Ravinder Kaushik ''Black Tiger'' : Jasusi mbobezi aliyefia jela ya ugenini

Ravinder Kaushik ''Black Tiger'' : Jasusi mbobezi aliyefia jela ya ugenini

Nashangaa watu wanao tamani kuwa majasusi
Ni bora uuze mchicha
Hilo ni kweli mkuu,

Hii kazi sio ya dezo kama watu wengi wanavoifikiria.

Kumbuka kua;
Ili kua spy mzur, ni lazma uweze Ku interact na ile jamii unayoispy

Na kanuni za kijeshi duniani znasema;
"Hakunaga msamaha kwa msaliti"

KWAHYO;
Hao unao waSPy, siku wakikugundua ni lazima wakupoteze
 
Kwa uelewa wangu mdogo kuna taasisi ya Serikali ya Marekani inayojitegemea GSA (General Services Administration) ambayo inashughulika na kusaidia utendaji kazi wa Federal agencies nyingine katika shughuli zao za kila siku kwa kutoa mawasiliano,usafiri,vifaa mbalimbali na shughuli za ugavi pamoja na kushauri na kutengeneza sera za matumizi nafuu.

Mara kadhaa vifaa vya jeshi vinapokuwa ''decommissioned'' (kutolewa kwa mifumo ya kivita na silaha) au kunapokuwa na surplus huwa wanafanya minada na kuziuza ambapo watu binafsi wanaruhusiwa japo kwa masharti kuweza kuzimiliki.Leseni ya urubani wa anga na declaration ya End user certificate ambapo utatakiwa utoe taarifa zako binafsi na matumizi ya kifaa hicho unachotaka kukinunua na kuzituma Department of Defence ambao wanafanya usaili yakinifu na ukiridhiwa utakuwa tayari kununua.Mshindi wa mnada ni lazima athibitishwe na Department of Defence kuweza kuondoka na kifaa chake.

Kutokana na masharti magumu pamoja na gharama za vifaa hivyo wanunuzi ni wachache.Mfano kuna Black Hawk UH-60A
iliuzwa USD 667,000 kwenye mnada ambao unabid deposit ya USD 100,000.Kulikuwa na bidders 4 tu na hii ni mwaka 2016.
Mbona hiyo Black Hawk iliuzwa ela ya mboga tu.

USD 667,000 Ukibadilisha ni sawa tu na Trillion 1.5 pesa halali za kitanzania.
 
Mi nasemaga jasusi wa kweli ni yule ambaye hakamatwi wala kujulikana,naam huyu ndiye jasusi aliyebobea.
 
Moja ya Changamoto kubwa sana kwenye mambo ya vita katika Karne hii ya 21 ni haya Majeshi binafsi, kwa lugha ya kitaalamu wanasema PRIVATIZATION OF THE MILITARY. Imefikia kipindi Serikali hazitumi tena wanajeshi wake na majasusi wake bali zinaajiri makampuni binafsi kufanya hizo kazi za kijeshi: Sasa kama makampuni binafsi yanaenda kufanya shughuli kubwa unategemea hawatakuwa na silaha nzito kweli ??? Kibaya zaidi ni kwamba Sheria za vita zilitengenezwa kwa kuwalenga wanajeshi wa nchi, makundi ya wadai uhuru na makundi ya waasi lakini hazikuyalenga haya makampuni binafsi ya ulinzi. Mfano kuna mikataba ya kimataifa inayohusu Vita inaitwa The GENEVA CONVENTION ya mwaka 1949, hii imewagusa tu wanajeshi wa nchi husika. Mpaka sasa hakuna Sheria au Mkataba wa kimataifa ambao umetengenezwa ili kuyabana haya makampuni binafsi ya Ulinzi ambayo yanaweza kumiliki silaha nzito.

Hapa kuna hatari kubwa kwasababu hizi silaha na teknolojia zinaweza kuangukia kwenye mikono ya magaidi na wakafanya mambo ya ajabu msiamini. Hivi kama wale BLACK WATERS wanapigana na wanajeshi wa Iraq na kuwaua unadhani hao watu wana silaha ndogo kweli ??? Tatizo hili la watu binafsi kumiliki silaha au jeshi madhara yake tumeyaona sana katika historia. Nchini Uchina miaka mia kadha iliyopita kulikuwa na wafanyabiashara "Merchants" ambao walikuja kupata pesa nyingi sana na wakaanza kumiliki vikosi vikubwa vya wanajeshi wao, hili lilipelekea ufalme wa Uchina kuwa katika vita zisizoisha hadi wakajikuta wamechelewa sana kwenye maendeleo.

Ushahidi mwingine ni K.G.B na Interpol,
Baada ya Urusi kuanguka majasusi wengi waliajiriwa na makundi ya kimafia ambayo mengi yao yalikuwa yanahusika na biashara haramu ya silaha nzito. Kuna jasusi wa K.G.B alikuwa anaitwa Victor Anatoliyevich Bout a.k.a Africa's Merchant of Death. Yeye alikuwa anachukua silaha nzito za kivita kutoka nchi zilizokuwa zinaunda Jumuiya ya kisovieti na kule sehemu kama Congo DRC, Sierra Leone, Angola, Rwanda, Burundi na kwingineko. Kibaya zaidi ni kwamba silaha nyingi zilikuwa zinapitia Bandari ya Dar es Salaam na Mombasa na baadhi ya wakubwa walikuwa wanajua na kushiriki kabisa. Nchi kama Uchina, Iran, India na Korea Kaskazini zilitumia huu mwanya kununua teknolojia nzito kutoka Urusi kupitia watu binafsi.
Sasa hii michezo yote michafu inafanywa kupitia BLACK MARKET kwasababu kukamatwa ni ngumu, hakuna kodi yoyote ile na mataifa mengi yanajihakikishia usiri mkubwa juu ya taarifa zao za manunuzi ya silaha. Yaani ni hatari sana haya makundi ya watu binafsi yanapoanza kufanya biashara za Vita na Ulinzi bila kuwepo na Mikataba maalumu ya kuwabana.

Hebu usiangalie tu kwenye vita ya hizi silaha la Kimakenika bali angali kwenye ulimwengu wa kimtandao sasa "THE WORLD OF CYBER SPACE" ambayo ni sehemu mbaya sana na hatari kuliko zote kwasasa. Watu wanasema INTERNET KNOWS NO BOUNDARIES. Hakuna sheria madhubuti ambayo imejaribu kuzungumzia hatari za mtandao kwenye mambo ya Usalama, NATO peke yao ndiyo walijitahidi kuaandaa THE TALLINN MANUAL inayozungumzia haya mambo. Lakini kuna makampuni makubwa sana ya kimtandao siku hizi, yanaajiri wasomi na wataalamu mbali mbali duniani kote. Yanaweza yakafanya vita ya kimtandao na kusababisha madhara makubwa sana kwa dunia. Hebu angalia makampuni kama GOOGLE, MICROSOFT, FACEBOOK, KASPERSKY na mengineyo jinsi ambavyo yana teknolojia kubwa sana kuliko hata nchi ya Tanzania na vyombo vyake vya Usalama (Haya ni makampuni binafsi). Ushahidi wa hili ni kipindi kile GOOGLE MAPS zimeingia, tulikuwa tunaweza hata kuangalia ramani nzima ya kambi ya jeshi ya LUGALO bure kabisaa.

Binafsi naona shirika kama hili kwa dunia yetu ya sasa ni hatari kuliko wale wanaomiliki RAPTORS au SUKHOI. Tumeona juzi Mark Zuckerberg kapata kashfa ya kuuza taarifa za wateja wake kwa wanasiasa. Nasikia GOOGLE nao wanauza kwa siri taarifa za watumiaji wao (Mimi na wewe) kwa makampuni mengine ya Urembo, Magari, Ngono na muziki ili yaweze kujua mwelekeo wa soko umekaaje. Sasa jiulize kama Tanzania inaingia kwenye Vita na baadhi ya mataifa au makundi ya Kigaidi halafu wakaamua kwenda Google kununua taarifa zao kuhusu Tanzania unadhani nini kitawazuia kuuza ??? Maana katika ubepari haya Makampuni yanachoangalia ni kupata faida kwa gharama yoyote ile.

NB: Mkuu pia usisahahu kwamba mpaka sasa Marekani imeshindwa kuyadhibiti hata makampuni makubwa ya Ulinzi, Silaha na Mafuta. Tumeona jinsi ambavyo makampuni makubwa ya mafuta kama Halliburton na Exxon Mobil yanawachezea wanasiasa wa Marekani ili kufanya migogoro nao wapate faida kubwa. Mfano hai kabisa Vita vya Iraq viliumiza sana Uchumi wa Marekani lakini kampuni la Mafuta la Halliburton lilipata faida mara tano na soko lake la hisa lilipanda balaa. Ukisoma vitabu kama MIDNIGHT IN THE AMERICAN EMPIRE na THE MERCHANTS OF DEATH haya yote kuhusiana na hizi hatari za makampuni binafsi kumiliki nguvu kubwa ya kijeshi. Leo hii kampuni la Exxon Mobil alikokuwepo Rex Tillerson kuna kitengi cha Intellijensia kinafanya kazi kama ambavyo TISS inafanya kwa Tanzania au CIA kwa Marekani. Sasa na jinsi walivyokuwa na pesa sidhani kama leo wakiamua kupigana na nchi kama Tanzania, Kenya, Uganda au Congo DRC tunaweza kushindana nao kwa Urahisi.

Hapa kuna hatari kubwa sana huko mbeleni,
Hapo bado hujagusa makampuni makubwa binafsi ya madawa kama Pfizer, Monsanto, Syngenta, NYSE na mengineyo ambayo mbali tu na kututengenezea madawa yanafanya tafiti hatari sana za silaha za kibaolojia na kuziuzia Serikali zao.
Miaka nyuma kadhaa niliwahi kushirikishwa kwenye tafiti moja inayohusiana na BIO-PIRACY barani Africa nikapewa niwaandikie wale walimu wangu baadhi ya vitu. Ndipo nikapata bahati ya kusoma nyaraka zinazohusu umafia ambao Africa tunafanyiwa na haya makampuni nikabaki nasikitika tu.....

CC: Red Giant , Consigliere, Nalendwa , SirChief , Prof, chige , Maalim Shewedy ,neo1
Uko vzur mkuu;

Nmelipenda sana andiko LAKO hili
 
Mi nasemaga jasusi wa kweli ni yule ambaye hakamatwi wala kujulikana,naam huyu ndiye jasusi aliyebobea.
Jasusi kukamatwa ni jambo la kawaida kwa sababu hata kama wewe umebobea namna gani; kosa linaweza kufanywa na wenzako na kosa hilo likapelekea kukamatwa kwako!

Aidha, Majasusi wengi hukamatwa baada ya kuchomwa na wenzao/mwenzao!

So, sio kila anayekamatwa ni mzembe!! Hata top CIA Spy anaweza kudakwa na polisi wa Tanzania!
 
Hawa Wahindi wamenikera kama walimtelekeza mwanang,kazi zingine basi tu
 
Mkuu Lumuba you couldn't be more clearer.Umenifanya nijikumbushe kuhusu tukio moja lililoripotiwa kwa wingi zaidi ingawa kuna matukio mengine mengi ambayo ama hayaripotiwi kabisa au yanaripotiwa kwa uchache mno.THE NISOOR SQUARE MASSACRE ilitekelezwa na hii kampuni ya BlackWater na kusababisha vifo kwa wananchi wengi wakiwa ni kina mama na watoto.Kampuni hii imekuwa mshiriki mkubwa wa Marekani katika kampeni za kivita tokea Afghanistan hata Iraq.

Kuna changamoto kubwa kimiongozo na kisheria kwa kuwa hivi vikundi / kampuni hayabanwi popote pale. 'They operate in a legal vacuum ' na hata wanapokuwa field ni rahisi mno kubadilika kutoka kuwa inactive/passive na kuwa active and offensive.Ni hatari kwa wananchi wa kawaida na hata jumuia ya kimataifa pia.
Hawa makampuni bora yasije uku Tz,

Maana Mkulu akikurupuka KICHWA KICHWA akakamata makinikia yao

REVENGE YAKE ITAKUA BALAA KWETU

Aisee,
Hii vita ya uchumi inahitaj akili sana, hasa hasa unapopambana na mtu alokuzd kwa kila kitu tena Kwa gap kubwa.
 
Jasusi kukamatwa ni jambo la kawaida kwa sababu hata kama wewe umebobea namna gani; kosa linaweza kufanywa na wenzako na kosa hilo likapelekea kukamatwa kwako!

Aidha, Majasusi wengi hukamatwa baada ya kuchomwa na wenzao/mwenzao!

So, sio kila anayekamatwa ni mzembe!! Hata top CIA Spy anaweza kudakwa na polisi wa Tanzania!
Kataa kubali,jasusi mbobezi ni yule asiyekamatwa.Hata iwe kwa kosa la nani.
 
The first mistake was to recruit the star to go undercover in foreign dominion. The second mistake is lack of coordination among
Indian spies in Pakistan. The major was supposed to be alerted of such trap. But shit happens....this reminds me Bradd Pitts movie in which he had married German spy
 
Sijaelewa hapa " Ravinder alikuwa mpenzi wa sanaa za sinema na maonesho na hivyo ilivyofika siku ya mahafali yake mwaka 1975 alikuwemo kwenye kikundi cha maonesho siku hiyo."

"Hatua ya kwanza kwa kijana Nabi aliyekuwa na umri wa miaka 23 kwa sasa ilikuwa ni kujiunga na Chuo Kikuu cha Kashmir akichukua masomo ya sheria (LLB) na mwaka 1975 alimaliza masomo hayo yote"


Mwaka 1975 graduation mbili ya home and away...?
 
Naam Naam Mkuu Dumbuya nafurahi kuona umeelewa kabiaa hii changamoto tuliyonayo. Umeongea msemo mzuri sana "They Operate in a Legal Vacuum" kwasababu kwenye uwanja wa vita wanaingia kama raia wa kawaida lakini hubadilika ghafla na kuanza kuwa wanajeshi kinyume kabisa cha sheria. Kisheria tunasema Direct Participation in Hostilities (DPH). Montreaux Convention imeyazungumzia tu haya makampuni kama raia wa kawaida na kusema kuwa kazi zao ni zile za kulinda Convoy, kusaidia kurekebisha silaha na ushauri wa kitaalamu kazi zote ambazo ni Indirect Participation in Hostilities. Lakini cha kushangaza hawa mamluki wakiingia huanza kufanya kazi kama wanajeshi wengine.. Balaa tupu.!
mambo ya Wagner groups huko Syria wanampiga USA na Washirika bila legal retribution inabidi kubaki viziana Jeshi halali Vs Military mercenaries 😀
 
Jasusi kukamatwa ni jambo la kawaida kwa sababu hata kama wewe umebobea namna gani; kosa linaweza kufanywa na wenzako na kosa hilo likapelekea kukamatwa kwako!

Aidha, Majasusi wengi hukamatwa baada ya kuchomwa na wenzao/mwenzao!

So, sio kila anayekamatwa ni mzembe!! Hata top CIA Spy anaweza kudakwa na polisi wa Tanzania!
Ubaya wa Ujasusi ni kwamba asilimia kubwa huwa wanafanya kazi katika Cells hivyo akidakwa moja tu huwa kundi zima linaathirika. Asilimia kubwa ya majasusi wanaokamatwa ni kuchomwa na wenzao au taarifa kuvijishwa kutoka nchini mwao wenyewe: Uzembe huwa upo lakini kwa asilimia ndogo sana kwasababu mara zote huishi macho wazi (Tip Toe) wakijua kabisa wakidakwa ni tatizo....
 
Hawa makampuni bora yasije uku Tz,

Maana Mkulu akikurupuka KICHWA KICHWA akakamata makinikia yao

REVENGE YAKE ITAKUA BALAA KWETU

Aisee,
Hii vita ya uchumi inahitaj akili sana, hasa hasa unapopambana na mtu alokuzd kwa kila kitu tena Kwa gap kubwa.
Mkuu haya makampuni yametuibia sana sana sanaa mali zetu. Mbali na tofauti zangu zote na Raisi Magufuli, katika hili la Makinikia mimi niko upande wake Asilimia 100% kwasababu najua hayaonei haya makampuni. Yanatuibia, yanachafua mazingira, yametengeneza matabaka makubwa ya Rushwa na Utakatishaji wa pesa kwa wanasiasa hapa nchini hadi hatari.
 
Back
Top Bottom