Rais wa Zanzibar tafuta washauri wazuri suala la ardhi ya Bagamoyo

Rais wa Zanzibar tafuta washauri wazuri suala la ardhi ya Bagamoyo

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2015
Posts
18,487
Reaction score
13,611
Hili sakata la ardhi ya Bagamoyo ya hekari elfu sita kuwa ni mali ya Zanzibar lina ukakasi na halifai kupita bila ya kupata mawazo mbalimbali yenye lengo la kuboresha uelewa mpana wa raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Ni kweli Mwalimu Nyerere aliwapa Zanzibar ardhi ya Bagamoyo ili waweze kulima miaka hiyo ya sabini, hilo halina ubishi. Na pia ni kweli hayati Rais Magufuli akaja kuwapa wawekezaji wa Azam ardhi hiyo hiyo ili wafanye shughuli zao halali.

Kumuona Charles Hillary akipiga mkwara kwamba ardhi hiyo ni mali halali ya Zanzibar ndio kinapokuja kichekesho chenyewe.

Cession ni mchakato ambao sehemu ya ardhi ya nchi moja inatolewa rasmi na kuwa ni mali ya nchi nyingine, zipo sababu nyingi zenye kuyafikia maamuzi hayo.

Kwa kiswahili tunaita KUKOMA, yaani ardhi hiyo inakoma kuendelea kutumiwa na wakazi wa nchi husika inakuwa ni sehemu halali ya nchi nyingine na kiutaratibu inawekwa bandera ya nchi iliyoichukua kuanzia siku hiyo inapokoma kuwa ni mali ya nchi inapopatikana ardhi hiyo.

Je tangu miaka hiyo ya sabini kuna bendera yoyote inayopepea hapo Makurunge Bagamoyo kuonyesha kukoma kutumika kwa kipande hicho cha ardhi?, haijawahi kuwekwa bendera ya Zanzibar kuonyesha kuwa sehemu hiyo imekoma kuwa ni mali ya Tanzania, kiutaratibu bado ukubwa wa nchi ni ule ule unaotambulika kisheria tangu Tanzania ianze kuwa nchi kamili mwaka sitini na nne.

Hayati Rais Magufuli alikuwa na haki kabisa kumpatia muwekezaji Bakhresa sehemu ya ardhi iliyo chini yake kwa mujibu wa katiba. Kitendo cha Rais Mwinyi kuja na agizo la kufukuza waliopo katika ardhi hiyo wakati mchakato wa Cession haukuwahi kufanyika ni kosa la kiufundi la serikali anayoiongoza.

Naona kama wenye mamlaka ya kumshauri Rais Samia wameamua kutulia kwanza kutazama upepo wa huko juu utapita vipi. Wameliona hili kosa la kiufundi na nahisi ni suala litakalomalizwa kimya kimya tofauti na ule mkwara wa Charles Hillary alioutoa mbele ya media kule visiwani Unguja.

Mchakato wa Cession haukufanyika na hakuna bendera mahali pale yenye kuonyesha kuwa eneo limeshamilikishwa moja kwa moja kwa serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Hayati Magufuli alikuwa na haki zote kuligawa eneo hilo na pengine sababu za Mwalimu Nyerere kuwapa serikali ya Mapinduzi miaka hiyo ya sabini hazikuwa na mashiko ya muda mrefu, zilikuwa ni temporary measures.

Rais wa awamu ya nane Zanzibar na washauri wake wamechemka katika suala hili, warudi nyuma na wajipange upya kabla ya kutoka hewani na matamko yenye kuzua maswali mengi yenye utata ndani yake.

THE LAND WAS NOT CEDED TO ZANZIBAR BUT GIVEN FOR USE BUT STILL UNDER TANGANYIKA.
 
Ardhi hiyo bado ni mali halali ya Serikali ya Zanzibar, Azam watafute namna ya kusuluhisha huo mgogoro. Mwendazake alikurupuka. Unless kuna formal instrument iliyo revoke ownership ya SMZ. Still revocation inafanywa kwa public interest. Sasa tuhoji, is it a public interest kuinyang'anya ardhi SMZ na kumpa AZAM?
 
Laiti wangejua haya wangewapa wazenji wajenge sana eneo hilo ila ndio basi tena.

Kama walidhani litabaki pori lao ni kosa na waalijutie tu

Miaka ya 70 kulikuwa na hamasisha nchi kwa kuwapa wananchi wote eka 3 kulima.

Wengine wakiwemo wafanya biashara.

Sasa mfanyabiashara akaamua kuliacha bila kuliendeleza bali kulima tu.

Serikali ikaamua kuchukua hiyo ardhi na kusema kwanini hamkuiendeleza hata kujenga kanyumba?

