Rais wa nchi kuiita pesa ya nchi yake pesa ya madafu, kiongozi kweli huyo?

Rais wa nchi kuiita pesa ya nchi yake pesa ya madafu, kiongozi kweli huyo?

wakati mwingine nashindwa kuntofautisha profesa na diamond na sasa nimejua tofauti ya alama ya kujumlisha na msalaba...sijui nimepatia
heri diomond kuliko profesa yaahi diomond anautumia ubongo wake 80% ila profesa nut kati ya ubongo na mdomo ilibaki bagamoyo .yaani ingekuwa ni enzi zile za kutoa mtu mmjo wakato wa sikukuu auwawe kura yangu ingemuangukia huyu baraba na keshokutwa angebadilishwa jina agriiiii
 
Na mimi nna msemo wangu naombeni muupokee.
Shilingi 1600 ya tanzania ni sawa usd 1 au sawa na kusema TSHS 1600 =PESA MOJA YA KISHOGA...
YAANI:USD NI PESA YA KISHOGA.
je, kwa msemo huu niko sawa au nimedhalilisha usd over tshs!?
 
Kwani hela ya ''madafu'' ina maana gani kwa sababu inawezekana tunalaumu kitu ambacho kinabeba uharisia wa maneno.

Kwani kusema hela ya ''madafu'' ina madhara gani ya moja kwa moja katika uchumi wa nchi?

Naomba unieleweshe kwa sababu sifahamu msingi wa hoja yako.
usiyejua madafu ni nini basi wewe ukosawa na aliye tamka neno hilo akifikiri sifa, kumbe anajipalia makaa kwa kutudharau watanzania tunayetumia fedha hiyo, kwani yeye anatumia za escro.
 
Watanzania tukome kuwapa watu wa pwani Urais, hawa watu asili yao ni uvivu na kukaa vijiweni, hata jana pale Diamond kilikuwa ni kijiwe cha wazee/waswahili wa Dar wasiojitambua. Mambo kama hayo mimi sikuona kulikuwa na haja gani ya kuweka kijiwe, ilikuwa ni kuchukua hatua basi

Unadhihirisha ujinga wako
 
Mimi sioni tatizo lolote kwa sababu haliondoi ukweli na halileti athari yoyote katika uchumi.

Mbona maneno ya utani au wakati hata UK wanaita utawasikia wanaita pesa yao majina kama quid, nicker, bin lid, vile vile hata Wamarekani wanaita pesa yao majina kama bucks.
Ulishawahi kuwasikia Rais wa Marekani au PM wa UK anaita hayo majina pesa zao tena kwenye hotuba zao????
 
kinyungu ulitaka afanywe nini? hii ni hela ya madafu na itabaki kuwa ya madafu mbele ya dola. huwezi kutegemea jipya kwa sababu hujajiandaa kisaikolojia kumsikiliza Rais wa nchi. wewe kwako Rais ni FAM au WS sasa akiongea JK hatukushangai ukyasema unayoyasema maana hata wazee wa dar es salaam umewapa jina wazee wa vijiwe vya ccm. Rais hajadharau sarafu ya nchi yake kwani ndilo jina linalotumika mitaani.

kwaiyo unakubali alitumia Lugha ya mitaani?
 
Mtanzania: anaumia sana kwa gharama za umeme kulipia viongozi wa nchi hii ili wagawane, Haingii akilini kama Mkuu wa nchi anatetea majizi wa fedha na kusema fedha si ya umma ila na ya wanyonyaji toka nje, Jamani tanzania Viongozi wetu wanatupeleka wapi? halafu nashangaa mtu wa mungu anayemwogopa mungu anaunga mkono chama hiki kinachoongozwa na mkuu wa nchi, Pole mtu wa mungu huna mbingu kabisaaaa, huwezi kuenenda katika njia za waovu kamwe.
 
....nchi hii sote machizi tu,nilishangaa!
 
Watu wabishe kadirg watakavyo, ukweli ni kwamba rais alikosea, tena sisi wengne alarm ililia kichwan pale tu alipotamka maneno yale. Hakuna fahari wala manufaa kiuchumi kama unatumia fedha za kigen kwa matumizi ya ndan ya kawaida. Kama hujui, waulize wachumi na wachambuz wa siasa za kimataifa.

Kenya na SA wanatumia fedha zao kwa kila malipo ya ndan. Inakuwa ngumu kwa serikal kuwashawish wafanyabiashara kutumia shiling ikiwa rais mwenyewe haiheshimu. 'Hela ya madafu' ni kauli ya kejeli kwa kila anayeijua. Labda kama wengne mmejifunza jana.

Ikumbukwe, moja ya sababu kubwa ya Nyerere kuikataa IMF na WB ni mashart yao ya kushusha thaman ya shilng ili wakupe msaada. Kwahili, Mtei gavana wa BOT alipgwa chini haraka kama rad ya sumbawanga kwa kuafiki mashart yao. Huyo ndo rais mzalendo na anayeheshimu sarafu ya nchi yake.
 
