Rais Wetu "Mchelea Mwana Kulia, Endelea Kuwachekea, Nyani "UKAWA!", Utayavuna Mabua

Rais Wetu "Mchelea Mwana Kulia, Endelea Kuwachekea, Nyani "UKAWA!", Utayavuna Mabua

tatizo kubwa ni kwamba HAAMINIKI ! Sijui umenielewa ?

nimekuelewa mkuu, unakumbuka hata Yesu alisema kama hamniamini mimi basi aminini hata kazi zangu na ishara nnazofanya.

Sio lazima kumwamini lakini kile alichokiandika kina maana? Shukrani.
 
Wewe kijana pasco unakahoja ka wazi kabisa japo umezunguka mlima.
1.tunataka katiba bora na si bora katiba .hii ni kwaajili ya maslahi mapana ya umma wa watanzania wote.
Japo mawazo na mwitiko wa watanzania walio wengi katika kuwaunga mkono hawa unao wa ita manyani ni mkubwa sana kihisia kuliko vitendo.maana huu ni mchezo hata hao unao waamini kuna wakati wana kaa na kukiri kuwa hii ngoma kuicheza ni lazima wajifunge vibwebwe.
2.unamtizamo chanya kwa walioko mamlakani kupitia kwa watu fulani japo inafika wakati unajilaumu nini ufanye ili upate kile walichonacho wakina fulani hata kama ni haramu,japo msingi wa mawazo yako ni ukombozi wa kifikira kwa uma.
3.ushauri unao utoa unafika kwa walengwa moja kwa moja maana hapa jukwaani tupo watu wa kada tofautofauti,hivyo hao vijana maalumu wanamawili kujitweza ubwana kwaajili ya maslahi ya mabwana zao ilihali katiba itawagusa baba na mama zao waloko madongo poromoka.
4.mwanzo wa vurugu chanzo ni kwaaliyezoea kuatamia mtungi na kulamba asali kwa ubabe.
Go ukawa.
 
pamoja na kwamba sijaona chama sahihi cha kuongoza nchi lakini ccm inatupeleka njia isiyo sahihi watendaji na makada wake wamejaa viburi na kujiona wao ndio wateule wanachokifanya wao ndiop sahihi ni bora wakae kando wajue ni nini wananchi wa tanzania wanataka na sio kugeuza nchi kama familia yao binafsi na kurithishana uongozi
 
Kijana naona umefurugwa yaani unataka kutuambia bila ccm nchi haitawaliki tena! Nafikiri hujijui wala hujielewi. Sikia kijana huu ni ukweli mchungu ambao hutapenda kuusikia lakini nitakwambia. Ndugu yangu hii ccm yako unaitetea sana lakini pengine hujajua kama mwisho wao umefika ccm chuma chao kimo motoni na hakuna ujanja. Kauli kwamba UKAWA wanatishia amani ya nchi ni kauli dhaifu hatanahivyo ni dhahri kwamba kama ccm wataendelea kujifanya wababe na kufikiri kwamba bado tuko miaka ya 1964 na kushindwa kujua wa Tanzania wamepefuka kimawazo. Nachelea kusema usitegemee amani, wa Tanzania tumesha jionea yakutosha na hatuta kubali tena. Na nilasima mjue kwamba mtalasmika kwa matukio
 
Tunalalamika kila siku rais apunguziwe madaraka Halafu wewe unaleta utani?nimeamua kuku-flush wewe na thread yako
 
Wanabodi,

Wengine wetu huu mchakato wa Katiba, tangu ulipoanzishwa, tulisema humu, hauwezi kutupatia "Katiba Bora!" bali utatupatia "Bora Katiba!". Tuliowaaminia kule bungeni tangu utungwaji wa sheriaya mabadiliko ya tuliwatahadharisha!, mwanzo wakasusa, baada ya chai na vitafunwa wakarejea, wakabariki, wakakubali, hivyo haya ni maji wameisha yavulia nguo hawana budi kuyaoga!.
Katiba: CHADEMA mlikosea! Kubalini yaishe, Tusonge Mbele Tupate Hiyo "Bora Katba!".

Sheria yenyewe ya Bunge Maalum, tumeitunga kwa haste haste, hivyo kuilipua lipua!, ikiwa na mapungufu kibao, na moja ya pungufu makubwa ni kwa sheria kumpa rais "appointments powers only" kwa mjumbe wa bunge hilo, baada tuu ya kuteuliwa, hakuna mamlaka yoyote ya kusitisha uteuzi wake!, hivyo kumpa mjumbe uhuru kamili wa kujiamulia lolote ikiwemo kutokuhudhuria vikao bila sababu yoyote ya msingi, kwa sababu hakuna kipengele chochote cha uwajibikaji kama kitu kinachofanywa na UKAWA kwa sasa, wamesusia kuendelea na mchakato na kutishia hata vikao vitakapoanza tena, wanadai hawatarejea!.

Kama hili ni kweli, na kama katika mahesabu ya akidi kupitishwa kwa hiyo "Bora Katiba" hakutawezekana kutimia mpaka UKAWA warudi Bungeni, japo naelewa wazi kipindi hiki cha mapumziko, "wale vijana wa kazi!", watasambazwa kote ndani UKAWA "man2mam!", kuhakikisha kila penye uzia!, watapenyeza rupia!, hadi akidi itimie!, lakini you can never tell with politics, jee wasipofanikiwa, itakuwaje?!. Imagine wajumbe wote wa UKAWA, wakiendelea kusimama imara na kushikilia msimamo wao wa kugomea BML, hali itakayopelekea kutukoseshea hiyo "Bora Katiba", mnaonaje tukimshauri Rais wetu JK, tuliomchagua wenyewe kwa ridhaa yetu, kuhakikisha mambo yafuatayo yanafanyika mapema na kwa haraka katika kikao kijacho cha Bunge la JMT.

  1. Sheria ya Bunge la Katiba ifanyiwe marekebisho, serikali ipeleke muswada wa marekebisho, kumpa rais Kikwete mamlaka ya kutengua uteuzi wa wajumbe wa BMK kama wajumbe hao watakosa sifa za kuendelea kuwa wajumbe wa BMK, na miongoni mwa sifa hizo, ni kutohudhuria idadi ya vikao fulani bila sababu za msingi, ikiwemo ulazima wa kuhudhuria vikao vya kufanya maamuzi!.
  2. Marekebisho mengine ni kuongezwa kipengele cha uwajibikaji kwa kuwalazimisha wajumbe wa BMK walioteuliwa, kuwajibika kwa kuhudhuria vikao vya BMK kwa lazima, kwa mujibu wa sheria na sio kwa hiyari kama ilivyo sasa!.
  3. Baada ya rais kupewa mamlaka ya kutengua uteuzi wa wajumbe watakaopoteza sifa, pia apewe mamlaka ya kuteua wajumbe wengine kutoka majina yale yale yaliyopendekezwa mwanzo, ila hakupata nafasi za uteuzi, hivyo mjumbe yoyote wa BMK akipoteza sifa za kuwa mjumbe wa Bunge hilo kwa sababu zozote zile, Rais ateue Replacement.
  4. Yaletwe marekebisho ya "Simbiosis Relationship" kati ya Wajumbe wa Bunge la Katiba ambao ni Wabunge wa Bunge la JMT na BLW, wakipoteza sifa za kuwa Wajumbe wa BMK, automatically wapoteze na sifa za ubunge wa JMT na ule wa BLW automatically na pia wazuiwe kugombea nafasi yoyote ya uongozi wa umma kwa kipindi cha miaka 10!, ili kuwashikisha adabu na kuwatia nidhamu wajumbe wanaoleta uasi na kutaka kutukoseshea hiyo "Bora Katiba" tuijarajiao!.
  5. Bunge lifanye marekebisho ya sheria ya uchaguzi ya NEC na ZEC, kuwa Mbunge yoyote au Mjumbe wa BLW atakaepoteza sifa za Ubunge au Ujumbe wa BLW, the 1st Runner Up kwenye uchaguzi wa mwisho, ateuliwe kuwa Mbunge au mjumbe wa BLW na hapo hapo ateuliwe mjumbe wa BMK, sio tuu ili akidi itimie tujipatie hiyo "Bora Katiba" wananchi wanaoisubiria kwa hamu ipatikane, bali pia kuokoa mabilioni ya fedha zinazotumika kuendesha chaguzi ndogo


Lengo la Mabadiliko haya ya sheria ya Bunge Maalum ni kuwaadabisha hawa waasi wa sio tuu wa UKAWA, bali kuzuia kabisa jaribio jingine lolote la uasi!, hivyo kuwafanya wajumbe wote wa BMK kuwa na nidhamu ya hali ya juu na utii wa kondoo!, ili mchakato uliobakia, uendeshwe fasta, tujipatie "Bora Katiba" tunayiosubiria kwa hamu, tuipigie kura ya ndio katika umoja wetu kama Watanzania!.

