Rais Wetu "Mchelea Mwana Kulia, Endelea Kuwachekea, Nyani "UKAWA!", Utayavuna Mabua

Rais Wetu "Mchelea Mwana Kulia, Endelea Kuwachekea, Nyani "UKAWA!", Utayavuna Mabua

Chamuhimu ni maridhiano sio nguvu na kuviziana.Umeongelea UKAWA vipi kauli za Komba na Lukuvi?
 
Jaman hata pasco mwenyewe amefika mwisho akajua hata eleweka aka bold alichoona kitaeleweka kwa kuwa naye alielewa sasa la kujiuliza kwanini kapoteza muda kuandika mada ambayo sentensi chache zingeeleweka.
 
Kwa akili hizi kama za Pasco Tanzania bado tunahitaji miaka 200 ili tuendelea,Cha ajabu kesho na keshokutwa utasikia huyu ndiye afisa mawasiliano wa Ikulu.KAZI KWELIKWELI
 
Na wewe eti unajiita msomi tena umefanya kazi ya uadishi ikulu shem on you
 
Katiba sio lazima ipatikane sasa. Hata baada ya uchaguzi mkuu wa 2015 Katiba inaweza kuandikwa. Uraisi ni Taasisi sio Jakaya Mrisho Kikwete. Baadhi ya watu humu ndani wanaibinafsisha Katiba Mpya kwa JK, sio kweli Katiba sio ya mtu kujipatia sifa.
Kwa kuwa tuna mambo mengi kwa kipindi kifupi ni bora tukaiahirisha mpaka hapo baadaye. Baada ya uchaguzi 2015, kutakuwa na sura mpya Bungeni hivyo kuleta mawazo mapya, wabunge wengine wenye misimamo ya UKAWA wanaweza kuwa wameshindwa uchaguzi, tutakuwa na rais mpya mwenye mawazo mapya pia. Watanzania pia watakuwa na mawazo mapya baada ya kuyatathimini ya sasa. 'Second thought is the best thought'. Subira yavuta kheri na harakaharak haina baraka. Ni bora kuyapima mawazo ya pande zote bila kuegemea upande mmoja na kufikiria kuafanyia kazi kwa pamoja bila ya kuathiri utaifa wetu kwa kuwa wote tu watanzania kuwa UKAWA au CCM hakutuondolei au kutuongezea hisa ya utaifa wetu. Sote ni watanzaia wenye mawazo tofauti juu ya Tanzania yetu iweje. Kuwa na mawazo tofauti ndiyo uhai wa Taifa lolote duniani, jambo lamsingi ni jinsi gani tuyaweke pamoja mawazo mazuri halafu tuendelee mbele. Kuzira mjadala ni ishara ya kutokomaa kimawazo lakini pia kulazimisha mawazo yako tu ni ishara ya ubabe au uwoga au kutojiamini au udikteta
 
Wewe akili yako ni ma------. Uliona hoja za watanzania kwenye tanzania tunayoitaka?
 
Pasco, umeeleweka na kifupi tu ni kwambaaaa; BMK lijadili rasimu iliyowasilishwa na tume. Full stop.
 
Last edited by a moderator:
Tatizo lililopo hapa nchini ni kuwa hakuna National Figure anayeheshimmika ambaye akiitwa na kusema neno watu watamsikia na kutekeleza. Mwanzo Warioba alikuwa na sifa inayofanana na hii lakini tangu awasilishe rasimu CCM wameamua kmushushia heshima. sijui kama mkapa ana sauti kubwa au pengine Mzee ruksa. Je, Mzee Salim! nadhani ana heshima fulani. Mtu mwenye nafasi hii ni lazima awe mkweli na akemee yeyote hata wa chama chake. Kwa sasa Kikwete kwa nafasi yake akiwa jasiri anayo nafasi kubwa sana ya kuokoa jahazi kama tu hatapendelea upande mmoja. CCM haina nafasi kabisa kwani inachofanya sasa ni mambo yasiyoeleka.nafasi pekee inabaki kwa mtu mwenye nafasi na mamlaka ambaye kwa sasa ni Kikwete!
 
Pasco kimsingi unapendekeza rais wa Jamhuri ya Muungano, kwa kutumia bunge la Muungano, apitishe sheria ya "mgogoro wa kisiasa". Hii ndiyo tafsiri niliyopata kutokana na mapendekezo yako.

Pili, mapendekezo yako yanakwenda kinyume kabisa na concept nzima ya uandikaji wa katiba (even katiba ya kikundi cha ngoma). Kwa kuweka sheria "inayolazimisha" wajumbe wa bunge la katiba kuwa "yes mzee" maana yake ni kutengeneza cosmetic katiba. haitadumu.

CCM wakubali tu kuwa Watanzania wameshuwa, ni watu wazima sasa na mtu mzima hashindii uji anakula ugali.
 
Last edited by a moderator:
Mhhh.Bora katiba tena!!! Kwa hiyo unamshauri raisi akubali Katiba isiyo na manufaa?! Tena kwa kulazimisha?!!
 
mimi nimekusoma vema mkuu Pasco! Jamani,mnapoisoma mada yake,isome kwa jicho la 3.
 
Last edited by a moderator:
kumbe bwana pasco usalama wa taifa kwako ni ccm kuendelea kuwa madarakani hata kama ni kwa gharama ya uhai na uhuru wa wengine!,sasa huwa mnafanya uchaguzi wa nini kama hamko tayari kusikiliza uamuzi wa wananchi?.heri umeweka wazi kuwa majeshi ya nchi hii yapo kwa ajili ya usalama wa ccm na si wananchi.
 
halafu kuna siku utasikia Pasco kawa mshauri wa rais kwenye maswala ya migogoro!!teh teh teh endelea kujitahid tu utafanikiwa!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom