RC Makonda: Yeyote anayeenda katika eneo la manunuzi lazima avae barakoa. Kwenye misongamano watu wakae umbali wa mita 2

natoa hoja hapa msimu huu wa CORONA.

Kanisa:
-shika pua yako iambie usinuse harufu mbaya
-shika mdomo wako uambie usinene mabaya
-shika macho yako yaambie yasitazame uovu
-mgeukie mwenzako mwambie kwa sauti (paza sauti mwambie usiwe kama popo)
-mshike mkono jirani yako mwambie umependeza
-shika kichwa chako tamka kipate akili
-asiyependa kukusanyika pamoja ibadani ni mchawi
-mpinga kristo yupo, kama hutaki kuhudhuria ibada wewe ni mpinga kristo
-hakuna lisilowezekana kwa Mungu kila ugonjwa unapona

serikali:
-usishike pua, macho wala mdomo
-msishikane mikono
-mkae mbali mbali angalau mita moja
-msikusanyike
-mvae mask

kanisani:
-imba toa sauti, omba kwa sauti usiombee tumboni toa sauti(watu wanapayuka mate yao yanaruka na kusambaa hovyo)
--hawavai balakoa
-wanatazamana na kushika hivyo vilivyokatazwa na serikali kuvishika
-wanakaa karibu sana chini ya robo mita
-wanaimba kwaya na kucheza miziki
-wanasali zaidi ya lisaa limoja
-watu wanafanya maombi kwa sauti kubwa wanarushiana mate, wanasali mara wanyenyue mikono juu mara washushe mara wapige magoti mara warukeruke...purukushani zote hizi wanazifanya wakiwa hawajavaa balakoa mwishoe wanakohoa kwa jasho na vumbi pamoja na kupiga chafya pasipo kuziba midomo. hawa watu wakitoka huko wanakuja mitaani tunajumuika nao katika shughuri za kijamii....si watalimaliza taifa lote endapo mwenye ugonjwa atakatiza miongoni mwao
NB: tuwe serious katika kupambana na majanga, kwanini serikali na dini vinavutana..yupi ni mpinga kristo na yupi ni mpinga uzima?
 
Ukiangalia kwa makini utakugundua viongozi wa serikali yetu hawapo siriasi na huu ugonjwa labda kwa kuwa wao ndio watakuwa wa kwanza kuwekewe ventilator.

Leo Dar watu wanahaha kutafuta barakoa hivi kweli serikali imeshindwa kuongea na wadau wa Dar wakagawa barakoa za kutosha mji mzima na ikiwezekana na sanitizer.

Barakoa za surgical moja ni kati ya shs 500 na 600 kama serikali ingefanya juhudi ingeweza kupata chini ya hapo na hatimae kungekuwa na barakoa za kutosha Dar es Salaam kuanzia leo.

Lakini badala yake wamewekwa mgambo wa jiji ili wakamate watu wasiovaa barakoa.

Hawa viongozi wetu sijui wanakwama wapi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wale watakaokaidi wacharazwe viboko

Sent using Jamii Forums mobile app
Hii idea ya kutumia viboko, mimi nilikuwa nafikiria itumike hata kwa watu wanaopatikana na makosa madogo madogo kiasi kwamba wanatakiwa kuwekwa mahabusu. Maana najiuliza sasa mahabusu sasa hivi watu wanaishije? Mwizi wa kuku aliyeko mahabusu achapwe viboko halafu aachiwe arudi nyumbani kwake badala ya kuendelea kuongeza msongamano wa watu kwenye mahabusu, atatuongezea wagonjwa wa corona bure
 
Ukitaka kujua "UKAIDI WA WATANZANIA" kesho kuna viongozi wa dini watapanda madhabahuni kufanya ibada kwenye mikusanyiko mikubwa ya watu.
Mh. Mkuu wa Mkoa watu hawajamwelewa vizuri. Alichosema kwa sasa ni kuwa, kwa kuanzia, watu wavae barakoa wakiwa wanaelekea Sokoni au kwenye daladala. Na hii taarifa inaonyesha KAMA kwa sasa cases zinazopatikana za waathirika walio wengi ni kutoka kwenye mikusanyiko ya daladala na ya Sokoni, ila sasa sisi uelwa wetu ni mdogo. Asingeweza kusema moja kwa moja hivyo kwa sababu angesababisha taharuki, watu wangeacha kupanda daladala na kuanza kutembea, na sokoni pia ingekuwa shida
 
Fuata masharti unayoelekezwa. Unanunua chakula cha elfu tano kwa siku unaacha kununua barakoa ya elfu 2 kisa unataka msaada wa serikali. Tumeambiwa tujikinge, jilinde wewe ilinde na familia yako na fuata maagizo ya viongozi kama huwezi stay home Corona inaua
 
"Wagonjwa wote waliyobaki (131) hali zao ni nzuri isipokuwa Wagonjwa 4 wanapatiwa matibabu ya Wagonjwa mahututi kutokana na kusumbuliwa na matatizo mengine ya kiafya."
 
Aache watu wajilinde wanavyoweza wao,kama walisema hawawezi kuweka watz lockdown kwakua maisha yao ni ya kubangaiza, hio hela ya kubadilisha mask kila baada ya Masaa 4 wanatoa wapi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ibada sisitishwe acha uboya wewe

Kama mama rwakatare kafa na corona unajua kawaambukiza wangapi
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…