Ushauri wangu huu, unafutia kitendo cha UKAWA, ambao sio tuu wanatishia hatari ya kutopatikana kwa "Bora Katiba", sasa hawa UKAWA inazidi kuwa ni tishio kwa "usalama wa taifa!", baada ya hawa UKAWA kufanya kitendo cha "hatari sana", kwa kuunganisha nguvu kwa wapinzani wote kuwa "kitu kimoja!", katika umoja ambao ni nguvu ya hatari sana kwa mustakabili wa taifa letu, mwaka 2015!, endapo zile juhudi za "vijana kuwafarakanisha wapinzani kuhakikisha wapinzania wanaendelea kuwa fragmented" zinaendelea kushtukiwa, hivyo kuna hatari kwa wapinzani, kuungana na wakisimamisha mgombea mmoja, wa urais, ubunge na madiwani, mwaka 2015, then kuna hatari kubwa ya CCM kuanguka!, (Zanzibar ni given!, hata kwa dawa CCM haiwezi tena kushinda!), hivyo kuhatarisha hali ya usalama na amani ya taifa hili kwa sababu CCM pekee, ndicho chama pekee nchini Tanzania chenye uzoefu wa long experience ya uzoefu wa muda mrefu wa kutawala nchi, kuendesha nchi, na kuunda serikali!, hivyo Tanzania bila CCM haiwezekani!.

Na kwa vile CCM haijawahi hata mara moja, sio tuu kufikiria , bali hata kuwaza uwezekano wa kuwezekanika kushindwa, hivyo hakuna maandalizi yoyote kwa mihimili mikuu ya dola, kupewa hata japo ka orientation ya probability ya yumkini ya kuyumkinika ya kukitumikia chama kingine chochote, zaidi ya chama dola CCM walichokizoea, ambao waserikali wote ni wanachama wake!, likiwemo jeshi letu la Wananchi wa CCM, Watanzania, ambalo tumelishuhudia juzi kwenye maonyesho jinsi lilivyo shupavu na imara, sijawahi kusikia warsha, semina au kongamano lolote la aina yoyote ya "Change of Arms" kwa Jeshi kuwa tayari kumtumikia Amiri Jeshi Mkuu mwingine yoyote nje ya CCM!, hivyo ikitokea CCM imeanguka!, Nchi itayumba!, Tanzania haitatawalika!, tutaingia katika machafuko makubwa ya ajabu!, hata huu umoja na ushirikiano wa UKAWA, ni ushirikiano wa "convenience tuu!", hiyo convenience ikiiisha, patazuka patashika kubwa ya ya ajabu ya nguo na mashati kuchanika!, nchi inawezekana isitawalike kabisa!, hivyo itakuwaje?!.

Sisi wengine kazi yetu ni kusema tuu, hapa tunamshauri, rais wetu, mwenzetu, na rafiki yetu JK, endelea kuwachekea tuu hawa UKAWA kwa kujiaminisha kuwa wako likizo!, huku ukiendelea kuwaacha wakizidi kukudekea huku wakipita huku na kule kuwaamsha waliolala!, haswa kwa kuzingatia kwa sasa UKAWA ndio wana "call the shots" na CCM inafutia nyuma kuziba mashimo, kama walivyofanya majuzi kwa kutangulia, Kiwani Pemba, ndipo leo CCM ikafuatia!, nakukumbushia tuu ule msemo wa Kiswahili usemao.

"Mchelea Mwana Kulia!"..... na "Ukiwachekea Nyani.....!", Jee Mpendwa wetu uko tayari "kulia wewe", na kipindi cha mavuno ya 2015, uvune mabua?!.

NB. Kwa wale ambao ni wavivu wa kusoma bandiko refu, nilichouliza hapa in short ni Jee hawa UKAWA, wanaotaka kutuharibia nchi yetu, kwa kutaka kutukwamishia hili zoezi la kujipatia "Bora Katiba" ya muungano wa serikali mbili, unaopendwa na Watanzania wote kabisa!, watimuliwe kwa "insubordination?!, au tuendelee kuwachekea tuu kama mtu awachekeaye nyani, tukijiandaa kuvuna mabua?!.

Swali la kujiuliza, ni Jee Wanachokifanya UKAWA ni kwa Maslahi ya Taifa?!.

Jumapili Njema!.

Wasalaam.

Pasco.

Ndugu yangu Pasco, hivi unadhani Rais kupewa nguvu zaidi ya hizo alizonazo, na hatimaye kuzitumia nguvu hizo (akipewa-na hilo si gumu) kuwatimua UKAWA itasaidia kuuwa wazo ambalo kwa sasa ni bivu? Kwa busara zako, unadhani tatizo ni UKAWA au uhuni unaoendelea huko kwenye Bunge la Katiba? Tell you what, laiti mchakato wa kupata Katiba mpya ungeendeshwa kwa kuzingatia maslahi ya Taifa badala ya kutanguliza itikadi za kisiasa, basi sio tu UKAWA isingekuwepo bali hata ingekuwepo isingekuwa na la kuwaeleza wananchi.

Tatizo lako umekimbilia kuangalia matokeo badala ya chanzo. Pengine wanachofanya UKAWA si kwa maslahi ya Taifa (maana kwa wana-CCM maslahi ya taifa ni synonymous na maslahi ya CCM) lakin ukirejea pointi yangu ya hapo juu, kilichosababisha uwepo wa UKAWA, na kinachoipa nguvu UKAWA ni taratibu fyongo za mchakato wa kupata Katiba mpya.

Lakini busara na akili ikirejea vichwani mwa CCM (including baba yao JK) basi wala hakutakuwa na haja ya kutunga sheria ya kuwabana UKAWA, maana hawatakuwa na la kuwaeleza wananchi. Halafu ni ufyongo wa kimtazamo kukerwa na harakati halali za kidemokrasia za UKAWA lakini unanyamazia uendawazimu wa watu kama Lukuvi. Kwa busara zako, UKAWA inayohubiri umuhimu wa kuzingatiwa taratibu zitakazowezesha kupatikana Katiba mwafaka kwa Tanzania na Watanzania ni tishio kwa usalama wa taifa kuliko Lukuvi anayehamasisha Jeshi lipindue nchi pindi kukiwa na serikali tatu! Na hayo hakuyaongea kwenye kilabu cha chimpumu bali kanisani. Lukuvi anachochea uhasama kati ya Wakristo na Waislam, viongozi wenye busara kwa Wakristo na Waislam wanamkemea, wewe unaishupalia UKAWA.

Tishio la usalama wa taifa linafanywa na hao wendawaziumu wanaodhani kuwa Watanzania ni mbumbumbu sana kiasi cha sio tu kuwatisha kuwa serikali tatuz zitaifanya Zanzibar kuwa Taifa la Kiislamu (ni taifa la kiislam hivi sasa) lakini pia kuhamasisha mapinduzi ya kijeshi.

Tishio pekee la UKAWA ni hilo wazo lao la kushirikiana kwa dhati (japo natambua wamewapa TISS nafasi ya kutengeneza operesheni ya muda mrefu kuwachonganisha). Na hilo si tishio kwa taifa bali CCM. Lakini kwa wenzetu ninyi, TAIFA=CCM.

Ninaamini ukinisoma bila jazba, na ukaweka itikadi za kisiasa pembeni utanielewa!
 
Pasco umevurugwa...

Mimi nimemchagua mbunge wangu kidemokrasia anitumikie miaka mitano, halafu itungwe sheria ya kumvua ubunge wa kidemokrasia kwa kuwa hajahudhuria vikao vya BMK ambalo ni kama TASK FORCE tu au tuseme KAMATI YA HARUSI!!!

Hivi hii katiba ya CCM kumbe imefanya maisha mengine yasimame eti, kwa hiyo nisidai vitanda hospitalini au dawa au maji safi ya kunywa au barabara kwa vile mbunge wangu kavuliwa ubunge kwa kushindwa kutunga katiba. Pasco lazima unatania tu, nami nakuchukulia hivyo hivyo kiutani utani.
 
Ungeshauri mh. Rais aufute mchakato huu ningekubaliana na wewe! Maana 300000@siku zidisha kwa 60*638, ni pesa nyingi ambazo zingeweza kutengeneza barabara zetu vijijini, kupeleka madawa mahospitalini nk.
 
Aisee wewe na Nguruvi3 mmeongelea ninachokifikiria juu ya mtazamo wa hatari alionao Pasco. ila mimi baada ya kuona maoni ya Pasco na baada ya kufuatilia BMK, UKAWA, Maneno ya viongozi serekalini na CCM na mpaka haya maazimisho ya miaka 50 ya Tanzani Nimeanza kuamini CCM na serekali yake inafikiria kama Pasco. Hawa jamaa wanaona nchi ni yakwao na hawafikirii kuna uwezekano sikumoja wakawa hawaitawali hii nchi. Nguvuvi3 ameto mifano mizuri ya kuonyesha Nguvu ya uma ilivyo watoa maraisi katika uongozi muda unapofika. ila na mimi ningependa kuongezea mfano wa Bashar Al-Assad na sio kwa kutabiri kwamba na yeye ataondolewa ila ni kwa jinsi yeye na serekali inachokifanya ili kuendelea kubaki madarakani. Ukweli nishaanza kuamini CCM wanaweza kupiga raia mabomu kama Bashar Al-Assad ili tu wabaki kwenye madaraka. Vitisho mnavyovisikia vya jeshi kuchua nchi na jinsi wanvyo jizalilisha kwenye BMK kwa hoja za kijinga ni wazi hawa jamaa wako radhi wafanye chochote wabaki madarakani. Naombea niwe nimekosea ila nikweli nishaanza kuona Tanzania tunaelekea pabaya
 
Wanabodi,

Wengine wetu huu mchakato wa Katiba, tangu ulipoanzishwa, tulisema humu, hauwezi kutupatia "Katiba Bora!" bali utatupatia "Bora Katiba!". Tuliowaaminia kule Bungeni tangu utungwaji wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, tuliwatahadharisha!, kuhusu "To fear the Greeks, especially when they brings gifts!". Japo mwanzo, walisua sua, wakasusa, baada ya kualikwa kufanya "rehearsals za kuikalia nyumba nyeupe", na zile chai na vitafunwa!, ni smiling faces na meno 32 nje!, wakasau yote!, wakarejea, wakabariki, wakakubali, hivyo hiki kinachoendelea sasa sio chanzo, ni matokeo tuu!, maadam haya ni maji na wameisha yavulia nguo hawana budi kuyaoga!, na kama wanatishia kutoendelea kuoga, tutawasokomezea huko bafuni na kuwamwagia maji waoge watake wasitake!.
Katiba: CHADEMA mlikosea! Kubalini yaishe, Tusonge Mbele Tupate Hiyo "Bora Katba!".

Sheria yenyewe ya Bunge Maalum, tumeitunga kwa haste haste, hivyo kuilipua lipua!, ikiwa na mapungufu kibao, na moja ya pungufu makubwa ni kwa sheria kumpa rais "appointments powers only" kwa mjumbe wa bunge hilo, baada tuu ya kuteuliwa, hakuna mamlaka yoyote ya kusitisha uteuzi wake!, hivyo kumpa mjumbe uhuru kamili wa kujiamulia lolote ikiwemo kutokuhudhuria vikao bila sababu yoyote ya msingi, kwa sababu hakuna kipengele chochote cha uwajibikaji kama kitu kinachofanywa na UKAWA kwa sasa, wamesusia kuendelea na mchakato na kutishia hata vikao vitakapoanza tena, wanadai hawatarejea!.

Kama hili ni kweli, na kama katika mahesabu ya akidi kupitishwa kwa hiyo "Bora Katiba" hakutawezekana kutimia mpaka UKAWA warudi Bungeni, japo naelewa wazi kipindi hiki cha mapumziko, "wale vijana wa kazi!", watasambazwa kote ndani UKAWA "man2mam!", kuhakikisha kila penye uzia!, watapenyeza rupia!, hadi akidi itimie!, lakini you can never tell with politics, jee wasipofanikiwa, itakuwaje?!. Imagine wajumbe wote wa UKAWA, wakiendelea kusimama imara na kushikilia msimamo wao wa kugomea BML, hali itakayopelekea kutukoseshea hiyo "Bora Katiba", mnaonaje tukimshauri Rais wetu JK, tuliomchagua wenyewe kwa ridhaa yetu, kuhakikisha mambo yafuatayo yanafanyika mapema na kwa haraka katika kikao kijacho cha Bunge la JMT.

  1. Sheria ya Bunge la Katiba ifanyiwe marekebisho, serikali ipeleke muswada wa marekebisho, kumpa rais Kikwete mamlaka ya kutengua uteuzi wa wajumbe wa BMK kama wajumbe hao watakosa sifa za kuendelea kuwa wajumbe wa BMK, na miongoni mwa sifa hizo, ni kutohudhuria idadi ya vikao fulani bila sababu za msingi, ikiwemo ulazima wa kuhudhuria vikao vya kufanya maamuzi!.
  2. Marekebisho mengine ni kuongezwa kipengele cha uwajibikaji kwa kuwalazimisha wajumbe wa BMK walioteuliwa, kuwajibika kwa kuhudhuria vikao vya BMK kwa lazima, kwa mujibu wa sheria na sio kwa hiyari kama ilivyo sasa!.
  3. Baada ya rais kupewa mamlaka ya kutengua uteuzi wa wajumbe watakaopoteza sifa, pia apewe mamlaka ya kuteua wajumbe wengine kutoka majina yale yale yaliyopendekezwa mwanzo, ila hakupata nafasi za uteuzi, hivyo mjumbe yoyote wa BMK akipoteza sifa za kuwa mjumbe wa Bunge hilo kwa sababu zozote zile, Rais ateue Replacement.
  4. Kwenye Bunge la JMT na kule BLW, yaletwe marekebisho ya "Simbiosis Relationship" kati ya Wajumbe wa Bunge la Katiba ambao ni Wabunge wa Bunge la JMT na BLW, wakipoteza sifa za kuwa Wajumbe wa BMK, automatically wapoteze na sifa za ubunge wa JMT na ule wa BLW automatically na pia wazuiwe kugombea nafasi yoyote ya uongozi wa umma kwa kipindi cha miaka 10!, ili kuwashikisha adabu na kuwatia nidhamu wajumbe wanaoleta uasi na kutaka kutukoseshea hiyo "Bora Katiba" tuijarajiao!.
  5. Bunge la JMT na BLW, wafanye marekebisho ya sheria za uchaguzi za NEC na ZEC, kuwa Mbunge yoyote au Mjumbe wa BLW atakaepoteza sifa za Ubunge au Ujumbe wa BLW, the 1st Runner Up kwenye uchaguzi wa mwisho, ateuliwe kuwa Mbunge au mjumbe wa BLW na hapo hapo ateuliwe mjumbe wa BMK, sio tuu ili akidi itimie tujipatie hiyo "Bora Katiba" wananchi wanaoisubiria kwa hamu ipatikane, bali pia kuokoa mabilioni ya fedha zinazotumika kuendesha chaguzi ndogo


Lengo la Mabadiliko haya ya sheria ya Bunge Maalum ni kuwaadabisha hawa waasi wa sio tuu wa UKAWA, bali kuzuia kabisa jaribio jingine lolote la uasi!, hivyo kuwafanya wajumbe wote wa BMK kuwa na nidhamu ya hali ya juu na utii wa kondoo!, ili mchakato uliobakia, uendeshwe fasta, tujipatie "Bora Katiba" tunayiosubiria kwa hamu, tuipigie kura ya ndio katika umoja wetu kama Watanzania!.

Ushauri wangu huu, unafutia kitendo cha UKAWA, ambao sio tuu wanatishia hatari ya kutopatikana kwa "Bora Katiba", sasa hawa UKAWA inazidi kuwa ni tishio kwa "usalama wa taifa!", baada ya hawa UKAWA kufanya kitendo cha "hatari sana", kwa kuunganisha nguvu kwa wapinzani wote kuwa "kitu kimoja!", katika umoja ambao ni nguvu ya hatari sana kwa mustakabili wa taifa letu, mwaka 2015!, endapo zile juhudi za "vijana kuwafarakanisha wapinzani kuhakikisha wapinzania wanaendelea kuwa fragmented" zinaendelea kushtukiwa, hivyo kuna hatari kwa wapinzani, kuungana na wakisimamisha mgombea mmoja, wa urais, ubunge na madiwani, mwaka 2015, then kuna hatari kubwa ya CCM kuanguka!, (Zanzibar ni given!, hata kwa dawa CCM haiwezi tena kushinda!), hivyo kuhatarisha hali ya usalama na amani ya taifa hili kwa sababu CCM pekee, ndicho chama pekee nchini Tanzania chenye uzoefu wa long experience ya uzoefu wa muda mrefu wa kutawala nchi, kuendesha nchi, na kuunda serikali!, hivyo Tanzania bila CCM haiwezekani!.

