:bored::bored::bored:
1) Atheist, mtu asiyekubali uwepo wa "a supernatural being", yani mtu mwenye nguvu zisizo za kawaida, AMBAYE NI MTAKATIFU, kama wanadini wanavyodai.
Hata mimi siamini uwepo wa mtu mwenye nguvu zisizo za kawaida,AMBAYE NI MTAKATIFU, kama Atheist mnavyodai.
Sijawahi kusikia deen ambayo inaamini juu ya uwepo wa mtu mwenye nguvu zisizo za kawaida,ndo kwanza nasikia kwako wewe...
2) Kwa kiwango kikubwa kwa kuwa throughout history hamna aliyeweza kuthibitisha uwepo wa kiumbe kama huyo, zaidi ya kupeana moyo kuwa ana sababu zake za kujificha na kuwa kimya, ikiwemo ile ya 'mungu ni mkuu sana kuliko wewe so ahitaji kukuthibitushia chochote"!!!
Lakini uwepo wa akili kichwani mwako umewahi kuuthibitisha, ukiitwa zu.zu unakataa,kama unakichwa na hujawahi kuthibitisha uwepo wa akili kichwani mwako,huku ukiulizwa kama una AKILI UNASEMA NDIYO, unaweza kuthibitisha kwamba wewe unazo akili ? kwako kila kitu ili kiwepo lazima kiweze kuthibitishwa kwa mtazamo wako. No wonder wewe ni umeamua kuwa muumini wa imani ya kutoamini uwepo wa mtu mwenye nguvu...iamni ambayo kiukweli ni uongo.kwa kuwa Hakuna mtu mwenye nguvu sizizo za kawaida duniani.
3) ona number moja
Ukweli ni nini ? hilo ndilo swali,unaacha kujibu unaandika maono yas kiATheist.
4) Labda kwakuwa sayansi kwako ni kitu cha ajabu, lakini jibu ni ndio. Kuna mambo watu wanaona "ya ajabu" na "ya kiroho" wakati yana maelezo "perfect" ya kusayansi. Mfano meditation. Hata mungu akijitokeza siku moja kila jicho likamwona, nayo ni sayansi. Na kwani mungu na ukuu wake wote anaona ugumu kutoa uthibitisho rahisi tu ambao hamna wa kupinga????! Kwanini kang'ang'ania kuwa 'tumwamini tu' na wale 'wachache' aliowatuma/anaowatumia? We hushituki tu!!! Au ndo hivyo, ni moyo sana hapaswi kuulizwa chochote?
Ficha upu.mbavu wako,Atheist hawana hati miliki ya sayansi,unajitekenya na kucheka mwenyewe, kama si kichaa nini ? binadam kamili unaandika kana kwamba Sayansi ni mali ya Atheist,wakati ukweli ni kwamba miongoni mwa wanasayansi nguli wengi walikuwa Theist,koma wala usirudie kuonesha kwamba sayansi ni kwa Atheist.mengine ni pumba tu.
5) wowote usiohusisha imani ya dini fulani; ambao hautapingwa hata miaka elfu ijayo; ambayo iko kifacts zaidi ya kiimani; ambayo either umeishi kwenye misitu ya Amazon miaka yako yote au pale New York, utajua; ambao kwa "uwezo wa kibinadamu" YAANI kisayansi utafunga mioyo yote inayothubutu kukataa uwepo wa mtu huyu MKUU , MWENYE NGUVU ZA AJABU.
wowote ndiyo kitu gani, andika kama mtu mzima,ushahidi gani unataka ili uweze jua kwamba kweli Mungu yupo ? acha kuandika kwa vile tu unajua kutumia key board,jibu swali uliloulizwa.
6) sio lazima maabara......kuna njia zingine ni ndogo sana ukilinganisha na ukuu wa huyu, mfano, sali chungwa litokee mkononi just to prove he's there.