Nilisikia na kusikitishwa sana. JK hawezi kuwa tofauti na aliyetamka 'vijisenti'.....hawa wote wanaashilia kutokujari pesa ya watanzania. Kwa undani zaidi wanaiona pesa ya kitanzania kuwa ovyo kabisa na hizo walizonazo (za kimarekani) ni bora kuliko. Hawa si 'watanzania' tena...japo ni viongozi wetu .
 
Mimi sioni tatizo lolote kwa sababu haliondoi ukweli na halileti athari yoyote katika uchumi.

Mbona maneno ya utani au wakati hata UK wanaita utawasikia wanaita pesa yao majina kama quid, nicker, bin lid, vile vile hata Wamarekani wanaita pesa yao majina kama bucks.
Je na zenyewe zina maana ya kukejeli fedha zao?
 
Kukejeli fedha ya Nchi haina tofauti na kukejeli bendera ya Nchi kwa kuiita dekio au taulo.
 
Wawekezaji wanaangalia kona tofauti, kwa mfano wewe ukisema huwekezi nchi yenye vita, wengine kwao ni opportunity ndio maana hata Kongo kuna wawekezaji, Sudan kuna wawekezaji, kwa hiyo wakati mwingine siasa, vita, thamani ya fedha, matamshi ya rais, sio vikwazo kwa mwekezaji yeye anaangalia atapata nini akiwekeza. Afrika ya Kusini iliwekewa vikwazo wakati wa utawala wa kibaguzi lakini wako waliowekeza pamoja na vikwazo hivyo. Kwa hiyo neno "hela ya madafu" sio kikwazo kwa mwekezaji makini na inawezekana ikawa ni opportunity iliyosababishwa na weakness ya upande wa pili. Unaweza kulinganisha Yen na $? au Yuan na $? au Stg na $? au na UG.Shs? KSh. nk? Mbona nchi hizo zina wawekezaji?

wawekezaji watakuja ni sawa. Lakini risk profile ikiwa kubwa kama vita na hali ya kutoaminika viongozi kama ilivyo bongo wawekezaji hao huongeza riba sana. Yaani investiment zinazokuja ni zile ambazo wawekezaji wake wanachukua faida hata kwa asilimia 200 au zaidi. Hiyo ndo inayosababisha tulalamike eti wawekezaji wanaokuja wanatupunja mfano kwenye dhahabu. Kwa kuwa risk yetu iko juu sana, wawekezaji hao huchukua returns kubwa mno kwa wasi wasi kwamba muda wowote mambo yao yanaharibika. Investiment za wawekezaji wa namna hiyo zinakuwa hazina faida yoyote kwa uchumi wa nchi kwani hata supplies zooote wananunua nje na ni sehemu ya masharti yanayotokana na risk ya nchi kuwa kubwa.

Wawekezaji walioko kongo au somalia, faida yao kwa uchumi wa nchi hizo ni karibu sifuri kwani kila kitu wanabeba. Wawekezaji wa namna hiyo ndo wengi tunaowapata ndo maana unaona wanakuja na mikataba yenye masharti ya ajabu ajabu; masharti ambayo hawayaweki wakienda nchi makini zenye low risk profile. Kwa ujumla risk profile yako inapokuwa juu ni balaa kwa nchi kwani gharama ya kufanya biashara iko juu na wawekezaji hutaka returns kubwa kubwa. Ndo maana unaona makampuni ya gas au gold yanayokuja kuwekeza Afrika yanakuja na masharti ambayo hawayaweki katika nchi nyingine, sababu ni risk profile ya nchi. Kwa vyovyote vile risk profile yako inapokuwa juu unaumia - kauli za viongozi zinachangia sana risk profile kuwa juu.
 
Kikwete siku zote amedhihirisha udhaifu kiuongozi na kifikra. Haelewi kabisa nguvu ya nafasi ya uraisi. Hotuba zake ukizichambua utaona ni utumbo mtupu.

.......na ndio maana hapendi Press Conferences bali hukimbilia kwenye kamera na mic zinazorekodi (bila kuulizwa maswali) ama Wazee wa Dar es Salaam walio wepesi kupiga makofi (na siyo wazee wa Mikoa mingine). Cha kushangaza ni wana habari kushindana kunadi vichwa vya habari ili kuuza habari zao (magazeti, redio nk).
Angekuwa kwenye press conference ANGELAZIMISHWA kufafanua hoja zake (nyepesi)...
 
Jaji Warioba aliongelea kumheshimu rais kwa sababu urais ni alama ya taifa.

Fedha za taifa ni alama nyingine ya taifa.

Inapotokea alama moja ya taifa (rais) inaidhalilisha alama nyingine ya taifa (fedha), inabidi tujiulize kama wanaomdhalilisha rais wanafanya makosa kweli au wamechoshwa na ukosefu wa nidhamu, staha na ujuzi unaoonyeshwa na rais kiasi cha kufanya watu waweke pembeni habari za Jaji Warioba za "rais ni alama ya taifa" na kumnanga JK tu.

Waingereza wanasema "Respect is earned", Waswahili wanasema "Jiheshimu uheshimike".

Rais anayeiita fedha ya nchi yake "hela ya madafu", anategemeaje kuheshimiwa?
 
Kunatofauti kubwa sana kati ya rais wetu na marais wa nchi zingine
 
Back
Top Bottom