RC Chalamila: Mimi kuchomoa mashine na kufanya vurugu ni dakika mbili tu, na hakuna yeyote wa kufanya chochote!

Madaraka ya kulevya
 
Aaaaah huyu leo saa nane usiku pdf linamhusu
 
Binafsi naona RC Chalamila yuko sahihi,, awamu hii wakandarasi wanachezea sana pesa za serikali acha atambae nao,, viongozi kama hawa ndio tunawataka
 
Tatizo hata madaktari wetu wa akili nao wagonjwa na sheria mbovu zinafanya hata mwehu apewe kazi ya kusimamia wazima
 
Ndugu zangu Watanzania.

Nawasihi sana msiache kuwaombea viongozi kwa sababu nilishayaona haya na nilishasema tangu mwaka jana kuwa Mungu ameondoa kauli kwenye ndimi za viongozi ni jambo ambalo sasa linazoeleka kwa kasi sana

Huyu anayeongea hayo ni mteule wa Rais ambaye anapaswa kusimamia maadili na utii wa sheria. Lakini anajinasibu kuwa na uwezo wa kujitwalia sheria mkononi na hakuna sheria ama yeyote anayeweza kumfanya lolote.

Aina hii ya viongozi ni replica ama wanaakisi haiba na tabia ya mteuzi.


Nchi inaporomoka kwa kasi, maadili ya viongozi yamekuwa ya hovyo kwa sababu bila wao, rais hana wa kumsaidia ndo maana teuzi zinarudia rudia hakuna fikra mpya na watu wapya
 
Mtu anatishia watu silaha na Polisi wanamchikilia kama Mlevi? Polisi ndo wanotoa kibali cha kumiliki silaha kupitia Kamati za ulinzi na usalama wilaya, mkoa Hadi Kwa Mkurugenzi wa Upelelezi ambaye ni Polisi. Sasa huyu Mleviugali anaposema yeye huwa anatoa silaha popote na Hakuna cha kumfanya amebakiza sifa gani ya kumiliki silaha(Pistol) aliyonayo?
 
Mkuu, unamaanisha Tanzania haiko serious?

-Kaveli-
Lini umeona iko serio? Kuanzia Rais Hadi Mwenyekiti wa kitongoji Hakuna aliye serious, ni mizaha tu. Ili Rais awe serious mpaka mteuliwa atoe kauli inayomkosoa yeye, hizi nyingine zinazotishia raia wa kawaida Rais anaona Sawa tu.
 
🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣
 
 

Attachments

  • F1964C05-9F97-4496-967C-F0F3F5CC8F57.jpeg
    56.4 KB · Views: 1
Uko sawa mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…