Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

Bacteria wanaochakata uchafu hawahitaji oxygen ili kuishi au bacteria wa kwako ni special?
Mkuu inaonesha kabisa umekuja kwa lengo la kupinga/majibizano, hakuna mahali nimetaja oxygen hapo. Najua lengo lako ni kutaka uonekane mjuzi zaidi mbele ya kadamnasi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kokoto za duara hazifai kutumika kwenye ujenzi; au nasema uongo ndugu zangu?
Na sio hizo tu, hata kokoto bapa (flaky aggregates), kokoto ndefu (elongated) hazifai hasa kwa high strength concrete. Kokoto ambazo unaweza kutumia kwa zege yoyote (low na high strength concrete) ni zile zenye thickness kubwa, fupi na zenye angle angle


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jamiiforums ni msaada mkubwa sana kwenye ulimwengu wa leo unaohitaji akili na matumizi sahihi ya pesa,post za mdau Hechy Essy zimenifungua akili kama hivi alivyoandika ningevijua mapema vingenisaidia sana.

Kwenye ujenzi tusiogope kutumia washauri kisa kukimbia gharama mimi sikuwa na akili hii majibu yake nimeshayaona,kwa mnaoanza ujenzi tafadhalini watumieni watu kama hawa watawasaidia sana.
Ahsante kwa ushauri.
 
PLN 0001 2BR

Ramani ya Vyumba Viwili
  • Living room (Sebule)
  • 1 Master bedroom with a Dressing room (W.I.C)
  • 1 Single bedroom
  • Kitchen (Jiko)
  • Public toilet (Choo cha jumuiya)

Ramani hii ina privacy na ventilation ya hali ya juu sana

Bei: Tsh. 100,000/=

Ramani inakuwa na Makadirio yake ya vifaa vya ujenzi kuanzia hatua ya msingi mpaka finishing ambapo itakusaidia kukuongoza katika manunuzi ya vifaa na kuepuka kulanguliwa na mafundi wenye tamaa ya kukuzidishia hesabu ili wajinufaishe zaidi.
View attachment 2694970
Inahitaji eneo lenye ukubwa wa mita ngapi?
 
Kama huna ujuzi na mambo ya ujenzi, ni vizuri ukamshirikisha mtaalam katika kila hatua ya ujenzi unayoiendea.

Hii inatakiwa uifanye kuanzia mwanzoni kabisa, watu wengi wanauziwa viwanja vidogo kwa sababu hawana ujuzi na mambo ya vipimo. Unakuta mtu ana malengo ya kutaka kujenga nyumba ya vyumba vinne lakini kiwanja alichonunua unakuta ni futi 40 kwa futi 40

Hapo nimezungumzia upande wa vipimo, lakini kuna vitu vingine vya kuangalia kabla ya kununua hicho kiwanja mfano aina ya udongo n.k

Hatua kama hizi ni vyema ukatafuta mtaalam ukaambatana nae kwenda site ambapo inaweza ikakusaidia kwa kiasi kikubwa. Katika uuzaji wa viwanja, wauzaji wengi wanapenda kutumia kizio cha futi badala ya mita kwa sababu upande wa futi inaonekana kama kiwanja ni kikubwa (kwa asiyejua). Mfano kiwanja cha futi 40 kwa futi 40 ni sawa na kiwanja cha mita 12 kwa mita 12

Karibuni kwa ramani, makadirio na ushauri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Moja ya test unayotakiwa kuifanya unapoenda kununua nondo ni kuikunja nondo mpaka angalau nyuzi 90 na kuirudisha. Kuna nondo mbichi na nondo kavu, nondo kavu ukiikunja inakatika yenyewe kama kijiti (hizi hazifai kabisa katika ujenzi) tofauti na nondo mbichi

Ni muhimu sana kufanya hii test kabla hujaanza kuzitumia nondo zako kwa sababu ukitumia hizo nondo kavu halafu ikafikia hatua jengo linataka kudondoka hutoona ishara yoyote (litadondoka tu muda huo huo ambao uwezo wake umezidiwa)

Kuna boss mmoja aliagiza nondo karibu tani moja na nusu...kwenda pale nikaanza kufanya hiyo test tukiwa site, ikawa kila nondo ninayoikunja inakatika, ikabidi nimuambie boss afanye utaratibu wa kuzirudisha alipozinunua abadilishiwe

Bado umuhimu wa kushirikisha wataalam wa ujenzi katika kila hatua upo pale pale

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakati mwingine sio lazima sana kuchukua vifaa vyote vya ujenzi vikiwa ktk hali yake ya uzima mfano unapoenda kununua tiles, unanunua box za tiles ambazo ni nzima na ukifika site tiles zingine unazikata ili upate vipande vya kujazia na wakati huo huo pale hardware uliponunulia hizo tiles kuna box za tiles ambazo baadhi ya vipande vimekatika na muuzaji anauza kwa bei ya hasara hivyo kama ungechanganya box nzima na zile zilizokatika ungeokoa kiasi flani cha pesa

Hii pia unaweza ukaapply kwenye gympsum board ktk uwekaji wa dari, tofali n.k kwa lengo la lengo kupunguza gharama

Kabla ya kufanya uamuzi inabidi ufanye mahesabu ili upate makisio kwamba nyumba yako itahitaji vitu vizima vingapi, ili uweze kujua sehemu iliyobaki itahitaji kiasi gani cha material ambazo sio nzima (hapa simaanishi ubovu, namaanisha utimilifu)
Hii idea ya tiles ni nzuri
 
Je wajua kwanini haishauriwi kutumia bati za migongo mipana katika nyumba za bati la kuficha?

Bati za migongo mipana, migongo yake kwa juu ipo flat na kwa sababu muinuko wa paa ni mdogo basi inafanya maji yatembee hata kwenye hiyo migongo tena kwa speed ndogo hivyo inaongeza risk ya maji kuingia kupitia matundu ya bati palipopigiliwa misumari

Kwa nyumba za paa la kuficha, ni vizuri zaidi kutumia bati za migongo midogo badala ya bati za migongo mipana ili kupunguza risk moja wapo ya uvujaji wa maji katika paa

Ramani, Makadirio na Ushauri tuwasiliane

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mkuu nina swali langu naomba unijibu
Hii kuweka nguzo nyumba ambayo ishajengwa zamani, na upandishe gorofa moja .juu yake je inawezekana ?na je gharama za kuweka nguzo zipoje mpka kuweka zege la juu?
Je umazubuti utakuwepo?
Nyumba ya chini ina vyumba 4 sio master,,puplic toil mbili,kuna dining room,siting room,store
Na juu nataka kuweka vyumba viwili master tu ,dining room,siting room..je inaweza ikani cost kiasi gani?
Asante
 
mkuu nina swali langu naomba unijibu
Hii kuweka nguzo nyumba ambayo ishajengwa zamani, na upandishe gorofa moja .juu yake je inawezekana ?na je gharama za kuweka nguzo zipoje mpka kuweka zege la juu?
Je umazubuti utakuwepo?
Nyumba ya chini ina vyumba 4 sio master,,puplic toil mbili,kuna dining room,siting room,store
Na juu nataka kuweka vyumba viwili master tu ,dining room,siting room..je inaweza ikani cost kiasi gani?
Asante
Kwa majengo ya ghorofa ni muhimu kuyafanyia kitu kinachoitwa Structural Analysis kabla ya kuanza ujenzi ili kujua kama hilo jengo litaweza kuhimili mzigo utakaobeba. Lakini pia ujenzi wa majengo ya ghorofa ni tofauti na ujenzi wa jengo la kawaida (chini), katika ujenzi wa ghorofa (Load bearing structures) tofali huwa zinalazwa ambapo sehemu ya mzigo inabebwa na hizo kuta lakini kwa nyumba za chini, tofali zake huwa zinasimamishwa.
Lakini pia msingi wa jengo la ghorofa huwa unaenda chini zaidi tofauti na msingi wa majengo ya kawaida n.k

Kiujumla jengo la ghorofa ni vizuri design yake ikaanzia chini kabisa na kama ikitokea kuna kitu ulisahahu na unataka ukiongeze huko juu basi inatakiwa ufanye tena hiyo analysis ili ujue kama hicho utakachokiongeza hakitaleta madhara ya kuanguka kwa jengo




Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa majengo ya ghorofa ni muhimu kuyafanyia kitu kinachoitwa Structural Analysis kabla ya kuanza ujenzi ili kujua kama hilo jengo litaweza kuhimili mzigo utakaobeba. Lakini pia ujenzi wa majengo ya ghorofa ni tofauti na ujenzi wa jengo la kawaida (chini), katika ujenzi wa ghorofa (Load bearing structures) tofali huwa zinalazwa ambapo sehemu ya mzigo inabebwa na hizo kuta lakini kwa nyumba za chini, tofali zake huwa zinasimamishwa.
Lakini pia msingi wa jengo la ghorofa huwa unaenda chini zaidi tofauti na msingi wa majengo ya kawaida n.k

Kiujumla jengo la ghorofa ni vizuri design yake ikaanzia chini kabisa na kama ikitokea kuna kitu ulisahahu na unataka ukiongeze huko juu basi inatakiwa ufanye tena hiyo analysis ili ujue kama hicho utakachokiongeza hakitaleta madhara ya kuanguka kwa jengo




Sent using Jamii Forums mobile app
Hujamsaidia bado ndugu yangu upeo ,

Mfano kwenye nyumba aliyokwishajenga akachafua angles zake nne za pembeni Kisha Kwa ndani akachagua sehemu hata tatu jumla 7 akatia nguzo za nguvu za hata mita 2 chini, hawezi kusimamisha ghorofa moja juu yake??

Sawa, awali tofali alisimamisha lakini si nguzo zipo kubeba hizo slab za juu?
images (12).jpeg


images (11).jpeg

Majengo kama haya hakuna tofali kabisa bali ni nguzo tu, kama zitawekwa baadae ni usalama tu sio kubeba slabs, na yanaenda juu floors kadhaa, hii moja tu ya ndugu yangu upeo itakua shida?
 
Hujamsaidia bado ndugu yangu upeo ,

Mfano kwenye nyumba aliyokwishajenga akachafua angles zake nne za pembeni Kisha Kwa ndani akachagua sehemu hata tatu jumla 7 akatia nguzo za nguvu za hata mita 2 chini, hawezi kusimamisha ghorofa moja juu yake??

Sawa, awali tofali alisimamisha lakini si nguzo zipo kubeba hizo slab za juu?
View attachment 2789950

View attachment 2789951
Majengo kama haya hakuna tofali kabisa bali ni nguzo tu, kama zitawekwa baadae ni usalama tu sio kubeba slabs, na yanaenda juu floors kadhaa, hii moja tu ya ndugu yangu upeo itakua shida?
Majengo ya ghorofa yako ya aina mbili, aina ya kwanza kuna haya ambayo huwa zinajengwa nguzo, mkanda, slab mpaka mwisho (kuta zinakuja kuwekwa baadae, kwa hivyo kuta zake huwa hazibebi mzigo bali zinakaa tu kama uzio). Aina ya pili ni haya ambayo kuta,nguzo na mkanda vyote vinajengwa kwa pamoja kwa hivyo kuta zake pia zinashiriki katika ubebaji wa mzigo na ndio maana huwa tofali zake zinalazwa.

Hiyo aina ya pili ndiyo huwa inatumika zaidi katika nyumba za kawaida za kuishi, na hiyo aina ya kwanza utaziona sana mijini kwenye yale majengo marefu

Kuwezekana inawezekana lakini ni vizuri ukaifanyia structural analysis hiyo plan. Ukiifanyia structural analysis ndio itakupatia majibu kwamba let say nguzo no 3 inatakiwa iwe na nondo 6 za milimita ngapi, hii iwe na nondo 4 n.k (nimetolea tu mfano) lakini pia itakuonesha kama nguzo,mkanda ama slab zako zitahimili kubeba mzigo au lah . Factors ni nyingi itategemea pia na uwezo wa udongo (bearing capacity) wa kubeba mzigo mahali hapo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom