RC Makonda: Anayemjua mwizi aje ofisini kwangu kusema, nitampa laki moja

RC Makonda: Anayemjua mwizi aje ofisini kwangu kusema, nitampa laki moja

Ndio ni mwenyekiti wa kamati, ila swali ni nani anayepeleleza makosa ya jinai?

Tuna vyombo vya ulinzi na mamlaka za kusimamia sheria zinavyofanya hiyo kazi sio kamati.

Hiyo ni sheria sio utashi binafsi wa mtu
Hizi ni kiki na kuna wajinga wanamuelewa sana, shida ya hii nchi mkuu ni Ujinga, Taifa lina ujinga acha kabisa, yaani watu kama Makonda wanaonekana ni kama wakina Elon Musk vile, tatizo ni ujinga.
 
Makonda kasema, atapeleleza, au Kawataka Wananchi wamletee Taarifa Mkoani ambapo kutakuapo tayari wahusika wanaoshighulikia ?.


Na hata kama hawatakuwepo, unadhan Taarifa hizo atazikumbatia??.
TAKUKURU imevunjwa? ilitakiwa kwa hilo tamko lake lei Mkuu wa TAKUKURU aachie ngazi kabisa, Nchi imejaaa wajinga sana ndio maana watu kama Makonda wanaonekana ni Big brain kumbe hakuna kitu.
 
Hahahah, kuna sheria inaitwa The Whistleblower and Witness Protection Act, 2015. kwa tafsiri rahisi ni Sheria ya Wafichuzi na Ulinzi wa Mashahidi. Pamoja na Kanuni zake za 2023

Nauliza tu hivi ndugu RC ameshauriwa kweli au kuambiwa juu ya uwepo wa hii sheria na kanuni zake na matakwa yake?

Haya bana yetu macho.
Hizo sheria weka pembeni mama, labda kwa vile hujawahi kukumbana na kadhia ya majambazi,wauwaji au wabakaji
Watajwe matukio yao yafwatiliwe na kufufuliwa!!
Naunga mkono hoja
 
Ili kuendelea kupinga vitendo vya uvunjifu wa amani mkoani Arusha Mkuu wa mkoa wa Arusha Paul Makonda amewaahidi wananchi wa mkoa huo hususani Bodaboda kuwa yeyote anayemjua mwizi na mwenye viashiria vya wizi basi akifika katika ofisi yake (yaani ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Arusha) atapatiwa Tsh. 100,000/- (laki moja tu)

Makonda ametoa ahadi hiyo leo, Jumapili Julai 14.2024 wakati wa hafla ya kufunga mashindano ya 'Samia Motocross Championship'

Yeye mwenyewe ni mwizi no 1
 
Watanzania mbona hamfahamu taratibu na sheria zenu wenyewe?.

Vyombo vinavyopeleleza makosa ya jinai unakijua?. Sasa hivyo vyombo ndio vyenye huo uwezo kisheria.

Kasome hiyo sheria niliyoitaja hapo juu.
Makonda anatafuta umaarufu tu wala hana lolote
 
Punguza ujinga kidogo Mkuu.

Wewe unafikiri mtu yoyote anaweza tu kutoka na kujiamulia maamuzi yake kwenye hii nchi?. Ni lazima sheria zifuatwe na zikiwa hazijafuatwa ielezwe wazi.

Unafahamu kuwa anayeweza kutoa zawadi kwa mfichuzi (whistleblower) ni Mamlaka yenye uwezo wa kufanya upelelezi?

Na Tanzania swala la kufanya upelelezi kwenye makosa ya Jinai halipo kwa RC bali ni Polisi, Takukuru, FIU, TCRA, n.k zote zina mifumo ya kushughulikia makosa ya kijinai.

Sasa swali ni RC anatoa zawadi kwa hao wafichuzi chini ya sheria gani?, lazima hili liulizwe ili ifahamike ni pesa yake binafsi au pesa ya umma inayopaswa kufuata mtiririko sahihi.
Makonda ni chizi haswa
 
Hahahah, kuna sheria inaitwa The Whistleblower and Witness Protection Act, 2015. kwa tafsiri rahisi ni Sheria ya Wafichuzi na Ulinzi wa Mashahidi. Pamoja na Kanuni zake za 2023

Nauliza tu hivi ndugu RC ameshauriwa kweli au kuambiwa juu ya uwepo wa hii sheria na kanuni zake na matakwa yake?

Haya bana yetu macho.
Yule ni mla unga huwa anaamka tu na lake kichwani
 
Sheria?. Hizi Sheria sindo ambazo Mtu anakua, Kisha anakua na Wakili Mzuri , Wakili anatumia Mapungufu ya Sheria zenyewe na hatimaye Muuaji anakua Huru?.


By the way Kwa Wanasheria gan??. Hawa wabungeni ??

Nchi hiii Ina wasomi wa KISHENZI wengi sana, Wazee wa mavyeti na Makaratasi but I tell you, Wana Uwezo ambazo ni 0 katika kuhakikisha Wana put into effect kile walichokisomea.

Makonda Yuko SAHIHI
Jitathmini
 
Kwani hufahamu kuwa RC ni Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wa mkoa,?

Hufahamu kuwa wafichuzi wanaenda Ofisi ya RC ambayo ina nyenzo zote ulizo zitaja hapo??
Sasa unaenda kumfichua muhalifu bila evidence yoyote? mnatafuta kushtakiwa bila sababu yoyote ile.
 
Kisheria hana hayo mamlaka ya kutoa zawadi kwa wafichuzi, labda kama atatoa pesa zake binafsi na pia hao watu hawata qualify kuwa wafichuzi na hata kuja kuwatumia Mahakamani kama mashahidi itasumbua sababu chain haijafuatwa.

Nitakupa mfano,

Polisi wanaweza wakakamata gunia la bangi, ila kama watalichukuana kulipeleka kituoni tu na kisha kwenda mahakamani kutoa ushahidi kuwa walimkamata mtuhumiwa na gunia la bangi, lazima washindae kesi. Kwanini?, sababu hawatakuwa wamefuata utaratibu.

Sasa hivyo hivyo kwa hao wafichuzi, lazima utaratibu ufuatwe sababu kuna mengi baada ya hapo.

Eleweni mifumo inavyofanya kazi Wakuu.

What if nikasema hiyo ni rushwa? Sababu ni ushawishi nje ya mfumo rasmi.

Hili ni jambo nyeti lililochukuliwa kiurahisi.
Alitokea Mbunge mmoja akawa anatoa zawadi ya baiskeli (phoenix) kwa mwananchi atakayefichua mtu anayefanya mapenzi na wanafunzi. Ile approach ilikuja kumletea shida sana na haikutekelezeka, RC ajifunze pia.
 
Hizo sheria weka pembeni mama, labda kwa vile hujawahi kukumbana na kadhia ya majambazi,wauwaji au wabakaji
Watajwe matukio yao yafwatiliwe na kufufuliwa!!
Naunga mkono hoja
Sheria zikiwekwa pembeni,hilo jambo linabaki kuwa ni la utashi wa Mkuu wa mkoa aliyepo..je akija mwingine ambaye hataki kufanya hayo anayo fanya makonda itakuaje? Tunataka iwe endelevu.
 
Ili kuendelea kupinga vitendo vya uvunjifu wa amani mkoani Arusha Mkuu wa mkoa wa Arusha Paul Makonda amewaahidi wananchi wa mkoa huo hususani Bodaboda kuwa yeyote anayemjua mwizi na mwenye viashiria vya wizi basi akifika katika ofisi yake (yaani ofisi ya Mkuu wa mkoa wa Arusha) atapatiwa Tsh. 100,000/- (laki moja tu)

Makonda ametoa ahadi hiyo leo, Jumapili Julai 14.2024 wakati wa hafla ya kufunga mashindano ya 'Samia Motocross Championship'

Hata sijqsikiliza ila hii ni ramli chonganishi
 
Tatizo hii nchi inawajuaji wajinga wengi sana ambao ujuaji wao ukifafilia haujawahi kuwasaidia chochote wao wenyewe achilia mbali familia au taifa.

Mnafahamu kabisa kashfa za Jeshi letu la kaki, mnafahamu namna wanavyofanya kazi bila weledi, ni jukumu lao kushughulikia uhalifu je nani anaweza kuwapelekea taarifa za uhalifu?
 
Sasa unaenda kumfichua muhalifu bila evidence yoyote? mnatafuta kushtakiwa bila sababu yoyote ile.
Sikiliza tena alichokisema RC. mbona unawaza juu juu tu, huyo RC yeye haelewi kuwa kuna watu wanaweza kudanganya?? due deligence itahusika,
 
Wewe ni mjinga sana.

RC ni Mwenyekiti wa kamati ya Usalama Mkoa, Ndani yake Kuna RPC, RSO n.k

RC Makonda anachofanya ni kuwamotisha Raia wema ambao Huwa Wana taarifa lkn hawajui wazipeleke wapi, Sasa wajue ni wapi zinaendaz na zitasaidia nini , na wao wanafaidika na nn kwa mustakibali wa nn.


Nilikuaga naamini JF Ina watu wenye akili kumbe baadhi yenu ni vichwa maji namna hii.

Makonda kawekesha Kambi ya Madaktari Mkoa mzima ,aliipata wapi Pesa?? Ana mawakili wa TLS wanaosaidia Raia, anapata wapi Pesa?

Wewe Hujui Katika Ma RC Bora na wabunifu hapa Nchini, Makonda ni Juu ya wote???

Kagawa Pikipiki Polisi, kapata wapi Pesa??.


Kuna Dhambi kutumia Pesa iwe yako au ya Raia Kwa jambo ambalo ni faida ya hao hao Raia???.

Hiyo MAMLAKA ndio kumbe inatakiwa itoke Hadharani iwaambie Raia, njooooni mtupe taarifa ,tutatoa Zawadi?.
Mgeni wa Jiji chuki kwa Makonda ndiyo inamsumbua,haya yote anayajua sema kaamua tu kujitoa ufahamu pale anapo mjadili Makonda, anamjadili kama Makonda na si kama Mkuu wa Mkoa na Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya Mkoa!!
 
Back
Top Bottom