Labda ntapata jibu hapa na mimi nikadai ardhi niliyopewa na Nyerere
 
Mtoa mada, Charles kasema ni mali ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanxibar na sio sehemu ya Zanzibar, bendera haikuhitajika kuwekwa kwa vile inabakia kuwa ni sehemu ya Tanganyika.

Kama hiyo ardhi ilikuwa haitumiki, however, mimi sioni ubaya kupewa mtu mwengine ambaye ataitumia na kuleta manufaa kwa Taifa.

Having said all that, hii ardhi walipewa Zanzibar kama ni fidia kwa kukubali kuunganisha vyama na kuunda CCM. In other words, waliiuza Zanzibar kwa kipande cha ardhi ndani ya Tanganyika.
 
Hivi siwanasemaga kwamba Rais wa jamuhuri wa muungano wa tz ndio in charge Wa ardhi yote Tanzania bara sasa kama Magufuli alibatlisha umiliki Wa ardhi hiyo kutoka nchi ya Zanzibar na kumpa Azam shida ikowapi? maguru Wa sheria watufafanulie .
 
Ardhi hiyo bado ni mali halali ya Serikali ya Zanzibar, Azam watafute namna ya kusuluhisha huo mgogoro. Mwendazake alikurupuka
Mwinyi ndio amekurupuka. Haikuwekwa bendera ya Zanzibar hapo Bagamoyo. Nyerere hakuondoa hata kilometa moja ya eneo la Tanganyika na kuisalimisha kwa visiwa vya Zanzibar.
 
Mtoa mada, Charles kasema ni mali ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanxibar na sio sehemu ya Zanzibar, bendera haikuhitajika kuwekwa kwa vile inabakia kuwa ni sehemu ya Tanganyika.

Kama hiyo ardhi ilikuwa haitumiki, however, mimi sioni ubaya kupewa mtu mwengine ambaye ataitumia na kuleta manufaa kwa Taifa.

Having said all that, hii ardhi walipewa Zanzibar kama ni fidia kwa kukubali kuunganisha vyama na kuunda CCM. In other words, waliiuza Zanzibar kwa kipande cha ardhi ndani ya Tanganyika.
Kuweka bendera hapo Bagamoyo huku Rais Nyerere akiwa ameridhia ndio kungekuwa ni urasimishaji wa eneo husika liwe ni mali ya Zanzibar.
 
Mwinyi ndio amekurupuka. Haikuwekwa bendera ya Zanzibar hapo Bagamoyo. Nyerere hakuondoa hata kilometa moja ya eneo la Tanganyika na kuisalimisha kwa visiwa vya Zanzibar.
Mkuu, SMZ ni taasisi katika JMT, ni taasisi iliyopo kwenye katiba ya JMT hivyo inaweza kumiliki mali ikiwa pamoja na shamba. Hilo shamba ni lao na wana nyumba na mali nyingine huku TZ bara kama ilivyo taasisi kama BoT ilivyo na mali kule visiwani. Nadhani utaelewa
 
Laiti wangejua haya wangewapa wazenji wajenge sana eneo hilo ila ndio basi tena.

Kama walidhani litabaki pori lao ni kosa na waalijutie tu

Miaka ya 70 kulikuwa na hamasisha nchi kwa kuwapa wananchi wote eka 3 kulima.

Wengine wakiwemo wafanya biashara.

Sasa mfanyabiashara akaamua kuliacha bila kuliendeleza bali kulima tu.

Serikali ikaamua kuchukua hiyo ardhi na kusema kwanini hamkuiendeleza hata kujenga kanyumba?

Labda ntapata jibu hapa na mimi nikadai ardhi niliyopewa na Nyerere
Ardhi yote ya Jamhuri ya Muungano inamilikiwa na Rais. Hivyo JPM alikuwa na haki kumpa Bakhresa eneo la kuwekeza akiwa ndio mmiliki mkuu wa ardhi yote.

Iwapo angekuta ni eneo lenye bendera ya Zanzibar na Mwalimu Nyerere akiwa amelisalimisha kwa majirani zetu asingeweza kulitoa kumpa Bakhresa ili awekeze,

Rais Mwinyi analeta ujeuri usiokuwa na msingi, anapenda mno kuonyesha anazo nguvu za kushindana na mamlaka ya Jamhuri ya Muungano, huwa anakwaruzana na baadhi ya wakurugenzi wa mamlaka za kiserikali kwa kigezo hicho hicho cha urais wake.
 
Mkuu, SMZ ni taasisi katika JMT, ni taasisi iliyopo kwenye katiba ya JMT hivyo inaweza kumiliki mali ikiwa pamoja na shamba. Hilo shamba ni lao na wana nyumba na mali nyingine huku TZ bara kama ilivyo taasisi kama BoT ilivyo na mali kule visiwani. Nadhani utaelewa
Huyo Charles Hillary amekosea kuagiza wakati huku kuna serikali nyingine yenye mamlaka kamili.

Elewa vyema maana ya Cession kabla ya kusema kuwa Zanzibar wana haki na eneo hilo la Bagamoyo. Mwalimu Nyerere aliwapa eneo lakini hakulitoa kutoka katika himaya ya Jamhuri na likawa ni sehemu ya Zanzibar, kwa kufanya hivyo ingesimikwa bendera ya Zanzibar.
 
Husein Mwinyi siku zote namuona empty kabisa ..manake Kwa makusudi anamchonganisha Samia na watanzania bara.

Kama anaona ana ardhi huku Tanganyika asubiri Samia akishaondoka ndo wallet hayo madai.

Kafanya upumbavu sana kumtuma Charles Hillary kutangaza upuuzi ule
Anapenda kutunishiana misuli na mamlaka za huku na haswa akimuona Samia mwanamama ndio rais.

Asingefanya huu utoto kama JPM angekuwa hai mpaka leo hii.
 
Huyo Charles Hillary amekosea kuagiza wakati huku kuna serikali nyingine yenye mamlaka kamili.

Elewa vyema maana ya Cession kabla ya kusema kuwa Zanzibar wana haki na eneo hilo la Bagamoyo. Mwalimu Nyerere aliwapa eneo lakini hakulitoa kutoka katika himaya ya Jamhuri na likawa ni sehemu ya Zanzibar, kwa kufanya hivyo ingesimikwa bendera ya Zanzibar.
Hakuna issue ya cessation, mwenye mali yoyote ana haki ya kutoa tamko ili watu wasije vamia na wavamizi watambue na wachukue hatua stahiki ikiwa ni pamoja na ku-vacate
 
Hivi siwanasemaga kwamba Rais wa jamuhuri wa muungano wa tz ndio in charge Wa ardhi yote Tanzania bara sasa kama Magufuli alibatlisha umiliki Wa ardhi hiyo kutoka nchi ya Zanzibar na kumpa Azam shida ikowapi? maguru Wa sheria watufafanulie .
Umeuliza vema mno, ndo nilichotaka kuuliza pia.
 
Hakuna issue ya cessation, mwenye mali yoyote ana haki ya kutoa tamko ili watu wasije vamia na wavamizi watambue na wachukue hatua stahiki ikiwa ni pamoja na ku-vacate
Cession inaonyesha uhalali wa umilikaji wa ardhi kumbuka inakwenda sambamba na usimikaji wa bendera yenye kuonyesha kipande cha ardhi sio mali ya nchi husika. Au kitu chenye kuonekana na kushikika mfano uwepo wa hati ya eneo husika.

Mwinyi kasubiri mpaka Bakhresa kakabidhiwa eneo tena na hayati JPM ndio anakuja kudai ardhi!!. Hayati JPM alikuwa na vigezo vyake na katiba ilimruhusu kumpa Bakhresa eneo la kufanya uwekezaji.
 
Cession inaonyesha uhalali wa umilikaji wa ardhi kumbuka inakwenda sambamba na usimikaji wa bendera yenye kuonyesha kipande cha ardhi sio mali ya nchi husika. Au kitu chenye kuonekana na kushikika mfano uwepo wa hati ya eneo husika.

Mwinyi kasubiri mpaka Bakhresa kakabidhiwa eneo tena na hayati JPM ndio anakuja kudai ardhi!!. Hayati JPM alikuwa na vigezo vyake na katiba ilimruhusu kumpa Bakhresa eneo la kufanya uwekezaji.
Mkuu unaenda kwenye vitu vikubwa sana, SMZ ni taasisi siyo nchi. Ukishajua hili then hoja yako ya cessation inakufa kibudu
 
Mkuu unaenda kwenye vitu vikubwa sana, SMZ ni taasisi siyo nchi. Ukishajua hili then hoja yako ya cessation inakufa kibudu
Taasisi ya SMZ na ile ya JMT zinaongozwa na marais kumbuka hilo ambao wanaongozwa na katiba za nchi. Katiba ya JMT inampa rais umiliki wa ardhi yote anaweza kumnyang'anya mtu au taasisi na kumpa mwingine kwa tamko lake tu.

Ukielewa mamlaka ya kiongozi wa taasisi ya JMT utaelewa maana ya cession.
 
Taasisi ya SMZ na ile ya JMT zinaongozwa na marais kumbuka hilo ambao wanaongozwa na katiba za nchi. Katiba ya JMT inampa rais umiliki wa ardhi yote anaweza kumnyang'anya mtu au taasisi na kumpa mwingine kwa tamko lake tu.

Ukielewa mamlaka ya kiongozi wa taasisi ya JMT utaelewa maana ya cession.
Mkuu una very strange way of thinking. I rest my case.
 
Back
Top Bottom