Ripoti ya Richmond Bungeni (FULL TEXT) na yatokanayo

Ripoti ya Richmond Bungeni (FULL TEXT) na yatokanayo

Riport Mtaipata muda si Mrefu............
Leo hii Lowasa Fikiria Kuji engua Serikalini...Acheni..Kutu ona Mafala...Tuna waheshimu sana..Sasa Mnapotaka kwenda..Hamtafika...

We Sitta Ok!! Muda Ulio utoa mpaka kesho .....Ok..Lakini Usirudie Tena...Haya mambo Ya kesho Mapaka lini? Tatizo La mafisadi RAM zao zina speed ndogo sana...

((((((((((((((AIBU)))))))))))))
 
endeleeni kutupa utamu

Jamani vyombo vyetu vya habari viko chini sana. Yaani baada ya hii taarifa, jumptv wana taarifa wala hata hawaongelei kilichotokea bungeni. Nilitegemea iwe Breaking News.

Yaani nilichosikia leo, kingelikuwa hapa UK, madhara yake yangeitikisa mno serikali. Lowassa asingelipona, hivyo hivyo Karamangi, Msabaha, mwanasheria mkuu, Hosea wa PCCB pamoja na wafanyakazi kibao wa chini.

Ningetegemea magazeti bila kusubiri na kutoa toleo maalumu za mchana na picha ya Lowassa chini ya kichwa cha habari "GUILTY"

Lakini kwa Tanzania sijui kutakuwa na madhara kiasi gani kwa serikali ya JK.

Kwa standard ya West, hii report ni mawe hasa, ila sina uhakika na uwajibikaji wetu huko nyumbani.

Wacha tusubiri na kuona mwisho wake. Ila kamati wamejitahidi mno, maana kumgusa Wazir mkuu wa nchi sio kitu rahisi, pamoja na kukwepa kwepa lakini
wamechomelea misumari hasa.

Yaani nchi yetu inatia aibu, wataalamu wetu wanatia aibu kweli kweli. Yaani
ni taabu tupu, maana inaelekea hakuna wanachofanya zaidi ya kuchukua kamisheni zao.

Vijana someni mkachukue nchi maana hao watu tulio nao ni bomu mno!
 
Mtanzania, aisee mimi nipo huku porini sina communication yoyte.... Mkuu unaweza kutuwekea hata dondoo/summary manake sio mchezo inaonekana mambo yameenda vile wengi tulivyofikiria na kumuomba Molla atusaidie kuweka hawa mafisaid nje juani tuwakome....

Gigo, tunangojea nyeti kaka manake hii kitu ni ya kusomwa kweli kweli.....

Wale mnaoona hii mambo ina kikao kinaidiscuss au ndio kusomwa leo hoja next tyme???
 
Jamani vyombo vyetu vya habari viko chini sana. Yaani baada ya hii taarifa, jumptv wana taarifa wala hata hawaongelei kilichotokea bungeni. Nilitegemea iwe Breaking News.

Yaani nilichosikia leo, kingelikuwa hapa UK, madhara yake yangeitikisa mno serikali. Lowassa asingelipona, hivyo hivyo Karamangi, Msabaha, mwanasheria mkuu, Hosea wa PCCB pamoja na wafanyakazi kibao wa chini.

Ningetegemea magazeti bila kusubiri na kutoa toleo maalumu za mchana na picha ya Lowassa chini ya kichwa cha habari "GUILTY"

Lakini kwa Tanzania sijui kutakuwa na madhara kiasi gani kwa serikali ya JK.

Kwa standard ya West, hii report ni mawe hasa, ila sina uhakika na uwajibikaji wetu huko nyumbani.

Wacha tusubiri na kuona mwisho wake. Ila kamati wamejitahidi mno, maana kumgusa Wazir mkuu wa nchi sio kitu rahisi, pamoja na kukwepa kwepa lakini
wamechomelea misumari hasa.

Yaani nchi yetu inatia aibu, wataalamu wetu wanatia aibu kweli kweli. Yaani
ni taabu tupu, maana inaelekea hakuna wanachofanya zaidi ya kuchukua kamisheni zao.

Vijana someni mkachukue nchi maana hao watu tulio nao ni bomu mno!


Sijawahi Kulizwa na Riport za kamati za Bunge Lakini leo Nimelia...
 
HII ni sokomoko kubwaa,niwakati sasa wa kunjua kikwete,nipigo kubwa kwa chama cha mafisadi,tusubiri tuone,asipomtoa EL,nitashangaa,
MUNGU IBARIKI TZ,WABARIKI WA TZ
 
Sijawahi Kulizwa na Riport za kamati za Bunge Lakini leo Nimelia...

kaka mimi sikuamini kuwa nachokisikia kinatoka kinywani mwa mbunge wa ccm. tena ndani ya jumba lilelile linalotetea uozo kwa maslahi ya chama.

.............kweli dalili za mwisho zimewadia.........

kazi kwa KIKWETE sasa kuwa fukuza maana ushahidi upo! au awakumbatie tujue kuwa anawalea

.............mungu saidia tanzania..........
 
Kitachofuata ni kuunda tume ya kutoa mapendekezo ya ni adhabu gani itolewe kwa wahusika.
 
.............kweli dalili za mwisho zimewadia.........

kazi kwa KIKWETE sasa kuwa fukuza maana ushahidi upo! au awakumbatie tujue kuwa anawalea

.............mungu saidia tanzania..........

JK hawezifanya chochote hapo, maana EL anadai Richmond ilikuwa kwa nia njema kwa wadanganyika...wanaompakazia ni maadui wake wa kisiasa....hahahahaha mambo mengine bwana unaweza ukana uraia wako bure kama PM anashiriki kufanya nchi yake iwe maskini zaidi...na kuwa wafanya wazalendo wote wajinga..
 
katika hali isiyotegemewa kila mmtu ameguswa na suala hili kila mtu aliyechungulia TV nasikia hana hamu na hii report. kama EL amesikia anatakiwa mwenyewe asirudi Bungeni kama Waziri Mkuu.

Kurudi bungeni ni aibu tupu namshauri angoke tu.

Msumali umepigwa na kuingia sawasawa
 
MAMBO HAYA NIMEYAIBUA TOKA "MICHUZI BLOGSPOT" AMBAKO IMEBANDIKWA PUNDE TU. Mjumbe hauawi, nawasilisha:

MWAKYEMBE AMWAGA LAZI BUNGENI
MH. HARRISON MWAKYEMBE


MBUNGE WA KYELA NA MWENYEKITI WA KAMA TEULE YA KUCHUNGUZA MADUDU KAMPUNI YA RICHMOND, MH. HARRISON MWAKYEMBE, DAKIKA TANO ZILOPITA AMEHITIMISHA KUSOMA RIPOTI YA KAMATI YAKE KWA UWAZI NA UKWELI KWA MUDA WA DAKIKA TAKRIBAN 80.


KAMATI TEULI HIYO IMEBAINI KWAMBA MKATABA WA RICHMOND ULIFIKIWA KWA UPENDELEO, RUSHWA NA UBABE WA VIONGOZI WAANDAMIZI SERIKALINI, NA KWAMBA LICHA YA USHAURI WA KITAALAMU NA HALI HALISI WAKUBWA WALILAZIMISHA USAINIWE. hIVYO PAMOJA NA MAMBO MENGINE KIBAO IMEPENDEKEZA MIKATABA YOTE YA NISHATI IPITIWE UPYA KAMA ILIVYO MIKATABA YA MADINI


KAMATI TEULE HIYO KUPITIA MDOMO WA MH. MWAKYEMBE IMETO MAPENDEKEZO KAMA 15 HIVI, BAADHI YAKE YAKIWA:


1. WAZIRI HUSIKA WA WAKATI HUO (MH. DR MSABAHA) NA KATIBU MKUU WAKE WAKATI HUO WAPEWE ADHABU KALI


2. WAZIRI WA SASA WA NISHATI NA MADINI MH. NIZAR KARAMAGI NA MWANASHERIA MKUU WAWAJIBISHWE KWA KUWEZESHA MKATABA WA RICHMOND KUHAMISHIWA KAMPUNI INGINE


3. UONGOZI WA TAKURU (SASA TAKUKURU) UFANYIWE MABADILIKO HARAKA KWA KILICHODAIWA KUTOA TATHMINI ISIYO SAHIHI JUU YA MAZINGIRA YALIYOUZUNGUKA MKATABA WA RICHMON.


4. MKATABA WA RICHMOND AMBAYO IMEIPASIA KAMPUNI YA DOWANS UCHUNGUZWE UPYA.


5. MSIMAMIZI MKUU WA SERIKALI AMBAYE NI WAZIRI MKUU ATUMIE BUSARA ZAKE KUAMUA NINI CHA KUFANYA BAADA YA RIPOTI KUANIKWA HADHARANI


AIDHA JUHUDI ZINAFANYIKA KUIPATA RIPOTI YOTE HIYO NA KUANGALIA NAMNA YA KUWEKA HADHARANI ILI HADHIRA IJUE KILA KITU KWA UWAZI NA UKWELI.

PSSST! SASA TUNASUBIRI RIPOTI YA MADINI YA KINA KABWE
 
Mtanzania, aisee mimi nipo huku porini sina communication yoyte.... Mkuu unaweza kutuwekea hata dondoo/summary manake sio mchezo inaonekana mambo yameenda vile wengi tulivyofikiria na kumuomba Molla atusaidie kuweka hawa mafisaid nje juani tuwakome....

Gigo, tunangojea nyeti kaka manake hii kitu ni ya kusomwa kweli kweli.....

Wale mnaoona hii mambo ina kikao kinaidiscuss au ndio kusomwa leo hoja next tyme???

Morani,

Ni ngumu kuelezea lakini mimi naona wameenda ndani mno kuliko hata nilivyotegemea. Mapendekezo yao kama yatafanyiwa kazi, basi tegemea wizara ya madini na ofisi ya Mwansheria mkuu kuwa affected hasa.

Pia Wameisagia mno PCCB, ingelikuwa huku West, Hosea alikuwa hana ujanja na badala yake kujiuzulu hapo hapo. Wameomba kuangalia muundo mzima wa PCCB na kuifanyia mabadiliko katika management yake.

Yule aliyekuwa katibu mkuu chini ya Msabaha pia kalaumiwa sana pamoja na Msabaha mwenyewe. Karamangi na yeye matatizoni tena.

Lowassa mbali ya kutajwa kwamba watu kama Msabaha na mwenyekiti wa Tanesco wanaamini kama Richmond ni mali ya Lowassa na Rostam lakini pia mwishoni imeonekana mapungufu mengi chini ya ofisi yake.

Wamesema kwasababu PM ni nafasi kubwa wanamwachia mwenyewe aamue nini cha kufanya. Kama mstaarabu inabidi akamwone JK na kusema mambo yamenishinda na kuachia hiyo nafasi.

Kuna mambo mengi sana, wacha tusubiri report kamili.

Jambo moja, very interesting, kuhusu maadili ya viongozi. Je JK aliiona hii report na ndio akatoa speech yake ya juzi? Wamependekeza kila kitu kama alivyosema JK. Ninaamini hii report iliwakilishwa zaidi ya wiki mbili kwa Speaker, kwahiyo sidhani kamati wameingiza huo ushauri dakika ya mwisho. Sina uhakika ila niliposikia hayo, nilishutuka.
 
MAMBO HAYA NIMEYAIBUA TOKA "MICHUZI BLOGSPOT" AMBAKO IMEBANDIKWA PUNDE TU. Mjumbe hauawi, nawasilisha:

MWAKYEMBE AMWAGA LAZI BUNGENI


MH. HARRISON MWAKYEMBE MBUNGE WA KYELA NA MWENYEKITI WA KAMA TEULE YA KUCHUNGUZA MADUDU KAMPUNI YA RICHMOND, MH. HARRISON MWAKYEMBE, DAKIKA TANO ZILOPITA AMEHITIMISHA KUSOMA RIPOTI YA KAMATI YAKE KWA UWAZI NA UKWELI KWA MUDA WA DAKIKA TAKRIBAN 80.


KAMATI TEULI HIYO IMEBAINI KWAMBA MKATABA WA RICHMOND ULIFIKIWA KWA UPENDELEO, RUSHWA NA UBABE WA VIONGOZI WAANDAMIZI SERIKALINI, NA KWAMBA LICHA YA USHAURI WA KITAALAMU NA HALI HALISI WAKUBWA WALILAZIMISHA USAINIWE. hIVYO PAMOJA NA MAMBO MENGINE KIBAO IMEPENDEKEZA MIKATABA YOTE YA NISHATI IPITIWE UPYA KAMA ILIVYO MIKATABA YA MADINI


KAMATI TEULE HIYO KUPITIA MDOMO WA MH. MWAKYEMBE IMETO MAPENDEKEZO KAMA 15 HIVI, BAADHI YAKE YAKIWA:


1. WAZIRI HUSIKA WA WAKATI HUO (MH. DR MSABAHA) NA KATIBU MKUU WAKE WAKATI HUO WAPEWE ADHABU KALI


2. WAZIRI WA SASA WA NISHATI NA MADINI MH. NIZAR KARAMAGI NA MWANASHERIA MKUU WAWAJIBISHWE KWA KUWEZESHA MKATABA WA RICHMOND KUHAMISHIWA KAMPUNI INGINE


3. UONGOZI WA TAKURU (SASA TAKUKURU) UFANYIWE MABADILIKO HARAKA KWA KILICHODAIWA KUTOA TATHMINI ISIYO SAHIHI JUU YA MAZINGIRA YALIYOUZUNGUKA MKATABA WA RICHMON.


4. MKATABA WA RICHMOND AMBAYO IMEIPASIA KAMPUNI YA DOWANS UCHUNGUZWE UPYA.


5. MSIMAMIZI MKUU WA SERIKALI AMBAYE NI WAZIRI MKUU ATUMIE BUSARA ZAKE KUAMUA NINI CHA KUFANYA BAADA YA RIPOTI KUANIKWA HADHARANI


AIDHA JUHUDI ZINAFANYIKA KUIPATA RIPOTI YOTE HIYO NA KUANGALIA NAMNA YA KUWEKA HADHARANI ILI HADHIRA IJUE KILA KITU KWA UWAZI NA UKWELI.

PSSST! SASA TUNASUBIRI RIPOTI YA MADINI YA KINA KABWE
 
sasa kweli imedhihiri na uongo kujitenga.

tunasubiri kwa hamu nn kitafuatia.

huwezi kuwadanganya watu muda wote tunasubiri nn kitatokea.

utabiri wa shetani kuwa mwaka huu una kishindo si uongo
 
Tuanzishe mada mpya. Mnyika naicopy ripoti yako ili kuanzisha mada (thread) mpya. Samahani
 
Tuanzishe mada mpya. Mnyika naicopy ripoti yako ili kuanzisha mada (thread) mpya. Samahani

Poa. Ripoti kamili pia ninayo. Ni ndefu na ningependa kuiweka kwa sasa kwa sababu maalum. Naamini wengine wataiweka.

JJ
 
hongera john mnyika kwa kuimwaga ripoti hapa JF ....WASHA MOTOO WAJUMBE..MAANA NAONA KABLA SPIKA HAJAIRISHA BUNGE KAMATI YA WABUNGE WA CCM WAMEITISHA KIKAO CHA KUWEKA MSIMAMO WA PAMOJA...SASA SIJUI WABUNGE WA UPINZANI NA WALE WENYE MAPENZI MEMA WA CCM KAMA NAO WATAKUWA NA KIKAO SAMBAMBA.....MSISAHAU WABUNGE WA CCM USIKU KUCHA JANA WALIKUWA KWENYE VIKAO VYA KUJIPANGA...LAKINI KWA TADHMINI YANGU YA HARAKA HARAKA INAONEKANA KIKAO CHA USIKU HUU HAKIKUFANIKIWA KUWAWEKA KWENYE MSIMAMO MMOJA WA KUTETEA UFISADI!!!!....JK ANAINGIA DODOMA MCHANA HUU ATAWEKA KAMBI CHAMWINO KAMA KAWAIDA YAKE BUNGE LINAPOKUWA LINAJADILI HOJA NZITO HUWA DODOMA.....LOLOTE LITAKALOTOKEA MJUE LINA BARAKA ZA KIKWETE!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Asante FD .Nina bahati nimesoma kabla sijaweka maana na mimi nilitaka kuweka .Very good .
 
..JK ANAINGIA DODOMA MCHANA HUU ATAWEKA KAMBI CHAMWINO KAMA KAWAIDA YAKE BUNGE LINAPOKUWA LINAJADILI HOJA NZITO HUWA DODOMA.....LOLOTE LITAKALOTOKEA MJUE LINA BARAKA ZA KIKWETE!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Udaku unasema ana jina la PM kapuni anasuburia tu!
 
Kwa mara ya kwanza kuanzia kuanzishwa kwa bunge la vyama vingi Tanzania. Nimeshuhudia mbunge shujaa kutoka chama tawala akielezea, kinaga ubaga, mapungufu ya serikali ya chama tawala, katika bunge bila ya kujali maslahi ya chama tawala.

Dr. Mwakyembe anstahili kila sifa iwe kutoka kwa wapinzani, chama tawala, au wasio na chama chochote cha kisiasa. Kwani amejitowa muhanga kwa ajili ya wananchi wote wa Tanzania.

Leo, Dr. Mwakyembe amefunguwa ukurasa mpya wa siasa Tanzania, kwa mara ya kwanza serikali inaanikwa madhambi yake hadharani na mbunge wa chama tawala.

Heko Dr. Mwakyembe, nakuombea Mwenyeezi Mungu akulinde na maadui na wote uliowa-wafichuwa wana kila sababu ya kukufanyia uadui.
 
Back
Top Bottom