TANZIA Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli afariki Dunia kwa ugonjwa wa Moyo hospitali ya Mzena jijini Dar

Status
Not open for further replies.
Unajibishana na watu wa humu? Utajipa makasiriko ya bure kama una roho nyepesi.
 
Acha unafiki wa kutusemea wengine,wakati wewe unafurahi sisi wengine tulikuwa kwenye mateso makali,kutesa kwa zamu sasa.
 
Nadhani adhabu tunaipata sie tunaobaki tukisikitika. Ila kusema kuwa fulani amekufa Mungu amemuadhibu sio kweli...maana wapo waliokufa ambao jamii/familia inawapenda na kuwakubali.
.
.
Kifo kina sababu ..inaweza ikawa ni nzuri au mbaya. Wanaofurahia hiki kifo cha Rais wetu hebu tuone Kama maisha yao binafsi yatabadilika. Ningependa warudi hapa miaka miwili ijayo kutoa ushuhuda.
 
Siwezi kuhukumu, la muhimu tuishi kwa kufanya mazuri zaidi ya mabaya, kwani siku, saa na dakika ya kuondoka hatuijui.
Wabaya wataendelea kuwa wabaya, na wazuri wataendelea kuwa wazuri au wanaweza kuwa wabaya pia.

Kiufupi mabaya yapo siku zote na hakuna kifo cha mtu kitakachombadilisha mtu mbaya kuwa mzuri.
 
Duniani tunapita tu tujaribu kutendeana mema maana hatujui siku wala saa .apumzike alipojichagulia
 
Huo ni mtizamo wako siwezi kukupinga ,kama Katelephone kadanganya mimi ni nani nisilete cheti cha kufoji? Kama wachina wamoji hati ya NEMC wakisaidiwa na maofisa wa serikali,mimi ni nani? Hapa kazi tu... mi7 tena.
Sawa boss
 
Daa Hii laana hii sijui nchi sasa inaelekea wapi
 
Kila nikipitia hizi coment nawaza hivi ule uwekezaji wa kule chato ndo tumeshakula hasara!
Aisee acha tu, Kama ile hifadhi ya Burigi naskui hata wale simba waligoma kabisa kuishi pale
 
Nilidhani Wazungu hawayajui ya Tanzania au hata Majirani zetu nao hawajui yaliyokuwa yakitendeka na kwamba tuliokuwa tunajua ni Sisi Watanzania tu Wenyewe.

Mama Samia Suluhu Hassan nakuomba sana Mama Ukiapishwa tu anza Kwanza Kusafisha Nyumba Tanzania kwani kwa niliyoyasoma huko ni dhahiri shahiri kuwa Nyumba yetu ilikuwa imeshachafuka vya Kutosha.

Wewe ni Mwanasheria Kitaaluma ( kama sijakosea ) lakini pia najua umeiva sana Kidiplomasia hivyo Uzoefu wako huo utakusaidia na kuiweka Tanzania katika Usafi kwani ilikuwa imeshachafuka vya Kutosha. Tafuta Watu sahihi wa Kukusaidia ila pia kuwa Makini kwani kwa sasa Wewe ni Twiga uliyezungukwa na Simba, Nyati pamoja na Chui wengi.

Mwenyezi Mungu atusimamie Mama Samia.
 
Nawaza kama ATCL, SGR na Stieglers gorge vita-survive
Wenye malori ya mizigo watahakikisha SGR hai take off.
Stieglers itaendelea.
ATCL. Ikiwa British airways, KLM, Emirates wanapumzisha ndege itakua sisi?
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…