Rais Wetu "Mchelea Mwana Kulia, Endelea Kuwachekea, Nyani "UKAWA!", Utayavuna Mabua


una minyoo ya kike wewe gamba!wewe serukamba nini?
 


Pasco,

Naona umevurugwa!

Jua kuwa hata kama CCM wakifanikiwa kurudisha serikali mbili, bado jamaa yako hataweza kuingia ikulu na wewe hutaweza kumrithi Salva. Hii ni kwa sababu jamaa hatapata kamwe theluthi mbili toka Zanzibar. Ningekuwa mimi wewe ningemshauri kuwa kwa kuwa bara anakubalika sana, akomae kutetea Tanganyika.
 
Pasco
Pamoja na mapendekezo yako, ningesema sheria unazopendekeza pia ziwe na sehemu ya kuwafikisha mahakamani, kutumia polisi kuhakikisha wabunge wanapiga kura kama CCM wanavyotaka.

Sheria hiyo iweke kifungu cha FFU kuwatafuta waliosusia na kuwatia adabu za mabuti na mabomu ya machozi.

Pia familia zao zizuiliwe kwa miaka 20 kutotoa kiongozi hata katibu kata.
Na sheria impe rais uwezo wa kuingiza mawazo yake bila kupingwa, na kuhakikisha vifaru na ndege za kijeshi zinatanda Dodoma ili kila mmoja awe na adababu kuwasikiliza CCM

Wasi wasi wangu kuhusu mapendekezo yako na yangu ya ziaida ni haya

Historia haionyeshi dola kushinda nguvu ya umma hata siku moja
Shah wa Iran alijaribu hakufanikiwa
Mfalme Ceusecue wa Romania alijaribu hakufanyikiwa
Fernando Marcos alijaribu hakufanikiwa
Idd Amin alijaribu hakufanikiwa
Pinochet, alijaribu hakufanikiwa
Orodha ni ndefu sana

Wasi wasi wangu wa pili, ni kuwa ile nguvu iliyoshinikiza mchakato uanzishwe haijafa lakini pia hatujui ilipo.

Hofu kubwa zaidi ni kuwa katiba ni muafaka na maridhiano ya kitaifa, Kenya walijaribu wakaishia tunapopajua.

Tunaweza kuwa na rasimu iliyoandikwa na Nape Nnauye na Mwigulu Nchemba kwa kutumia Polisi, FFU na JWTZ.

Tutapamba jukwaa na maua, ze komedi wakaiburudisha na Tambalizeni akisoma mashairi.
Komba ataimba nyimbo, Shehe Jongo atamwaga chozi, Askofu Mtetemela akileta mapambio, mambo yote yakiwa 'live'TBC

Halafu watafuata CNN na BBC wakionyesha wananchi wakiwa wamebeba magodoro wakivuka mpaka.

Tutasikia wale waliokimbikia misikitini na makanisani kunusuru roho zao wamefuatwa huko huko na viberiti.

Watakuja watu kutoka Commonwealth kutafuta chanzo cha mgogoro, baada ya siku mbili tu za utafiti watatoka na conclusion inayosema 'katiba haikuwa muafaka wala kuridhiwa na wanaoitumia'

Mapendekezo, wafutao wapitie Nairobi kuungana na Ruto na Kenyatta kwa safari ya the Hague.
Ticket zitakuwa za first class KLM.

Pendekezo la pili, serikali itenge maeneo kwa ndugu waliotangaulia mbele ya haki.

Mimi na Pasco kama tutanusurika tutakuwa tunamwaga chozi kila tutakapohesabu marafiki na ndugu zetu tusiojua wapo wapi. Tuatajialumu kwa kulisailiti taifa na kwamba kwanini hatukutambua kuwa kuzuia ni bora kuliko kuponya? machozi zaidi pwapwa pwaaa!

Ahsante
 
@ bwana Pasco
yaonesha ata sheria za tz huzijui, bunge la jamhuri ya muungano wa tanzania, halina mamlaka ya kushurutisha sheria ya utenguaji wa wa uwakilishi kw wajumbe wa baraza la wawakilishi zanzbar,
 
Bora katiba!!! Pasco nimekusoma Nimekuelewa kama uatabahatika kuwa mmoja wa watakao enda kunywa juisi ikulu kwa mara nyingine tena na mimi usinisahau naunga mkono mapendekezo yako yote tunahitaji kufanya ili angalau tuipate haraka hiyo bora katiba bila kujali kama iko Ki-ccm ccm au Ki-ukawa ukawa tunahitaji kuokoa pesa zetu zinazoliwa bure na wasakaTonge wa Dodoma
Muhimu: Kama utapata mda naomba unitafutie katiba ya Ukawa
 
Last edited by a moderator:
wewe pasco usiingilie fani za watu wewe fani yako ni uandishi sio sheria so jitahidi kutokuandika pumba
unasema bunge lirekebishe sheria ya nec na zec,dont you know kwamba sheria yoyote ikitungwa na bunge itumike znz haiwezi kutumika znz mpaka ipite blw according to znz constitution?acha kuzungumzia usiyoyajua inaniuma sana kutumia miaka mingi kusoma sheria then unakuja upumbavu km huu usio na kichwa wala miguu tena na mtu ambae hana hata weledi wa masuala ya kisheria,acha kudhalilisha fani za watu ndugu,jikite katika fani yako usipaparie ya wengine
hypocrite!!!!!!!!!!!!!!!
 
Siku nyingine ndugu Pasco punguza fasihi, watanzania tuna shida ya kutafakari tunasoma juu juu tu si unaona ulivyopoteza watu waliokuelewa ni wachache mno.
 
Pasco utapata shida sana kwa sababu watu wanasoma kichwa cha habari, wanatoa maoni na mawazo yao bila kusoma bandiko lote na kujaribu kuelewa unachomaanisha. Wadau hata mantiki yako ya KATIBA BORA na BORA KATIBA hawaielewi kabisa, pole sana.
 
Mkuu bandiko umetumia exaggeration hivyo mtu anahitaji akili nyingi kukuelewa nini umemaanisha
 
Sijui kama pasco yuko serious,???? kwake maslahi ya chama kwanza nchi badae!!!!!!!! Katiba bora??? sasa ameona bora katiba!!!! Njoo huku Pasco weka mambo sawa
Hivyo ndivyo alivyofundishwa sasa unategemea ataenda tofauti na walimu wake?
 
Pasco ana ujumbe mzito someni mtamwelewa. .!

Ukitumwa ujumbe mzito utaleta huu? we boya kweli anataka mawazo ya sisiem tu ndo yaheshimiwe kama wana hati miliki ya nchi hii kisha unamsifia eti ana ujumbe mzito? kakojoe ulale
 
Pasco utapata shida sana kwa sababu watu wanasoma kichwa cha habari, wanatoa maoni na mawazo yao bila kusoma bandiko lote na kujaribu kuelewa unachomaanisha. Wadau hata mantiki yako ya KATIBA BORA na BORA KATIBA hawaielewi kabisa, pole sana.

Acha ujuha kwa hiyo unataka BORA KATIBA kwa muda na rasilimali zilizotumika? liwalo na liwe ukawa endeleeni kutoa elimu
 
Acha ujuha kwa hiyo unataka BORA KATIBA kwa muda na rasilimali zilizotumika? liwalo na liwe ukawa endeleeni kutoa elimu

Ati, niache ujuha? Yaani tatizo lako la kutokuelewa liwe ujuha wangu! Umeelewa vizuri alichokiandika Pasco?
 
Last edited by a moderator:
Pasco utapata shida sana kwa sababu watu wanasoma kichwa cha habari, wanatoa maoni na mawazo yao bila kusoma bandiko lote na kujaribu kuelewa unachomaanisha. Wadau hata mantiki yako ya KATIBA BORA na BORA KATIBA hawaielewi kabisa, pole sana.

tatizo kubwa ni kwamba HAAMINIKI ! Sijui umenielewa ?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…