TANZIA Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli afariki Dunia kwa ugonjwa wa Moyo hospitali ya Mzena jijini Dar

TANZIA Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli afariki Dunia kwa ugonjwa wa Moyo hospitali ya Mzena jijini Dar

Status
Not open for further replies.
Wazungu na Waafrika wametoa Madukuduku yao juu ya hali ya Tanzania ( hasa Kiutawala, Kidemokrasia, Kiustawi na Kimwenendo wake ) mzima kuliko vile ambavyo Sisi tuliopo hapa hapa nchini tungeweza Kuelezea ( Kuchambua ) Kiundani zaidi.
Sisi siyo kisiwa, na nakumbuka maneno yako kwamba tusijidanganye kuwa wazungu hawajui tunachofanya.
 
Mimi ninachosema tu ni kuwa Magufuli atakumbukwa sana kwa mengi, sio wanachato tu, sio kwa SGR na reli ya kisasa tu.

Hata kama hakupendwa na wengi ila atakumbukwa na wengi.
We ngoja mambo yachanganye watu si wanaona ni heri ila tutamkumbuka sana kwa mazuri ila kwa kweli hichi kifo cha huyu mtu kimenitoa katika amani ya moyo sana, hakuna binadamu mkamilifu
 
Taarifa walikua nazo. Lakini nadhani walikua na hopes halafu pia kuepusha taharuki nadhani hivyo walivyofanya ni sahihi despite the bad credibility walopata

Tuanze kuuza midege maana inatuingiza hasara tu.
Mjomba mpaka 2025 mambo yatakuwa zigizaga, tatizo one man show ndiyo imetufikisha hapa. Kifo kinaumiza haijalishi mtu aliishi vipi na watu duniani lakini kuna vifo vinaweza kuepukika. Hawa watu waache sasa sayansi ifanye kazi mambo ya nyungu sijui nini nini ni porojo tu zisizo na kichwa wala miguu
 
DUH, RAIS WETU, ILA MUNGU ATUPE WEPESI
Mungu nakushuru sana kwa maisha ya kiongozi wetu Dr Joseph Pombe Magufuli. Alikuwa mzalendo kweli kweli na pengo hakika litakuwa ni kubwa. Tunakuomba Mungu wetu utupe faraja yako ya kweli na ulivushe salama taifa letu. Amen.
 
Wewe kweli umevurugwa,Bunge na Baraza la Mawaziri vina kazi gani,mbona watangulizi wake hawakufanya hivyo?
Jamaa amechanganyikiwa upigaji tena hakuna,mbuyu waliokuwa wameegemea umedondoka.

Nasikia lissu angekuwa Rais bc ungepata nafasi mzur huko serikalini
Mkuu sipo kabisa kwenye siasa na wala sitakuja kujihusisha na siasa ila nitatumia haki yangu kikatiba kutoa maoni,kwahiyo haya ni maoni yangu na wala sitaki cheo chochote,kazi yangu ya kuchoma mkaa,udalali na ufundi ujenzi unanitosha kuendesha maisha.
 
IMG-20210317-WA0012.jpg

Kwanza natoa pole kwa Watazania wote walioguswa na msiba huu. Tuko kwenye kipindi kigumu na chenye majaribu mengi.

Pamoja na yote haya nitoe rai kwa watanzania tusife moyo, Tanzania ni nchi iliyo simama kwenye nguzo za amani, utu na kujitegema.

Mzee wetu ametuacha tukiwa mahali ambapo tunaliona jua linachomoza. Ametupa moyo kama tukijaribu tunaweza. Leo hii Tanzania katika ukanda huu ndio nchi inauwezo wa kujilisha bila kutegemea senti tano ya mfadhili.

Kila sekta imeguswa na inamuelekeo au roadmap. Tunapata picha kama yajayo yanafurahisha. Si umeme, si usafirishaji, si rushwa, madini hata muungano. Ni kipindi cha maombolezo lakini ni kipindi cha kusherekea maisha ya mtu aliyejitolea maisha yake kwa manufaa ya ustawi wa Tanzania.

MUNGU IBARIKI TANZANIA.

 
Kwanini afya ya mtumishi wetu ifichwe na ifanywe Siri? No hili wanaohusika wametukosea watuombe radhi afya ya Rais wa nchi inafanywa Siri? Kwanini tusingeambiwa tukamuombea pengine angepona maana Jambo lolote mola hulibadili kwa maombi

Sent from my Infinix X624 using JamiiForums mobile app
Ukizingatia kuwa alikuwa muumini wa maombi na siku zote alitutaka watanzania tumuombee
 
Nasikia mpak 2025.
Cha muhimi atibu madonda ya chuki yaliyopandikizwa na boss wake.
Watu warudishiwe uhuru wao.
Inakera sana kuishi kwa uoga nchini mwako.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Umeandika mambo muhimu sana mkuu.

Natumaini Rais Samia atalitambua hili.

Kama kuna kazi anayoweza kuifanya na kujijengea heshima kwa waTanzania, huyu mama ajikite zaidi katika kujenga mshikamano wetu kitaifa.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom