Rais Wetu "Mchelea Mwana Kulia, Endelea Kuwachekea, Nyani "UKAWA!", Utayavuna Mabua

Rais Wetu "Mchelea Mwana Kulia, Endelea Kuwachekea, Nyani "UKAWA!", Utayavuna Mabua

Wanabodi,

Wengine wetu huu mchakato wa Katiba, tangu ulipoanzishwa, tulisema humu, hauwezi kutupatia "Katiba Bora!" bali utatupatia "Bora Katiba!". Tuliowaaminia kule bungeni tangu utungwaji wa sheria tuliwatahadharisha!, mwanzo wakasusa, baada ya chai na vitafunwa wakarejea, wakabariki, wakakubali, hivyo haya ni maji wameisha yavulia nguo hawana budi kuyaoga!.
Katiba: CHADEMA mlikosea! Kubalini yaishe, Tusonge Mbele Tupate Hiyo "Bora Katba!".

Sheria yenyewe ya Bunge Maalum, tumeitunga kwa kuilipua lipua, ikiwa na mapungufu kibao, na moja ya pungufu kubwa ni kwa mjumbe baada ya kuteuliwa, kuwa na mamlaka ya kujiamulia lolote, bila sheria hiyo kumbana kwa uwajibikaji kama kitu kinachofanywa na UKAWA kwa sasa, wamesusia kuendelea na mchakato na kutishia hata vikao vitakapoanza tenza, hawatarejea!. Kama hili ni kweli, na kama katika mahesabu ya kupitishwa kwa hiyo "Bora Katiba" hakutawezekana kwa akidi kutimia mpaka UKAWA warudi Bungeni, then mnaonaje kama mambo yafuatayo yangefanyika.

  1. Sheria ya Bunge la Katiba ifanyiwe marekebisho, serikali ipeleke muswada wa marekebisho, kumpa rais Kikwete mamlaka ya kutengua uteuzi wa wajumbe wa BMK kama wajumbe hao, hawatahudhuria baadhi ya vikao, vikiwemo vile vikao vya kufanya maamuzi.
  2. Marekebisho mengine ni ya kuwalazimisha wajumbe wa BMK walioteuliwa, kuwajibika kwa kuhudhuria vikao vya BMK kwa lazima, kwa mujibu wa sheria na sio kwa hiyari kama ilivyo sasa!.
  3. Baada ya rais kupewa mamlaka ya kutengua uteuzi wa wajumbe waasi, pia apewe mamlaka ya kuteua wajumbe wengine kutoka majina yale yale yaliyopendekezwa mwanzo, ila hakupata nafasi za uteuzi, hivyo mjumbe yoyote wa BMK akipoteza sifa za kuwa mjumbe wa Bunge hilo kwa sababu zozote zile, Rais ateue Replacement.
  4. Yaletwe marekebisho ya "Simbiyosis Relationship" kati ya Wajumbe wa Bunge la Katiba Ambao ni Wabunge wa la JMT na BLW, wakipoteza sifa zao za kuwa Wajumbe wa BMK, automatically wapoteze na soifa zao za ubunge wa JMT na BLW automatically na pia wazuiwe kugombea nafasi yoyote ya uongozi wa umma kwa kipindi cha miaka 10!, ili kuwashikisha adabu na kuwatia nidhamu!.
  5. Bunge lifanye marekebisho ya sheria ya uchaguzi, kuwa Mbunge yoyote au Mjumbe wa BLW atakapoteza sifa za Ubunge au Ujumbe wa BLW, the 1st Runner Up kwenye uchaguzi wa mwisho, ateuliwe mbunge au mjumbe wa BLW na hapo hapo ateuliwe mjumbe wa BMK, akidi itimie tujipatie hiyo "Bora Katiba" wanamchi wanaoisubiria kwa hamu!.
Lengo la Mabadiliko haya ya seria ya Bunge Maalum ni kwa lengo la kuwaadabisha waasi wa UKAWA, ambao sio tuu wanatishia hatari ya kutopatikana kwa "Bora Katiba", sasa UKAWA inazidi kuwa ni tishio kwa usalama wa taifa!, wameunganisha nguvu kwa wapinzani wote kuwa kitu kimoja, na mwaka 2015, wakisimamisha mgombea mmoja, kuna hatari kubwa ya CCM kushindwa (Zanzibar ni hata kwa dawa CCM haiwezi tena kushinda), hivyo kuhatarisha hali ya usalama na amani ya taifa hili kwa sababu CCM ndicho chama pekee nchini Tanzania chenye uzoefu wa kutawala na kuendesha nchi, hivyo Tanzania bila CCM haiwezekani!.

Na kwa vile CCM haijawahi hata kuwaza uwezekano wa kushindwa, hivyo hakuna maandalizi yoyote kwa mihimili mikuu ya dola, kupewa hata orientation ya kukitumikia chama kingine chochote, likiwemo jeshi letu ambalo tumelishuhudia juzi kwenye maonyesho jinsi lilivyo imara, sijawahi kusikia warsha, semina sau kongamano lolote la "Change of Arms" kwa Jeshi kuwa tayari kumtumia Amiri Jeshi Mkuu mwingine yoyote nje ya CCM, hivyo ikitokea CCM imeanguka!, Tanzania haitatawalika!, tutaingia katika machafuko makubwa ya ajabu!, hata huu umoja na ushirikiano wa UKAWA, ni ushirikiano wa "convenience tuu!", hiyo convenience ikiiisha, patazuka patashika ya ajabu ya mashati kuchanika!, nchi haitatawalika kabisa!.

Sisi wengine kazi yetu ni kusema tuu, hapa namwambia rafiki yetu JK, endelea kuwachekea tuu hawa UKAWA kwa kujiaminisha wako likizo!, huku ukiendelea kuwaacha wakudekee!, nakukumbusha tuu ule msemo wa Kiswahili usemao.

"Mchelea Mwana Kulia!.....

NB. Kwa wale ambao ni wavivu wa kusoma bandiko refu, nilichouliza hapa ni Jee Hawa UKAWA, wanaotaka kutuharibia nchi, watimuliwe kwa "insubordination?!, au tuendelee kuwachekea nyani, tukijiandaa kuvuna mabua?!. Swali la kujiuliza, ni Jee Wanachokifanya UKAWA ni kwa Maslahi ya Taifa?!.

Jumapili Njema!.

Wasalaam.

Pasco.

una minyoo ya kike wewe gamba!wewe serukamba nini?
 
Wanabodi,

Wengine wetu huu mchakato wa Katiba, tangu ulipoanzishwa, tulisema humu, hauwezi kutupatia "Katiba Bora!" bali utatupatia "Bora Katiba!". Tuliowaaminia kule bungeni tangu utungwaji wa sheriaya mabadiliko ya tuliwatahadharisha!, mwanzo wakasusa, baada ya chai na vitafunwa wakarejea, wakabariki, wakakubali, hivyo haya ni maji wameisha yavulia nguo hawana budi kuyaoga!.
Katiba: CHADEMA mlikosea! Kubalini yaishe, Tusonge Mbele Tupate Hiyo "Bora Katba!".

Sheria yenyewe ya Bunge Maalum, tumeitunga kwa haste haste, hivyo kuilipua lipua!, ikiwa na mapungufu kibao, na moja ya pungufu makubwa ni kwa sheria kumpa rais "appointments powers only" kwa mjumbe wa bunge hilo, baada tuu ya kuteuliwa, hakuna mamlaka yoyote ya kusitisha uteuzi wake!, hivyo kumpa mjumbe uhuru kamili wa kujiamulia lolote ikiwemo kutokuhudhuria vikao bila sababu yoyote ya msingi, kwa sababu hakuna kipengele chochote cha uwajibikaji kama kitu kinachofanywa na UKAWA kwa sasa, wamesusia kuendelea na mchakato na kutishia hata vikao vitakapoanza tena, wanadai hawatarejea!.

Kama hili ni kweli, na kama katika mahesabu ya akidi kupitishwa kwa hiyo "Bora Katiba" hakutawezekana kutimia mpaka UKAWA warudi Bungeni, japo naelewa wazi kipindi hiki cha mapumziko, "wale vijana", watasambazwa kuhakikisha kila penye uzia!, watapenyeza rupia!, hadi akidi itimie!, lakini you can never tell with politics, then jee mnaonaje kama wajumbe wote wa UKAWA, wakiendelea kogoma hali itakayopelekea kutokoseshea hiyo "Bora Katiba"", then Rais wetu JK, hakikisha mambo yafuatoyo yanafanyika kwa haraka katika kikao kijacho cha Bunge la JMT.

  1. Sheria ya Bunge la Katiba ifanyiwe marekebisho, serikali ipeleke muswada wa marekebisho, kumpa rais Kikwete mamlaka ya kutengua uteuzi wa wajumbe wa BMK kama wajumbe hao watakosa sifa za kuendelea kuwa wajumbe wa BMK, na miongoni mwa sifa hizo, ni kutohudhuria idadi ya vikao fulani bila sababu za msingi, ikiwemo ulazima wa kuhudhuria vikao vya kufanya maamuzi!.
  2. Marekebisho mengine ni kuongezwa kipengele cha uwajibikaji kwa kuwalazimisha wajumbe wa BMK walioteuliwa, kuwajibika kwa kuhudhuria vikao vya BMK kwa lazima, kwa mujibu wa sheria na sio kwa hiyari kama ilivyo sasa!.
  3. Baada ya rais kupewa mamlaka ya kutengua uteuzi wa wajumbe watakaopoteza sifa, pia apewe mamlaka ya kuteua wajumbe wengine kutoka majina yale yale yaliyopendekezwa mwanzo, ila hakupata nafasi za uteuzi, hivyo mjumbe yoyote wa BMK akipoteza sifa za kuwa mjumbe wa Bunge hilo kwa sababu zozote zile, Rais ateue Replacement.
  4. Yaletwe marekebisho ya "Simbiosis Relationship" kati ya Wajumbe wa Bunge la Katiba ambao ni Wabunge wa Bunge la JMT na BLW, wakipoteza sifa za kuwa Wajumbe wa BMK, automatically wapoteze na sifa za ubunge wa JMT na ule wa BLW automatically na pia wazuiwe kugombea nafasi yoyote ya uongozi wa umma kwa kipindi cha miaka 10!, ili kuwashikisha adabu na kuwatia nidhamu wajumbe wanaoleta uasi na kutaka kutukoseshea hiyo "Bora Katiba" tuijarajiao!.
  5. Bunge lifanye marekebisho ya sheria ya uchaguzi ya NEC na ZEC, kuwa Mbunge yoyote au Mjumbe wa BLW atakaepoteza sifa za Ubunge au Ujumbe wa BLW, the 1st Runner Up kwenye uchaguzi wa mwisho, ateuliwe kuwa Mbunge au mjumbe wa BLW na hapo hapo ateuliwe mjumbe wa BMK, sio tuu ili akidi itimie tujipatie hiyo "Bora Katiba" wananchi wanaoisubiria kwa hamu ipatikane, bali pia kuokoa mabilioni ya fedha zinazotumika kuendesha chaguzi ndogo!


Lengo la Mabadiliko haya ya sheria ya Bunge Maalum ni kwa lengo la kuwaadabisha waasi wa sio tuu wa UKAWA, bali kuzuia kabisa jaribio lolote la uasi, hivyo kuwafanya wajumbe wote wa BMK kuwa na utii wa kondoo!, mchakato uendeshwe fasta, tujipatie "Bora Katiba" tunayiosubiria kwa hamu, tuipigie kura ya ndio katika umoja wetu kama Watanzania!.

Ushauri wangu huu, unafutia kitendo cha UKAWA, ambao sio tuu wanatishia hatari ya kutopatikana kwa "Bora Katiba", sasa hawa UKAWA inazidi kuwa ni tishio kwa "usalama wa taifa!", baada ya hawa UKAWA kufanya kitendo cha "hatari sana", kwa kuunganisha nguvu kwa wapinzani wote kuwa "kitu kimoja!", katika umoja ambao ni nguvu ya hatari sana kwa mustakabili wa taifa letu, mwaka 2015!, endapo zile juhudi za "vijana kuwafarakanisha wapinzani kuhakikisha wapinzania wanaendelea kuwa fragmented" zinaendelea kushtukiwa, hivyo kuna hatari kwa wapinzani, kuungana na wakisimamisha mgombea mmoja, wa urais, ubunge na madiwani, mwaka 2015, then kuna hatari kubwa ya CCM kuanguka!, (Zanzibar ni given!, hata kwa dawa CCM haiwezi tena kushinda!), hivyo kuhatarisha hali ya usalama na amani ya taifa hili kwa sababu CCM pekee, ndicho chama pekee nchini Tanzania chenye uzoefu long experience ya uzoefu wa muda mrefu wa kutawala nchi, kuendesha nchi, na kuunda serikali!, hivyo Tanzania bila CCM haiwezekani!.

Na kwa vile CCM haijawahi hata mara moja, sio tuu kufikiria , bali hata kuwaza uwezekano wa kushindwa, hivyo hakuna maandalizi yoyote kwa mihimili mikuu ya dola, kupewa hata japo ka orientation ya probability ya yumkini ya kuyumkinika ya kukitumikia chama kingine chochote, likiwemo jeshi letu ambalo tumelishuhudia juzi kwenye maonyesho jinsi lilivyo imara, sijawahi kusikia warsha, semina sau kongamano lolote la "Change of Arms" kwa Jeshi kuwa tayari kumtumia Amiri Jeshi Mkuu mwingine yoyote nje ya CCM, hivyo ikitokea CCM imeanguka!, Tanzania haitatawalika!, tutaingia katika machafuko makubwa ya ajabu!, hata huu umoja na ushirikiano wa UKAWA, ni ushirikiano wa "convenience tuu!", hiyo convenience ikiiisha, patazuka patashika ya ajabu ya mashati kuchanika!, nchi haitatawalika kabisa!.

Sisi wengine kazi yetu ni kusema tuu, hapa namwambia rafiki yetu JK, endelea kuwachekea tuu hawa UKAWA kwa kujiaminisha wako likizo!, huku ukiendelea kuwaacha wakudekee!, nakukumbusha tuu ule msemo wa Kiswahili usemao.

"Mchelea Mwana Kulia!.....

NB. Kwa wale ambao ni wavivu wa kusoma bandiko refu, nilichouliza hapa ni Jee Hawa UKAWA, wanaotaka kutuharibia nchi, watimuliwe kwa "insubordination?!, au tuendelee kuwachekea nyani, tukijiandaa kuvuna mabua?!. Swali la kujiuliza, ni Jee Wanachokifanya UKAWA ni kwa Maslahi ya Taifa?!.

Jumapili Njema!.

Wasalaam.

Pasco.


Pasco,

Naona umevurugwa!

Jua kuwa hata kama CCM wakifanikiwa kurudisha serikali mbili, bado jamaa yako hataweza kuingia ikulu na wewe hutaweza kumrithi Salva. Hii ni kwa sababu jamaa hatapata kamwe theluthi mbili toka Zanzibar. Ningekuwa mimi wewe ningemshauri kuwa kwa kuwa bara anakubalika sana, akomae kutetea Tanganyika.
 
Pasco
Pamoja na mapendekezo yako, ningesema sheria unazopendekeza pia ziwe na sehemu ya kuwafikisha mahakamani, kutumia polisi kuhakikisha wabunge wanapiga kura kama CCM wanavyotaka.

Sheria hiyo iweke kifungu cha FFU kuwatafuta waliosusia na kuwatia adabu za mabuti na mabomu ya machozi.

Pia familia zao zizuiliwe kwa miaka 20 kutotoa kiongozi hata katibu kata.
Na sheria impe rais uwezo wa kuingiza mawazo yake bila kupingwa, na kuhakikisha vifaru na ndege za kijeshi zinatanda Dodoma ili kila mmoja awe na adababu kuwasikiliza CCM

Wasi wasi wangu kuhusu mapendekezo yako na yangu ya ziaida ni haya

Historia haionyeshi dola kushinda nguvu ya umma hata siku moja
Shah wa Iran alijaribu hakufanikiwa
Mfalme Ceusecue wa Romania alijaribu hakufanyikiwa
Fernando Marcos alijaribu hakufanikiwa
Idd Amin alijaribu hakufanikiwa
Pinochet, alijaribu hakufanikiwa
Orodha ni ndefu sana

Wasi wasi wangu wa pili, ni kuwa ile nguvu iliyoshinikiza mchakato uanzishwe haijafa lakini pia hatujui ilipo.

Hofu kubwa zaidi ni kuwa katiba ni muafaka na maridhiano ya kitaifa, Kenya walijaribu wakaishia tunapopajua.

Tunaweza kuwa na rasimu iliyoandikwa na Nape Nnauye na Mwigulu Nchemba kwa kutumia Polisi, FFU na JWTZ.

Tutapamba jukwaa na maua, ze komedi wakaiburudisha na Tambalizeni akisoma mashairi.
Komba ataimba nyimbo, Shehe Jongo atamwaga chozi, Askofu Mtetemela akileta mapambio, mambo yote yakiwa 'live'TBC

Halafu watafuata CNN na BBC wakionyesha wananchi wakiwa wamebeba magodoro wakivuka mpaka.

Tutasikia wale waliokimbikia misikitini na makanisani kunusuru roho zao wamefuatwa huko huko na viberiti.

Watakuja watu kutoka Commonwealth kutafuta chanzo cha mgogoro, baada ya siku mbili tu za utafiti watatoka na conclusion inayosema 'katiba haikuwa muafaka wala kuridhiwa na wanaoitumia'

Mapendekezo, wafutao wapitie Nairobi kuungana na Ruto na Kenyatta kwa safari ya the Hague.
Ticket zitakuwa za first class KLM.

Pendekezo la pili, serikali itenge maeneo kwa ndugu waliotangaulia mbele ya haki.

Mimi na Pasco kama tutanusurika tutakuwa tunamwaga chozi kila tutakapohesabu marafiki na ndugu zetu tusiojua wapo wapi. Tuatajialumu kwa kulisailiti taifa na kwamba kwanini hatukutambua kuwa kuzuia ni bora kuliko kuponya? machozi zaidi pwapwa pwaaa!

Ahsante
 
@ bwana Pasco
yaonesha ata sheria za tz huzijui, bunge la jamhuri ya muungano wa tanzania, halina mamlaka ya kushurutisha sheria ya utenguaji wa wa uwakilishi kw wajumbe wa baraza la wawakilishi zanzbar,
 
Bora katiba!!! Pasco nimekusoma Nimekuelewa kama uatabahatika kuwa mmoja wa watakao enda kunywa juisi ikulu kwa mara nyingine tena na mimi usinisahau naunga mkono mapendekezo yako yote tunahitaji kufanya ili angalau tuipate haraka hiyo bora katiba bila kujali kama iko Ki-ccm ccm au Ki-ukawa ukawa tunahitaji kuokoa pesa zetu zinazoliwa bure na wasakaTonge wa Dodoma
Muhimu: Kama utapata mda naomba unitafutie katiba ya Ukawa
 
Last edited by a moderator:
wewe pasco usiingilie fani za watu wewe fani yako ni uandishi sio sheria so jitahidi kutokuandika pumba
unasema bunge lirekebishe sheria ya nec na zec,dont you know kwamba sheria yoyote ikitungwa na bunge itumike znz haiwezi kutumika znz mpaka ipite blw according to znz constitution?acha kuzungumzia usiyoyajua inaniuma sana kutumia miaka mingi kusoma sheria then unakuja upumbavu km huu usio na kichwa wala miguu tena na mtu ambae hana hata weledi wa masuala ya kisheria,acha kudhalilisha fani za watu ndugu,jikite katika fani yako usipaparie ya wengine
hypocrite!!!!!!!!!!!!!!!
 
Siku nyingine ndugu Pasco punguza fasihi, watanzania tuna shida ya kutafakari tunasoma juu juu tu si unaona ulivyopoteza watu waliokuelewa ni wachache mno.
 
Pasco utapata shida sana kwa sababu watu wanasoma kichwa cha habari, wanatoa maoni na mawazo yao bila kusoma bandiko lote na kujaribu kuelewa unachomaanisha. Wadau hata mantiki yako ya KATIBA BORA na BORA KATIBA hawaielewi kabisa, pole sana.
 
ImageUploadedByJamiiForums1399227770.875758.jpg
 
Mkuu bandiko umetumia exaggeration hivyo mtu anahitaji akili nyingi kukuelewa nini umemaanisha
 
Sijui kama pasco yuko serious,???? kwake maslahi ya chama kwanza nchi badae!!!!!!!! Katiba bora??? sasa ameona bora katiba!!!! Njoo huku Pasco weka mambo sawa
Hivyo ndivyo alivyofundishwa sasa unategemea ataenda tofauti na walimu wake?
 
Pasco ana ujumbe mzito someni mtamwelewa. .!

Ukitumwa ujumbe mzito utaleta huu? we boya kweli anataka mawazo ya sisiem tu ndo yaheshimiwe kama wana hati miliki ya nchi hii kisha unamsifia eti ana ujumbe mzito? kakojoe ulale
 
Pasco utapata shida sana kwa sababu watu wanasoma kichwa cha habari, wanatoa maoni na mawazo yao bila kusoma bandiko lote na kujaribu kuelewa unachomaanisha. Wadau hata mantiki yako ya KATIBA BORA na BORA KATIBA hawaielewi kabisa, pole sana.

Acha ujuha kwa hiyo unataka BORA KATIBA kwa muda na rasilimali zilizotumika? liwalo na liwe ukawa endeleeni kutoa elimu
 
Acha ujuha kwa hiyo unataka BORA KATIBA kwa muda na rasilimali zilizotumika? liwalo na liwe ukawa endeleeni kutoa elimu

Ati, niache ujuha? Yaani tatizo lako la kutokuelewa liwe ujuha wangu! Umeelewa vizuri alichokiandika Pasco?
 
Last edited by a moderator:
Pasco utapata shida sana kwa sababu watu wanasoma kichwa cha habari, wanatoa maoni na mawazo yao bila kusoma bandiko lote na kujaribu kuelewa unachomaanisha. Wadau hata mantiki yako ya KATIBA BORA na BORA KATIBA hawaielewi kabisa, pole sana.

tatizo kubwa ni kwamba HAAMINIKI ! Sijui umenielewa ?
 
Back
Top Bottom