Sihitaji mfano nahitaji kitu thabiti,kwa nini unapenda kudhani badala ya kuandika kitu kuntu ili usaidiwe...Kutokea kwako ni mujiza kuliko chungwa, ungekuwa na uwezo wa kutafakari japo kidogo usingetoa mfano wa Chungwa. DNA ya mwili wako ni muujiza ambao kwa wenye akili wanakili kuwepo kwa designer wa ajabu wa DNA yako. Lakini kwa Atheist hivyo sio big deal...
7) mungu siku aongee dunia nzima imsikie na imuelewe, aongee either kama mtu mkatili na mwenye mamlaka kama tulivyomzoea, mfano aseme "BADO HAMTAKI KUNIAMINI, MOTO NI WENU", au aongee kama yule mungu aliyekuja dunuani, "EEEENYI WANAANGU, MBONA MNA MIOYO MIGUMU KUAMNI? KILA KITU UTHIBITISHO TU. BASI KWAKUWA NAWAPENDA SANA, LEO NIMEWAPA UTHIBITISHO MKUU KULIKO YOTE"...dah, itabidi siku hiyo kila mtu afunge na kusali na kuvaa magunia. BTW angekuwa anatupenda sana angeondoa mateso toka miaka mia elfu iliyopita....jamaa either ana moyo mgumu kweli, au hawapendi tu na anafurahia mateso yenu, au HAWEZI, au HAYUPO.
Hata akiongea, lazima uwe na masikio yua kuweza kumsikia,tulio wake tunamsikia na anaongea nasi siku zote, pumbafu,mateso ambayo wewe unajitakia mwataka Mungu ayaono=doe, Kuishi duniani kuna TERMS AND CONDITIONS wewe unaishi bila kufuata Terms and Conditions,kwa ujinga wako mateso yakikupata wataka Mungu ayaondoe. too low
8) the fact kwamba the universe inatanuka ni FACT na sio UNABII, so uhitaji kuamini unahitaji kujua.
Unajua nini ndivyo ulivyo kariri,siku akija mwingine na hesabu tofauti,tutegemee total paradigm shift na hiyo ndiyo sayansi,sayansi haina fact za kudumu kwa kuwa bado haijui siri zote za uumbaji wa Ulimwengu,Wanasayansi nguli wamejitahidi kutafuta formula Mungu alitumia Kuumba dunia bado hawajapata.that being the case,kilichopo ni current knowledge na sio fact.
Tatizo watu wengi wanajifanya wanajua evolution wakati hawajui....mimi kwenye mijadala ya evolution huwa mkweli kuwa sijasoma evolution hasa katika macro-level. Evolution katika micro-level uhitaji hata ufike darasa la saba. Nani asiyejuwa vijidudu hugeuka na kuwa resistant kwa dawa? Ingawa ukifikiria utajiuliza hivi vidudu vitakuwaje miaka hata elfu tu ijayo? Hence, macro evolution.....
evolution at macro-level is a HOAX, ni mazu.zu hasa Athesit wanaoweza kuikubali kwa kuwa common sense ZERO.
Kutanuka kwa moyo???
Maswali mengine ni ya kichokozi tu, sasa wewe kama unaona vitu vinabadilika baada ya muda kwa nini unauliza tena kama mtu anaamini atabadilika? unless the process stops, organisms WILL go on changing.
evolution at work, washangaa nini na hiyo ndiyo kweli ya waji.nga.
9)unamaanisha advance in technology ndo evolution au?
Ndio maana atheists got to work, wanajua ni juu yetu kutunza hii dinia na si kusubiri kiama....kwanza kuwa mkweli, katika historia yote ya mwanadamu, watu walipigana kwa misingi ipi kama si mungu na imani....hata waliogombania mali na wanawake walisema ni mungu ametupa.
advance in tech, ndiyo nini ? evolution ipo why bother with tech, wakati ni swala la wakati tu evolution inaweza kuleteleza IPHONE ZIWE ZINACHUMWA KWENYE MIEMBE due to evolution, haihatajiki Artist, designer, wala maker as far as Atheism is concerned, all that is need ni time (millions of years) Yaani ninyi hata kukuiteni vich.aa ni kuwapendelea...
Atheisism, kama Theism, ikitumiwa vibaya italeta maafa.
Atheism yaweza tumiwaje vibaya ?
:wave::wave: