Ripoti ya CAG imefichua madudu mengi ya awamu ya tano, kulikuwa na ufisadi wa kutisha



Which school did you attend to?
 
Mwezi hupatwa. Jua pia hupatwa. Ukweli sio exception! Yote matatu hupatwa(hufichika) kwa muda mfupi sana!
 
Marehemu hakupaswa kuzikwa kiheshima vile. Maiti yake ingetupwa hata uko zanzibar baharini katikati.

Mtu aliyeua uchumi wa tanzania na kumwaga damu pia za watanzania.

Hatujawahi kupata rais wa hovyo kama huyu aliyejiita mzelendo.

Hovyo kabisa.
 
Anajipanga ...hii sio lelemama..inaenda kuunguza malisho ya wengi
wakikaliwa kimya Mshana wananchi hawataelewa kabisa kama nawaona walivyo busy kutoa hela ndani yasije kuwakuta ya kigogo wa TPA 😀
 
wakikaliwa kimya Mshana wananchi hawataelewa kabisa kama nawaona walivyo busy kutoa hela ndani yasije kuwakuta ya kigogo wa TPA 😀
TUNASHANGAA TAARIFA ZA CAG, KWA SABABU TULINYIMWA TAARIFA SAHIHI.

Taarifa za mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG) zimeivua nguo serikali ya awamu ya tano iliyokuwa chini ya Dikteta John Magufuli.
Angalau sasa watanzania wanajifunza jambo moja; faida za uhuru wa habari.

Dikteta Magufuli alidhibiti vyombo vya habari kwa kutunga sheria ngumu zilizowanyima wakosoaji wa serikali uhuru wa kuchapisha habari. Ilibidi vyombo vya habari vitoe taarifa nzurinzuri za kumpendeza Dikteta Magufuli.

Shirika la habari la Taifa (TBC) likaongoza ngonjera za kumsifu Dikteta Magufuli.
Mashirika binafsi ya habari yakaitikia kwa beti za kusifu na kumpamba Dikteta Magufuli.

Chombo cha habari kilichochapisha taarifa zisizopendeza kilishughulikiwa.

Tafsiri ya uzalendo ikawa kumsifu Dikteta Magufuli, kuandika habari za kupendeza hata kama ni za uongo na kuficha madudu ya serikali. Huo ndio uzalendo wa nyakati za Dikteta Magufuli.

Waliotaka kuutafuta ukweli, walikiona cha mtema kuni. Walitekwa na kupotezwa. Ukweli ungepatikana, nani angemsifu Dikteta Magufuli kwa nyimbo na mapambio?

Propaganda za kusifu zilibamba kwelikweli. Watu wakaaminishwa kwamba eti Magufuli amefanya mambo makubwa ndani ya muda mfupi. Wajinga ambao ni wengi wakaamini kwamba hakuna Rais aliyewahi kufanya makubwa zaidi ya Dikteta Magufuli.

Yote hayo ni kwa sababu wanahabari walitakiwa kuandika hayo. Aliyethubutu kuandika kinyume aliandamwa na vitisho, makaripio na hata kufanyiwa mambo yasiofaa kwa utu.

Lakini sasa Dikteta Magufuli hayupo.
Tumejua; kumbe alibinya uhuru wa habari ili wananchi wapate habari za kumpamba tu na sio zile zinazomchafua hata kama zina ukweli.

Kama kungelikuwa na uhuru wa habari, yapo mambo ambayo kama yangesemwa hadharani, yangepigiwa kelele na serikali ingechukua hatua (hata kwa aibu tu) kuyarekebisha. Taarifa za CAG zimeonesha ufisadi wa kihistoria ndani ya ardhi ya Tanzania baada ya Dikteta Magufuli kuondoka. Laiti kama angekuwa hai, pengine tusingepata taarifa hizi za ufisadi.

Hata hivyo, tukubaliane kwamba tatizo kubwa la nchi yetu halikuwa Dikteta Magufuli peke yake, bali ni Watanzania wenyewe. Kwa sehemu kubwa wahusika wa ufisadi ni WATANZANIA. Ni bahati mbaya tu tulikuwa na kiongozi dikteta aliyebana uhuru wa habari na hivyo kuwa sehemu ya Tatizo la nchi yetu. Tulikuwa na kiongozi aliyeamini katika uongo mzuri kuliko ukweli unaouma - tingatinga liloharibu mazao kwa kisingizio cha kusafisha shamba.

Tunahitaji uhuru wa habari ili mambo mengi yawekwe hadharani. Tuyajue, tupige kelele, tusutane, tubishane, tusemane, tuzomeane, turekebishane kabla ya kukaguliwa na kuumbuliwa na CAG.

C & P
 
Gharama za matibabu ya Spika wa Bunge, Job Ndugai, nchini India kwa kipindi cha miezi mitano kufuru!

Kwa uchambuzi wa ripoti ya CAG, Bw. Job Ndugai alikaa India kwa miezi mitano, sawa na siku 150. Kwa siku moja alilipwa posho ya dola 500 sawa na Sh. 1,160,100.00, na hivyo kwa miezi mitano alilipwa dola 75,000 sawa na Sh. 174,015,000.00.

Akiwa India alikuwa na wasaidizi wawili – maana alihamishia ofisi yake huko huko hotelini. Kwa gharama ya dola 450 sawa na Sh. 1,044,090.00 kila moja kwa siku, walilipwa dola 900 sawa na Sh. 2,088,180.00 kwa siku. Kwa siku 150 walizokaa India, walilipwa dola 135,000 sawa na Sh. 292,950,000.

Kwa ujumla, matibabu ya Ndugai kwa miezi mitano huko India yalitumia posho za sh. 466,965,000. na hapo bado gharama za hospitali huko India, na tiketi za ndege kwa watu wote hao, na bado gharama alizokuwa anatumia mkewe.

Takwimu hizi zilikuwa ni kwa mujibu wa ukaguzi wa CAG katika Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto katika hospitali za India.

Wakati huo huo tusisahau kuwa Bw. Job Ndugai aliendelea kupata mshahara wake na posho zake kama Spika wa Bunge ambazo idadi yake naomba kama kuna watu humu wanazijua watusaidie kuzitoa.

Hakuna anayejua kwa uhakika Bw. Job Ndugai alikuwa anaumwa ugonjwa gani uliosababisha hadi ofisi yake ihamishiwe 5-star hotel nchini India ambako alichukua VIP suite nzima. Mpaka sasa gharama za matibabu yake ni siri kama ulivyo ugonjwa wake.

Ana apartments 78 dodoma,ivi CAG huku hafiki??

Mungu tupe nguvu....

Veronica France[emoji1241]
 
Hii salaam mpya: Nawasalimia kwa jina la CAG
Mnaitikia: Tumepigwa sana
 
Mission yote ya hii mambo ni Bandari ya Bagamoyo
 
Chini ya CCM hatuwezi kupata mabadiliko ya MFUMO TULIONAO wa utawala. Sasa hivi wapigaji wanajipanga upya kupiga chini ya SSH kama akiendelea na MFUMO TULIONAO.
 
Hatuna bunge.
Hili la Ndugai ni kamati ndogo ya CCM.
 
Siku ya leo sijui tuuiteje huko; Mbaya? Au nzuri sana?

Taarifa za mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG) zimeivua nguo serikali ya awamu ya tano iliyokuwa chini ya Dikteta John Magufuli.
Angalau sasa watanzania wanajifunza jambo moja; faida za uhuru wa habari.

Dikteta Magufuli alidhibiti vyombo vya habari kwa kutunga sheria ngumu zilizowanyima wakosoaji wa serikali uhuru wa kuchapisha habari. Ilibidi vyombo vya habari vitoe taarifa nzurinzuri za kumpendeza Dikteta Magufuli.

Shirika la habari la Taifa (TBC) likaongoza ngonjera za kumsifu Dikteta Magufuli.
Mashirika binafsi ya habari yakaitikia kwa beti za kusifu na kumpamba Dikteta Magufuli.

Chombo cha habari kilichochapisha taarifa zisizopendeza kilishughulikiwa.

Tafsiri ya uzalendo ikawa kumsifu Dikteta Magufuli, kuandika habari za kupendeza hata kama ni za uongo na kuficha madudu ya serikali. Huo ndio uzalendo wa nyakati za Dikteta Magufuli.

Waliotaka kuutafuta ukweli, walikiona cha mtema kuni. Walitekwa na kupotezwa. Ukweli ungepatikana, nani angemsifu Dikteta Magufuli kwa nyimbo na mapambio?

Propaganda za kusifu zilibamba kwelikweli. Watu wakaaminishwa kwamba eti Magufuli amefanya mambo makubwa ndani ya muda mfupi. Wajinga ambao ni wengi wakaamini kwamba hakuna Rais aliyewahi kufanya makubwa zaidi ya Dikteta Magufuli.

Yote hayo ni kwa sababu wanahabari walitakiwa kuandika hayo. Aliyethubutu kuandika kinyume aliandamwa na vitisho, makaripio na hata kufanyiwa mambo yasiofaa kwa utu.

Lakini sasa Dikteta Magufuli hayupo.
Tumejua; kumbe alibinya uhuru wa habari ili wananchi wapate habari za kumpamba tu na sio zile zinazomchafua hata kama zina ukweli.

Kama kungelikuwa na uhuru wa habari, yapo mambo ambayo kama yangesemwa hadharani, yangepigiwa kelele na serikali ingechukua hatua (hata kwa aibu tu) kuyarekebisha. Taarifa za CAG zimeonesha ufisadi wa kihistoria ndani ya ardhi ya Tanzania baada ya Dikteta Magufuli kuondoka. Laiti kama angekuwa hai, pengine tusingepata taarifa hizi za ufisadi.
 
Bashiru hana raha, hana amani kutokana na kuhusishwa na madudu kadhaa kwenye ugonjwa na msiba wa mwendazake. Yeye anajitetea mbele ya wazee wastaafu na maprofesa wastaafu kuwa Mwanasheria Mkuu (AG) ndiye aliwapotosha msiba ulipotokea.

