Report ya Mapigano ya mpaka wa India na China ya 2020

Report ya Mapigano ya mpaka wa India na China ya 2020

Bravo snr

Senior Member
Joined
Aug 16, 2020
Posts
182
Reaction score
477

Chanzo: www.trt.net.tr

Wanajeshi 4 wa China wadaiwa kufariki kwenye mapigano ya mpaka wa India mwaka 2020


Mapigano ya mpaka wa India na China


Wanajeshi 4 wa China wameripotiwa kufariki mwaka jana kwenye mzozo wa mpaka wa India katika Bonde la Galvan.

Kulingana na ripoti ya Jeshi la Ukombozi wa Umma (PLA) ya gazeti la siku, ilielezea mapigano ya China na India katika mpaka wa Bonde la Galvan ya Juni 2020 kwa kuandikwa,

"Tangu Aprili 2020, jeshi la kigeni lililohusika limevuka mpaka ili kujenga madaraja na barabara, na kwa makusudi ya kusababisha matatizo kwa kubadilisha hadhi ya mpakani."

Ripoti hiyo pia ilidai kwamba India iliwashambulia jeshi la China na wanajeshi 4 walifariki, ambao ni miongoni waliokuwa wametumwa kwa ajili ya mawasiliano na India.

Katika vyombo vya habari vya China, majina ya wanajeshi yalitangazwa kuwa Çın Hongcün, Çın Şiangrong, Şiao Sıyüen na Vang Cuoran.

Kwa mara ya kwanza, serikali ya China ilitangaza kupoteza wanajeshi katika mapigano ya mpakani.

India ilikuwa imepoteza wanajeshi 20 katika mapigano yaliyotokea mwezi Juni 2020 na kudai kuua wanajeshi 45 wa China na wengine kujeruhiwa, lakini China ilikanusha madai haya.

Katika taarifa baada ya mapigano, Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China Cao Licien alisema kuwa Bonde la Galvan ni mali ya China, na Cang Shuili ambaye ni Msemaji wa Kikosi cha Ukombozi cha Wananchi wa China Magharibi alisema, "Eneo la Bonde la Galvan daima ni mali ya China."

Msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya China Wu Zian alitangaza mnamo Februari 10 kwamba wanajeshi wa China na India walianza kujiondoa kutoka Ziwa la Pangong wakati huo.
 
Haya mapigano wahindi waliingia cha kike.....mchina anakucharaza na rungu lenye misumali hata muda wa kuimba masongi yao walikosa
Hahaaa ila jua zote nchi zipo vizuri kijeshi na vifaa pia, wote wana nuclear weapons
 
Hahaaa ila jua zote nchi zipo vizuri kijeshi na vifaa pia, wote wana nuclear weapons
Kwenye hayo mapigano walifata makubaliano yao ya miaka kadhaa nyuma huko haikutakiwa kutumia silaha zozote za moto mfano bunduki na mabomu....kama kuchapana ilikua kiume tu mkono kwa mkono mchina ndo akatengeneza marungu na mafimbo mengine akapigilia misumali na kuweka zile waya za fensi zinazokua kama na mibamiba ndo wakawa wanaenda kuwachapia wahindi
 
Kwenye hayo mapigano walifata makubaliano yao ya miaka kadhaa nyuma huko haikutakiwa kutumia silaha zozote za moto mfano bunduki na mabomu....kama kuchapana ilikua kiume tu mkono kwa mkono mchina ndo akatengeneza marungu na mafimbo mengine akapigilia misumali na kuweka zile waya za fensi zinazokua kama na mibamiba ndo wakawa wanaenda kuwachapia wahindi
Sijajua hayo makubaliano ila kama ni kweli basi ni kichekesho, ngoja nitafiti ndugu.. Ila hivyo vita vitakuwa vinachekesha sana. Siwezi kukubishia bila utafiti wa kina
 
Sijajua hayo makubaliano ila kama ni kweli basi ni kichekesho, ngoja nitafiti ndugu.. Ila hivyo vita vitakuwa vinachekesha sana. Siwezi kukubishia bila utafiti wa kina
Ni kichekesho sana. Ngoja na mimi nicheki ukweli wake.
 
Ha ha ha ha ha ingekuwa afrika zingechapwa nachopendeaga africa linapokuja swala la ugomvi wa mipaka huwa hatuogopani mfano tanzania na malawi kuhusu ziwa nyasa ilibakia kidogo tulianzishe kenya na somalia kuhusu eneo la bahari wakenya na jeshi lao lenye nguvu lakin wanasita kungia kwenye mgogoro na somalia
 
Wahind ni mdebwedo tu wale .....hawana kitu .....ATA TZ ....TUNAWACHAPA
 
Ha ha ha ha ha ingekuwa afrika zingechapwa nachopendeaga africa linapokuja swala la ugomvi wa mipaka huwa hatuogopani mfano tanzania na malawi kuhusu ziwa nyasa ilibakia kidogo tulianzishe kenya na somalia kuhusu eneo la bahari wakenya na jeshi lao lenye nguvu lakin wanasita kungia kwenye mgogoro na somalia
Kenya na Uganda kisiwa Cha migingo
 
Back
Top Bottom