Ripoti ya Richmond Bungeni (FULL TEXT) na yatokanayo

Ripoti ya Richmond Bungeni (FULL TEXT) na yatokanayo

wewe nawe..hivi hujasikia bunge limeahirishwa ghafla...hahaaaa
 
Nimesikia best ndo maana nkasema huu mjadala labda tusubiri bunge lijalo baada ya uchaguzi mwezi wa kumi.Kazi ipo!
 
wewe nawe..hivi hujasikia bunge limeahirishwa ghafla...hahaaaa

kikao kilichoahirishwa ni cha jioni ya leo na sio mkutano huu unaoendelea. kuna tofauti na kuahirisha kikao cha bunge na kufunga mkutano wa bunge.

kwa hiyo mzee, richmondi itajadiliwa japo obvious muda hautatosha kwani itajadiliwa siku ya mwisho ambayo iwe isiwe mkutano huu wa bunge utafungwa
 
Hatimaye ile taarifa ya serikali kuhusu utekezaji wa Azimio la Bunge kuhusu Richmond, inawasilishwa kwa mara ya tatu na ya mwisho katika kikao cha bunge cha leo, na wabunge wa CCM, wameshakubali kwa kauli moja, kuipokea taarifa hiyo na kuikubali bila kipingingamizi chochote, kwa mtindo wa funika kombe, mwanaharamu apite!.

Uamuzi huo umefikiwa usiku huu wa manane, katika kikao cha wabunge wa CCM, kilichofanyika ukumbi wa Msekwa kwa hoja kama hawatakubali kulimaliza suala hilo katika kikao hiki, muda uliobakia wa maisha ya bunge hili katika kikao kijacho ni miezi mitatu tuu, hivyo kuendelea kuisulubu serikali kuelekea uchaguzi, ni sawa na kukata mti huku umekalia tawi la mti uukatao.

Hivyo kesho kwa kauli moja, wabunge wote wa CCM, watakuwa kitu kimoja kuunga mkono taarifa hiyo ya serikali, hivyo kuhitimisha rasmi mjadala huu uliosubiriwa kwa hamu na umma wa watanzania.

Uungwaji mkono huo, pia ndio utakuwa ishara ya kuvunjwa rasmi kwa ile kambi ya wabunge, waliojipambanua kama wapambanaji dhidi ya ufisadi, baada ya kundi hili, kuishikia bango serikali kuiamuru kutekeleza azimio la bunge, ambapo serikali siku zote imekuwa ikakaidi.

Kama ni kweli, wabunge hao wapambanaji, watakubali kufunika kombe, huu pia ndio utakuwa uthibitisho wa jibu sahihi la swali la mwana JF, maarufu na mashuhuri, kuliko wana JF wengine wote, Mzee Mwanakijiji, alilouliza siku za nyuma, "Jee Wapiganaji Walioko CCM, Wanapigania Nini?".

Kuungwa mkono kwa hoja ya serikali, pia kutathibitisha ukweli wa kile kitisho dhidi ya Spika Sitta, wengi wakidhani kuwa anatishiwa nyau, hivyo atasimama imara, kumbe sio kitisho cha nyau, ni kitisho kweli, hivyo Bunge la Kasi na Viwango, hatimaye litapiga magoti kwa serikali na kusujidia.

Kama kweli, hao makamanda watakubali funika kombe hiyo, kwa kazi yote na mbwembwe na majigambo ya Kamati Teule ya Dr. Mwakyembe, huu ndio uthibitisho tena wa chama kushika hatamu za kuiongoza serikali, na kele zote za wapiganaji, kumbe hizo ndizo zilizokuwa tisha nyau.

Na mwisho kabisa, huu ndio utakuwa mwanzo mzuri wa utakaso kumsafisha Muzee, na consolidation ya ule mtandao uliosambaratika, kuunda the 'winning coalition' ya 2015, chini ya The King Maker in absentia, yuko kwa Mandela sasa hivi huku nyuma mambo yanaiva!.

Majibu ya hayo yote, yashuhudie live leo , baada ya kipindi cha maswali na majibu, Bungeni kupitia TBC na Star TV!

Update 1: Ripoti inashushwa live na Mwenyekiti, wa Kamati ya Nishati na Madini, Mbunge wa Bumbuli, Mhe. William Shelukindo.

Ripoti imeridhia kujiuzulu kwa EL imetosheleza na kuridhika na uamuzi wa serikali. Kwa vile bunge lilitaka Hosea awajibishwe, na Hosea akaamua kuwachunguza wabunge, Kamati imeonelea imwachie mkuu wa nchi kuamua cha kufanya.

Kombe limefunikwa, Mwendawazimu Richmond, kapita!

Wachangiaji ni 6 tuu.

Uchangiaji unafuatia...
 
Samuel Sita alishashindwa........na nina uhakika
hawatamchagua tena kuwa spika bunge lijalo......

na Mwakyembe tatizo lake alikosea calculation....
yeye alifikiri ukimuondoa Lowassa tu,tatizo limekwisha...
angekuwa smart angemkaba Kikwete toka mwanzo..
under pressure Kikwete angeweza ku bend......
 
Mwakyembe hatma yake itakuwa nini?
.
CCM wamekuta usiku huu wakaambizana wafunike kombe, Dr. Mwakiembe ni mbishi na king'ang'anizi, hivyo keshi ndicho kipimo chake kujipambanua kimsimamo, na yeye akikubali kufunika kombe, then jibu langu kwa lile swali la Wapiganaji walioko CCM, wanapigania nini, nilijibu wanapigania nafsi zao, njaa zao na matumbo yao, akikataa kufunika kombe, ina maana atakuwa amekubali kusimama, ahesabiwe.
 
kazi ipo mi nilisema mwakyembe hana lolote la maana na kweli litatimia leo
 
Mwakyembe, Sitta, Selelii, Mpendazoe, Kilango, Ole Sendeka, Beatrice Shelukindo na Kimaro kweli wandugu mtatuangusha? Pasco na wengineo mtakaokuwa na habari za bunge mtuhabarishe, maana nahisi leo mambo yakienda ndivyo sivyo, nitaona haya kujiita TzPride...JF moderators mtaniruhusu ni badili jina kuwa TzShame.....sidhani kama itafika huko.
 
Nilishasema before, ilimradi umo ndani ya CCM huna sifa za kujiita eti mpambanaji wa ufisadi, kitu gani!kila siku Richmond,Richmond mpaka wengine wamefanya mtaji wa kisiasa kwenye majimbo yao kisa Richmond. Hao kina shelukindo na wenzake nilijua watakumbana na the so called NIDHAMU YA CHAMA, na hapo ndo mwisho wao, walaaniwe kwa kuwalaghai watanzania eti kwamba wao ni wapambanaji wa ufisadi!!
 
Mamaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!mimi siamini kama ndivyo tumekwisha!!
 
CHADEMA????? bonge la track linakuja. DJ usiweke tangazo ..
 
...
Hivyo kesho kwa kauli moja, wabunge wote wa CCM, watakuwa kitu kimoja kuunga mkono taarifa hiyo ya serikali, .
...Majibu ya hayo yote, yashuhudie live leo , baada ya kipindi cha maswali na majibu, Bungeni kupitia TBC na Star TV!
Sorry Pasco, unamaanisha siku gani, leo au kesho?
 
hakuna lolote ndani ya ccm....hakuna jipya!!! kama kuna jipya basi kikweta ni rais wetu 2010 to 2015.....kama sio hivyo tutabaki masikini mpaka kufa..ccm ni chama tu,uzalendo ndio utaweza kunyanyua kwa ukweli.
 
Update 1: Ripoti inashushwa live na Mwenyekiti, wa Kamati ya Nishati na Madini, Mbunge wa Bumbuli, Mhe. William Shelukindo.
 
Ripoti imeridhia kujiuzulu kwa EL imetosheleza na kuridhika na uamuzi wa serikali. Kwa vile bunge lilitaka Hosea awajibishwe, na Hosea akaamua kuwachunguza wabunge, Kamati imeonelea imwachie mkuu wa nchi kuamua cha kufanya.

Kombe limefunikwa, Mwendawazimu Richmond, kapita!
 
Hivi hawa wapambanaji wa ufisadi kwanini walingangania hoja hii wakati wakijua ubavu zero.

muonenni leo shelukindo anavyojikanyaga
 
Back
Top Bottom