Na kwa vile CCM haijawahi hata mara moja, sio tuu kufikiria , bali hata kuwaza uwezekano wa kuwezekanika kushindwa, hivyo hakuna maandalizi yoyote kwa mihimili mikuu ya dola, kupewa hata japo ka orientation ya probability ya yumkini ya kuyumkinika ya kukitumikia chama kingine chochote, zaidi ya chama dola CCM walichokizoea, ambao waserikali wote ni wanachama wake!, likiwemo jeshi letu la Wananchi wa CCM, Watanzania, ambalo tumelishuhudia juzi kwenye maonyesho jinsi lilivyo shupavu na imara, sijawahi kusikia warsha, semina au kongamano lolote la aina yoyote ya "Change of Arms" kwa Jeshi kuwa tayari kumtumikia Amiri Jeshi Mkuu mwingine yoyote nje ya CCM!, hivyo ikitokea CCM imeanguka!, Nchi itayumba!, Tanzania haitatawalika!, tutaingia katika machafuko makubwa ya ajabu!, hata huu umoja na ushirikiano wa UKAWA, ni ushirikiano wa "convenience tuu!", hiyo convenience ikiiisha, patazuka patashika kubwa ya ya ajabu ya nguo na mashati kuchanika!, nchi inawezekana isitawalike kabisa!, hivyo itakuwaje?!.

Sisi wengine kazi yetu ni kusema tuu, hapa tunamshauri, rais wetu, mwenzetu, na rafiki yetu JK, endelea kuwachekea tuu hawa UKAWA kwa kujiaminisha kuwa wako likizo!, huku ukiendelea kuwaacha wakizidi kukudekea huku wakipita huku na kule kuwaamsha waliolala!, haswa kwa kuzingatia kwa sasa UKAWA ndio wana "call the shots" na CCM inafutia nyuma kuziba mashimo, kama walivyofanya majuzi kwa kutangulia, Kiwani Pemba, ndipo leo CCM ikafuatia!, nakukumbushia tuu ule msemo wa Kiswahili usemao.

"Mchelea Mwana Kulia!"..... na "Ukiwachekea Nyani.....!", Jee Mpendwa wetu uko tayari "kulia wewe", na kipindi cha mavuno ya 2015, uvune mabua?!.

NB. Kwa wale ambao ni wavivu wa kusoma bandiko refu, nilichouliza hapa in short ni Jee hawa UKAWA, wanaotaka kutuharibia nchi yetu, kwa kutaka kutukwamishia hili zoezi la kujipatia "Bora Katiba" ya muungano wa serikali mbili, unaopendwa na Watanzania wote kabisa!, watimuliwe kwa "insubordination?!, au tuendelee kuwachekea tuu kama mtu awachekeaye nyani, tukijiandaa kuvuna mabua?!.

Swali la kujiuliza, ni Jee Wanachokifanya UKAWA ni kwa Maslahi ya Taifa?!.

Jumapili Njema!.

Wasalaam.

Pasco.

Note:
Kwa wasionifahamu: Pasco wa jf, hana chama, hana kambi, na hana mtu wa 2015, bali ana watu anao waaminia!.

Msimamo wangu kwenye hoja ya serikali ngapi ni huu [h=3]Kama Kweli Nia ya Dhati ni Kuimarisha Muungano, Then...[/h]Uzuri wa Msimamo wa CCM kutetea Serikali Mbili, nimeueleza Hapa [h=3]Topic: Chonde Chonde Rais JK: Msimamo wa CCM wa Serikali Mbili, Ndio Utakauvunja Muungano!.[/h]Uhalali wa Bunge la Katiba nimeuleza hapa!
[h=3]Katiba: Nashauri Bunge Lililopo Livunjwe!, Liundwe Bunge ...[/h]Na kwa Wale Vimbelembele Kwenye BMK Wanaojidai eti wametumwa na Wananchi, pia nao niliwapatia ujumbe wao hapa
[h=3]Wito kwa Bunge la Katiba: Kura iwe ya Siri kwasababu Hakuna Yeyote Aliyetumwa na Wananchi!. [/h]
hoja yako #1 . unategemea huo msawaada utakaopelekwa na serikali wenye % kubwa ya kuupitisha au kutoupitisha ni akina nani??
hoja #2 hadi 5 ni udikteta tu ndio unaoupigia chepuo.
Mwisho, wkifanyacho UKAWA kinawaza kisiwe sahihi.... lakini wao wameona ndio suluhisho pekee....
 
