Ripoti ya CAG 2021/2022. ATCL, NHIF, Deni la Taifa, Vyura wa Kihansi, risiti za kielektroniki, Biswalo. Vyazua Mjadala

Magufuli alikuwa anamchukia Assad. Sasa Magufuli ameondoka tuone jambo gani litawafika hawa watu wanaotiliwa mashaka na CAG.
Je,watu wanayo appetite ya hawa vigogo kusakwa mmoja baada ya mmoja na kutiwa pingu?
 
Tuna taka ukaguzi wa ofisi zifuatazo 1. Ikulu 2. TANROAD 3. TANESCO 4. Wizara(Maji, Fedha, Nishati, Ujenzi na Afya)
 
Hii nchi yetu ngumu sana aisee.

CAG anatusomea mambo ambayo yataishia hewani tu without any action.

Ukiwa na serikali zinazoingia madarakani kwa kunajisi chaguzi, tegemea mifumo ya nchi hiyo kufubaa, moja wapo ni hilo la ripoti za fedha kutofanyiwa kazi ipasavyo.
 
Haya mambo bora hata wangekuwa hawatuambii.
 
Adhabu iliishia hapo
Huyu hapendelei kutia watu kwenye roba au mlitaka afanye hivyo? Rais ameagiza Taasisi husika kuchukua hatua mnasema hajachukua hatua! Mlitaka avae mavazi ya Jaji awahukumu watu?

STUPID
 
Nitumie Copy la Report Mkuu
 
Kwa Report wanayo muda mrefu wangekuja na njia zilizochukuliwa wanasoma Report huku wezi wakisikiliza wakiwa Nje wakimcheka CAG maana wanajua hakuna kitakachofanyika...
 
Mbona arudia tena kusoma ripoti ileile?

Alipaswa kujiandaa kuja kujibu masuali mbalimbali ya waandishi na wapashaji habari.

Waandishi na wapashaji habari walipaswa kuja na masuali ambayo yametokana na kuchambua ripoti hiyo.

Hii nchi ngumu hii.
Waandishi na hao uliowaita "wapashaji" hasingeweza kufanya uchambuzi wa ripoti wasiyonayo, leo ndio imekuwa wazi kwa umma hivyo itachambuliwa sasa. Na kuhusu maswali, hasa hiyo ripoti ndiyo maswali yenyewe. Wanaotakiwa kuulizwa ili wajibu ni serikali.
 
Ucheleweshaji malipo umesababisha riba ya bilioni 418.77
CAG amesema alibaini ucheleweshaji wa malipo na kuzaa riba ya bilioni 418.77 katika taasisi mbalimbali za Serikali.
Kwa mtindo huu watanzania nawaambia hivi hatutoboi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…