Aliwashauri wenzake kwamba mambo ya kumwapisha Samia kuwa rais yangeweza kufanyika baada ya mazishi. Kauli hiyo ikatafsiriwa kuwa yeye Bashiru anathubutu kuzuia Samia kuwa rais. AG akakaa kimya kabisa. Bashiru amemchukia sana AG. Kunahitaji upatanisho.

Bashiru anakana kuhusika na ukwapuaji wa fedha BoT. Kumekuwa na tuhuma kuwa yeye, Mpango, Dotto na Dr. Mchembe (daktari wa JPM) walichota fedha BoT wakati wa ugonjwa na msiba wa JPM. Samia aliagiza ripoti ya ukaguzi toka kwa CAG inayoonyesha matumizi Kati ya Jan na Machi.

Uteuzi wa Bashiru kuwa Katibu Mkuu Kiongozi ulitia shaka. Yeye anadai hakuwa consulted na JPM. Alimwita usiku kumwambia kesho yake anamteua. Na siku ya kuapishwa, JPM alikuwa tayari anaumwa. Alitokea kwenye drip kuja kumwapisha. Baada ya kuapishwa Bashiru hakukutana naye tena

Kwa muda ambao JPM hajazidiwa kabisa, Bashiru alikuwa anapewa maelekezo yote kwa simu.

Bashiru anadai kuwa alilalamika kwa JPM kwamba watu, hata ndani ya chama chake, wananung'unika kuwa anamuandaa kuwa mgombea 2025; JPM akajibu, "kuna ubaya gani?"

Bashiru anawaambia baadhi ya mabalozi rafiki zake na maprofesa wa UDSM kuwa ni kweli JPM alizungukwa na "majizi na majambazi" ndani na nje ya Ikulu; kwamba JPM alishayajua lakini hakuweza kuyashughulikia kwa vile alishawekeza muda na mali kuyajenga na kuyatetea hadhrani.

Dk Mchemba alikuwa daktari wa JPM siku za mwisho akichukua nafasi ya Dk Ng'wale aliyehamishiwa kwa First Lady. Alikuwa CEO wa Hospital ya Mzena. Pia ni ofisa TISS. Alishika nafasi zote 3 kwa amri ya JPM. Alienda BoT na Dotto wakiwa na saini ya Mpango wakamzonga Gavana.

Taarifa zinasema tayari Dk Mchemba amefutwa kazi na amenyang'anywa kitambulisho cha TISS baada ya "kusota ndani."

Hapo hapo kuna bifu la Bashiru dhidi yaMufti Mkuu. Bashiru anadai kuwa wakati serikali inasita kutangaza msiba wa JPM, Mufti alitumia vibaya muda huo Mufti Zubeir alikuwa rafiki wa JPM. Na alimtumia katika mengi. Baada JPM kufariki dunia, kabla ya kifo kutangazwa, Dk. Mchembe na kundi lake walimdanganya Mufti awasaidie kumshauri Samia ajiuzuru umakamu kwa hoja kuwa JPM akitoka hospital anamfukuza kazi bila kujali katiba
Walitaka Samia kwanza ajiuzuru ndipo watangaze msiba, ili apatikane mwanaume mwenzao ashike uongozi wa nchi. Samia alikataa. Ikumbukwe Mufti ndiye alikuwa anatumwa na DPP kwenda mahabusu kushawishi watu wakiri makosa (plea bargain). Wengine walikuwa wanampa hela ampelekee DPP.

Bashiru anamshangaa Samia kwa kumteua DPP kuwa Jaji. Anamuona kama mmoja wa majangili ya utawala wa JPM. Anampongeza Former DGIS Robert Makungu (RAS TABORA) kuwa ni mtu mwadilifu anayefa kuwa DG wa TISS
Kisa, eti Makungu alimheshimu sana JPM ila fitna zilimfanya rais asigundue uadilifu wa Makungu. Bashiru anamlaumu sana Kabudi kwa kumshauri vibaya JPM kuhusu jumuiya ya kimataifa. Ndiye alimzuia rais kumwajibisha Makonda kwa madai kuwa atawapa kiburi Wamarekani

Bashiru anasema kuwa Makonda ni kiumbe mchafu kuliko kitu chochote duniani.
Anatamba kuwa yeye na JPM walirejesha mali za chama na kukusanya mapato makubwa. Waliendesha uchaguzi bila kutegemea misaada ya wafadhili na wakibakiwa na salio zaidi 20bn. kwenye account ya chama

Bashiru anajiandaa kuandika kitabu ili kujisafisha. Anamwona JK kama adui wa taifa. Eti alimzonga sana JPM wakati wote mpaka akatishia kususia Ikulu na kwenda kuishi Chato; na kwamba Rais Museveni ndiye alisaidia "kumrejesha." Kifupi, Bashiru aweza hata kujinyonga! He's stressed!
#SautiKubwa
 
Bunge ndiyo hilo hii ripoti ya CAG wameidharau kwa mara nyingine tena.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…