Ripoti ya CAG Ina mapungufu makubwa ya kimantiki; "non-compliance" imetumika kama ubadhirifu kufurahisha umma

Ripoti ya CAG Ina mapungufu makubwa ya kimantiki; "non-compliance" imetumika kama ubadhirifu kufurahisha umma

Ok mimi umenipa kazi ya kupeleka wafanyakazi ofisini na kurudi umenilipa kwa mwaka mzima

Mabasi yangu nikaona yana shida kidogo nikaenda kuchukua mabasi kwa Aboud bus service mazuri kuliko hata yangu wafanye kazi hiyo ili nisivunje uaminifu wafanyakazi waende na kurudi kazini bila shida kipindi chote cha mkataba na ikawa hivyo wewe shida yako nini hata kama ulinilipa bilioni moja Aboud.nikamlipa milioni mia lakini huduma ulipewa kinsmuuma nini? Mkataba mimi na wewe nimeuvunja wapi? Ulinitaka nikuletee mabasi nimepita kwa bilioni moja sasa huyo third party unamtakia nini? Kazi ikiwa mbovu nilaumu mimi sio huyo third party lakini issue ya kuwa huyo third party nimemlipa kiasi gani non of your business
Mfano unaotoa ni irrelavant kabisa. Kinachozungumzwa hapo ni wewe uache kutoa huduma badala yake umuachie Abood na kampuni yake wewe uingie mitini.Tuliingia mkataba na wewe au Abood? Muwe mnasoma vizuri ripoti sio kukaza shingo tu.

CAG ni mtu makini sana. Unachosema wewe ni sawa na huyo mkandarasi angepungukiwa mitambo akaenda kukodi kwa wenzie ili apige kazi,kitu ambacho sio issue
 
Ok mimi umenipa kazi ya kupeleka wafanyakazi ofisini na kurudi umenilipa kwa mwaka mzima

Mabasi yangu nikaona yana shida kidogo nikaenda kuchukua mabasi kwa Aboud bus service mazuri kuliko hata yangu wafanye kazi hiyo ili nisivunje uaminifu wafanyakazi waende na kurudi kazini bila shida kipindi chote cha mkataba na ikawa hivyo wewe shida yako nini hata kama ulinilipa bilioni moja Aboud.nikamlipa milioni mia lakini huduma ulipewa kinsmuuma nini? Mkataba mimi na wewe nimeuvunja wapi? Ulinitaka nikuletee mabasi nimepita kwa bilioni moja sasa huyo third party unamtakia nini? Kazi ikiwa mbovu nilaumu mimi sio huyo third party lakini issue ya kuwa huyo third party nimemlipa kiasi gani non of your business
Broo soma sheria ya manunuzi imeweka wazi ndio maana unaskia wanatangaza tenda sio kwamba unaenda tuu wakishakuhoji wanakuambia uanze kubeba wafanyakazi na hapo ndio tatizo linaanzia kwa ufupi lazma watakagua ubora wa vitu ulivyo navyo ikiwemo magari na ufanisi wa kazi yako kwa kipindi cha muda waliokupa kuhakikisha kwamba unakidhi vigezo na masharti mliyokubaliana ,moja wapo ni kulinda mkataba mlioingia huwezi kuingia mkataba alafu ukaenda kinyume na makubaliano ukienda kinyume ni ubadhirifu.....kwa maana hiyo inawezekana umekusanya tuu magari ili upewe iyo kazi (mchongo)kumbe huna vigezo kwa hiyo sheria itakubana ili taasisi nyingine zisiingie makubaliano ya kidalali namna iyo
 
naweza sema umetunga hadithi ili kusindikiza hoja yako na ndiyo maana umesema mwenyewe haipo kwenye ripoti. tujadili facts za kwenye ripoti sio kuleta hadithi. hata mimi hapa nikija naweza kusema CAG nilimpa nyaraka zote akaficha halafu akaandika kuna ubathirifu.

Kuhusu hoja yako
Serikali imeweka sheria magari yake yote yatengenezwe Temesa au kampuni iliyosajiliwa. Sasa wewe unampa dereva atengeneze,hiyo sio kazi ya dereva. Tunapimaje performance na ufanisi wa dereva? Akibumba matengenezo je. Ndio haya magari mengi ya serikali yamechoka kwa sababu ya service za kihuni.

Halafu ukiruhusiwa kila mtu anafanya anavyojisikia nje ya utaratibu,hiyo ni serikali au pori la manyani?

CAG sio mwehu akute gari imetengenezwa na dereva na docs za manunuzi ya vifaa zote zipo, vifaa vilikaguliwa, vimeingizwa kwenye reja na service yako imekaguliwa kama kweli imefanyika,halafu aseme kuna wizi. Nachojua ataonyesha utaratibu uliokiukwa.

Kama umeruka stage nilizotaja hapo watakuletea noma tu,kitu ambacho ni sahihi. Nyinyi mnajinunulia tu bidhaa bila kufuata utaratibu halafu mnalaumu wakaguzi. Kibaya zaidi mnafanya makusudi kuficha nia ovu
Kubishana na wewe ni kupoteza muda kwani huna unachojua na hujawahi hata kuongoza timu ndani ya serikali!
 
Hata majizi huwa kama wewe usemavyo,wanadai wamepoteza docs. Huyu CAG alikuwa na wewe wakati unanunua tofali? Yeye anaaminishwa na nyaraka na UHALISIA WA KAZI.
Mtu kama wewe hata kwenye hiyo nafasi hutoshi. Unatakiwa kuwekwa pembeni

Sasa anataka uhalisia upi zaidi ya tofali alilokuta site na akauliza bei kwenye soko akakuta ipo sawasawa au juu kidogo ya bei nilimwambia nimenunua tofali?
Nakubali wapo wengi sana wanasingizia kupoteza risit kuficha wizi lakini since auditing inafanywa na binadam na sio mashine, they must be able to tell the difference.
Hivi hata yeye tukikagua matumizi ya ofisi yake tutakuta kila kitu kipo sawa?
 
Hilo nalo litapita na hakuna mtu atakaye chukuliwa hatua. Sana sana ni mtu mmoja kiongozi katika taasisi kutumbuliwa lakini watendaji wanabaki
 
Kwahiyo hakuna upotevu wa pesa, bali sheria tu ndio zilikiukwa?! Mkuu hata hili nahitaji kusoma alichoandika mama Kamugisha? Mama Kamugisha kaonyesha kuna baadhi ya sehemu zinahitajika ufafanuzi kwenye hiyo ripoti, na sio kasema kuwa ripoti yote hakuna wizi bali ni kutofuata sheria tu.

Hapo tuko pamoja, siyo kila audit query ni wizi. Zingine ni kutofuata utaratibu tu. Pia zinaweza kujibika.
 
Sasa anataka uhalisia upi zaidi ya tofali alilokuta site na akauliza bei kwenye soko akakuta ipo sawasawa au juu kidogo ya bei nilimwambia nimenunua tofali?
Nakubali wapo wengi sana wanasingizia kupoteza risit kuficha wizi lakini since auditing inafanywa na binadam na sio mashine, they must be able to tell the difference.
Hivi hata yeye tukikagua matumizi ya ofisi yake tutakuta kila kitu kipo sawa?
Mkuu kwani kazi ya risit ni nini? tuanzie hapo. Kuhusu kukaguliwa CAG anakaguliwa kila mwaka ripoti wanayo PAC. Kama hawakukuta risit hawajasema unamlalamikia CAG? Zingatia taratibu za fedha na manunuzi hutogombana na mtu tofauti na hapo wale wabwana watakuandika sana tu.
 
Magufuli alikuwa analazimisha watu watii sheria na kufuata utaratibu, iweje yeye asifuate huo utaratibu kama alikuwa na nia njema? Kwa hiyo wale aliowatumbua alikuwa anatumia grounds zipi wakati sio lazima kufuata utaratibu?

Ni kweli, nyakati nyingine hakufuata sheria, kanuni na taratibu, licha ya kuwa alifanya kupisha urasimu ili jambo lifanyike kwa haraka.
 
Hata majizi huwa kama wewe usemavyo,wanadai wamepoteza docs. Huyu CAG alikuwa na wewe wakati unanunua tofali? Yeye anaaminishwa na nyaraka na uhalisia wa kazi.
Mtu kama wewe hata kwenye hiyo nafasi hutoshi. Unatakiwa kuwekwa pembeni

Wewe unaishi kwenye UTOPIA au unataka vyovyote vile tafsiri ya hii ripoti iwe ni inayomshusha JPM so kubishana na wewe naona ni kupoteza muda.
 
Ni kweli, nyakati nyingine hakufuata sheria, kanuni na taratibu, licha ya kuwa alifanya kupisha urasimu ili jambo lifanyike kwa haraka.
kama angeona sheria inaleta urasimu angeiboresha kama sio kuibadilisha. unajenga mradi wa mabilioni bila kufanya upembuzi yakinifu halafu unasema unapisha urasimu?
 
Acha story, TOR za audit ya CAG unazijua? Kama huna empirical evidence ya malipo ambayo ni risiti unataka mtu aamini vipi kama legal transaction zilifanyika? Hii nchi tunapenda kuongea ongea kila kitu, mambo ya kitaalamu tuache yafanywe na gurus husika!

Wengine tunadhani audit ya CAG ni kama ukaguzi wa mauzo ya sigara na soda dukani, tuwe na heshima na vitu tusivyojua!
 
Hayo mambo yaache kama yalivyo . Nliwahi kuhusika katka mradi mmoja wa ujenzi wa jengo la serikali . hao jamaa hawana huruma kabisa yaani kitu anakiona ila anakudai resit . Unajaribu kumuelewesha hakuelewi . Lakini na Mimi nakiri kuwa kupitia kutokuwa na resit ndo tulimokuwa tunapigia humo. So jamaa wako sahihi kwa namna Fulani .

WIzi mkubwa huwa una risiti.
 
From a person who has been an auditor and an auditee at one point in time...najitahidi kutokua biased bt ukweli ni kua report hii imekaa kisiasa sana...

wanawapa mnachotaka kuskia na km kawaida ya watanzania tulivyo na mihemko basi tuna demka tu...

99% ya watu wanaodemka na hii report hakuna alieisoma hii report wala kujua taratibu za auditing zipoje, wanapewa heading habari kamili wanajazia wao.

Unapofanya audit, kuna kitu kinaitwa auditing queries and its not necessary wizi au ukiukwaji wa sheria, na ndicho kilichopo ktk report ya CAG hizo hoja zinabidi zijibiwe bt kabla wajibu hoja hawajajibu teyari ashaitoa in public(public judgement)- Haya ni Makosa ya Makusudi CAG anayafanya kila mwaka bt who to question?.

Hii ndo sababu baada ya report kua tabled bungeni, inarudi kwa watuhumiwa wanajibu hoja then hakuna kinachoendelea wala watu kuchukiliwa hatua maana wanakuja kugundua hoja nyingine zina majibu bt at that time inakua too late to clear people's name, na hua humuoni CAG akirudi kusema kuna hoja zimefanyiwa kazi tunazitoa kwenye report.

Ungeonekana msomi kama ungeweka page au sehemu ya ripoti yenye kasoro!

Lasivyo utaonekana kama wanawake wa pwani wakisutana saluni.
 
Ungeonekana msomi kama ungeweka page au sehemu ya ripoti yenye kasoro!

Lasivyo utaonekana kama wanawake wa pwani wakisutana saluni.
Wapumbavu wasiokua na hoja ndo hua wanajibu hoja kwa personal attacks.
Grow up.
 
Kubishana na wewe ni kupoteza muda kwani huna unachojua na hujawahi hata kuongoza timu ndani ya serikali!
Umenyosha mikopo kiutu uzima,sio?! siku nikiongoza timu ndani ya serikali watu kama wewe lazima niwazingue tu. Najiuliza serikali imewezaje kuwa na watu hovyo kama wewe, badala ya kupeleka gari temesa au fundi aliyesajiliwa unapeleka kwa dereva. Dereva amesomea kutengeneza magari au kuendesha? Gari lako mpe dereva atengeneze,la serikali peleka kwa wahusika. Umenisikia broo
 
Back
Top Bottom