Rais wangu Samia wale jamaa hawatishiwi!

Rais wangu Samia wale jamaa hawatishiwi!

Naona leo umejitutumua mama yangu!

Umewapiga biti kweli na kuwaeleza wasikupangie cha kufanya. Na umewatisha kweli.

Tahadhari yangu kwako. Wale jamaa hawajibiwi hovyo. Kukaa kimya nayo ni busara tu na hutapungukiwa chochote!

Najua unawajua kina Sadam Hussein, Muamar Gadaffi, Gamal Abdi Nasser, The late former president of Iran, Mugabe, Patrice Lumumba na wengineo wengi. Basi usisahau hata mtangulizi wako Magufuli

Kama unaishi nyumba ya vioo usirushe mawe. Unayemtegemea Putin anapigana vita Ukraine mwaka wa 3 sasa na hajui atashinda lini.

Soma Pia
- Rais Samia kwa Mabalozi: Hatupo hapa kuelekezwa nini cha kufanya kwenye nchi yetu
Huyu mama ame zowea tabia za uswahili. Ukiwa kiongozi hutakiwi kuwa mtu wa mipasho.
Mipasho waachiwe waimba taarabu
The United States of America .....mwisho wa KUNUKUU
Ndege tu anazosafiri nazo zimetengenezwa na kampuni zoo. Teknolojia zote wanazo wao!

Wakitaka kukufudisha wanaweza kukuzimia mitambo ndege yako ikiwa angani tu tukarudisha mpira kati!
Usiombe wale jamaa waanze kukuchukulia kama threat rasmi.

Kagame anawapigaga biti alafu anarudi mlango wa nyuma kuwapa Cobalt za Congo kusawazisha maneno yake.

Sasa wewe kila kitu unawapa wachina alafu unakuja kuwapiga biti za kitoto alafu ndege tu unayotumia teknolojia yote wanayo wao si unajitafutia shida?

Awe mpole tu asipende kujibishana nao. Wakimuamulia hata sekunde hachukui.
Haswaa!

Asipende kabisa kulumbana na hao Watu, akae kimya.Wakiamua kumshughulikia kamwe hataweza kumaliza hata wiki moja, kazi itakuwa imekwisha.
Hata aliyekuwa Rais wa zamani wa Msumbiji Samora Machel naye alianzisha vurumai ya namna hii hii huko miaka ya 1980s, hawa hawa kwa kushirikiana na Makaburu walimnyoosha Samora Machel mpaka akasalimu amri mazima hadi leo.
 
Kama anamgonga vizuri mbona vita vinaendelea mwaka wa 3 huu?
Vita ya Ukrain ina muda zaidi ya huo, ile vita haitaisha leo kwasababu NATO wanaitumia kujaribu siraha zao, ndo maana ndege ya kivita ya urusi imeonekana alaska baada ya mmarekani kutaka kuruhusu makombora ya masafa marefu
 
Toka kutetea DP World hadi kufika huku. Kweli ukistaajabu ya MUSSA utayaona ya firahuni. Binafsi naona watu kama ninyi ni hatari sana kwa maendeleo ya taifa hili.
 
Toka kutetea DP World hadi kufika huku. Kweli ukistaajabu ya MUSSA utayaona ya firahuni. Binafsi naona watu kama ninyi ni hatari sana kwa maendeleo ya taifa hili.
Uzuri unanijua vizuri. Mimi ni ukweli na uongo kwangu mwiko. Nashauri ipasavyo!
 
Hao jamaa ni SAILENSA ukijashtuka Tayari....wanakuzuumu tu kama Koribastadi
 
Ndege tu anazosafiri nazo zimetengenezwa na kampuni zoo. Teknolojia zote wanazo wao!

Wakitaka kukufudisha wanaweza kukuzimia mitambo ndege yako ikiwa angani tu tukarudisha mpira kati!
Na watu watashangilia. Goaaaaaal
 
Akiona silaha za kichina zile za JWTZ anaona ana ulinzi. Angejua hata hao China wanawaogopa hao anaowapiga biti kwa silaha angetulia tu
Angejua hata hao china wanawaogopa hao anaowapiga biti. 🙌
 
Risasi moja tu itapigwa angani, kwa woga kila mtu atakimbilia anapopajua. Sisi ni waoga sana.
 
Naona leo umejitutumua mama yangu!

Umewapiga biti kweli na kuwaeleza wasikupangie cha kufanya. Na umewatisha kweli.

Tahadhari yangu kwako. Wale jamaa hawajibiwi hovyo. Kukaa kimya nayo ni busara tu na hutapungukiwa chochote!