Kwann tupoteze hela kupata bora katiba, kama CCM hawaitaki rasimu na sisi hatutaki katiba yao walioitunga wnyw, bunge livunje tu tutaonana 2015
 
Pasco utapata shida sana kwa sababu watu wanasoma kichwa cha habari, wanatoa maoni na mawazo yao bila kusoma bandiko lote na kujaribu kuelewa unachomaanisha. Wadau hata mantiki yako ya KATIBA BORA na BORA KATIBA hawaielewi kabisa, pole sana.

Usimfariji wala!!!!!!
Kaandika la kwanza akaja kuongeza nyama baadaye ila hakuna juha wa kutoelewa mantiki yake isipokuwa mnaosoma bila.kulinganisha dhamira yake ndio mumuaminio muandishi asiye huru ni hatari kuaminika!!!!!
 
Pasco,maswala ya kututisha na jeshi letu wenyewe hayasaidii kitu,ningekuelewa zaidi km ungemshauri Mhs.Rais kufuata matakwa ya wananchi na sio itikadi za kichama.....jua juu ya yote you cant change the hands of time na msemo wa kwetu "wengi wape,usipowapa......?"
 
Anafaa kuchukua mikoba ya Ngurumo pale msondo make kwa mashahiri haya Pasco anatisha ...mara "vijana wa kazi",mara ccm ndo imezoe kutawala,Tanu ilivyopewa nchi kabla ya hapo ilikuwa imewahi kuongoza nchi gani?,eti UKAWA wamehasi,kwanini isiwe CCM walioamua kujadili tofauti na mapendekezo yetu wananchi?
 
pasco siku zote huwa ni vuguvugu...punguza mifalsafa ,si unaona unavyopokea mitusi!
 
Sijui kama pasco yuko serious,???? kwake maslahi ya chama kwanza nchi badae!!!!!!!! Katiba bora??? sasa ameona bora katiba!!!! Njoo huku Pasco weka mambo sawa

BALAKI;
Mbona mambo kayaweka wazi tuu? Tangu kengele ya go ilipolia kwamba tunakwenda kupata Katiba Bora, ni hapo hapo mambo yaligeuka na kuwa kumbe! Tunaenda kupewe Bora Katiba. Yalipoendelea tukakuta kumbe walipelekwa kule watu waliokuwa wanatafutiwa njia au uchochoro wa kulipwa fadhila. Kodi yako ikawa Sadaka kuwashibisha walio mpigia kampeini, kwa mgongo wa mteule wa mkuu kwenda kuwa Mbunge wa BMK. Unategemea nini kitokee? Ni Ndiyooooooo.
Mawazo ya wananchi yakatupwa kulee, yakaletwa ya M/kiti mwenye Fikra sahihi. Nasema Pasco kaona, mwisho ni Bora Katiba.
 
Pasco unachekesha sana. kinyago mmechonga wenyewe sasa mnalialia awasaidie nani? Hoja yako dhaifu sana ya kutaka rais amiliki mchakato wa katiba mpya. Jenga hoja na sio kumtaka rais abague wajumbe. Mmeshikwa pabaya na kinyago chenu hadi burudani
 
Unataka JK awafanye nini UKAWA? Hivi na wewe umo miongoni mwa wahafidhina wanaoamini kuwa CCM imeumbwa kutawala milele na hakuna chama kingine chochote kinachoweza kutawala zaidi ya CCM?

Nadhani kama unawaza haya, na kama vijana wengi wa umri wako wanawaza kama wewe, basi tuna safari ndefu sana katika kuikomboa Tanganyika na Tanzania yetu!

Mkuu naona hujamuelewa kabisa Pasco, si lazima kuchangia kama hujaelewa kilichoandikwa. Read between lines...
 
Back
Top Bottom