RC Mwanamvua Mrindoko: Zaidi ya Trilioni 1.2 Zatolewa Kubadilisha Katavi Miaka Mitatu ya Rais Samia

RC Mwanamvua Mrindoko: Zaidi ya Trilioni 1.2 Zatolewa Kubadilisha Katavi Miaka Mitatu ya Rais Samia

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301
Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mwanamvua Mrindoko kwa kushirikiana na wakuu wa wilaya zote zilizopo ndani ya mkoa wa Katavi wameeleza mafanikio yaliyofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta Samia Suluhu Hassan kwa kipindi cha miaka mitatu ya uongoziwake ambayo yameleta matokeo chanya katika jamii​

Wakizungumzia miradi mbalimbali iliyotekelezwa ndani ya mkoa wamesema Serikali ya Rais Dkt Samia Suluh Hassan imetoa fedha zaidi ya Trilion moja ambazo zimekamilisha baadhi ya miradi katika sekta mbalimbali huku mingine ikiendelea na ujenzi

Akizungumza kwa niaba ya MKuu wa wilaya ya Mpanda mstaiki Meya wa Manispaa ya Mpanda Haidary Sumry amesema kwa kipindi cha miaka mitatu ya Samia wanaendelea kuboresha miondombinu ya afya huku Chifu wa kabila la Wakonongo akidai Rais Samia ameweza kusimamia amani ya nchi toka amekabidhiwa madaraka ya uongozi.

Kongamano la kuelezea mafanikio ya miaka mitatu ya Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dokta samia Suluh Hassan limehudhuliwa na viongozi mbalimbali wa chama na Serikali pamoja na wananchi wa maeneo mbalimbali ya mkoa wa Katavi.

one.PNG
two.JPG
 

RC MRINDOKO: KATAVI IMEPOKEA ZAID YA TRIL. 1.2 NDANI YA MIAKA 3 YA RAIS SAMIA

Mkuu wa mkoa wa Katavi, Mh. Mwanamvua Mrindoko amesema katika kipindi cha miaka Mitatu ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mkoa huo umefanikiwa kupokea zaidi ya Trilioni 1.2
ambazo zimesaidia katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya Afya na Elimu.

Mh. Mrindoko amebainisha hayo katika mkutano wa Katibu Mkuu wa CCM na viongozi wa Chama hicho Mkoa wa Katavi Kwa ajili ya kuzungumza mambo mbalimbali ya utekelezaji wa Ilani ya Chama na Muelekeo wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025.

Amesema Fedha hizo zimesaidia kupatikana kwa Hospitali Mpya ya Mkoa ambayo Ujenzi wake unaendelea huku Ujenzi ikiendelea kutoa huduma, ikiwa na vifaa tiba vya kibingwa. pia Ujenzi wa Hospitali nne za Halmashauri ambazo pia zimeanza kutoa huduma, vituo vya afya 20, Zahanati 36 na Magari ya Waginjwa zaidi ya 16.

Amesema kwa upande wa Sekta ya Elimu Shule mpya 95 zimejengwa huku elimu bila malipo ikiendelea pamoja na Ujenzi wa madarasa zaidi ya 773 na Ujenzi wa miundombinu ya Barabara Kuu Mpanda -Tabora, Vikonge, Kibaoni pamoja na Ujenzi wa madaraja.

Aidha, ametumia nafasi hiyo kuishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya maendeleo na kujikita katika kutatua matatizo ya wananchi wa mkoa huo.
 

Attachments

  • WhatsApp Video 2024-04-13 at 21.17.43(1).mp4
    17 MB
Back
Top Bottom