Najua unawajua kina Sadam Hussein, Muamar Gadaffi, Gamal Abdi Nasser, The late former president of Iran, Mugabe, Patrice Lumumba na wengineo wengi. Basi usisahau hata mtangulizi wako Magufuli

Kama unaishi nyumba ya vioo usirushe mawe. Unayemtegemea Putin anapigana vita Ukraine mwaka wa 3 sasa na hajui atashinda lini.

Soma Pia
- Rais Samia kwa Mabalozi: Hatupo hapa kuelekezwa nini cha kufanya kwenye nchi yetu
Kifungu cha 41 cha Mkataba wa Vienna Kuhusu Mahusiano ya Kidiplomasia na Umuhimu Wake kwa Mabalozi

Wakati wa hotuba yake kwa vikosi vya polisi, Rais Samia Suluhu Hassan alitumia fursa hiyo kuwaeleza na kuwakumbusha mabalozi waliopo nchini kuhusu mipaka ya majukumu yao na wajibu wao wa kuheshimu mamlaka na uhuru wa Tanzania.

Mkataba wa Vienna kuhusu Mahusiano ya Kidiplomasia, uliosainiwa mwaka 1961, ni mkataba wa kimataifa unaoweka misingi na sheria zinazoratibu mahusiano ya kidiplomasia kati ya mataifa. Moja ya vifungu muhimu vya mkataba huu ni Kifungu cha 41, ambacho kinafafanua majukumu na wajibu wa wanadiplomasia wanapokuwa katika nchi mwenyeji. Kufuatwa kwa kifungu hiki ni muhimu katika kuhakikisha usawa na uwazi katika mahusiano ya kidiplomasia, huku balozi zikifanya kazi zao ndani ya mipaka iliyowekwa.

Kifungu cha 41 Kinaeleza Nini?

Kifungu cha 41 kinaweka bayana wajibu wa wanadiplomasia kuheshimu sheria na taratibu za nchi wanakowakilisha, huku wakiwa na kinga ya kidiplomasia. Kinaainisha misingi muhimu kama ifuatavyo:

1. Kuheshimu Sheria za Nchi Mwenyeji: Wanadiplomasia wanapaswa kufuata sheria na kanuni za nchi mwenyeji licha ya kuwa na kinga dhidi ya kushitakiwa.

2. Kutokujihusisha na Masuala ya Ndani: Wanadiplomasia hawapaswi kuingilia mambo ya ndani ya nchi mwenyeji, ikiwemo kuepuka shughuli za kisiasa zinazoweza kuathiri masuala ya ndani ya nchi hiyo.

3. Shughuli Rasmi Kufanyika Kupitia Wizara ya Mambo ya Nje ya Nchi Mwenyeji: Shughuli zote rasmi za kidiplomasia zinapaswa kufanywa kupitia Wizara ya Mambo ya Nje ya nchi mwenyeji au njia za kidiplomasia zilizokubalika. Hii ni njia ya kudumisha uwazi na uwajibikaji kwa pande zote.

Umuhimu wa Kufuatwa kwa Kifungu cha 41

1. Kudumisha Kinga na Haki za Kidiplomasia
Kinga ya kidiplomasia inalinda wanadiplomasia dhidi ya kushitakiwa nchini mwenyeji, lakini inapaswa kuambatana na uwajibikaji. Kifungu cha 41 kinahakikisha kuwa kinga hii haivunji sheria za nchi mwenyeji. Ikiwa wanadiplomasia watashindwa kuheshimu sheria za ndani au kuingilia masuala ya nchi mwenyeji, wanahatarisha uaminifu wa kinga yao. Nchi mwenyeji inaweza kumtangaza mwanadiplomasia kuwa persona non grata na kumfukuza nchini.

2. Kudumisha Mamlaka na Heshima ya Nchi Mwenyeji
Diplomasia inategemea misingi ya kutokuingilia masuala ya ndani ya nchi nyingine. Kifungu cha 41 kinahakikisha kuwa wanadiplomasia wanabaki wasioegemea upande wowote, bila kushiriki kwenye siasa za ndani. Kuvunja sheria hizi kunaweza kuleta mvutano na kupunguza uaminifu kati ya nchi.

3. Kufanya Shughuli Kupitia Njia Rasmi
Kifungu cha 41 kinashikilia kuwa shughuli rasmi za kidiplomasia zinapaswa kufanyika kupitia Wizara ya Mambo ya Nje ya nchi mwenyeji. Hii inalinda utaratibu wa kiserikali na kuzuia mawasiliano yasiyo rasmi ambayo yanaweza kuvuruga mahusiano ya kidiplomasia.

4. Kuimarisha Uaminifu na Ushirikiano
Uaminifu ni msingi wa diplomasia yenye mafanikio. Wanadiplomasia wanapofuata sheria za nchi mwenyeji na kufanya shughuli zao kupitia njia sahihi, wanajenga uhusiano imara wa ushirikiano na heshima kati ya mataifa, na hivyo kukuza mazungumzo yenye tija na ushirikiano wa kibiashara, kisiasa, na kijamii.

5. Kulinda Mahusiano Kutokana na Mvutano
Balozi ambazo zinakiuka Kifungu cha 41 zinaweza kusababisha madhara makubwa kwa mahusiano ya kidiplomasia. Kujihusisha na masuala ya ndani bila ruhusa kunaweza kusababisha kufukuzwa kwa wanadiplomasia na kuzorotesha mahusiano kati ya mataifa hayo mawili.

Hitimisho

Kifungu cha 41 cha Mkataba wa Vienna ni nguzo muhimu kwa usimamizi wa mahusiano ya kidiplomasia duniani. Kinaweka uwiano kati ya kinga za wanadiplomasia na wajibu wao wa kuheshimu sheria za nchi mwenyeji. Aidha, kutekeleza majukumu yao kupitia Wizara ya Mambo ya Nje kunahakikisha ushirikiano wa uwazi na wenye tija kati ya mataifa.

Kwa kuzingatia hayo hapo juu, Rais Samia Suluhu Hassan alikuwa na haki na wajibu wa kuwakumbusha mabalozi umuhimu wa kuheshimu uhuru wa Tanzania na kufuata mipaka iliyowekwa kidiplomasia. Kufuatwa kwa Kifungu hiki ni msingi wa kuhakikisha mahusiano ya kidiplomasia yanaendelea kuwa imara na yenye manufaa kwa pande zote.
 
Naona leo umejitutumua mama yangu!

Umewapiga biti kweli na kuwaeleza wasikupangie cha kufanya. Na umewatisha kweli.

Tahadhari yangu kwako. Wale jamaa hawajibiwi hovyo. Kukaa kimya nayo ni busara tu na hutapungukiwa chochote!

Najua unawajua kina Sadam Hussein, Muamar Gadaffi, Gamal Abdi Nasser, The late former president of Iran, Mugabe, Patrice Lumumba na wengineo wengi. Basi usisahau hata mtangulizi wako Magufuli

Kama unaishi nyumba ya vioo usirushe mawe. Unayemtegemea Putin anapigana vita Ukraine mwaka wa 3 sasa na hajui atashinda lini.

Soma Pia
- Rais Samia kwa Mabalozi: Hatupo hapa kuelekezwa nini cha kufanya kwenye nchi yetu
umejificha lakini unaonekana
 
Kifungu cha 41 cha Mkataba wa Vienna Kuhusu Mahusiano ya Kidiplomasia na Umuhimu Wake kwa Mabalozi

Wakati wa hotuba yake kwa vikosi vya polisi, Rais Samia Suluhu Hassan alitumia fursa hiyo kuwaeleza na kuwakumbusha mabalozi waliopo nchini kuhusu mipaka ya majukumu yao na wajibu wao wa kuheshimu mamlaka na uhuru wa Tanzania.

Mkataba wa Vienna kuhusu Mahusiano ya Kidiplomasia, uliosainiwa mwaka 1961, ni mkataba wa kimataifa unaoweka misingi na sheria zinazoratibu mahusiano ya kidiplomasia kati ya mataifa. Moja ya vifungu muhimu vya mkataba huu ni Kifungu cha 41, ambacho kinafafanua majukumu na wajibu wa wanadiplomasia wanapokuwa katika nchi mwenyeji. Kufuatwa kwa kifungu hiki ni muhimu katika kuhakikisha usawa na uwazi katika mahusiano ya kidiplomasia, huku balozi zikifanya kazi zao ndani ya mipaka iliyowekwa.

Kifungu cha 41 Kinaeleza Nini?

Kifungu cha 41 kinaweka bayana wajibu wa wanadiplomasia kuheshimu sheria na taratibu za nchi wanakowakilisha, huku wakiwa na kinga ya kidiplomasia. Kinaainisha misingi muhimu kama ifuatavyo:

1. Kuheshimu Sheria za Nchi Mwenyeji: Wanadiplomasia wanapaswa kufuata sheria na kanuni za nchi mwenyeji licha ya kuwa na kinga dhidi ya kushitakiwa.

2. Kutokujihusisha na Masuala ya Ndani: Wanadiplomasia hawapaswi kuingilia mambo ya ndani ya nchi mwenyeji, ikiwemo kuepuka shughuli za kisiasa zinazoweza kuathiri masuala ya ndani ya nchi hiyo.

3. Shughuli Rasmi Kufanyika Kupitia Wizara ya Mambo ya Nje ya Nchi Mwenyeji: Shughuli zote rasmi za kidiplomasia zinapaswa kufanywa kupitia Wizara ya Mambo ya Nje ya nchi mwenyeji au njia za kidiplomasia zilizokubalika. Hii ni njia ya kudumisha uwazi na uwajibikaji kwa pande zote.

Umuhimu wa Kufuatwa kwa Kifungu cha 41

1. Kudumisha Kinga na Haki za Kidiplomasia
Kinga ya kidiplomasia inalinda wanadiplomasia dhidi ya kushitakiwa nchini mwenyeji, lakini inapaswa kuambatana na uwajibikaji. Kifungu cha 41 kinahakikisha kuwa kinga hii haivunji sheria za nchi mwenyeji. Ikiwa wanadiplomasia watashindwa kuheshimu sheria za ndani au kuingilia masuala ya nchi mwenyeji, wanahatarisha uaminifu wa kinga yao. Nchi mwenyeji inaweza kumtangaza mwanadiplomasia kuwa persona non grata na kumfukuza nchini.

2. Kudumisha Mamlaka na Heshima ya Nchi Mwenyeji
Diplomasia inategemea misingi ya kutokuingilia masuala ya ndani ya nchi nyingine. Kifungu cha 41 kinahakikisha kuwa wanadiplomasia wanabaki wasioegemea upande wowote, bila kushiriki kwenye siasa za ndani. Kuvunja sheria hizi kunaweza kuleta mvutano na kupunguza uaminifu kati ya nchi.

3. Kufanya Shughuli Kupitia Njia Rasmi
Kifungu cha 41 kinashikilia kuwa shughuli rasmi za kidiplomasia zinapaswa kufanyika kupitia Wizara ya Mambo ya Nje ya nchi mwenyeji. Hii inalinda utaratibu wa kiserikali na kuzuia mawasiliano yasiyo rasmi ambayo yanaweza kuvuruga mahusiano ya kidiplomasia.

4. Kuimarisha Uaminifu na Ushirikiano
Uaminifu ni msingi wa diplomasia yenye mafanikio. Wanadiplomasia wanapofuata sheria za nchi mwenyeji na kufanya shughuli zao kupitia njia sahihi, wanajenga uhusiano imara wa ushirikiano na heshima kati ya mataifa, na hivyo kukuza mazungumzo yenye tija na ushirikiano wa kibiashara, kisiasa, na kijamii.

5. Kulinda Mahusiano Kutokana na Mvutano
Balozi ambazo zinakiuka Kifungu cha 41 zinaweza kusababisha madhara makubwa kwa mahusiano ya kidiplomasia. Kujihusisha na masuala ya ndani bila ruhusa kunaweza kusababisha kufukuzwa kwa wanadiplomasia na kuzorotesha mahusiano kati ya mataifa hayo mawili.

Hitimisho

Kifungu cha 41 cha Mkataba wa Vienna ni nguzo muhimu kwa usimamizi wa mahusiano ya kidiplomasia duniani. Kinaweka uwiano kati ya kinga za wanadiplomasia na wajibu wao wa kuheshimu sheria za nchi mwenyeji. Aidha, kutekeleza majukumu yao kupitia Wizara ya Mambo ya Nje kunahakikisha ushirikiano wa uwazi na wenye tija kati ya mataifa.

Kwa kuzingatia hayo hapo juu, Rais Samia Suluhu Hassan alikuwa na haki na wajibu wa kuwakumbusha mabalozi umuhimu wa kuheshimu uhuru wa Tanzania na kufuata mipaka iliyowekwa kidiplomasia. Kufuatwa kwa Kifungu hiki ni msingi wa kuhakikisha mahusiano ya kidiplomasia yanaendelea kuwa imara na yenye manufaa kwa pande zote.
Kuna Sheria ya Nchi inayosema muue raia wenu? Mabalozi wanaposema msiue na kuteka wanting ilia mambo ya ndani kivipi?
 
Sitaki kuwa mwerevu kwa masuala ambayo siyajui kwa undani ni bora nikaonekana mjinga siku ziende,na sio lazima kuendelea kuwa mjinga wakati maarifa yapo ya kuendelea kujifunza.
 
Back
Top Bottom