Ramadhan Kayoko ndiye mwamuzi mbovu katika NBC Premier League! Freekick uliyowazawadia Yanga imeigharimu Simba

 
Ningekua karibu na kayoko saiz nna kesi ya mahuaji kudadeki faulo mbili ndani ya boks wanacheza mwili badala ya mpira anatoa macho tu kayoko sasa faulo ya fernandez faulo gan ile
Rudi shule ukajifunze kuandika ndio uje hapa
 
Mimi ni Simba ila nashangazwa na hizi shutuma kwa refa, Mimi nadhani refa na wasaidizi wake walikuwa na game nzuri tu. Ni lazima tuwe tunakubali matokeo na kama kuchambua basi tuangalie madhaifu ya team zetu. Mpira kipindi cha kwanza quality haikuwa nzuri mechi ya kawaida kipindi cha pili kilikuwa kizuri,

Simba alianza vizuri na chance mwanzoni tu tukapoteza ilikuwa goal wazi kabisa Yanga wamekuja kuamka kipindi cha pili kidogo kidogo wakawa hatari unaziona lakini tukija kwenye goal nikosa la goal keeper, makipa bora mipira kama ile wanaisukuma nje tu, Kamara kanikumbusha mipira ya miaka ya 90 kipa kama hujaruka kama nyani unaonekana sio kipa, ukitema sio kipa siku hizi kipa haruki hovyo na akiruka anasukuma mpira nje tu, Kamara ni kipa mzuri wajibu wa kocha wa makipa kuondoa udhaifu huo. Simba na Yanga wamepambana na goal kosa moja tu ila tusikimbilie refa huko hapana, waamuzi wamejitahidi sana ukichukua hakuna VAR.
 
SIMBA KILA SIKU MTAKUWA MNAFUNGWA NA YANGA...MPAKA MKUBALI KUWA MLIFUNGWA KWA KUZIDIWA UWEZO...MAANA HAKUNA SIKU MMEFUNGWA NA YANGA MKAKOSA KISINGIZIO...
 
Basiii sawa poleni sana.....next time mje na mwamuzi kutoka kenya
 
Mpira ni namba na sio maneno, leta hizo namba za Simba zilizokuwa zinakufanya uamini kwamba Simba anaenda kupata matokeo dhidi ya yanga, yanga mpaka anakwenda kwenye derby alikuwa ajaruhusu goli lolote, kacheza mechi 4 na kafunga goli 9, Simba alikuwa ameruhusu goli 2, kacheza mechi 5 na kafunga goli 12, iyo tu ilikuwa inakuonyesha kwamba yanga wako vizuri kwenye defence line kuliko Simba, ivyo Simba walitakiwa wafanye kazi ya ziada kuifungua defence ya yanga!
Ukiangalia pia kiufundi namna Simba alivyopata matokeo yake ktk mechi izo 5 alizokuwa amecheza kuanzia mechi ya Azam kule Zanzibar, ukaja Dodoma Jiji, aikuhitaji darubini Wala elimu ya chuo kikuu kupata majibu kwamba wasingeweza kwa namna yoyote Ile kupata matokeo dhidi ya yanga!
 
Hao unaowataja bado wanacheza mpira? Yaani mambo ya miaka 10 nyuma unatolea mfano leo
 
wewe ni mtu wa mpira [emoji2935]
 
Kwani tangu mwanzo tulipowaambia huyu dogo hana uwezo wa kuchezesha mechi kubwa, si mlitukejeli na kutuambia tunatafuta visingizio!!
 
Sio Yanga hii ya misimu mitatu iliyopita, katika kumbukumbu za yanga hii,timu zilizokuwa pungufu zilikula kuanzia goli nne na kuendelea. Kipindi cha pili mlipoteana kabisa ndio maana mkaingiziwa Mastriker wawili, maanake kwenye kiungo hamkuwa na madhara,sasa pata picha mngekuwa pungufu....... mpira mchezo wa wazi sana tatizo lako hauoni.
 
red card ni sawa, ila ile ya ateba sio offside hujui mpira wewe maandazi ya kuchoma.
Wewe ni kolo og, huwa tunawajua kwa matusi mazito na una povu zito usipuuzwe, hakika umeumia sana kudungwa kidude mara nne mfululizo inauma sana, tena kimoko mara mbili acha tu, pole sana na unahitaji panadol ,

Kiufupi ile ni offside, tuliza jazba mtani itakuwa hukuona ilipofika half time Azam TV walirudia tukio, walichora mstari kuonesha Ateba yuko offside na wachambuzi wakasema ni offside na ikaonekana wazi mguu mmoja wa Ateba uko mbele na huku mshika kibendera yuko mbele ya Ateba tayari katangulia kwenda kufunga iwapo Ateba asingekuwa mbinafsi na kumpasia !! Ateba alifikiri golini kuna shuka tu!!

Naamini kabisa Mkuu unahitaji kuvaa miwani na kama wewe ni muha badili kabila si kwa ubishi huo!!

Jaribu kujitazama kwenye kioo, ukibisha kuwa si wewe basi ujue kuna tatizo lishughulikie haraka!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…