii taasisi ya urais kumbe ni kubwa sana na inatisha.
 
Samia anahusika kwenye huo mchongo
 

Ndio nikijiuliza Mosad wajichunguze wakati wanajua walichofanya!!!!!!!
 
Unajua ndugu yangu wakati mwingine Mungu uruhusu jambo litokee pengine liwe baya au zuri anasababu zake. Mie si nabii wala mtume wala mchungaji.

Lakini mwaka 2019 niliota tupo Ikulu Dar, kuna sherehe kubwa lkn Magufuli hatumuoni, yupo tu Waziri Mkuu Majaliwa tukimuuliza Magufuli yuko wapi yeye hasemi anatuyeyusha.

Nikajiuliza sherehe kubwa ikulu? Tunakula vyakula kibao. Mwaka 2020, 2021 ndoto ilijirudia vile vile ila wakati huu nikaota Tanzania inarais mwanamke. Nikampigia Rafiki yangu mmoja nikamwambia labda uchaguzi wa 2030 Tanzania tutaongozwa na mwanamke. Anyway tukacheka yakaisha.

Mwaka 2021 February ndoto ile ikajirudia vile vile. Ila wakati huu watu walikuwa hawana raha, Usalama wa Taifa walikuwa busy. Nilijiuliza tu hii ndoto inamaana gani? Sikujali. Ndo baada kusikia Magufuli kafariki ndo sasa nikakumbuka ndoto nilio iota kwa miaka mitatu mfululizo.
Mtoa mada msije mkaniingiza kwa wale watu wakuchunguzwa. Tafadhali hii ilikuwa ndoto tu!
 
Niwakati ambao kama umepewa kurithi kiti basi kuongoza mka pale muda unaisha wa alie fariki nankukaa pembeni wenye nchi wamchaguwe wanaye mtaka ama usubiri kuona giza mbele kama giza liliwakumba watu wa zambia.
Hili umeliona leo tu. Wenye nchi wachague wanayemtaka ama asubiri Giza kama la Zambia??

ccm ilishakufa inadumu kwa nguvu ya kamba mbovu. Muda si mrefu itakatika.
 
Amenishangaza hapo kwa maslahi ya taifa. Mi siyaoni.
 
Wananchi ni watu wazima....

Katiba ndiyo DIRA ya kila aina ya utata....

Ndiyo maana ukaitwa msahafu...HISIA HAZIWEZI ZIKAWA JUU YA UHALISIA KATIKA MAISHA YAENDELEAYO....

Hatuwezi kuishi ndotoni....JPM is no more...haijalishi tulimpenda vipi....kumpenda kwake ni KUYAISHI yale mazuri aliyotufanyia....na hatutakiwi kumuishi peke yake bali mazuri ya Marais wote waliopita tokea kwa baba wa Taifa hayati JKN.....

Nchi ipo....
Itakuwepo hata baada ya vitukuu vyetu na marais wao .....

#NchiKwanza
#SiempreJMT
 


Kwa hiyo ile picha maarufu kule USA inawezekana ilikuwa ni kipimo?
 
Aisee Mungu alikutumia. Sasa ninavyoona kumbe tuna safari ndefu kwa sababu ukiangalia 90% ya viongozi wakubwa serikalini kuna kauli wamezitoa za kushangilia/kufurahia kifo cha Dkt Magufuli. Kumbe maskini hawajui kumbe ni kuidharau idara nyeti. Mpaka hapo 2025 haijulikani kabisa. Jambo lingine ilikuwaje Mama akatangaza nia wakati bado hata mwaka haujaisha???? Nani alimshauri???? Kwa sababu ukiangalia ni kama taifa bado lipo linaomboleza, yaani ni tofauti kama rais Dkt Magufuli angeondoka kupitia njia za uchaguzi nadhani Mama tungemzoea haraka na idara nyeti ingekuwa imejiandaa. Ila kwa hili mtu waliyemuandaa for almost a decade then aje afe kizembe tena kwa kufungiwa na taifa lipate taarifa tu ya kifo tena wengine wafanye sherehe dahhh sijui
 
Nilichokuwa naongea ni ufafanuzi wa hoja kuelezea juu ya hali ya utulivu hasa wa kisaikolojia na utawala kutokuwepo. Hii haimaanishi kuwa haya hayatokwisha. Yataisha ila ni kawaida ya binadamu. Hata nyumbani wazazi wanapofariki hali ya sintofahamu utokea, na baadae hali uwa sawa.
Kuhusu katiba ndugu yangu, katiba si jambo linaloleta maendeleo. Unaweza ukawa huna katiba bado ukapata maendeleo. Nchi nyingi za mashariki ya kati hazina Katiba lakini zimeendelea. Angalia tu huko Dubai. Waingereza hawana katiba iliyoandikwa lkn wameendelea.

Zamani hata wazee wetu hawakuwa na katiba lakini waliishi kwa kuwa na uongozi imara.
Kikubwa ni kupata viongozi weye nia njema ya kuleta maendeleo katika nchi, walio wazalendo. Kwani hii katiba tulionayo kuna sehemu inazuia maendeleo? Hakuna, shida tuna viongozi waliojaa tamaa na wabinafsi, Hii haijalishi wako chama tawala au wako Upinzani.
Pia demokrasia haitokaa ituletee maendeleo, wazungu wametutega nasi tumeingia bichwa bichwa. Angalia nchi zote zilizoendelea duniani pamoja na hiyo marekani, hazikuendelea kwa mfumo wa demokrasia. Marekani yenyewe wanawake wameanza kuruhusiwa kupiga kura miaka ya 60, wakati uhuru walipata toka karne ya 18.

Sweden ilikuwa nchi ya utawala wa Mfalme ambae alikuwa mkorofi na tunaweza mwita dikiteta, alilazimisha wananchi wake kulipa kodi, mambo mengi aliamua yeye mwenyewe. Lakini leo ukienda Sweden wanamuona ndo Baba wa Taifa lao, wanasema japo alikuwa dikiteta lakini aliwapa maendeleo, hawamsemi vibaya, na alipenda vita.

Dubai, mtawala wake wa kwanza aliota ndoto na kuanza kuijenga, hawana cha balaza la mawaziri. Alipofariki, mrithi wake akasema atatimiza ndoto ya aliepita kwanza, akimaliza anaanza naye anavyotaka dubai iwe. Angalia China, Ujerumani, Urusi na nyingi nyinginezo ulikuwa ni udikiteta ndo umeleta maendeleo.

Mfano tu angalia Zanzibar, Yale majengo ya Michenzani na kwingineko huko shamba, mabomba ya maji wao wanaita mifereji na barabara kwenda shamba, haya yote yalifanyika kipindi cha hayati Karume. Unaambiwa yeye hakuwa msomi ila alikuwa katoka nje, alisafiri akifanya kazi ktk meli, akaona dunia ilivyo. Alipokuwa Rais alikuwa anatamka tu, jenga hiki hivyo hayo majengo yalijengwa hata bila ramani yaani alitamka ujenzi ukaanza hata nae alishiriki katika ujenzi. Alieneza maji vijijini, na kujenga barabara. Haya yote alitamka na ikafanyika.

Nambie na demokrasia yetu, ni Rais gani wa Zanzibar kaweza fanya alofanya Karume.
Huyu Karume Mungu angeendelea muweka Zanzibar ingekuwa mbali, alikuwa kiongozi mwenye maono na maamuzi. Hiki ndo kinatakiwa. Wala hakuwa hawa wanasiasa wanaoilalamikia Bara kuwa inainyonya Zanzibar. Yeye alifanya. Na Zanzibar ilipiga hatua, Zanzibar ilikuwa ya kwanza kuwa na Television ya rangi Africa. Hii yote ni Karume.
Viongozi wa leo wamejawa tu na ubinafsi na tamaa za madaraka na kujitajirisha ila hawana maono na uzalendo. Wanabaki kusingizia mara katiba mara muungano.
 
Nikuulize swali,
Mfano raisi Magufuli alovogariki, unataka kusema nchi ilikuwa kwenye hatari? Kivipi? Hatari gani? Hebu fafanua?
Huyo aliyeandika huu uzi, anaonekana ni sukuma gang😁

Bado anaweweseka na kuondoka kwa Mwendazake
 
Kipindi baada ya Rais kufariki ni kigumu lakini sio kwa sababu ulizo orodhesha. Sinto fahamu hiyo inaweza kuleta vurugu ndio maana ni muhimu kufata utaratibu na kubadilisha viongozi kama ipasavyo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…